Duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere liliuza mafuta ya taa pekee au mafuta ya taa na Coca Cola?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,912
30,254
UBISHI MKUBWA: DUKA LA MAFUTA YA TAA LA MAMA MARIA LILIUZA MAFUTA YA TAA AU MAFUTA YA TAA NA COCA-COLA?

Pamekuwa na ubishi mkubwa kuhusu duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere katika moja ya mitandao ya kijamii kuhusu duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere.

Ubishi uko katika bidhaa.

Mama Maria duka lake aliuza mafuta ya taa peke yake au na bidhaa nyingine?

Chanzo ni makala ya Mama Maria kufikisha miaka 93.

Katika makala hiyo mwandishi aliandika kuwa Mama Maria alikuwa na duka la kuuza mafuta ya taa Magomeni.

Mimi nikaandika kueleza kuwa duka hili lilianza Mtaa wa Mchikichi na Livingstone mwaka wa 1955 wakati huo Mwalimu Nyerere akiishi na Abdul Sykes.

Nikaendelea na kueleza kuwa hilio duka likahamia nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu, Magomeni ambae alifungua tawi la TANU nyumbani kwake na akampatia sehemu Mama Maria kuweka duka lake la mafuta ya taa baada ya Mwalimu kuhamia Maduka Sita Magomeni.

Inaelekea wasomaji wengi hawakupoendezwa na historia hii na hapo ndipo mashambulizi dhidi yangu yakaanza.

Duka lilikuwa linauza mafuta ya taa peke yake au na Coca-Cola?

Sababu ya watu hawa kusema hivyo ni kuwa kuwa kulikuwa na bango linalotangaza soda hiyo katika picha niliyoweka.

Ubishi wa kuuza soda ulimalizika kiasi kwa mmoja wa jamaa zangu kuniletea taarifa kuwa duka la Mama Maria lilikuwa linauza pia na Coca-Cola na mtu aliyekuwa anapeleka soda hiyo hapo dukani anaitwa Amal Bafadhil.

Mashambulizi hayakuacha wako walioniita muongo nk. nk.

Nami nikawajibu kwa kusema kuwa mbona hili la soda na mafuta ya taa ni jambo dogo kwa nini hamuulizi Ali Msham alikuwa nani katika kupigania uhuru wa Tanganyika kiasi kwanza atoe nyumba yake kuwa tawi la TANU na kisha kutoa nafasi kwa Mama Maria kuweka duka lake la mafuta ya taa hapo kwake?

Nikawauliza kama wangependa kujua jina la kijana wa Ali Msham ambae yeye kila siku alikuwa akimsindikiza Mama Maria nyumbani kwake baada ya kufunga duka jioni Maghrib na kiza kishaingia?

Wakati huo kutoka Mtaa wa Jaribu kwenda Maduka Sita sehemu kubwa ilikuwa miembe na mikorosho hapakuwa na nyuma nyingi na taa za mtaani hakuna.

Niliuliza kama wangependa hata kujua historia ya mtoto huyu wa Ali Msham.

Wako kimya hadi leo.

Huyu mtoto wa Ali Msham jina lake ni Abdallah Omar Likonda sasa ni mzee lakini yu hai anaishi Mvuti, Chanika.

Abdallah Omar Likonda ana historia nzima ya nyakati zile.

Leo ni nimepita nyumbani kwa marehemu Ali Msham na kuangalia lilipokuwa duka la Mama Maria.

Nimepiga picha nyumba ambayo nimeelezwa imebadilka sana lakini walinionesha lilipokuwa duka la Mama Maria na wakanionyesha pia sehemu upande wa kulia wa nyumba ilipokuwa shule ya TAPA aliyofungua Ali Msham na upande wa kushoto kulipokuwa na nafasi kubwa ambayo ndipo TANU ilipokuwa ikifanya mikutano yake ya ndani.

Katikati ya hii nyumba mpaka leo bado iko fremu na ndipo lilipokuwa duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere.

