Dunia na maajabu yake, hivi viongozi wetu mnaona elimu ya hivi ni sawa?

TheMnyonge

JF-Expert Member
Mar 25, 2022
739
1,869
Juzi ijumaa nilimtembelea mpwa wangu shule ya sekondari MGULASI, hii ni shule ya kata ya CHAMWINO iliyopo Manispaa ya Morogoro!

Nilienda kupata ufafanuzi wa maendeleo mabovu ya huyo mpwa wangu, nilipofika nikaona msingi uliochimbwa na kutelekezwa (inaelekea ilikuwa ujenzi wa madarasa, lakini uliishia kuchimbwa na kuachwa) japo ujenzi unaendelea eneo la uwanja wa mpira wa miguu, inamaana shule hii haitakuwa na uwanja wa mpira kwa wanafunzi wa shule hii?

Kubwa zaidi, nilishangazwa na idadi kubwa ya wanafunzi ukilinganisha na idadi ya walimu, mwalimu alinifahamisha kwamba shule ina wanafunzi zaidi ya 1600, lakini ina walimu 57 tu, najiuliza watu wenye dhamana ya kusimamia elimu yetu wanaona sawa? Hivi watoto wao wangekuwa kwenye hizi shule wangeacha watoto wao wajazane namna hii?

Niliambiwa kwamba madara yanayojengwa ni kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023, wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 800!

Katika maandalizi hayo, hakuna ongezeko la walimu, hii ina maana kwamba Mwl. Mmoja wa somo X atawajibika kufundisha watoto 800! Hivi kuna muujiza gani unaweza kufanya wanafunzi wajifunze na kuelewa? Hivi Mwl gani ataweza kutoa kazi na kuzisahihisha ipasavyo kwa wanafunzi 800 pèke yake?
Naamini Kuna uwezekano mkubwa hali ikawa hivyo kwenye maeneo mengine mengi nchini, kama ndiyo watoto wetu wanapata elimu ya namna gani?

Au zikishakuwa shule za sisi masikini basi inakuwa bora liende? Kwa kadri muda unavyokwenda matokeo ya shule za umma hasa za kata, yanazidi kuzorota, sio kwa sababu yoyote, isipokuwa mlundikano mkubwa wa wanafunzi bila kuwa n'a idadi ya kutosha ya walimu.

Walimu wapo wengi sana mtaani, waajirini wasaidie kusukuma gurudumu la elimu nchini, nina hakika MGULASI SEKONDARI itakuwa na matokeo mabovu mno, kwa nilivyoona kutokana na sababu nilizozisema hapo juu.

Wenye dhamana mkumbuke, hata sisi masikini tunastahili elimu bora, tungeweza kuwapeleka watoto wetu huko mnakowapeleka nyie, ila kwa kuwa mnatukamua kodi n'a tozo kubwa kubwa bila huruma, tunashindwa!

Walau basi tupeni walimu wengi, kukidhi mahitaji ya watoto wetu, vinginevyo inakuwa dhuluma kubwa sana mnapotumia pesa nyingi kununua magari ta kifahari, na kutumia kodi zetu kulipia watoto wenu shule kubwa kubwa na za ghali, huku sisi tukiendelea kutopea kwenye umasikini!

Viongozi wetu, iangalieni elimu kwa jicho la kipekee, kwani ndiyo mkombozi wa familia nyingi masikini!
 
Kulalamika haijawaiga kuwa dawa au soluhisho la tatizo send him/her to private school

Hata hapa shule za mjini hakuna Walimu fatilia vizuri
 
Kulalamika haijawaiga kuwa dawa au soluhisho la tatizo send him/her to private school
Hata hapa shule za mjini hakuna Walimu fatilia vizuri
Ndugu yangu, utasomesha private ndugu wangapi? Na kama ndivyo inamaana tusilipe kodi kwa kuboresha huduma za kijamii?

Haikubaliki hata kidogo!
 
Walimu wote wanataka wapangiwe dar wakipangiwa vijijini wanahangaika kuhama walimu wengi wamerundikana sehemu moja vijijini kunabakia vile vile kila siku hakuna walimu.
 
Siyo walimu tuu katika sekta ya elimu kuna maboresho mengi sana yanahitajika
 
Walimu wote wanataka wapangiwe dar wakipangiwa vijijini wanahangaika kuhama walimu wengi wamerundikana sehemu moja vijijini kunabakia vile vile kila siku hakuna walimu.
Mkuu hapo ni Morogoro Mjini, hali ipo hivyo, wanafunzi 1600 walimu 57, huko vijijini sijui hali ipoje!
 
Nilikuwa nafuatilia kwa ukaribu réaction ya watu kwenye hii issue ya hali za shule zetu, naona watu hamsomi wala kuchangia,lakini kwenye zile mada za kimaskhara tuko moto kweli kweli yaani...


Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
 
Nilikuwa nafuatilia kwa ukaribu réaction ya watu kwenye hii issue ya hali za shule zetu, naona watu hamsomi wala kuchangia,lakini kwenye zile mada za kimaskhara tuko moto kweli kweli yaani...


Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
Watz wengi ndivyo tulivyo, na usidhani tunajipendea...maisha yanatia stress sana kiasi wengi tupo mitandaoni kurelease stress na si kuendelea kuchosha akili.

Wachache ndio mnakuwa huku kuongea mambo ya msingi na yenye tija Kwa jamii, Kwa hiyo isikushangaze mkuu. Wenye mlengo mmoja na wewe utaona wanachangia.

Na Kuna mambo Kwa serikali yetu hata tuamue kuandamana bila nguo kuongea hayatabadilika. Kwa sababu mfumo wa serikali ni ule ule wa tangu na tangu. Hakuna ushindani wa kupokezana kijiti kwenye upande wa vyama kuongoza serikali, na hapa ndio mzizi wa yote ulipo.

Kungekuwa na kupokezana kijiti Cha vyama vya siasa kuongoza nchi, basi Kila chama ambacho kingeshika hatamu kingefanya mambo mazuri Kwa kuhofia muda wowote wananchi tutawarudisha uraiani.
 
Back
Top Bottom