DU! Goli la NNE.... CCM wanajifunga tena hapa....

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Kuendeleza katika topic ya Jenerali ulimwengu kuwa CCM walishajifunga magoli matatu, yote yakifungwa na Makamba; (Hat trick), naona sasa Makamba anaongeza goli la nne kwa kusimamia kuondolewa kwa Sitta Katika uspika. What a goal......... Huyu jamaa naona sasa sio tu ataondoka na mpira uliotumika, bali apewe na vili vibendera vya waamuzi wasaidizi...
 
hiyo ndiyo ccm husimamia maamuzi yake hata kama hayo maamuzi yatakuwa na madhara ndani ya chama wao huwa hawa jari ilimradi tu wanaotakiwa kulidhishwa wamelizika

naimani hawatajutia maamuzi yao kama ilivyotokea ktk kula za maoni

mapinduziiiiiiiii daimaaaaa
 
Inawezekana CCM hawajajifunga hilo goli la nne.
Pengine wamerudisha goli moja sasa ni 3 - 1.
Sidhani kama wanaweza wakafanya makosa mfululizo namna hiyo lazma kutakuwa kuna kitu tu.
 
Kuendeleza katika topic ya Jenerali ulimwengu kuwa CCM walishajifunga magoli matatu, yote yakifungwa na Makamba; (Hat trick), naona sasa Makamba anaongeza goli la nne kwa kusimamia kuondolewa kwa Sitta Katika uspika. What a goal......... Huyu jamaa naona sasa sio tu ataondoka na mpira uliotumika, bali apewe na vili vibendera vya waamuzi wasaidizi...

Halafu kwa nini maamuzi yote ya ovyo wanamwachia huyu mzee mwenye kiherehere ndio ayatangaze kwa mbwembwe? Nina mashaka sana na upeo wa Ma-kamba
 
Hiyo ndio CCM chama ambacho kimesahau kuangalia na kusimamia maslahi ya wengi (wananchi) na kukumbatia maslahi ya watu wachache au kikundi cha watu. Kwa mtazamo wangu maamuzi kama haya ndio yaliuwa vyama vingine vya ukombozi Afrika kama KANU-Kenya na UNIP-Zambia na CCM wanaelekea huko huko. That's their final destiny people!
 
Kuendeleza katika topic ya Jenerali ulimwengu kuwa CCM walishajifunga magoli matatu, yote yakifungwa na Makamba; (Hat trick), naona sasa Makamba anaongeza goli la nne kwa kusimamia kuondolewa kwa Sitta Katika uspika. What a goal......... Huyu jamaa naona sasa sio tu ataondoka na mpira uliotumika, bali apewe na vili vibendera vya waamuzi wasaidizi...

Tuko

CCM wamesawazisha - na sasa tupo kwenye muda wa nyongeza. Mchezo unavyoelekea wataondoka na ushindi maana Upinzani unaonekana kuweka UKUTA wakati bado dk 30!
 
Tuko

CCM wamesawazisha - na sasa tupo kwenye muda wa nyongeza. Mchezo unavyoelekea wataondoka na ushindi maana Upinzani unaonekana kuweka UKUTA wakati bado dk 30!

Nakuhakikishia Baba Enock, hakuna walichosawazisha. Fikiria kwamba wabunge wapinzani watakuwa wanauliza maswali magumu na ya mtego kwa waziri mkuu, na mawaziri wengine. Huyu mama kwa kufanya kazi aliyotumwa atakuwa anajitahidi kupangua yale anayohisi yataidhalilisha serikali, kwa kufanya hivyo atawachonganisha wananchi na bunge.

La pili, fikiria kuwa kundi la wabunge 'wapambana na ufisadi' wa CCM, bado litakuwepo (Mwakyembe, Kilango, Lembeli, Manyanya na wengi wataongezeka kutoka kwenye wabunge wapya); Kwanza kwa sasa wanajua kuwa wamehujumiwa kwa kuondolewa kwa kamanda wao Sitta, kwa hiyo watakuja kwa hasira. Wataichachafya serikali, huyu mama atakuwa anapangua, na atajenga makundi ndani ya bunge. Kiuhalisia ni kuwa wakati akina Mwakyembe walikuwa wanaheshimu kiti cha bunge kwa sababu spika alikuwa upande wao, kwa sasa watakuwa wanafyatuka kisawasawa, kwa hasira za kuhujumiwa kiti cha uspika.

Mwashoni itakuwaje.. Kwa kuogopa maamuzi ya wananchi hapo 2015, wabunge wa kuchaguliwa watakaokuwa upande wa mafisadi watakuwa kimya na kufanya kazi zao za kuunga mkono kwa njia ya kura peke yake. Hii itasababisha hoja nyingi ziombwe kuchangiwa na wabunge wanaopambana na ufisadi na hapo watapata nafasi ya kung'ara bungeni. CCM itapanic, na inawezekana kwa mara ya kwanza ikaawavua uanachama wabunge wake, kwa ajili ya kujilinda 2015...
 
Nakuhakikishia Baba Enock, hakuna walichosawazisha. Fikiria kwamba wabunge wapinzani watakuwa wanauliza maswali magumu na ya mtego kwa waziri mkuu, na mawaziri wengine. Huyu mama kwa kufanya kazi aliyotumwa atakuwa anajitahidi kupangua yale anayohisi yataidhalilisha serikali, kwa kufanya hivyo atawachonganisha wananchi na bunge.

La pili, fikiria kuwa kundi la wabunge 'wapambana na ufisadi' wa CCM, bado litakuwepo (Mwakyembe, Kilango, Lembeli, Manyanya na wengi wataongezeka kutoka kwenye wabunge wapya); Kwanza kwa sasa wanajua kuwa wamehujumiwa kwa kuondolewa kwa kamanda wao Sitta, kwa hiyo watakuja kwa hasira. Wataichachafya serikali, huyu mama atakuwa anapangua, na atajenga makundi ndani ya bunge. Kiuhalisia ni kuwa wakati akina Mwakyembe walikuwa wanaheshimu kiti cha bunge kwa sababu spika alikuwa upande wao, kwa sasa watakuwa wanafyatuka kisawasawa, kwa hasira za kuhujumiwa kiti cha uspika.

Mwashoni itakuwaje.. Kwa kuogopa maamuzi ya wananchi hapo 2015, wabunge wa kuchaguliwa watakaokuwa upande wa mafisadi watakuwa kimya na kufanya kazi zao za kuunga mkono kwa njia ya kura peke yake. Hii itasababisha hoja nyingi ziombwe kuchangiwa na wabunge wanaopambana na ufisadi na hapo watapata nafasi ya kung'ara bungeni. CCM itapanic, na inawezekana kwa mara ya kwanza ikaawavua uanachama wabunge wake, kwa ajili ya kujilinda 2015...

Nadhani, kuwavua ubunge ni kuongeza shimo la kaburi kwa chama! Kitakachotokea ni BORA LIENDE, na ndipo litakapoenda kweli.
 
Haiwezekani makosa yawe mengi na mfululiza hivyo!! KInachotokea kwa sasa ni kupanga safu ya kulinda mafisadi!!!

Hata kesi za kina mramba sasa zitamalizwa... maana kazi yake imekwisha!!!:doh:
 
Ni vigumu sana kushindana na ukweli,unaweza kujitahidi kuficha ficha ila haiwezekani.CCM wamejaribu kwa kila njia kukwepa kwenda kaburini,ila kaburi la ccm liko palepale halikwepeki.CCM bye bye.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom