Dunia yashangazwa na kubadilika ghafla kwa Rais Samia kutoka kuwa mtenda haki na kuanza uonevu

Nafikiri hotuba ya SSH ilijieleza vya kutosha juu ya swala la katiba, yeye aliwaomba kistaarabu kabisa kuwa mmpe muda kidogo Ili amalize shughuli zinazomkabili Ili akimaliza ageukie swala la katiba.
Kiongozi wenu akaotisha kongamano na kumjibu kwa ngebe kuwa hawezi kumpa muda Rais,yeye kama nani? Ile miaka mitano ya JPM alikuwa wapi mbona hakuwahi kumjibu hivyo licha ya JPM kutangaza wazi kuwa hataki kusikia swala la katiba? Leo hii huyu aliekubali ndo amjibu hivyo?

Kivyovyote vile mbowe alimdharau saana SSH.
Na sasa Mbowe anataka huruma ya Mama.

Akae kwa kutulia, rais ana kazi nyingi sana
 
Hata kama haitamzuia tembo kunywa maji tayari mmesimama jalalani,CNN inasikika duniani sio hapo geita ulipo peke yake.
Mkuu KITAMBI...Kwani kipindi kile Robert Amsterdam hakuhojiwa na CNN ?!!!

Kagame anachafuliwa kila uchao ,je ameanguka?!!!

ENDELEA KUJIOTESHA🤣

#KaziIendelee
 
Thanks Sasa Kama Dunia ilivyo mduala, atakuonyeshe yu hai na anaishi kila siku katika ,shughuli,zako na familia yako, BWANA NJOO ,na shughulika nae, ajue utukufu wako ni wajabu, tenda, fanya, kazia zege KWA ndugu huyu ,mpaka akutambue, na sio bule BWANA mpaka asaidie maskini na vilema wasiozidi 747 ,imekua bwana
Mungu hawezi kuamua kwa kutumia akili zako,


Ndio maana huwa tunawacheka sana mnaposema magu alikufa sababu akikuwa anaionea chadema alafu sasa hivi mnakutana na moto zaidi ya ule!..
. Na bado
 
Bora wangeandamana na kupendekeza solution ya tozo (kitu ambacho upunzani ilikua mzuri Sana kwenye kutoa alternative budgets and solutions enzi zile) kuliko hii ya sasa
Wao hawawezi kutetea masuala ya wananchi wote maana si agenda zao.

Agenda yao kubwa ni kutumia njia yoyote ile, hata iwe ma ghiliba kisi gani ili tu wapate madaraka. Hawajui kwamba ili upate madaraka ni lazima Sisi Watanzania tukuchague.

Last time I checked, wananchi waliwakataa vibaya sana kwenye sanduku la kura
 
Machafuko yangetokea wapi kama polisi wangewaacha tu wafanye tu kongamano lao tena LA ndani bila bugudha.

Nchii hii mavhafuko yataletwa na ccm.
Kwa taarifa tu mkuu, nchi zilizoingia kwenye machafuko zilianza hivi hivi. Nenda ukarejee suala la Libya.

Baada ya kudai hizo so called haki zao za kikatiba , wale waliowaingiza mkenge hawakuwaona tena. Tutailinda amani yetu na vizazi vyetu.
 
Mimi yote sawa tu ila huyu mama kaharibu kabisa imani ya wananchi kuwa mwanamke anaweza kuwa kiongozi mkubwa wa nchi. Ilikuwa ndo chance ila ndo imeisha hiyoo wacha amalizie muda wake.
 
Mbona unatumia nguvu nyingi sana kutetea uonevu, udhalimu na ujinga?
Sitetei uonevu wala udhalimu wala ujinga. Najua fika agenda za Chadema, wala sisemi agenda za upinzani maana wapo wapinzani wengine wanafanya siasa za kistaarabu. ACT Wazalendo ni wapinzani pia, NCCR Mageuzi Ni wapinzani pia ila mbona hawapo kama Chadema??

Chadema mnachotaka ni hii nchi iingie machafukoni, hatuko tayari kwa hilo mkuu. Hii nchi ina umri wa miaka 60 sasa, angalieni wenzetu kama Rwanda Libya Ethiopia DRC na wengine wengi hali zao. Je mnataka mtupeleke huko ndugu zetu?

Hawa CNN na BBC na AL JAZEERA hawana jema lolote kwetu. Haya mataifa ya Ulaya tusidhani kwamba eti wanatutakia mema sana. Hapana!
 
Sitetei uonevu wala udhalimu wala ujinga. Najua fika agenda za Chadema, wala sisemi agenda za upinzani maana wapo wapinzani wengine wanafanya siasa za kistaarabu. ACT Wazalendo ni wapinzani pia, NCCR Mageuzi Ni wapinzani pia ila mbona hawapo kama Chadema??

Chadema mnachotaka ni hii nchi iingie machafukoni, hatuko tayari kwa hilo mkuu. Hii nchi ina umri wa miaka 60 sasa, angalieni wenzetu kama Rwanda Libya Ethiopia DRC na wengine wengi hali zao. Je mnataka mtupeleke huko ndugu zetu?

Hawa CNN na BBC na AL JAZEERA hawana jema lolote kwetu. Haya mataifa ya Ulaya tusidhani kwamba eti wanatutakia mema sana. Hapana!
Maneno kuntu kabisa.....

Ndio maana CHADEMA wana siasa za "people's power".....maana yake ni nini ?!!

Hivi lini chama chenye mrengo usio wa KIKOMUNISTI Wala KIJAMAA wanachama wake wanavaa MAGWANDA NA BERETI NYEKUNDU VICHWANI?!!?

Hili wengi hawataki KULITAFAKARI.......

Julius Malema wa EFF ni mkomunisti....na anaeleweka siasa zake.....

#PundaAfeMzigoUfike
#MzigoNiUtulivuWaJMT
 
Back
Top Bottom