323324850_682481950238140_8963938120987024443_n.jpg

321103413_2158080364383105_9080886621585898165_n.jpg
323340159_1098307150840592_2738467061108790416_n.jpg
324180829_855493975655940_7703644358626602109_n.jpg
 
Mzee wangu natamani sana siku moja tuonane nikupatie kipooza koo kidogo upate kunitembeza maeneo yote yenye historia ya TANU na uhuru wetu ndani ya jiji la Dar es Salaam.
 
Unajua kwanini wapo kimya mzee wangu!!!Kuna kitu hakipo sawa ungewaauliza kwanini wapo kimya?????Moja ya sifa ya msomi ni kuuliza!!!
Nelson...
Wako kimya kwa historia ya Ali Msham na yanayomuhusu Ali Msham.
Historia hizi za wazalendo kama Ali Msham zinawatisha.

Nadhani umesoma hapa nimeeleza jinsi gazeti la Africa Events (1988) lilivyo kusanywa lote na kutolewa kwenye mzunguko kwa kuwa lilikuwa limechapa makala yangu iliyokuwa imemtaja Abdul Sykes na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika historia ya kudai uhuru.

Kimya hiki kinasababishwa na hofu ya kusikia mengi katika historia ya TANU kutoka watu kama Ali Msham.
 
Nelson...
Wako kimya kwa historia ya Ali Msham na yanayomuhusu Ali Msham.
Historia hizi za wazalendo kama Ali Msham zinawatisha.

Nadhani umesoma hapa nimeeleza jinsi gazeti la Africa Events (1988) lilivyo kusanywa lote na kutolewa kwenye mzunguko kwa kuwa lilikuwa limechapa makala yangu iliyokuwa imemtaja Abdul Sykes na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika historia ya kudai uhuru.

Kimya hiki kinasababishwa na hofu ya kusikia mengi katika historia ya TANU kutoka watu kama Ali Msham.
Hapana kuna sababu kwanini wapo kimya!!!Kuna kitu hakipo sawa ndio maana wapo kimya!!!Ukiona wasomi wapo kimya sisi wachambuzi huwa tunapata mawazo mtambuko mzee wangu
 
UBISHI MKUBWA: DUKA LA MAFUTA YA TAA LA MAMA MARIA LILIUZA MAFUTA YA TAA AU MAFUTA YA TAA NA COCA-COLA?
Pamekuwa na ubishi mkubwa kuhusu duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere katika moja ya mitandao ya kijamii kuhusu duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere.

Ubishi uko katika bidhaa.

Mama Maria duka lake aliuza mafuta ya taa peke yake au na bidhaa nyingine?

Chanzo ni makala ya Mama Maria kufikisha miaka 93.

Katika makala hiyo mwandishi aliandika kuwa Mama Maria alikuwa na duka la kuuza mafuta ya taa Magomeni.

Mimi nikaandika kueleza kuwa duka hili lilianza Mtaa wa Mchikichi na Livingstone mwaka wa 1955 wakati huo Mwalimu Nyerere akiishi na Abdul Sykes.

Nikaendelea na kueleza kuwa hilio duka likahamia nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu, Magomeni ambae alifungua tawi la TANU nyumbani kwake na akampatia sehemu Mama Maria kuweka duka lake la mafuta ya taa baada ya Mwalimu kuhamia Maduka Sita Magomeni.

Inaelekea wasomaji wengi hawakupoendezwa na historia hii na hapo ndipo mashambulizi dhidi yangu yakaanza.

Duka lilikuwa linauza mafuta ya taa peke yake au na Coca-Cola?

Sababu ya watu hawa kusema hivyo ni kuwa kuwa kulikuwa na bango linalotangaza soda hiyo katika picha niliyoweka.

Ubishi wa kuuza soda ulimalizika kiasi kwa mmoja wa jamaa zangu kuniletea taarifa kuwa duka la Mama Maria lilikuwa linauza pia na Coca-Cola na mtu aliyekuwa anapeleka soda hiyo hapo dukani anaitwa Amal Bafadhil.

