Dunia haina usawa

Mama sina ukorofi ninaoufanya acha tu napewa ban sababu za kijinga sana hata nikikohoa napewa ban woiiii huyo mod huyu aendelee tu
Mara ya mwisho kupigwa ban ilikuwa 2012 kipindi hicho nilikuwa mgeni bado JF!
 
Hii story iko safi sana... Natamani tungekuwa na Directors wazuri wa movies... Imagine hii ingekuwa movie yenye effects za technology ya juu kama ma movie ya kina Denzel au Jack Bauer
 
Mama sina ukorofi ninaoufanya acha tu napewa ban sababu za kijinga sana hata nikikohoa napewa ban woiiii huyo mod huyu aendelee tu
sababu za kijinga kama zipi labda..?
unachangamsha...wakikubana wana.....
 
ERIC SHIGONGO
DUNIA HAINA USAWA

Siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu iliwadia, kila mtu alikuwa na presha, muda wa kampeni ulikuwa umekwisha na kilichobaki kilikuwa ni kwa wananchi kupiga kura na kumchagua rais ambaye angewaongoza kwa muda wa miaka mitano.
Japokuwa Kambili alikuwa na uhakika wa kuchukua nafasi hiyo lakini alikuwa na wasiwasi mkubwa, hakuona kama alitakiwa kujiamini kwani binadamu wengi walibadilika, ilikuwa ni rahisi kukubaliana leo lakini baada ya siku kadhaa kubadilika na kujifanya kama hakuwa mtu uliyeelewana naye.
Alilijua hilo, hakuwa na amani hata kidogo. Aliondoka na kundi lake kuelekea katika kituo cha kupiga kura na kupiga huko huku waandishi wa habari wakiwa kila kona kwa ajili ya kuchukua matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitokea siku hiyo.
Alipomaliza, akapigwa picha nyingi na kurudi katika makao makuu ya Chama cha Tanzania National Party ambapo huko akaanza kusikilizia kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Kwa kipindi hicho hakutaka kumwamini mtu yeyote yule, kila aliyekuwa akimwangalia, alihisi kama hakumpigia kura. Alibaki mahali hapo kwa dakika thelathini ndipo akaamua kumpigia simu mke wake na kuzungumza naye.
Huyo ndiye alikuwa faraja yake, alimpenda, ndiye mtu aliyekuwa akimfariji hata katika kipindi alichokuwa na matatizo mengi. Alizungumza naye kwa dakika kadhaa, akakata simu na kutulia kimya.
Hakutaka kuzungumza na mtu yeyote yule, alikuwa na presha, aliwaza vitu vingi kwamba kama asingefanikiwa kuwa rais nini kingetokea? Nani angemuonyeshea upendo kama alivyokuwa akimuonyeshea kipindi cha nyuma?
Wakati mwingine alitamani kumpigia simu Godwin na kumwambia afanye kila linalowezekana ili kubadilisha matokeo kwani kwa kipindi hicho yalikuwa yakihesabiwa kwa kutumia kompyuta.
“Hivi nitashinda kweli? Mbona sijiamini? Mbona kila mtu namuona kama amebadilika, ana wasiwasi, hivi kweli nitakuwa rais au ndiyo itakuwa kama miaka mingine?” alijiuliza huku akionekana kutokuwa na furaha kabisa.
Alihitaji muda wa kukaa peke yake kwanza, kila mtu aliyemwangalia aliuona wasiwasi wake aliokuwa nao, alitetemeka kana kwamba kulikuwa na baridi kali, akasimama na kuelekea katika chumba kimoja kilichokuwa wazi na kutakiwa kubaki humo.
Kichwa chake kilikuwa kikimfikiria Godwin tu, alijua kwamba kijana huyo alikuwa na nguvu ya kubadilisha matokeo yale, kama wangezungumza kwa kirefu basi angecheza na kompyuta, matokeo yale angayachezea na mwisho wa siku kushinda kwa asilimia kubwa.
Alimfahamu kijana huyo, alipambana kwa nguvu zote, katika vitu ambavyo hakuwa akivipenda ni kumpendelea mtu. Alikuwa akipigana kwa kila hali lakini mwisho wa siku haki ipatikane. Hakuona kama lilikuwa jambo sahihi kumshirikisha kijana huyo katika jambo kubwa kama hilo.
