Dunia ipo katika process ya kujiangamiza?

Lukwangule

Senior Member
May 25, 2009
157
2
Kuna majanga mengi yanatokea duniani hasa yanayohusiana na mabadiliko ya tabia nchi, matetemeko na milipuko ya volkano.Maelezo haya yanayokuja chini ni matokeo ya maneno na maulizo niliyokutana nayo na washiriki wenzangu ndani ya JF wakizungumzia Haiti na Chile na Japan pia. lakini kuna tetemeko kubw ala China na nikasema ngoja namie niwapatie watu mambo niliyosoma katika kitabu kimoja kilichopandikwa 2004 Hercolubus or Red Planet.
Kitabu hiki niliomba niletewe baada ya kukisoma katika mtandao na kweli watu hao waliniletea. Ukikisoma kitabu hiki walahi unaweza kupatwa na wazimu.
Lakini siku zote wanadamu ndio chanzo cha wazimu wa wanadamu wenzao. Kitabu hiki hakiingiliani na imani zako ingawa unatakiwa kwenda na akili katika kukisoma.
Ni kitabu ambacho kinaelezea kinagaubaga kwa mfumo wa akili tambuzi kuhusu maangamizi ya dunia hii.
Kitabu hiki hakina uhusiano wa wazi na Biblia ambayo ninajenga mazoea ya kuisoma.Lakini ndani ya kitabu neno upendo na utunzaji wa mazingira ni kitu kinachozungumzwa sana. Kitabu hiki kinaitwa Hercolubus or Red Planet.
Kwa mujibu wa mwandishi, kitabu hiki ni onyo kwa wanadamu kuhusu maangamizi ya dunia wanaoishi kutokana na kuwa sayari Hercolubus kuendelea kuikaribia dunia.
Imeelezwa kuwa sayari hii kubwa ina nguvu kubwa ya mvutano ambayo itasababisha matetemeko ya ghafla yaliyo makubwa na yanayoweza kutokea kwa mkupuo mmoja pamoja, mawimbi makubwa ya bahari, milipuko ya volkano na mambo mengine ambayo ni tishio kubwa kwa sayari hii ya wanadamu.
Kitabu kimeelezwa kuwa matukio yatazidi ukubwa na ukali wake kwa jinsi sayari hiyo inavyozidi kuiakribia dunia na hali itaendelea mpaka dunia itakapomezwa na kuangamizwa kabisa.
Mwandishi V.M. Rabolú anaelea kwa undani majanga yanayoikabiuri dunia ikiwa na pamoja na yale ambayo tayari yameshaanza kutokea yakiwa ni ishara ya uharibifu mkubwa duniani.
Pia katika kitabu chake kuna kitu alichodai ni fomula ya kuepuka maangamizi.
kwa maelezo zaidi ingia http:lukwangule.blogspot.com
 
Asante mkuu kwa kutupa habari hii. Ngoja nami niingia katika blog hiyo ili nipate copy ya kitabu hicho.
 
lakini pamoja na hayo maelezo ukweli unabaki palepale kwamba hayo matetemeko na volcano eruption ni matokeo ya Geological internal proces, na sio kweli kwamba sasa yamezidi kuliko hapo zamani, kuna uwezekano kwamba sasa yamepungua kwa sababu kwa asilimia kubwa dunia ilifikia katika kiwango chake cha kujibalance,
Mfano chukulia pale Ngorongoro Crater, ule ulikuwa ni mlima mkubwa labda zaidi hata ya kilimanjaro lakini kwa sababu ya eruprtion ya volcano kutoka huo mlima ndio hiyo crater ika form (Crater formation)

kweli nakubliana na wewe kuwa shughuli za kibinadamu zinaweza kwa kiasi kikubwa kutokea kwa haya matetemeko
chukua mfano wa bara la Africa, kwa hapa lilipo linaonekana kama liko sattled na limejibalance vizuri kutokana na uzito wake relative to the entire Earth (Isostance), sasa imagine madini yote yanayochimbwa Africa millions of tons (Iron, Copper,gold, nickel, diamond, caco3 ect), na kumbuka hizi tani zinaenda out of Africa say europe or America, sasa Automatically Bara la Africa litakuwa linaloose weight na same time Europe ina gain weight, sasa katika kujibalance na kucompersent weight loss na weight gain lazima haya mambo yatokee na yatatokea sana
 
lakini pamoja na hayo maelezo ukweli unabaki palepale kwamba hayo matetemeko na volcano eruption ni matokeo ya Geological internal proces, na sio kweli kwamba sasa yamezidi kuliko hapo zamani, kuna uwezekano kwamba sasa yamepungua kwa sababu kwa asilimia kubwa dunia ilifikia katika kiwango chake cha kujibalance,
Mfano chukulia pale Ngorongoro Crater, ule ulikuwa ni mlima mkubwa labda zaidi hata ya kilimanjaro lakini kwa sababu ya eruprtion ya volcano kutoka huo mlima ndio hiyo crater ika form (Crater formation)

kweli nakubliana na wewe kuwa shughuli za kibinadamu zinaweza kwa kiasi kikubwa kutokea kwa haya matetemeko
chukua mfano wa bara la Africa, kwa hapa lilipo linaonekana kama liko sattled na limejibalance vizuri kutokana na uzito wake relative to the entire Earth (Isostance), sasa imagine madini yote yanayochimbwa Africa millions of tons (Iron, Copper,gold, nickel, diamond, caco3 ect), na kumbuka hizi tani zinaenda out of Africa say europe or America, sasa Automatically Bara la Africa litakuwa linaloose weight na same time Europe ina gain weight, sasa katika kujibalance na kucompersent weight loss na weight gain lazima haya mambo yatokee na yatatokea sana
Nataka kusema kwamba maelezo ya kituko ni bomba na yalienda shule thanks kwa kunielimisha. this is what i call knowledge beyond what what, thanks man I apprecciate
 
Kwakuwa kitabu hicho kina ukaribu na Bible nitakitafuta nikisome, nashukuru
 
hiyo sayari kwa jina inaitwa Nibiru au Planet X.
imekua ikija karibu na dunia kwa interval ya muda mrefu sana. sio lazima iimeze ila kile kitendo cha kuikaribia tu ndicho kinachofanya uharibifu huo.
 
kwangu maisha ni "Ni ubatili, ni ubatili!...ubatili mtupu! Kila kitu ni ubatili.
Dunia iwepo ama isiwepo, ni ubatili.
 
Haya yote yametabiriwa ndani ya kitabu cha biblia. Tofauti pekee nninayoweza kuiona ni lugha ya kitaalamu iliyopo kwenye kitabu cha Red planet ya kuweza kuufikisha ujumbe kwa lugha ya kueleweka kwa waliowengi ambapo lugha ya nabii zilizopo ndani ya biblia ni ngumu kwao kuzitafsiri.
 
ukitaka kujua ugumu ulioko kwenye kutafasiri unabii ndani ya biblia- ingia kichwakichwa kwenye daniel chapter 11. utapata habari yake.
inadaiwa hiyo sura imebeba unabii mgumu kuliko nabii zote kueleweka ndani ya biblia na unabii mrefu ulioanzia tangu babylonia ya zamani hadi siku ya mwisho wa dunia
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom