Dubai ni Mfano wa Kuigwa: Jifunze Kutumia Mali ya Asili na Kuwekeza kama Wenzetu

houseboy

Member
Jul 22, 2007
39
3
Dubai ni moja ya sehemu inayoendelea kwa kasi kubwa. Cha kupendezesha ni kwamba jamaa wameamua kutumia mali ya asili waliyonayo, kama vile mafuta, kuendeleza nchi yao. Mainvesta kutoka sehemu zote za dunia wanawekeza pale. Tanzania nasi tunaweza kufanya kama Dubai kama tunataka, kwani tuna kila kitu. Hata hivyo, inatubidi tuanze sasa kabla ya vitu vilivyobaki kuuzwa kwa wajanja. Naona kwa kuanzia, Gorv ijenge barabara zote zinazounganisha wilaya kwa wilaya kwa kiwango cha lami. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana. Kisha, tuache kutumia jembe la mkono na badala yake tujenge utaratibu wa kutumia matrekta katika kilimo, kuvuna, na kuwa na wakulima wachache sana. Pia, tunaweza kuanzisha viwanda vipya ambavyo tutazalisha mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. Elimu pia iongezewe nguvu zaidi ili kila mtoto apate elimu. Kwa kufanya hivyo, basi tutakuwa tunakwenda na mageuzi kama ya Dubai, India, na China.
 
What's new???????

Ingekuwa better ukaanza kutaja tatizo ni nini linalotukabili bongo kwani uliyoyataja ni theory lakini application yake ndo muhimu zaidi ambayo lazima ufanye reflection kwenye tatizo linalotukabili.
 
Dubai bi moja sehemu inayoendelea kwa kasi kubwa,cha kupendezesha jamaa wameamua kutumia mali ya asili waliyonayo mafuta kuendeleza nchi yao mainvesta kutoka sehemu zote za dunia wanawekeza pale,Tanzania nasi tunaweza kufanya kama Dubai kama tunataka kwani tuna kila kitu,ila inatubidi tuanze sasa kabla ya vitu vilivyobaki kuuzwa kwa wajanja.naona kwa kuanzia Gorv ijenge barabara zote zinazounganisha wilaya kwa wilaya kwa kiwango cha lami,kwa kufanya ivyo tutakuwa tumepiga atua kubwa sana kisha kuacha kutumia jembe la mkono na kutumia matrekta katika kilimo,kuvuna na tuwe na wakulima wachache sana,pia kuanzisha viwanda vipya,ambavyo tutazalisha maitaji ya soko la ndani na nje ya bongo,pia elimu iongezewe nguvu zaidi na kila mtoto apate elimu kwa kufanya hivyo basi tutakuwa tunakwenda na mageuzi kama ya Dubai,India na China.

Dubai waliweka wawekezaji kama Tanzania. Lakini pesa walizopata walizitumia kama mitaji ya kufungua biashara zingine kwa sababu walijua rasimali zao zitakwisha.

Watanzania mkipata kidogo, mnaacha kufanya kazi. Mnataka pesa zisomeshe watu bure, viongozi wajirushe na Ma-prado na mikutano isiyokwisha.
 
Hata Mobutu aliwaambia Zaire 'nchi yenu tajiri sana hivyo tusherekee!' Wakaanza kucheza ndombolo ya solo kusherekea hadi leo! Wengine (Unganda, Rwanda na Ujelgigi) ndo wanachangamkia madini DRC hadi leo!
Belive me - ndo maana mziki wa Kizaire ukapata charti sana wakati wa Mobutu! Sijua kama bado wanasherekea hadi leo au sasa wameamaka!
 
Hata Mobutu aliwaambia Zaire 'nchi yenu tajiri sana hivyo tusherekee!' Wakaanza kucheza ndombolo ya solo kusherekea hadi leo! Wengine (Unganda, Rwanda na Ujelgigi) ndo wanachangamkia madini DRC hadi leo!
Belive me - ndo maana mziki wa Kizaire ukapata charti sana wakati wa Mobutu! Sijua kama bado wanasherekea hadi leo au sasa wameamaka!

Old Habit Die Hard. Wakati DRC wako kwenye muziki sisi tupo kwenye siasa.

Unajua idadi ya vyuo vya siasa Tanzania ilizidi idadi ya vyuo vikuu. Wakati nchi nzima ina chuo kimoja kikuu (UDSM), kila mkoa ulikuwa una zaidi ya chuo kimoja cha mafunzo ya siasa.

