Dunia nzima hakunaga Mabadiliko yaliyowahi kuletwa na Watu Wengi

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,227
26,047
1. Wakati wa harakati za kupinga ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini ni watu wachache sana wenye ujasiri walioongoza harakati zile. Wengi wakiwemo waliokuwa wanafanya kazi kwenye mashamba na makampuni ya wazungu waliona sio sawa na walipinga harakati za kina Mandela na Walter Sisulu. Wengi waliona ingawa wanafanya kazi na kupata mishahara basi hakuna shida kumbe hawakujua harakati zile zingewanufaisha wao na vizazi vyao Leo hii harakati zimeisha na wao na vizazi vyao wanaona mabadiliko makubwa.

2. Wakati wa harakati za uhuru kwenye nchi za Africa ikiwemo Tanzania, sio watu wote waliunga mkono. Wengi waliona ni sawa kutawaliwa na wazungu. Ila baada ya Uhuru wengi walijitokeza kuwapongeza kina Nyerere na watu waliopigania uhuru na walifaidika wao na vizazi vyao.

3. Wakati wa mapinduzi ya Ufaransa, kuna wengi ambao waliunga mkono utawala wa kifalme ufaransa na waliona wapigania mapinduzi Kama watu wanaopoteza mda na wangepigwa na kuumizwa na askari na wasingepata kitu. Ila Leo hii baada ya Mapinduzi ya ufaransa, vizazi vyao vinafurahia maisha.

4. Wakati Martin Luther King wa Marekani anapigania haki za weusi pamoja na kina Malcom X kuna watu waliwaona kama watu wanaopoteza muda na kukataa kuwaunga mkono wakifikiri kuwa wangeuliwa na kukatizwa maisha ya duniani. Ila baada ya harakati za Martin Luther King na Malcom X Kufanikiwa vizazi vya wale waliokuwa wakiwakebehi ndio hawa leo wanafurahia maisha mazuri Marekani.

Tunajifunza nini?
Chadema na ACT watakebehiwa sana na watanzania ( baadhi) kuhusu kuandamana, wataambiwa andamaneni nyie, nendeni na wake zenu na watoto wenu. Mara sie hatutaki kupigwa risasi. Ila siku madai yanayodaiwa na Chadema na ACT yakifanikiwa ni watanzania hawahawa na vizazi vyao ndio watakuja kufaidika na mabadiliko yanayodaiwa Leo na watakuja kuwasifu sana Chadema na ACT kwa hizi harakati zao za leo.

Rai yangu kwa Chadema na ACT.

Endeleeni kupigania mnaloliamini, Tupo watanzania tunaowaunga mkono. Kwa wale ambao hawawaungi mkono na wanawakebehi, wala msijali, watakuja kuwashukuru siku moja. Mlilolianza wala msirudi nyuma hadi likamilike.

No Hate No Fear!
 
Katika jamii iliyostaarabika, ukiona hujaridhika na jambo unafuata taratibu za kisheria, kijamii au kisiasa kutafuta utatuzi.

Uchaguzi ulikuwa huru na umefanyika kwa amani.

Kama kuna mgombea hajaridhika. Anatakiwa akashitaki mahakamani. Kama anaona mlango wa mahakama hauingiliki, basi afanye maongezi na upande wa pili kutafuta kile kinachoweza kumridhisha.

Ukiandamana tu bila kufanya jitihada za maongezi, hakuna mstaarabu yeyote duniani atakayekuunga mkono. Swali la kwanza utaulizwa, je ulifanya hatua gani kabla ya kuandamana? Ukisema hajafanya hatua nyingine yoyote, unaonekana mshari.

Kwahiyo, ushauri wangu, hawa ambao hawajaridhika wawasiliane na Humphrey Polepole wapange kufanya maongezi. Au wanaweza kumtafuta mzee kama Butiku akawasaidia kufikisha ujumbe wao kwa Bashiru.

Tanzania ni nchi ya amani. Tuilinde.
 

Attachments

  • 1604141211394.gif
    1604141211394.gif
    42 bytes · Views: 2
Ni mahakama ipi utapinga matokeo ya uraisi? Ni mahakama ipi itawasikiliza wapinzani Tanzania? Hizi walizowafunga chadema kwa kumuua akwilina huku kila mtu akiwa anajua akwilina alipigwa Risasi na polisi?

Msimamo wako haunishangazi, wewe ni mmoja wa wanufaika wa utawala huu dhalimu, huwezi kuona sawa kupigania haki kwa Chadema na ACT. Ila najua wakifanikiwa sio wewe tu utafaidika, hadi kizazi chako cha nne kitafaidika na misingi mipya watakayoiweka Chadema na ACT.
 
Hahahhaha... Tulikuonya humu ile wiki iliyopita kwamba hizi ngebe zenu zitaisha tu!

Yani wiki ile ulikuwa unasema polisi haiwezi kuwashinda umati wa raia, leo unasema tena watu wengi hawajawahi kuleta mabadiriko?