Mashambulizi hayakuacha wako walioniita muongo nk. nk.

Nami nikawajibu kwa kusema kuwa mbona hili la soda na mafuta ya taa ni jambo dogo kwa nini hamuulizi Ali Msham alikuwa nani katika kupigania uhuru wa Tanganyika kiasi kwanza atoe nyumba yake kuwa tawi la TANU na kisha kutoa nafasi kwa Mama Maria kuweka duka lake la mafuta ya taa hapo kwake?

Nikawauliza kama wangependa kujua jina la kijana wa Ali Msham ambae yeye kila siku alikuwa akimsindikiza Mama Maria nyumbani kwake baada ya kufunga duka jioni Maghrib na kiza kishaingia?

Wakati huo kutoka Mtaa wa Jaribu kwenda Maduka Sita sehemu kubwa ilikuwa miembe na mikorosho hapakuwa na nyuma nyingi na taa za mtaani hakuna.

Niliuliza kama wangependa hata kujua historia ya mtoto huyu wa Ali Msham.

Wako kimya hadi leo.

Huyu mtoto wa Ali Msham jina lake ni Abdallah Omar Likonda sasa ni mzee lakini yu hai anaishi Mvuti, Chanika.

Abdallah Omar Likonda ana historia nzima ya nyakati zile.

Leo ni nimepita nyumbani kwa marehemu Ali Msham na kuangalia lilipokuwa duka la Mama Maria.

Nimepiga picha nyumba ambayo nimeelezwa imebadilka sana lakini walinionesha lilipokuwa duka la Mama Maria na wakanionyesha pia sehemu upande wa kulia wa nyumba ilipokuwa shule ya TAPA aliyofungua Ali Msham na upande wa kushoto kulipokuwa na nafasi kubwa ambayo ndipo TANU ilipokuwa ikifanya mikutano yake ya ndani.

Katikati ya hii nyumba mpaka leo bado iko fremu na ndipo lilipokuwa duka la mafuta ya taa la Mama Maria Nyerere.

323324850_682481950238140_8963938120987024443_n.jpg

321103413_2158080364383105_9080886621585898165_n.jpg
323340159_1098307150840592_2738467061108790416_n.jpg
324180829_855493975655940_7703644358626602109_n.jpg
Nakukubali sana ingawa enzi zenu. Sikuwepo ila nafatilia sanahbr zako ingawa unamkubali Sana Abdul Sykes kuliko Nyerere

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Usiogope ubishano , wengi humu ni vijana sana hivyo hayo mambo hawayajui.

Mama Maria hakuwa na nguvu kwenye amsha amsha za uhuru, pengine mwalimu hakutaka.

Na vile walisema kuhusu bad food hivi hili lina ukweli wowote ?

Ile nyumba ya Mwalimu ya magomeni hivi ipo? Inafanyiwa nini sasa.
 
Mzee wangu una mambo mengi ya kuongea sema ni vile tu hakuna utulivu. Ningekuwa nipo Dar es Salaam ningekuja kuchota historia fulani fulani kutoka kwako.
 
Afu utakuta kuna mtoto wa mwaka 90 anabishana na huyu mzee na kumtukana kabisa.....wasamehewe
 
Hapana kuna sababu kwanini wapo kimya!!!Kuna kitu hakipo sawa ndio maana wapo kimya!!!Ukiona wasomi wapo kimya sisi wachambuzi huwa tunapata mawazo mtambuko mzee wangu
Nelson...
Kughitilafiana ni silka yetu binadamu.

Mimi nimekueleza ninayoyajua tena mimi mwenyewe nikiwa muhusika kuwa makala yangu katika Africa Events mwaka wa 1988 ilizuiwa watu wasiisome gazeti likakusanywa.

Inasemekana yalichomwa moto yote.
Nawe umenijibu kama ulivyoona katika fikra zako.

Hakuna neno.
Wasomaji ndiyo waamuzi.

1673118599392.jpeg
 
Back
Top Bottom