Kupata kadi ya CCM uliitaji mafunzo ya miezi sita na baadaye kupunguza miezi mitatu.
 
What's new???????

Ingekuwa better ukaanza kutaja tatizo ni nini linalotukabili bongo kwani uliyoyataja ni theory lakini application yake ndo muhimu zaidi ambayo lazima ufanye reflection kwenye tatizo linalotukabili.

Ukitaka kuona mawazo ya watanzania angalia wanavyoendesha Simba na Yanga. Maana ya ligi ni kupata ushindi wa kikombe na sio Yanga kumshinda Simba au Simba kumshinda Yanga.

Viongozi wa Yanga wanataka milioni 40 za kamati ya ufundi wa kuishinda Simba (40 millioni). Wangetumia pesa hizo kwa ajili ya malipo ya wachezaji wangepata wachezaji wazuri wa kushinda ubingwa.

Matatizo yanayotukabili yanajulikana lakini tunategemea sana miujiza na kamati za ufundi.
 
Mipango ya kuikuza kiuchumi Emirates haikuanza leo! Bahati nzuri, wenzetu waliweza ku-negotiate bei nzuri kwa raslimali waliyonayo! Na kama haitoshi, wakawatumia Wazungu haohao kuleta maendeleo! Si kwamba wao hawakula rushwa [kama mnamfahamu Adnan Khashoggi], bali walipenda nchi yao pia! Ndio maana wakaiendeleza pamoja na rushwa yote waliyokula toka kwa Marekani na Uingereza et al. Vitu vya muhimu walivyofanya ni kuendeleza miundo mbinu, kupanga miji [Abu Dhabi ni mfano], huduma za afya, elimu, na uwekezaji kwenye nyanja ambazo hazihusiani na mafuta! Tatizo letu Waswahili ni kutofuata dira tulizojiwekea au kuzitekeleza kwa pupa!

Angalia tunavyopiga kelele kila siku kwamba kilimo ni uti wa mgongo [uti wa mgongo my foot!] Halafu, je? Ardhi yetu ina thamani? [Huwezi kuwa na maendeleo ya kilimo kama ardhi haina thamani, nenda benki utajijua!] Je? Tunapiga hatua gani kwenye kuthaminisha ardhi! Jengine ni uwekezaji, kwetu iwe ni kilimo, je? Tuna commercial farmers wangapi? Tuache story za Zimbabwe, hata Mswahili aweza kuwa! Sasa, tunao wangapi?

Je? Tunafikiri kwamba kilimo cha peasant kitatufikisha kwenye mapinduzi ya kilimo? Au tunajidanganya! Unajua, nchi hii wakulima [sio wakwangua ardhi!] kumi tu waliogawanywa kati ya nyanda za juu kusini, jimbo la kati na kaskazini wanatosha kulisha nchi miaka nenda rudi? Sasa, tunapoongelea kuwa kama Dubai, japo kwa mbali, lazima tuyaone hayo na mengine mengi! Simply put, hatuna viongozi wa kutosha kutufikisha hapo, kwa sasa!
 
..mipango ya kuikuza kiuchumi emirates haikuanza leo!

..bahati nzuri wenzetu waliweza ku-negotiate bei nzuri kwa raslimali waliyonayo!na kama haitoshi wakawatumia wazungu haohao kuleta maendeleo!

..si kwamba wao hawakula rushwa[kama mnamfahamu adnan kashoggi]bali walipenda nchi yao pia!ndio maana wakaiendeleza pamoja na rushwa yote waliyokula toka kwa marekani na uingereza et al.

..vitu vya muhimu walivyofanya ni kuendeleza miundo mbinu,kupanga miji[abu dhabi ni mfano],huduma za afya,elimu,na uwekezaji kwenye nyanja ambazo hazihusiani na mafuta!

..tatizo letu waswahili ni kutofuata dira tulizojiwekea au kuzitekeleza kwa pupa!angalia tunavyopiga kelele kila siku kwamba kilimo ni uti wa mgongo[uti wa mgongo my foot!]halafu,je?ardhi yetu ina thamani?[huwezi kuwa na maendeleo ya kilimo kama ardhi haina thamani,nenda benki utajijua!]je?tumepiga hatua gani kwenye kuthaminisha ardhi!

