Duh siku ya wapendanao hiyooo inabisha hodi

Quemu

JF-Expert Member
Jun 27, 2007
984
127
Hii siku huwaga inanitoa nishai sana. Kwa sababu huwa inakuja just before payday. kwa wale wenye akaunti zinazotuna terehe 15 na siku ya mwisho wa mwezi wanaelewa nina maana gani.

Inanitoa nishai kwa sababu huwa inakuja wakati mifuko imetoboka vibaya mno. Na mamsapu huwa atulii mpaka apate maua ya roza, dina, kadi na kazawadi kadogo. Yani huwa hata haelewi nikimwambia kuwa mwenzio sina ngawira hata chembe.

Kwa mahesabu ya haraka haraka, yani inabidi niwe na kama kiasi hiki ili niweze kuipitisha siku ya valentina nimelala kitandani, badala ya kwenye kochi.
1) Maua ya roza - $80
2) Dina - $50
3) Kadi - $5
4) Zawadi - $100
Total = $235. Yes, mamsapu wangu huwa anaweka kiwango cha kuspendi nae. Haya ndio matatizo ya kutulia na sistaduu...gademu!

Sasa hebu nishaurini, kwa mfuko uliotoboka, ni vipi nitaweza kufanikisha hii siku ipite murua?......Na siku hizi hata hot-check huwezi andika tena. Zamani ulikuwa unaweza kwenda agalau Wal-Mart na kuandika check wakati unajua hauna hela kwenye akaunti. Mambo yalikuwa yanajipa mbele kwa mbele. Lakini siku hizi hata Wal-Mart wana sisitimu ambayo ina access akaunti yako kucheki kama kuna ngawira kabla hujaanza mbele na bidhaa. Na haya mambo ya Payday Advances yamekuwa magumu kweli kweli siku hizi. Mpaka wampigie simu bosi wako ndio wakupe ki $200 chao. Na bosi ni mbeya kishenzi...haitachukua masaa 2 kabla dipatimenti mzima haijajua yaliyojiri kwenye ulimwengu wa mfuko wako. Na kwa bahati mbaya au mzuri, tumejazana wabongo kinoma kwenye warehouse ninayopiga mzigo (si unajua tena mambo ya kupiga boksi). Sasa hebu niambie hizi habari zikifika masikioni mwa wabongo, sijui nitajificha wapi...maana ndani ya masaa 2 zitakuwa zimebandikwa kwa Michuzi.. Duh jamani!!!

Anewei, sasa nifanyeje? Hivi kwani ni lazima yawe maua ya rozi? Hivi ni vipi nikimpatia maua ya saa nne? Unajua kwanza wakidada huwa hawafikirii vizuri. Maua ya saa nne pengine ni romantiki zaidi ya maua ya roza. Maua ya rosa yanachanua pale mwanzo mwanzo tu, kesho yake yanaanza kufifia. Lakini maua ya saa nne huwa yanachanua kila siku saa nne....kila siku saa nne huwa yana kuwa "mwarumwaru."...hebu niambie kuna kitu romantiki kama kile chenye uhakika wa kutabasamu kila siku...tena muda ule ule. yani huna hata haja ya kuwa na wasiwasi wa kujua ni saa ngapi yata chanua.

Gademu!!!
 
1) Maua ya roza - $80
2) Dina - $50
3) Kadi - $5
4) Zawadi - $100
Total = $235.
QUOTE]

In Bongo below would be your budget na if you actually treated a lady in Bongo to this type of expense during valentine, hawezi kukunyima kitu. manake this is would be an out-of-this-world experience!
1) Maua - $15
2) Dinner - $30 (top restaurant)
3) Kadi - $3
4) Zawadi - $20
Total = $68
 
In Bongo below would be your budget na if you actually treated a lady in Bongo to this type of expense during valentine, hawezi kukunyima kitu. manake this is would be an out-of-this-world experience!
1) Maua - $15
2) Dinner - $30 (top restaurant)
3) Kadi - $3
4) Zawadi - $20
Total = $68

Really? Guess I should know better. Lakini mbona huyu kidenishi wangu wa huku ni mbongo nae. Sasa kwanini ananichorea mstari wa gharama za juu? Nilifikiri kwa kuwa sote tu wabongo, pengine tungeishi kibongo bongo huku ughaibuni? It's not fair...
 
Aisee its better maandalizi yakaanza mapema kwa wale wenye wandani wao. Ila Siku hii ni dedication kwa Mhe. Geoff ambaye atakuwa ukoooooooo mkoani,
 
Really? Guess I should know better. Lakini mbona huyu kidenishi wangu wa huku ni mbongo nae. Sasa kwanini ananichorea mstari wa gharama za juu? Nilifikiri kwa kuwa sote tu wabongo, pengine tungeishi kibongo bongo huku ughaibuni? It's not fair...

Mkuu hapo binti anaufuata vyema msemo wa ukienda Roma ishi kama waroma. Hehe!
 
Aaagh mwambie aelewe hali yako ya kipato bwana, kama mnapendana kweli deeply basi kila siku kwenu ni valentine.,aache ulimbukeni, kama siku hiyo hautakuwa poa basi utamtoa siku nyingine ukiwa fresh, sidhani kama itaharibu mapenzi yenu, otherwise kila la kheri katika ubebaji mabox nadhani ushakuwa bonge la baunsa sasa.
 
In Bongo below would be your budget na if you actually treated a lady in Bongo to this type of expense during valentine, hawezi kukunyima kitu. manake this is would be an out-of-this-world experience!
1) Maua - $15
2) Dinner - $30 (top restaurant)
3) Kadi - $3
4) Zawadi - $20
Total = $68[/QUOTE]

yani mkuu tena hapo ni wale wa uzunguni wauswazi ata nusu inaweza isifike bongo raha bana
1)maua- unachuma katawi (free)
2)dinner -$5 chips kuku
3)kadi-$ 0.99
4)zawadi- $10 kama ukimega
 
Pole....ila hayo yote umejitakia mwenyewe. Ungekuwa singo wala usingesumbuka. Ungepiga boksi lako au kuendesha fokolifta na mamumivu ya ukapa ungeyasikilizia mwenywe tu.

Mimi sijanunua hayo maua ya waridi tokea sijui lini na hata sijui yanapatikana wapi. Msomeshe tu mama watoto na atakuelewa. Si mlikubaliana kuwa wote katika shida na raha bana...sasa kwa nini alete za kuleta?
 
yani mkuu tena hapo ni wale wa uzunguni wauswazi ata nusu inaweza isifike bongo raha bana
1)maua- unachuma katawi (free)
2)dinner -$5 chips kuku
3)kadi-$ 0.99
4)zawadi- $10 kama ukimega

Nimeipenda sana hii, lakini umesahau kuongeza outing ya kwenda kucheki muvi ya Kanumba kwenye kibanda $ 0.20
 
Pole....ila hayo yote umejitakia mwenyewe. Ungekuwa singo wala usingesumbuka. Ungepiga boksi lako au kuendesha fokolifta na mamumivu ya ukapa ungeyasikilizia mwenywe tu.

Mimi sijanunua hayo maua ya waridi tokea sijui lini na hata sijui yanapatikana wapi. Msomeshe tu mama watoto na atakuelewa. Si mlikubaliana kuwa wote katika shida na raha bana...sasa kwa nini alete za kuleta?
Mkuu wewe ukija kujua utanunua kila siku kwanza hadi meusi, kwahiyo subiria wakti wako tu unakuja
 
Ah mambo ya kuiga haya unapeleka maua mwenzio anataka cash kesho unayakuta kwenye dust bin
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom