Wanajamii hii imekaaje ndani ya JWTZ?

nditolo

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
3,609
4,096
Je, suala la ajira kwa wataalamu hasa wa afya (matibabu) ikoje ndani ya jeshi letu, mpaka inafikia kuwa na wataalamu wachache mno, hali ambayo inapelekea taifa kupoteza pesa nyingi kwa ajili ya kutibu wanasiasa na viongozi wa ngazi za juu nje ya nchi.

Ni muda mrefu JWTZ imekuwa ikitangaza ajira na kutaja vivutio mbalimbali ikiwa ni pamoja na marupurupu but still haina madaktari (MD's) na wanasayansi wa tiba (BSc. health laboratory) wakutosha ambao wanaweza kuifanya Lugalo iwe refferal hospital. Samahani naomba tujadili kidogo kwamba ni kitu gani kinaifanya JWTZ isiweze kusomesha au kuajiri watalamu hao muhimu kwa Taifa, kwa miaka zaidi ya 47 tangu kuanzishwa kwake?

1. Je ni ukiritimba wa viongozi ndani ya jeshi hilo unaofanya wataalamu hao wazalendo wasiweze kuvumilia kufanyakazi na hivyo kuacha.

2. Au ni ukosefu wa ubunifu wa mipango madhubuti ya kuifanya sekta ya afya ndani ya jeshi kuboreshwa.

3. Je ni siasa zinaharibu mipango ya jeshi kutokana na kwamba zamani chama kilishika hatamu na hivyo kifanya JWTZ kuongozwa kisiasa zaidi kuliko taratibu za jeshi.

4. Inasememekana JWTZ ina MD's wasiozidi 20 na BSc. laboratory scienticit chini ya 3 tu, je serikali inalichukuliaje hili au haina taarifa?

Najua watu wengi wanakumbuka mgomo wa Muhimbili mwaka 2005, ilikuwa ni kiama walipopelekwa hawa jamaa, bank ya damu iliisha sababu wengi Muhimbili haikuwa kaliba yao na hivyo watu kupoteza maisha sana.
Je hii imekaaje tulinusuru taifa? Tutapona kweli kama huko kuko hivyo?
 
Ndugu yangu nataka nikuelezee ukweli kuhusu swali lako, sio kweli kama Lugalo ina Waganga chini ya 20, u kweli no kwamba inayo wasomi lakini wengi wako maofisini na sio hospitali. Umeshaenda makao makuu pale upanga ukaangalia elimu za hap watu. Au kule posta kwenye ile ofisi yao? JWTZ ni nzuri kuliko unavyodhani kwani huwa inawapeleka wataalamu wake nje ya nchi kusoma. Tatizo linakuja kwenye kutafuta wataalamu wengi wao wanashindwa kihitimu Yale mafunzo ya miezi sita (depo) kwasababu wanakuwa legelege.Tatizo lililopo JWTZ ni kwamba watu wengi wanawapeleka watoto wao ndio maana unakuta akina mwita,marwa n.k wako wengi.
 
kwa sasa hakuna taasisi ya serikali ambayo iko ''serious'' hata kidogo!, mpaka ikulu ni bora liende!
 
Back
Top Bottom