..jengine ni uwekezaji,kwetu iwe ni kilimo,je?tuna commercial farmers wangapi?tuache story za zimbabwe,hata mswahili aweza kuwa!sasa,tunao wangapi?je?tunafikiri kwamba kilimo cha peasant kitatufikisha kwenye mapinduzi ya kilimo?au tunajidanganya!unajua,nchi hii wakulima[sio wakwangua ardhi!] kumi tu waliogawanywa kati ya nyanda za juu kusini,jimbo la kati na kaskazini wanatosha kulisha nchi miaka nenda rudi?

..sasa,tunapoongelea kuwa kama dubai,japo kwa mbali,lazima tuyaone hayo na mengine mengi!

..simply put,hatuna viongozi wa kutosha kutufikisha hapo,kwasasa!


Dira waliyofuata ni Pure Capitalism. Unatumia mtaji kutafuta mtaji.

Tanzania hata kama tungepata mtaji mkubwa bado tungeboronga. Dira ya UJAMAA haifikishi nchi popote. Hivyo usiseme tulikuwa na dira na hatukuzifuata. Hakuna uwezekano wa kufuata UJAMAA.
 
Haya mambo ya kusema tuige kwa fulani na fulani hayana mpango. Wakati mwingine tunalazimisha mazingira ya nchi tunayotaka tuige yawe sawa na ya Tz. Tunajidanganya.

Wengine wanasema tuige Japan, wengine China, wengine Singapole. Upumbavu! Mbona hatusikii wakisema tuige nchi iliyo katika bara la Africa. Kwanini?...hivi si ingekuwa rahisi kama tungeshauriwa tuige kutoka kwenye nchi zeneye mazingira yanayofanana kwa asilimia kubwa?

Maendeleo ya nchi ni taswira ya wananchi wake, mazingira yake, tamaduni zake, mazingira ya nchi zinazoizunguka,historia yake nk. Tunaposema tuige Japan au Dubai tunadharau umuhimu wa mambo haya katika maendeleo. Tulazimisha gogo linaloelea habarini liwe mamba ati tu kwasababu limekuwa likielea sambamba na mamba kwa miaka nenda rudi. Benki ya dunia wamejaribu kulazimisha nchi za Africa ziige Asian Tigers wameshindwa na badala yake wamejikuta wakizitumbukiza nchi za Afrika kwenye madeni yakunuka.

Aliyesema IGA UFE hajakosea, mana kuiga siasa za uchumi na miundombinu kutoka kwenye nchi zeneye tamaduni, historia, na mazingira tofauti kuna athari zisizolipika.
 
At least watu wanajaribu hata kusema tuige. Lakini kama watu wa pwanai wanavyosema ussige kunya kwa Tembo. Lakini kuna mengi ambayo yanaweza kufanyika Tanzania, hayafanyiki. Kuna mengi ambayo yako ndani ya uwezo wetu tunayotakiwa kufanya lakini hayafanyiki, swali lingekuwa ni kwanini hatufanyi hivyo.
Kama ni Kuiga nisingesema tuige Malaysia, Marekani, China, Dubai au Singapore. Ningependa tuanze kuiga Kenya, tukiona tuko step ahead ndio tungeanza Afrika Kusini, and so on.....................
 
Dira waliyofuata ni Pure Capitalism. Unatumia mtaji kutafuta mtaji.

Tanzania hata kama tungepata mtaji mkubwa bado tungeboronga. Dira ya UJAMAA haifikishi nchi popote. Hivyo usiseme tulikuwa na dira na hatukuzifuata. Hakuna uwezekano wa kufuata UJAMAA.

..Niliposema dira, sikuongelea Ujamaa! Na hata huo Ujamaa ulikuwa na mazuri yake! Muulize Maryam alisomaje, na kama unamfahamu Babayo, muulize pia! [Ya baba na mama, no pun intended]

..Nchi hii ina dira kadhaa, zinazohusu sekta kadhaa na nchi kwa ujumla! Ndicho maana nikaongelea kilimo hapo juu!

..JK ni typical Tanzanian! Ahadi nyingi, utekeleza kidogo tena hurriedly!

..Nasema hivi, dira zipo, zilikuwapo, tena nzuri, tatizo hatuzifanyi kwa matendo, zipo kwenye nyaraka tu! Seek and you shall see!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom