Dunia inatakiwa kujiunga na China kupinga kivitendo “utaifa wa chanjo”

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,008
1,026
Hivi karibuni, miji mingi nchini China ikiwemo Beijing, Shanghai na Guangzhou imezindua kazi ya kuwapatia kwa hiari raia wa kigeni chanjo dhidi ya ugonjwa wa COVID-19, ikiwa ni juhudi za kuwapa wageni haki sawa za kuchanjwa kama wachina.

Kijana Adhere Cavince kutoka Kenya ni mwanafunzi wa shahada ya tatu anayesoma katika Chuo Kikuu cha Ualimu cha Huazhong, mjini Wuhan na kazi ya kuchanjwa inaendelea katika chuo hicho. Hivi karibuni, katika makala aliyoandika kwenye gazeti la Daily Nation la Kenya, kijana huyo alisema, “wanafunzi wenzake wanasisimuka na uzoefu wa kuchanjwa, wana imani kubwa na chanjo ya China, na kuisifu serikali ya China kwa kuwapatia wanafunzi wa kigeni fursa ya kuchanjwa bure.”

QQ图片20210416082811.jpg
Kuwapatia bure chanjo wanafunzi wa kigeni wanaosoma China ni kitendo halisi cha nchi hiyo kutekeleza sifa ya chanjo dhidi ya COVID-19 kuwa “bidhaa ya umma”. Kwa wanafunzi wa Afrika, hatua hiyo ina maana kubwa zaidi. Kwanza, idadi ya wanafunzi wa Afrika wanaosoma China ni kubwa. Takwimu zimeonesha kuwa, mwaka 2018, kati ya wanafunzi wa kigeni laki 5 waliosoma hapa China, asilimia 17 walitoka Afrika idadi ambayo ilishika nafasi ya pili kwa kulifuata bara la Asia.

Pili, si rahisi kuchanjwa Afrika. Hivi sasa wanafunzi wengi wa Afrika watakuwa au wamemaliza masomo yao nchini China na kuwa tayari kurudi nyumbani. Kutokana na athari ya “utaifa kuhusu chanjo”, nafasi ya kupata chanjo barani Afrika ni ndogo, haswa kwa wale ambao si watu wenye hatari ya kuambukizwa, uwezekano wa kuchanjwa ni karibu sifuri. Kwa hivyo baada ya kuchanjwa, wanafunzi wa Afrika wataweza kurudi nchini mwao, kwani sio tu wanajua si rahisi kwao kuambukizwa virusi, bali pia hawana hatari ya kuingiza virusi kwa jamii watakazoishi.

Ukweli ni kuwa baada ya mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19, jamii na idara mbalimbali za vyuo vikuu hapa China wametoa chakula, dawa, nguo za kujilinda na ushauri wa kiafya kwa wanafunzi wa kigeni, na kuwapatia raia wa kigeni wakiwemo wanafunzi chanjo dhidi ya ugonjwa huo ni mfano mwingine wa serikali ya China kuunga mkono juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo duniani.

Nje ya nchi, China inaongoza mchakato wa upatikanaji wa chanjo duniani, na kwa njia moja ama nyingine, inatoa chanjo kwa nchi na mashirika ya kimataifa zaidi ya 100, ili kutuwezesha sisi binadamu kujikwamua kwenye maambukizi makubwa ya COVID-19 hatua kwa hatua na kwa njia ya kibinadamu.

QQ图片20210416082818.jpg
Kuhakikisha chanjo zinapatikana kwa usawa ni kulinda haki za binadamu, lakini kulimbikiza chanjo kunaweza kusababisha watu wengi duniani kuambukizwa virusi, na hata kupoteza maisha ambayo yangeweza kuokolewa. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani WHO, hadi sasa dozi milioni 700 za chanjo dhidi ya COVID-19 zimetolewa kote duniani, lakini katika nchi zenye kipato cha juu, robo moja ya watu wamechanjwa, huku katika nchi zenye kipato cha chini, idadi hiyo ikiwa ni 1 kwa 500 tu.

Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika Matshidiso Moeti wiki iliyopita mjini Nairobi alisema idadi ya watu waliochanjwa katika nchi za Afrika inachukua asilimia mbili tu ya watu waliochanjwa kote duniani, na usambazaji wa chanjo barani humo pia unakosa uwiano na kwamba nchi 10 zimepata asilimia 93 ya chanjo zote za Afrika.

QQ图片20210416082825.jpg
Kwa nchi nyingi za Afrika, chanjo zilizotolewa na China ni sehemu ya kwanza ya chanjo kwao, zimepunguza kwa kiasi fulani“pengo la chanjo”kati ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea, na kuwezesha upatikanaji wa chanjo kwa watu wengi barani humo.

Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe aliielezea chanjo ya China kama ni “mwanga baada ya kiza kinene cha handaki”, rais Hage Geingob wa Namibia alisema “nchi zilizoendelea zinajiangalia zenyewe tu, na kuwasahau watu wa Afrika.” Naye makamu wa rais wa Guinea Ikweta Teodoro Nguema Obiang Mangue alisema, “ni China tu inatujali na kutusaidia.” Lakini kwa kutegemea juhudi ya China pekee haitoshi, “utaifa kuhusu chanjo” umedhoofisha vibaya hali ya kuaminiana kati ya nchi na nchi, na watu na watu.

Ni ndoto za Alinacha kwa binadamu kurudi kwenye maisha ya kawaida kama sehemu hata moja duniani itakuwa virusi vya Corona. Nchi mbalimbali zinatakiwa kushikilia wazo la “jumuiya yenye hatma ya pamoja”, kuvuka mipaka ya nchi katika usambazaji wa chanjo, kutoa msaada kwa nchi zenye mahitaji ili tumalize msukosuko huo wa kiafya kwa pamoja.
 
Sijaelewa mantiki yako. Kwamba china wanatupenda sn na wanatusaidia sn kuliko mataifa ya magharibi au? Ni tahira pekee ndiye atakuelewa. China ni hatari sn kwa afrika na waafrika bora hata wazungu.

Hata Urusi nayo ndo walewale wabaguzi tena hawa warus ndo hawanaga hata msaada wowote wazee wa masiraha ya kvita. Kuhusu chanjo zao kwel kwann tuspate za kwao japo nazo hatujui zna madhara gani kwan haztangazwi.
 
Sijaelewa mantiki yako. Kwamba china wanatupenda sn na wanatusaidia sn kuliko mataifa ya magharibi au? Ni tahira pekee ndiye atakuelewa. China ni hatari sn kwa afrika na waafrika bora hata wazungu.

Hata Urusi nayo ndo walewale wabaguzi tena hawa warus ndo hawanaga hata msaada wowote wazee wa masiraha ya kvita. Kuhusu chanjo zao kwel kwann tuspate za kwao japo nazo hatujui zna madhara gani kwan haztangazwi.
Duh!
 
Sijaelewa mantiki yako. Kwamba china wanatupenda sn na wanatusaidia sn kuliko mataifa ya magharibi au? Ni tahira pekee ndiye atakuelewa. China ni hatari sn kwa afrika na waafrika bora hata wazungu.

Hata Urusi nayo ndo walewale wabaguzi tena hawa warus ndo hawanaga hata msaada wowote wazee wa masiraha ya kvita. Kuhusu chanjo zao kwel kwann tuspate za kwao japo nazo hatujui zna madhara gani kwan haztangazwi.
Hivi wewe mswahili ni kitu gani kina kusukuma mpaka unafikia hatuwa yakuwa driven na rabid hatred ya everything Chinese!! 'am being curious!!

Hawa Wachina unao wachukia hawajawahi kuwa na makoloni ndani ya bara la Afrika, hawakuwahi hata siku moja kubeba Waafrika kwenye majahazi na kuwasafirisha huko Uchina ili watumikishwe kwa nguvu kwenye mashamba ya pamba,ngano na manyumbani kama watumwa un-like Mataifa ya Amerika na Uarabuni - sasa wewe chuki zako zinahibuka/sababishwa na nini? - ebu tufafanulie mkuu.

