Dstv Tanzania inasikitisha sana; Channel za news 7 za Kenya, channel ya news 1 ya Tanzania

Kabla ya kuwatupia lawama DSTV, angalia kwanza sheria za nchi zinasemaje. Halafu pia jiulize kama hao unaotaka wawekwe wanakubaliana na masharti ya DSTV.
 
asante sana mkuu nilitaka kununua kumbe na diesitivi nao ni utopolo, ngoja niendelee na kisimbuzi ninachotumia.HIvi kwa bongo kisimbuzi kipi ni bora, hapa na maanisha, ina channel za kueleweka na hata usipolipia local channels unazipata

Azam iko poa na startimes
 
Kabla ya kuwatupia lawama DSTV, angalia kwanza sheria za nchi zinasemaje. Halafu pia jiulize kama hao unaotaka wawekwe wanakubaliana na masharti ya DSTV.

Hayo masharti ya Dstv ni tofauti na masharti ya azam au startimes? Basi mwenye tatizo si unamuona kabisa.
 
Kwa watumiaji wa Dstv tunapata tabu sana kwenye upande wa local news. Inashangaza Dstv kuna channel 7 za local news za kenya KBCTV, NTV, KTN, Citizen TV, KTN News, K24 na kisomali ya Kenya STN TV, hizi zote zinaonesha local news za Kenya ila Tanzania mnatuwekea TBC1 peke yake. Hayo mazagazaga mengine mliyotuzuga nayo sijui Wasafi, Cloudplus, TVe, Safari TV, hayana tofauti na machannel ya YouTube au online streaming ni utopolo.

Tunaomba mtuheshimu subscribers wenu turudishieni local channel zinazoeleweka ITV, Channel 10, Star TV, Clouds TV, EATV, Capital TV.
Tumechoka huu upuuzi tutahamia Azam na Startimes kama kama mtaendelea na hizi hujuma zenu Dstv.
DSTV walikuwa wameweka channels zote muhimu za taarifa kweye decoder yao hapo awali. Kutokana na sherio mbovumbovu za hili taifa, imebaki TBC pekee. Zingine zilizobaki ni za entertainment tu, akina TVE, Wasafi, Clouds Tv nk. Lakini akina Star Tv, ITV na zingine ziliondolewa kabisa
 
Kajifunze kwanza maana ya free to air ndo uje na vpl zako. Unadandia hoja wakati kichwani mtupu kabisa.
tatizo umeisha jazwa ujinga wa kushadadia vya bure bure, kwenye dunia ya leo hakuna vya bure, hakuna kitu kama hicho sijui 'free to air' fikiria nje ya box
 
DSTV walikuwa wameweka channels zote muhimu za taarifa kweye decoder yao hapo awali. Kutokana na sherio mbovumbovu za hili taifa, imebaki TBC pekee. Zingine zilizobaki ni za entertainment tu, akina TVE, Wasafi, Clouds Tv nk. Lakini akina Star Tv, ITV na zingine ziliondolewa kabisa

Izo walizoweka za wasafi na zingine ni channel za streaming na wala siyo free to air kama ITV na Clouds Tv ndiyo mana wanazijazia mle kukamilisha quota ya 5 local channels kwa mujibu wa sheria.
 
Kwa watumiaji wa Dstv tunapata tabu sana kwenye upande wa local news. Inashangaza Dstv kuna channel 7 za local news za kenya KBCTV, NTV, KTN, Citizen TV, KTN News, K24 na kisomali ya Kenya STN TV, hizi zote zinaonesha local news za Kenya ila Tanzania mnatuwekea TBC1 peke yake. Hayo mazagazaga mengine mliyotuzuga nayo sijui Wasafi, Cloudplus, TVe, Safari TV, hayana tofauti na machannel ya YouTube au online streaming ni utopolo.

Tunaomba mtuheshimu subscribers wenu turudishieni local channel zinazoeleweka ITV, Channel 10, Star TV, Clouds TV, EATV, Capital TV.
Tumechoka huu upuuzi tutahamia Azam na Startimes kama kama mtaendelea na hizi hujuma zenu Dstv.


Wanachifanya mie naona sawa ..mtu anayejitambua haez check tbc .waziache zote za Kenya..mtajiju
 
Izo walizoweka za wasafi na zingine ni channel za streaming na wala siyo free to air kama ITV na Clouds Tv ndiyo mana wanazijazia mle kukamilisha quota ya 5 local channels kwa mujibu wa sheria.
Asante kwa kunielimisha. Lkn pia hizo ni free to air, ukitega dish kubwa kwenye nyuzi 46E unazipata hio local zote FREE kabisa. Hizo sio subscription channels.
 