Mwambie Lisu aekti anaenda kununua nyanya kariakoo tena watu watamfuat
 
Hahahhaha... Tulikuonya humu ile wiki iliyopita kwamba hizi ngebe zenu zitaisha tu!

Yani wiki ile ulikuwa unasema polisi haiwezi kuwashinda umati wa raia, leo unasema tena watu wengi hawajawahi kuleta mabadiriko?

Mwambie Lisu aekti anaenda kununua nyanya kariakoo tena watu watamfuat
Ndugu, ndo kwanza kumekucha!! Usishangilie hakika!

Uzuri haya unayoyakebehi yatakufaidisha wewe na vizazi vyako vyote hadi cha 10 pale yakikamilika.
 
Ndugu, ndo kwanza kumekucha!! Usishangilie hakika!

Uzuri haya unayoyakebehi yatakufaidisha wewe na vizazi vyako vyote hadi cha 10 pale yakikamilika.
Hamjawahi kuacha kujifariji,

Kuna mwandishi kampiga Lisu kwamba vipi ulisema utapeleka watu barabarani inakuwaje juzi ukiwa nyumbani kwako unataka watu waende huku wewe ukiwa uko tu nyumbani.?

Akaishia kutapatapa tu
 
Ni mahakama ipi utapinga matokeo ya uraisi??? Ni mahakama ipi itawasikiliza wapinzani Tanzania??? Hizi walizowafunga chadema kwa kumuua akwilina huku kila mtu akiwa anajua akwilina alipigwa Risasi na polisi????

Msimamo wako haunishangazi, wewe ni mmoja wa wanufaika wa utawala huu dhalimu, huwezi kuona sawa kupigania haki kwa Chadema na ACT. Ila najua wakifanikiwa sio wewe tu utafaidika, hadi kizazi chako cha nne kitafaidika na misingi mipya watakayoiweka Chadema na ACT.
Kama huamini mahakama, bado zipo njia nyingine za dialogue.
 
Hakuna kikunukisha, ni maandamano ya amani.Nimerudi Songwe. Kituo kimojawapo cha mabadiliko. Mtapata salamu jumatatu.
Nilifikiri yanaanza juzi kama mgombea wako alivyoshauri, kumbe tungojee wiki ijayo?

By the way, vipi kigogo alisema ana kituo chake cha matokeo hivyo nec na Magu wakae mkao wa kuumbuliwa, huku wewe ukishangilia sana, vipi kashatoa tokeo nani kashinda?
 
Hamjawahi kuacha kujifariji,

Kuna mwandishi kampiga Lisu kwamba vipi ulisema utapeleka watu barabarani inakuwaje juzi ukiwa nyumbani kwako unataka watu waende huku wewe ukiwa uko tu nyumbani.?

Akaishia kutapatapa tu
Hunishangazi kwa maneno yako. Nilikuwa wa kwanza kumshauri Lissu na Chadema juu ya nini cha kufanya humu. Uzuri ushauri wangu wameuchukua na waneufanyia kazi Leo.

Napenda kukuhakikishia tu, mabadiliko wanayopigania Chadema na ACT, wewe na uzao wako wote ndo mtakuwa wa kwanza kufaidika nayo.
 
Nilifikiri yanaanza juzi kama mgombea wako alivyoshauri, kumbe tungojee wiki ijayo?

By the way, vipi kigogo alisema ana kituo chake cha matokeo hivyo nec na Magu wakae mkao wa kuumbuliwa, huku wewe ukishangilia sana, vipi kashatoa tokeo nani kashinda?
Kwani matokeo ya kura yaliyotangazwa ni kura zilizohesabiwa vituoni au ni matokeo waliyokuwa wameyaandaa baadhi ya watu wa Tiss wakishirikiana na NEC na ccm???

Kama kura zilizopigwa hata hazikuhesabiwa huyo kigogo angepata matokeo wapi???
 
Hunishangazi kwa maneno yako. Nilikuwa wa kwanza kumshauri Lissu na Chadema juu ya nini cha kufanya humu. Uzuri ushauri wangu wameuchukua na waneufanyia kazi Leo.

Napenda kukuhakikishia tu, mabadiliko wanayopigania Chadema na ACT, wewe na uzao wako wote ndo mtakuwa wa kwanza kufaidika nayo.
Nenda road mkuu!

Wenye ari ya maandamano ya mabadiriko huwa hawatangazi siku maalumu, huwa wanaibuka tu hata saa nane za usiku unakuta wapo road wamekinukisha.

Hapa kwetu mnasubiri kupangiwa siku maalumu ili hata polisi wajiandae kuwafurusha

Lisu kapiga kelele weeee mpka sauti imemkauka kwamba jamani andamaneni! Hakuna hat nzi anamsikiliza
Leo naona kawa mpole nafikir ameshajua rangi halisi ya watz.
 
Back
Top Bottom