Kitu ambacho wengi wenu mnakisahau ni kwamba Wachina na Warusi wali-play a pivotal role katika ukombozi wa mataifa mengi barani Afrika ambayo yalikuwa bado yapo chini ya udhalimu wa wakoloni mpaka hapo UChina/Urusi walipo ingilia kati kwa kutoa misaada ya mafunzo ya kijeshi kwa wapigania uhuru, walipewa silaha, fedha, kuwapatia scholarship wanafunzi wa kiafrika kwenda kusomea: Udaktari, Uinjinia, kilimo, ualimu nk - walitoa mpaka msaada wa chakula, tatizo tulilo nalo hivi sasa linatokana na kizazi hiki cha dot com ambacho si rahisi kizazi hicho kulitambua hilo, baada ya kuzaliwa walikuta mataifa yao yako huru, hawajui kwamba watu wengi walipoteza maisha katika jitihada za kukomboa nchi zao dhidi ya minyororo ya wakoloni, mpo mpo tu mkisha kunywa Coca Cola/Pepsi, chewing gum, colgate ie products zinazo zalishwa USA basi mnafikiri Dunia ni Amerika na nchi za Ulaya basi, mna sujudu mataifa ambayo ndiyo yalikuwa wahusika wakuu ku-underdevelop bara la Africa by plundering our vast Natural resources kwenda kuendeleza kwao, je, Wachina au Warusi lini waliwahi kupora mali asili za Afrika kinguvu and giving nothing in return - when?

Wachina wamewekeza na kujenga viwanda vingi na vya maana barani Afrika na kuzalisha ajira nyingi kwa vijana pia na ujenzi wa: mabarabara, reli, shule za ufundi,Hospitali,mawasiliano nk.

Tuwe wakweli hapa Wachina wamebadirisha kabisa sura ya Afrika kimaendeleo, mwenye macho ahambiwi tazama - sasa wewe mwenzetu ebu twambie Amerika iliwahi kujenga viwanda vingapi Tanzania tangu tupate uhuru,je,Hospitali ngapi,barabara nganpi nk.

Mkuu ni hivi: wakati mwingine tunapo lahumu Wachina/Warusi tujifunze kubakiza akiba za maneno, Waafrika tusikubali kutumiwa na wazungu kama conduit ya kueneza propaganda zao chafu dhidi ya Uchina - watu wenye akili timamu Duniani nzima wanajua kwamba crusade inayo endeshwa na Mataifa ya magharibi dhidi ya Uchina inatokana na vita vya chini chini vya kiuchumi baina ya China na USA/Uingereza, wasituingize sisi Wafrika ku-join their band wagon ya kutisha/chukia ujio wa Wachina barani Afrika. Na wewe kwa bahati mbaya hupo kwenye league ya kusema vibaya/chukia Wachina without any good reason to speak about, you simply emulating to the letter western inempt propaganda designed to demonise China. Hii inasikitisha sana sana.
 
Hivi wewe mswahili ni kitu gani kina kusukuma mpaka unafikia hatuwa yakuwa driven na rabid hatred ya everything Chinese!! 'am being curious!!

Hawa Wachina unao wachukia hawajawahi kuwa na makoloni ndani ya bara la Afrika, hawakuwahi hata siku moja kubeba Waafrika kwenye majahazi na kuwasafirisha huko Uchina ili watumikishwe kwa nguvu kwenye mashamba ya pamba,ngano na manyumbani kama watumwa un-like Mataifa ya Amerika na Uarabuni - sasa wewe chuki zako zinahibuka/sababishwa na nini? - ebu tufafanulie mkuu.

Kitu ambacho wengi wenu mnakisahau ni kwamba Wachina na Warusi wali-play a pivotal role katika ukombozi wa mataifa mengi barani Afrika ambayo yalikuwa bado yapo chini ya udhalimu wa wakoloni mpaka hapo UChina/Urusi walipo ingilia kati kwa kutoa misaada ya mafunzo ya kijeshi kwa wapigania uhuru, walipewa silaha, fedha, kuwapatia scholarship wanafunzi wa kiafrika kwenda kusomea: Udaktari, Uinjinia, kilimo, ualimu nk - walitoa mpaka msaada wa chakula, tatizo tulilo nalo hivi sasa linatokana na kizazi hiki cha dot com ambacho si rahisi kizazi hicho kulitambua hilo, baada ya kuzaliwa walikuta mataifa yao yako huru, hawajui kwamba watu wengi walipoteza maisha katika jitihada za kukomboa nchi zao dhidi ya minyororo ya wakoloni, mpo mpo tu mkisha kunywa Coca Cola/Pepsi, chewing gum, colgate ie products zinazo zalishwa USA basi mnafikiri Dunia ni Amerika na nchi za Ulaya basi, mna sujudu mataifa ambayo ndiyo yalikuwa wahusika wakuu ku-underdevelop bara la Africa by plundering our vast Natural resources kwenda kuendeleza kwao, je, Wachina au Warusi lini waliwahi kupora mali asili za Afrika kinguvu and giving nothing in return - when?

Wachina wamewekeza na kujenga viwanda vingi na vya maana barani Afrika na kuzalisha ajira nyingi kwa vijana pia na ujenzi wa: mabarabara, reli, shule za ufundi,Hospitali,mawasiliano nk.

Tuwe wakweli hapa Wachina wamebadirisha kabisa sura ya Afrika kimaendeleo, mwenye macho ahambiwi tazama - sasa wewe mwenzetu ebu twambie Amerika iliwahi kujenga viwanda vingapi Tanzania tangu tupate uhuru,je,Hospitali ngapi,barabara nganpi nk.

Mkuu ni hivi: wakati mwingine tunapo lahumu Wachina/Warusi tujifunze kubakiza akiba za maneno, Waafrika tusikubali kutumiwa na wazungu kama conduit ya kueneza propaganda zao chafu dhidi ya Uchina - watu wenye akili timamu Duniani nzima wanajua kwamba crusade inayo endeshwa na Mataifa ya magharibi dhidi ya Uchina inatokana na vita vya chini chini vya kiuchumi baina ya China na USA/Uingereza, wasituingize sisi Wafrika ku-join their band wagon ya kutisha/chukia ujio wa Wachina barani Afrika. Na wewe kwa bahati mbaya hupo kwenye league ya kusema vibaya/chukia Wachina without any good reason to speak about, you simply emulating to the letter western inempt propaganda designed to demonise China. Hii inasikitisha sana sana.
Narudia tena mchina hana msaada kwa africa. Hzo mbwembwe ulzoweka mabepari wanafanya zaid ya hayo hapa africa huo ujenz wa hayo unayoyasema unadhan wanajenga bure eti waulze zambia na ethiopia.
Hakuna cha maana mchina au mrusi anafanya africa ni bora hata urusi huwa hajihusish sn na africa huyo mchna wako hafai kbs ni mwz tu hakuna cha mchna wala bepari wala urus wote hawa hawaipend africa wote ni maslah tu. Naona povu limekutoka sn hamia china.
 
Sijaelewa mantiki yako. Kwamba china wanatupenda sn na wanatusaidia sn kuliko mataifa ya magharibi au? Ni tahira pekee ndiye atakuelewa. China ni hatari sn kwa afrika na waafrika bora hata wazungu.

Hata Urusi nayo ndo walewale wabaguzi tena hawa warus ndo hawanaga hata msaada wowote wazee wa masiraha ya kvita. Kuhusu chanjo zao kwel kwann tuspate za kwao japo nazo hatujui zna madhara gani kwan haztangazwi.
Kweli bora wazungu wanaroho nzuri na ndio maana wamewaambia muolewe
 
Back
Top Bottom