mcfm40
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,452
- 3,150
Kuna vilio kila mahali na dua mbaya kuelekea kwa rais Magufuli na serikali yake hali ambayo sasa inaogopesha! Kila ukifungua mtandao wa kijamii utakutana na malalamiko, dua na laana zikuelekezwa kwa Magufuli na serikali yake.
Hata wale waliokua wanamuunga mkono sasa wamemgeuka na kushangaa anayofanya.
Wengi wanamlaumu kwa uonevu na kutumia dola vibaya kukandamiza haki za raia.
Kumkosoa rais na serikali yake sssa kunaonekana ni kumtusi na uchochezi.
Kwa sasa watu wapo katika hofu kubwa. Hujui ni wakati gani ukikosoa au kutoa maoni yako juu ya utawala huu utaitwa
mchochezi au umemtusi rais.
Kwa mfano nikisema namchukia rais Magufuli nitaambiwa nimetoa lugha ya uchochezi. Yaani sio maoni yangu binafsi bali etu ni uchochezi.
Serikali hii ina hofu kubwa. Sijui ni kwa nini? Labda wamegundua kwamba waliyoahidi wananchi ni vigumu kutekelezeka hivyo wanazuia wakosoaji wasiseme? Hofu kuu iliyonayo serikali hii dhidi ya wakosoaji wake inafanya wajikute wanajihami hata kwa mambo madogomadogo yasiyokuwa na msingi! Mambo ambayo yanafanya kila mwenye akili timamu ashangae! Kuna nini?
Hii model ya utawala anayoijaribu Magufuli hapa nchini haitafanikiwa. Tanzania sio Rwanda wala North Korea. Tanzania kwa miaka mingi tumezoea uhuru wa kukosoana na kupingana bila kupigana.
Sasa naona huu utamaduni mzuri unaminywa. Nimekuwa najiuliza hivi kile kikosi kazi alichounda Mh Magufuli wakati wa kampeni kumshauri namna ya kufanya mabadiliko makubwa katika nchi ndiyo haya wsliyomshauri?
Hivi ni kweli tutasonga mbele kimaendeleo huku kukiwa nacauti nyingi namna hii zikiulaumu utawala wa nchi hii. Natumia neno 'utawala' kwa makusudi kwa sababu hii awamu ya tano inatawala badala ya kuongoza! Yaani nchi inaendeshwa kikoloni zaidi.
Nimalizie kwa kuulizs tena swali, je, ni kweli rais ataweza kufanikiwa kutekeleza mipango yake ya maendeleo huku akipingwa na kulaaniwa vikali hivi na wananchi wake? Rais aliyejipambanua kama mcha Mungu, akionekana kwenye nyumba za ibada kila siku, leo analaaniwa na kuombewa dua mbaya hivi?
Ni wakati muafaka kwa rais na serikali yake kujitafakari upya namna ya kuileta nchi pamoja na kuattract zaidi support kutoka kwa wananchi badala ya kufanya mambo yanayochochea chuki dhidi ya serikali na kuwagawa watanzania!
Hii mambo ya kuminya uhuru wa maoni na taarifa hayajawahi kusaidia nchi yoyote kusonga mbele. Demokrasia na maendeleo ni vitu pacha. Vinakwenda pamoja. Demokrasia huleta maendeleo na maendeleo huleta demokrasia! Maendeleo ya kweli ni maendeleo ya watu sio maendeleo ya vitu. Na bila uhuru na demokrasia hakuna maendeleo ya watu!
Mwenye masikio na asikie!
Hata wale waliokua wanamuunga mkono sasa wamemgeuka na kushangaa anayofanya.
Wengi wanamlaumu kwa uonevu na kutumia dola vibaya kukandamiza haki za raia.
Kumkosoa rais na serikali yake sssa kunaonekana ni kumtusi na uchochezi.
Kwa sasa watu wapo katika hofu kubwa. Hujui ni wakati gani ukikosoa au kutoa maoni yako juu ya utawala huu utaitwa
mchochezi au umemtusi rais.
Kwa mfano nikisema namchukia rais Magufuli nitaambiwa nimetoa lugha ya uchochezi. Yaani sio maoni yangu binafsi bali etu ni uchochezi.
Serikali hii ina hofu kubwa. Sijui ni kwa nini? Labda wamegundua kwamba waliyoahidi wananchi ni vigumu kutekelezeka hivyo wanazuia wakosoaji wasiseme? Hofu kuu iliyonayo serikali hii dhidi ya wakosoaji wake inafanya wajikute wanajihami hata kwa mambo madogomadogo yasiyokuwa na msingi! Mambo ambayo yanafanya kila mwenye akili timamu ashangae! Kuna nini?
Hii model ya utawala anayoijaribu Magufuli hapa nchini haitafanikiwa. Tanzania sio Rwanda wala North Korea. Tanzania kwa miaka mingi tumezoea uhuru wa kukosoana na kupingana bila kupigana.
Sasa naona huu utamaduni mzuri unaminywa. Nimekuwa najiuliza hivi kile kikosi kazi alichounda Mh Magufuli wakati wa kampeni kumshauri namna ya kufanya mabadiliko makubwa katika nchi ndiyo haya wsliyomshauri?
Hivi ni kweli tutasonga mbele kimaendeleo huku kukiwa nacauti nyingi namna hii zikiulaumu utawala wa nchi hii. Natumia neno 'utawala' kwa makusudi kwa sababu hii awamu ya tano inatawala badala ya kuongoza! Yaani nchi inaendeshwa kikoloni zaidi.
Nimalizie kwa kuulizs tena swali, je, ni kweli rais ataweza kufanikiwa kutekeleza mipango yake ya maendeleo huku akipingwa na kulaaniwa vikali hivi na wananchi wake? Rais aliyejipambanua kama mcha Mungu, akionekana kwenye nyumba za ibada kila siku, leo analaaniwa na kuombewa dua mbaya hivi?
Ni wakati muafaka kwa rais na serikali yake kujitafakari upya namna ya kuileta nchi pamoja na kuattract zaidi support kutoka kwa wananchi badala ya kufanya mambo yanayochochea chuki dhidi ya serikali na kuwagawa watanzania!
Hii mambo ya kuminya uhuru wa maoni na taarifa hayajawahi kusaidia nchi yoyote kusonga mbele. Demokrasia na maendeleo ni vitu pacha. Vinakwenda pamoja. Demokrasia huleta maendeleo na maendeleo huleta demokrasia! Maendeleo ya kweli ni maendeleo ya watu sio maendeleo ya vitu. Na bila uhuru na demokrasia hakuna maendeleo ya watu!
Mwenye masikio na asikie!