Dunia imekwisha ( MAAJABU YA NABII WA KIKE) kuna Manabii mpaka wa kike?

Huwa napata shida sana kuelewa nafasi ya Mungu iko wapi miongoni mwetu binadamu. Ukiwa mzinzi, unaambiwa we ni wa motoni tu. ukiwa jambazi we ni wa motoni tu, Ukiokoka unaambiwa zamani ulikuwa malaya sasa maisha yamekushinda ndo unaokoka. Mchungaji/pastor akitenda mema utasikia ni nguvu za giza, na akibaka ndo kabsaaaaaaaaaaaa! Basi najiuliza viongozi wa dini watende lipi jema ili lihusishwe na maajabu ya Mungu, nipeni jibu, loh!
 
View attachment 40692

View attachment 40693

Na Haruni Sanchawa
MAAJABU ya uponyaji ndani ya Kanisa la Huduma ya Maombezi lililopo Mbezi Beach chini ya Kiongozi wake, Flora Peter yameendelea kutokeaa baada ya hivi karibuni, Halima Awazi aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa kuombewa na kuanza kuona.

Akizungumza na Amani kanisani hapo hivi karibuni, Halima alisema, haamini kama sasa anaona kwani ni kama ndoto kwa sababu hakufikiria kama siku moja ataondokana na ulemavu wa macho.

"Mimi ni Muislamu lakini baada ya kupata taarifa za mtumishi huyu, niliomba ndugu zangu wanipeleke kwake ili aniombee, sasa ninaona na kutambua hiki ni kitu gani, jambo ambalo sikulitarajia. Kwangu haya ni maajabu ya dunia," alisema Halima.

Naye Faraja Tweve aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa alisema alifikishwa kanisani hapo akiwa hoi huku amebebwa na watu walioamini kuwa atakufa lakini baada ya kuombewa na nabii Flora alipona.

"Nilikuwa nasoma Tumaini (Chuo Kikuu) lakini nilikatisha masomo kutokana na kuugua ugonjwa nisioujua, namshukuru Mungu nimepona na kwa hali niliyonayo, naamini mwakani nitaanza mwaka wangu wa kwanza wa masomo baada ya kuokoka na kifo," alisema Tweve.

Uponyaji wa magojwa yaliyoshindikana unaofanywa na nabii huyo, umepelekea idadi kubwa ya wageni kutoka Kenya na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kumiminika kwa wingi kanisani hapo kwa lengo la kupata huduma ya maombezi

kama kawaida, the first clients are always ladies
 
Naukumbuka kwa hisia kali sana wimbo wa marehemu Angel Chibalonza akisema "kubarikiwa si kuwa na mali nyingi (kama ilivyozoeleka kwa wengi sasa) ila kubarikiwa ni kukutana na YESU. Leo hii tulio wengi tunapenda injili yenye majibu ya papo kwa papo, yaani uombewe upate kazi, ufaulu, uwe na afya njema lakini upande wa pili maisha yako yana walakini mbele za MUNGU. Tumuombeni MUNGU kwenye privacy zetu halafu hawa watumishi tubaki kuwashirikisha lakini maisha yako na maombi yako yawe ni wewe na MUNGU pekee. Mbarikiwe sana
 
Imani yako itakuponya.
Yule 'babu' wa loliondo atafunguliwa mashtaka muda si mrefu. Sasa wanazuka wengine wanatumia nguvu za kiza, kisha baadae tunashuhudia vilio. Kibwetere wa kike huyo eeenh? Uongo mtupu. Moto mkali unawangoja siku ya hukumu.
 
Babu wa Loliondo kaenda na sasa nabii kaja. Kwa ushenzi huu Tanzania inateketea tunaona watu wazima.
 
Back
Top Bottom