Duka la miwani la macho

luangalila

JF-Expert Member
Jan 12, 2014
6,325
6,868
Wadau habari za jioni naulizia eti hapa DSM kuna duka gani wanauza miwani za macho yenye upungufu wa uwezo wa kuona .. maana kuna hospitali moja nilipimwa macho nikaambiwa niko na shida ila sasa miwani zao bei kali sanaaa
 
Hiyo gharama uliyoambiwa ni kiasi gani na kwa tatizo gani?, pia lazima ujue namba ya lens unayotakiwa kutumia.
Ni vyema aliyekupima ndio akuchongee na lens hapohapo maana za kununua pengine zinaweza zisifae kwa tatizo lako.
Wagonjwa wenzako tunachofanya huwa tunanunua frame mtaani unachagua unayotaka na ni bei rahisi hata buku 2 unapata, halafu ndio unaenda nayo kwa daktari wa macho akuchongee lens inayoweza kufit kwenye hiyo frame, hapo gharama huwa unakuwa nafuu sana, maana wao madaktari kinachopandisha gharama ni frame tu unakuta wanakuuzia laki 2, wakati ukienda na ya kwako uliyonunua kwa machinga gharama inakuwa eflu 30 tu mpaka 50.
 
Mkuu,nenda kariakoo,mtoro,kuna maduka ya miwan mengi sana pale.Ulizia miwani inayopita waya pembeni,achana na hyo ya 2000,3000.

Hizo ndio za bei rahisi,lakini zina ubora unaofaa.Bei ni kati ya 5000-10000.Baada ya hapo,tafuta wanapotengeneza miwani ya macho,unapachika lenzi


Lenzi,kama alivyosema mdau inategemea na tatizo,lakini haitozidi 40000,kwa namba kubwa,mfano -0.6
 
Mkuu,nenda kariakoo,mtoro,kuna maduka ya miwan mengi sana pale.Ulizia miwani inayopita waya pembeni,achana na hyo ya 2000,3000.

Hizo ndio za bei rahisi,lakini zina ubora unaofaa.Bei ni kati ya 5000-10000.Baada ya hapo,tafuta wanapotengeneza miwani ya macho,unapachika lenzi


Lenzi,kama alivyosema mdau inategemea na tatizo,lakini haitozidi 40000,kwa namba kubwa,mfano -0.6
nafikiri ulimaanisha -6.0
 
Back
Top Bottom