Dubai ni moja ya sehemu inayoendelea kwa kasi kubwa. Cha kupendezesha ni kwamba jamaa wameamua kutumia mali ya asili waliyonayo, kama vile mafuta, kuendeleza nchi yao. Mainvesta kutoka sehemu zote za dunia wanawekeza pale. Tanzania nasi tunaweza kufanya kama Dubai kama tunataka, kwani tuna kila kitu. Hata hivyo, inatubidi tuanze sasa kabla ya vitu vilivyobaki kuuzwa kwa wajanja. Naona kwa kuanzia, Gorv ijenge barabara zote zinazounganisha wilaya kwa wilaya kwa kiwango cha lami. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana. Kisha, tuache kutumia jembe la mkono na badala yake tujenge utaratibu wa kutumia matrekta katika kilimo, kuvuna, na kuwa na wakulima wachache sana. Pia, tunaweza kuanzisha viwanda vipya ambavyo tutazalisha mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. Elimu pia iongezewe nguvu zaidi ili kila mtoto apate elimu. Kwa kufanya hivyo, basi tutakuwa tunakwenda na mageuzi kama ya Dubai, India, na China.