Wakati amekaa katika chumba hicho, akaiona simu yake ikianza kuita, akakiangalia kioo, namba ilikuwa mpya kabisa, akabaki akijiuliza kama ilikuwa sahihi kuipokea namba hiyo hasa katika kipindi kama hicho au la. Akapiga moyo konde na kuipokea.
“Halo!” aliita kwa hofu kubwa.
“Mbona unaitikia kinyonge hivyo?” lilikuwa swali la kwanza alilouliza mpigaji simu.
“Kawaida. Nani? Godiwn?’ aliuliza.
“Ndiyo!”
“Mungu wangu! Nilikuwa nakufikiria wewe hapa,” alisema Kambili huku kidogo uso wake ukianza kuonyesha tabasamu la mbali kabisa.
Hakutaka kumficha, akamwambia kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwamba moyo wake ulikuwa na hofu kubwa kwamba angeweza kushindwa katika uchaguzi huo kwani hakumwamini mtu yeyote yule.
Badala ya kumuondoa wasiwasi aliokuwanao, Godwin akaanza kucheka kwa sauti kitendo kilichomshangaza Kambili kwani hakutegemea kumsikia mwanaume huyo akicheka na wakati alikuwa akimwambia kitu kilichomfanya kukosa furaha kabisa.
“Unacheka nini?”
“Una wasiwasi sana. Umeshinda uchaguzi kwa silimia tisini, asilimia ambazo hazikuwahi kufikiwa na mtu yeyote yule,” alisema Godwin huku sauti ya kicheko chake ikianza kupungua.
“Unasemaje?”
“Umeshinda uchaguzi. Nilikuwa nataka nikupe habari hiyo tu,” alisema Godwin, hakutaka kuendelea kuzungumza naye, akakata simu.
Kambili alibaki akiwa amesimama tu, hakuamini aichokuwa amekisikia, aliiangalia simu yake huku kutetemeka kule kukianza kuisha. Hakuamini, aliita kuona kama Godwin alikuwa hewani lakini hakusikia sauti yoyote ile.
Moyo wake uliokuwa umekata tamaa ukaanza kurudi katika hali ya kawaida, haraka sana akatoka chumbani mule na kwenda walipokuwa wenzake, akaanza kurukaruka kwa furaha kitendo kilichomshangaza kila mtu kwamba nini kilitokea mpaka kiongozi wao kuwa kweye hali ya furaha kiasi kile.
“Tumeshinda uchaguzi,” alisema Kambili huku akionekana kuwa na furaha kupita kawaida.
Kila mtu alimshangaa, hawakuamini kile alichowaambia kwani matokeo hayakuwa yametangazwa, ndiyo kwanza kura zilipelekwa katika kompyuta tayari kwa kuhesabiwa, ilikuwaje aseme kwamba alikuwa ameshinda uchaguzi huo?
Kila mmoja akatamani kuuliza swali hilo, hata kabla hawajapata jibu Kambili akawaambia kuwa kila mmoja alitakiwa kuamini kwamba alikuwa ameshinda uchaguzi huo na kilichokuwa kikisubiriwa ni matokeo kutangazwa tu.
Wakatulia na kusikilizia kile kilichokuwa kikiendelea. Hawakuondoka, kila mtu mtaani alitaka kujua kilichotokea, kila mmoja alitamani kumuona Kambili akishinda uchaguzi huo kwani alihangaika kwa kipindi kirefu kuipigania nchi hiyo, katika uchaguzi mwingine alikuwa akishinda lakini kura ziliibwa na ushindi kupewa mtu mwingine.
Siku iliyofuata Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi, Bwana Hidifonce Kipunde akaanza kutangaza matokeo ya uchaguzi huo ambayo yalikuwa yakisubiriwa kwa hamu kubwa na kila mtu. Jina lake na chama chake ndivyo vilivyokuwa vikitawala, alipata kura nyingi mno kiasi kwamba kila mtu alishangaa.
Matokeo yalitangazwa kwa saa kadhaa na kufungwa huku akiwa ameshinda kwa asilimia tisini kama alizoambiwa na Godwin. Moyo wake ukafurahi, baada ya kupambana kwa miaka kadhaa kwa ajili ya kuiongoza nchi hiyo hatimaye alifanikiwa kuwa rais wa nchi hiyo.
Ilikuwa shangwe mitaani, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba Kambili angewafikisha kule walipokuwa wakitaka kufika kwa sababu tu aliaminiwa na Godwin aliyekuwa akipendwa na kila mtu kutokana na umaarufu mkubwa aliokuwa amejiwekea katika kufanya yale ambayo kila mtu alitaka kuyaona yakifanyika nchini kwake.
“Hatimaye nimekuwa rais! Siamini mke wangu,” alisema Kambili huku akimkumbatia mkewe.
Taarifa hizo zilitangazwa kila kona, watu wengi walifurahi kuona upinzani ukiwa umechukua nchi baada ya mapinduzi ya kumtoa Bokasa kufanyika kwa nguvu kubwa. Shukrani za kila Mtanzania zilikuwa kwa Godwin ambaye hawakujua hata alifananaje.
Baada ya kukaa wiki moja na nusu, hatimaye Kambili akaapishwa mbele ya Watanzania lakini moja waliokuwa uwanjani na milioni ishirini waliokuwa katika televisheni zao na hivyo kuwa rais wa kwanza wa nchi hiyo kutoka katika chama cha upinzani.
“Nitaanza upya kila kitu, nitafanya mambo mengi ambayo hayakufanywa. Nitachagua viongozi wengi makini. Tunamshukuru Godwin kwa kila kitu. Yeye atakuwa waziri wa ulinzi kivuli asiyeonekana, kazi yake kubwa ni kutuambia kila kitu kinachoendelea kutoka kwa maadui zetu ambao bila shaka watakuwa wakiwasiliana kupitia simu na kompyuta,” alisema Rais Kambili maneno yaliyoibua shangwe kubwa uwanjani hapo.
“Kila kitu kitakwenda kama kinavyotakiwa. Uchumi utapanda, pesa itaongezeka,” alimaliza kusema Kambili maneno ambayo pia yalipokelewa kwa shangwe kubwa kila kona ya Tanzania.
***
“Nitapambana mpaka nihakikishe Tanzania imebadilika na kuwa ile ambayo kila mtu anatamani sana kuiona! Kuna watu wengi wamenyonywa, wengine wameteswa, wengine wamekimbia nchini kwa kuhofia kufa njaa, umasikini uliwaua, ninawahakikishia kwamba kila kitu kitakwenda kama kinavyotakiwa kuwa,” alisema Kambili huku akiwaangalia watu wote waliokusanyika kushuhudia kuapishwa kwake.
Aliongea mambo mengi jukwaani kipindi cha kuapishwa kwake. Moyo wake uliamua kujitoa asilimia mia moja kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania ambao walimpa kura zao kwa ajili ya kuona mabadiliko yakitokea nchini.
Alidhamiria kuibadilisha Tanzania, miziz ya utawala uliokuwa umepita, alitaka kuing’oa na kutengeneza Tanzania mpya ambayo aliamini kwamba kila mtu angeipenda. Alitaka kurahisisha maisha, Watanzania wale waliokuwa wamepigika maishani mwao alitaka kuwapa tumaini jipya, alitaka kuwaona wakiyafurahia maisha yao kana kwamba waliishi peponi.
Alipomaliza kuzungumza, akashuka jukwaani na kwenda kukaa sehemu yake. Macho yake yalikuwa yakiwaangalia wananchi waliokuwa wamekusanyika katika Viwanja vya Jangwani, kwa jinsi watu walivyoonekana, nyuso zao zilikuwa na matumaini makubwa kwamba kila kitu kingekwenda kuwa kama kilivyotakiwa kuwa kipindi hicho.
Baada ya kumaliza sherehe za kuapishwa kwake, watu wakatawanyika huku wakiwa na nguvu mpya kwamba hatimaye Tanzania mpya ilikuwa njiani kutengenezwa. Mitaani, bado sherehe zilikuwa zikiendelea kama kawaida, watu walirukaruka kwa furaha huku kila mmoja akijaza matumaini makubwa moyoni mwake.
Kambili alipoanza kazi yake ofisini, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuzifunga zile akaunti za mawaziri ambao walijitajirisha kwa kutumia pesa za serikali, mali zao zikachukuliwa na kila kitu walichokuwa nacho kikarudi mikononi mwa serikali.
Mikataba mipya iliyokuwa imesainiwa, ikaanza kupitiwa upya, kila kitu kilichokuwa kimefanyika kwa ajili ya kumpendalea mtu fulani muda huo ulikuwa ni wa kukirekebisha na kuwekwa vile kilivyotakiwa kiwepo.
Pesa za serikali ambazo Bokasa alikuwa amezihamishia nchini Ubelgiji na hatimaye Godwin kuzirudisha, zikaingia katika akaunti ya serikali na hata zile za mawaziri wengine ambazo zilihamishwa kutoka katika Benki ya Geneva, zote zikaingizwa katika akaunti ya serikali.
Mfumo wa utozaji kodi ukakaguliwa na kupangwa upya, kila kitu kilichokuwa kimefanyika kwa kusudi la kuwanyonya wananchi kikarekebishwa na kuwa kama kilivyotakiwa kuwa kipindi hicho.
Mabadiliko makubwa yakafanyika, hata kabla ya kuwachagua mawaziri Kambili alihakikisha anarekebisha kila sehemu iliyoonekana kuwa na uozo mkubwa. Ilikuwa kazi ngumu na kubwa kwani kila kitu alichokuwa akikigusia kilionekana kuwa uozo mkubwa na kilifanywa na msururu wa watu wengi.
Watu wote waliokuwa wamejilimbikizia mali wakapokonywa na kuanza kufuatilia namna ya walivyofanikiwa kuzipata mali hizo. Hakukuwa na tajiri aliyebaki salama, wengi walionekana kujipatia pesa kwa njia ambazo hazikuwa halali kabisa.
Kila kitu alichoanza kufanya Kambili alionekana kuwa mkombozi wa taifa hilo, hakuwa akifanya kazi nyingine kwa kipindi hicho zaidi ya kurekebisha pale kote kulipokuwa na uozo mkubwa. Wananchi wakampenda na kuona kwamba huyo ndiye alikuwa mtu aliyekusudiwa kuwaongoza japokuwa alichelewa sana kufika.
Kwa upande wa Godwin, kazi yake ilikuwa ni kufuatilia mawasiliano ya watu waliokuwa karibu na viongozi waliotoka madarakani, alitaka kuangalia kama kulikuwa na kitu chochote kile kilichokuwa kikiendelea.
Alikuwa bize lakini muda mwingi alikuwa na nafasi ya kuzungumza na Winfrida, alimpenda msichana huyo na kila siku alimsisitizia kwamba ilikuwa ni lazima kumuoa kwani hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa naye kwa karibu kama ilivyokuwa kwake.
Akawasiliana na mchungaji wa Kanisa la Praise God lililokuwa Mwenge jijini Dar es Salaam na kumwambia kuhusu hitaji lake la kutaka kufunga ndoa na msichana huyo. Hilo halikuwa tatizo, kitu pekee walichotakiwa kufanya ni kuanza kuhudhuria mafunzo ya ndoa ndani ya kanisa hilo kitu ambacho hakikuwa tatizo hata kidogo.
Baada ya mwezi mmoja wa mafunzo, wakafunga ndoa ndani ya kanisa hilo huku kukiwa hakuna mtu hata mmoja aliyegundua kama Godwin huyo ndiye yule shujaa aliyekuwa akisifika Tanzania nzima, mwanaume ambaye kila mtu alitamani sana kumuona.
Kwenye harusi hiyo, marafiki zake walikusanyika kwa wingi, hawakuamini kama kweli dsiku hiyo rafiki yao alikuwa akiolewa. Happiness, msichana ambaye alikuwa naye tangu siku ya kwanza alipoonana na Godwin kituoni alibaki akimshangaa Winfrida kwani mpaka kufikia kitendo cha kuolewa na mpiga debe, kilimaanisha kwamba alikuwa na mapenzi ya dhati moyoni mwake.
Winfrida hakujua mahali Godwin alipopata pesa lakini baada ya kufunga ndoa, wakahama Tandale na kuhamia Masaki katika jumba moja kubwa la kifahari na kuanza maisha hapo. Alimfahamu kama mipiga debe tu, ilikuwaje mpaka awe na kiasi hicho cha pesa, kwa mbali moyo wake ukaanza kuwa na hofu kwamba inawezekana mumewe huyo alikuwa jambazi au mtu yeyote wa madili.
“Nahisi kuna mengi unanificha,” alisema Winfrida huku akimwangalia Godwin.
“Hakuna. Umejua mengi kuhusu familia yangu, wazazi wangu na kila mtu niliyewahi kuwa naye, hutakiwi kuhofia lolote lile,” alisema Godwin huku akimwangalia mke wake huyo.
“Kwa hiyo unajua mahali kaburi la mama yako lilipo?”
“Ninafahamu! Nitakwenda nawe siku yoyote ile, nilitamani sana katika maisha haya niwe na Irene, dada yangu niliyempenda kwa moyo wote. Hakika hakustahili kufa, alikuwa mdogo mno,” alisema Godwin huku akimwangalia mke wake machoni, alionekana kuumizwa sana na kile alichokuwa akimwambia.
Siku iliyofuata, wakaondoka na kuelekea makaburini, ilipita miaka mingi pasipo kuona makaburi hayo, moyo wake ulimuuma mno alipoyaona kwa mara ya pili. Aliyaangalia huku kumbukumbu zake zikirudi nyuma kabisa tangu walipotoka nchini Marekani baada ya kifo cha baba yake aliyekufa katika ajali ya kupangwa.
Kilichofanyika ni kuwasiliana na mafundi kwa ajili ya kuyatengeneza makaburi hayo ili yawe ya kisasa na yasipotee kwani kwa jinsi yalivyokuwa kipindi hicho, muda wowote ule yasingeweza kuonekana tena.
Hakuacha kuwasiliana na Rais Kambili, yeye ndiye aliyemuweka mwanaume huyo katika madaraka japokuwa hawakuwahi kukaa pamoja na kuzungumza, mtu pekee ambaye kwa mara chache sana alikuwa akionana naye alikuwa Ojuku, walikuwa wakiyapanga mambo mengi na namna ya kuilinda nchi hii dhidi ya maadui ambao walikuwa wakitumia mitandao ya kijamii, barua pepe na hata kwa kutumia simu, alitaka kuhakikisha kila kitu kinakuwa salama mahali pote na ili kuwaongeza wataalamu wengine, akashauri wapelekwe vijana kwenda kusoma katika Chuo cha Waseda nchini Japan kwa ajili ya kusomea mafunzo ya kompyuta kwa miaka kadhaa ili hata kama kuna siku atakufa basi nchi iendelee kuwa salama kabisa katika masuala yote ya kompyuta.
Hakukuwa na kitu kilichoharibika, kila kitu kilikwenda kama kilivyotakiwa kwenda na baada ya mwaka mmoja, Godwin na mkewe wakafanikiwa kupata mtoto wa kike na kumpa jina la Irene kama kumbukumbu ya dada yake aliyeuawa miaka mingi iliyopita.
“Nitawapenda miaka yangu yote na nina hakika kwamba hakutokuwa na mtu yeyote atakayenitenganisha nanyi,” alisema Godwin huku akiwakumbatia wote kwa pamoja.

MWISHO.
Asante sana jackal,final tumefika mwisho
 
Naona imeisha, ilikuwa ni nzuri sana, sometime imetuliza machozi tukasahau kabisa kama ni hadithi lkn sometimes tumefurahi pia, ahsanteni kwa kutuletea hapa Jackal na Shunie. Hongera Erick kwa utunzi uliotukuka, huyo Godwin tunaomba umlete atufundishie mtu mmoja hivi but pole na msiba pia
Atufundishie nan mkuu namba yA godwin hii hapa 0625416321
 
Back
Top Bottom