Hawa kenge na sasa ivi kifurushi cha bei rahisi ni elfu 29 na wamepunguza chanel kibao!! Soon watatuwekea kifurushi cha chini ni elfu39!! yani nashidwa kuelewa hawa kima kwanini wanapunguza chanel aisee
 
tatizo umeisha jazwa ujinga wa kushadadia vya bure bure, kwenye dunia ya leo hakuna vya bure, hakuna kitu kama hicho sijui 'free to air' fikiria nje ya box

Dunia ya sasa ndiyo ipi uliyopo wewe. Kanunue television yoyote mpya dukani lazima utakuta kuna channel za Free to air kwenye source. Wewe ndiyo uliyedanganywa kuwa hakuna channel za bure. Kuna free to air FTA channels zaidi ya elfu 50 duniani wewe umekalia eti hakuna.
 
Kwanini serikali iwazuie dstv pekeyao mbona startimes na azam channel nyingi zipo? Jamaa wanasingizia serikali ila tatizo ni uroho tu wanazani wakiweka iTv na zingine kwakua hazitakiwi kulipiwa basi watu hawatakua wanalipi kingamuzi. Ni uroho tu wa dstv wala usiilaumu serikali ndugu yangu
So una maana walivyozitoa ndiyo wamesaidia watu kulipia king'amuz ? Nsaidie hapa, kuzitoa na kuziweka kuna athiri vipi watu kulipia king'amuzi?
 
Tcra ilitupigania sisi watazamaji kwakuwa tulikua tunalipishwa hadi local channels ambazo ni za free to air mfano ITV. Jamaa baada ya kupigwa fine wakaziondoa badala waziachie ziwe free wakaona wakiziacha sisi hatutalipia vingamuzi. Jamaa ni waroho sana wanawaza pesa hawatujali sisi wateja wao.
Nsaidie hapa, kuzitoa na kuziweka kuna athir vip watu kulipia king'amuzi
 
Asante kwa kunielimisha. Lkn pia hizo ni free to air, ukitega dish kubwa kwenye nyuzi 46E unazipata hio local zote FREE kabisa. Hizo sio subscription channels.

Ni kweli FTA unazipata kwenye dishi kubwa ila usiniambie wasafi pia inapatikana kwenye dishi
 
Binafsi sijalipia muda mrefu sana DSTV ila nilikuwa na king'amuzi cha star times vile vya mwanzo na nilikuwa nataka nikigawe ile kujaribu naona napata channel karibu zote za local tena bila malipo yoyote nikaona basi DSTV sababu naipenda nikianza kutulia mjini ndio nitakuwa nakilipia kwa ajili ya documentary na mpira.
 
Kwanini serikali iwazuie dstv pekeyao mbona startimes na azam channel nyingi zipo? Jamaa wanasingizia serikali ila tatizo ni uroho tu wanazani wakiweka iTv na zingine kwakua hazitakiwi kulipiwa basi watu hawatakua wanalipi kingamuzi. Ni uroho tu wa dstv wala usiilaumu serikali ndugu yangu
Aisee ni kweli yaaan Dstv hapaa wamepuyanga mnooo
 
Nsaidie hapa, kuzitoa na kuziweka kuna athir vip watu kulipia king'amuzi

Unajua FTA channels ni za free hazitakiwi kulipiwa kwakuwa ziko free kwa yeyoye mwenye dishi kubwa zamani ilikua ukiwa na antennae yako ya mwiba unaipata. Sasa Dstv walikua wanaziweka izo ITV nk, lakini ukimaliza muda wako wa kulipia huzioni hata hizo FTA channel mpaka ulipie upya. Nakumbuka startimes wao kifurushi chako kikiisha channel zingine zinaondoka ila zinabaki za FTA kama ITV, star tv nk. Ila dstv wao kifurushi kikiisha wanakata zote. Tcra wakawalima fine kwakuwa wanawalazimisha wateja kulipia hadi kuoma channel za FTA ambazo zipo kwenye vifurushi vyao kwenye vingamuzi walivyowauzia. Sasa dstv wakaona kuliko wawaachie wateja waendelee kuona channels za FTA hata kama vifurushi vimeisha ngoja waviondoe kabisa kwenye package zao.
 
Kwa akili yako shida ni DSTV au CCM na vyombo vyake ikiwemo TCRA? DSTv wamepigwa pini, wanataka muangalie TBCCM tu ili wote muimbe mapambio na kusifu 24/7! wengine hata hiyo TBCCM tumeiblock tunaangalia vyombo vya nje tu

Mwaka wa uchaguzi huu fanya maamuzi sahihi...


Wewe ni mwenzangu kabisa mimi hilo TBC CCM niliblock siku nyingi sana. Sijawahi hata kuhitaji tena local chanel maana sidhani km zitanisaidia chochote kama ni news nazipata kabla hata ya kusomwa,

Asante sana DSTV kwa kunifungisha jinsi ya kublock chanel
 
Back
Top Bottom