Drogba na Eboue kuadhibiwa kwa kumshukuru Mandela

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Chama cha Soka cha Uturuki kimewaita wachezaii wawili wa Ivory Coast, Didier Drogba and Emmanuel Eboue ili kuwaadhibu kutokana na kutenda kosa la kuvaa na kuonyesha uwanjani nguo zinazomkumbuka na kumshukuru Mandela. Wachezaji hao walionyesha nguo zao za ndani zenye maandiko ya kumkumbuka na kumshukuru Mandela kwenye mechi kati ya Galatasaray na B Elagizspor kumalizima.

Chama cha soka cha Uturuki hakiruhusu wachezaji kuvaa nguo zinazoonyesha maandiko yenye ujumbe wa kisiasa, kidini, kibiashara au maandiko binafsi. Hii ni kwa mujibu wa sheria ya FIFA inayokataza wachezaji to "reveal undershirts which contain slogans or advertising". Kwa mujibu wa sheria hiyo, "basic equipment must not contain any political, religious, or personal statements".

Sheria hiyo inaendelea kusema kuwa mchezaji ambaye atakiuka sheria hii ataadhibiwa na waandaji na wa shindano husika. Pia timu anayochezea mchezaji husika nayo itaadhibiwa na FIFA au waandaji wa shindano husika. Aidha sheria inamtaka refa aweke kosa hilo kwenye taarifa yake baada ya mechi.

1054553_orig.jpg


2999692_orig.jpg


5816203_orig.jpg


[video=youtube_share;4pM0MjRznHg]http://youtu.be/4pM0MjRznHg[/video]
 
Usishangae kwa sababu wenye FIFA si ndio Makaburu wenyewe wabaguzi wa rangi.
 
Sheria zinapokuwa rigid mpaka zinakosa mantiki. Ungekuwa ni ujumbe wa chuki ingekuwa na maana. Kwa hiyo siku Blatter akifariki (Mungu epusha) wachezaji watakao kuwa na flana zenye ujumbe wataadhibiwa?
 
hvi na baloteli aliadhibiwa after "WHY ALWAYS ME"

Alipewa kadi ya njano. Kiutaratibu kama refa akisha-deal the kosa husuka uwanjani ndiyo imetoka hiyo.

Kwa hiyo ya akina Drogba hawakupewa kadi yoyote na kama unavyoona kama vile marefa walikuwa hawajui wafanye nini.
 
Ha wapewe kadi vipi wakati mpira umekwisha na walikuwa wanaaga wapenzi wa timu yao.
Baloteli alipewa kadi sababu alivua shati akishangilia goli au ??

Alipewa kadi ya njano. Kiutaratibu kama refa akisha-deal the kosa husuka uwanjani ndiyo imetoka hiyo.

Kwa hiyo ya akina Drogba hawakupewa kadi yoyote na kama unavyoona kama vile marefa walikuwa hawajui wafanye nini.
 
Kwani si wakiwa kwenye Mechi? Wakati wa Mechi hata ukivua tu unaadhibiwa ila mechi ikiisha, hata huwa wanabadilishana mashati/t-shirt. Mbona hapo huwa hawaadhibiwi? Jamaa wamewekwa kwenye mtihani mgumu sana. Labda iwekwe kwamba hawatakiwi kuvua nguo hadi watoke kabisa uwanjani.
 
Usishangae kwa sababu wenye FIFA si ndio Makaburu wenyewe wabaguzi wa rangi.

Hapana, tusivunje sheria tukasingizia ubaguzi, ndo hayo mambo ya marais wa Afrika wanaendesha mauaji halafu wanasema ICC ipo kwa ajili ya Afrika tu! Drogba na Eboue ni professional players wa muda mrefu tu, wanalielewa hilo na sidhani kama wanapinga hiyo adhabu kama inavyopingwa humu JF!
 
Kwani si wakiwa kwenye Mechi? Wakati wa Mechi hata ukivua tu unaadhibiwa ila mechi ikiisha, hata huwa wanabadilishana mashati/t-shirt. Mbona hapo huwa hawaadhibiwi? Jamaa wamewekwa kwenye mtihani mgumu sana. Labda iwekwe kwamba hawatakiwi kuvua nguo hadi watoke kabisa uwanjani.
Sasa hivi refa anaruhusiwa kukuonyesha kadi nyekundu hata nje ya dakika 90 za mchezo
 
Drogba na Eboue ni professional players wa muda mrefu tu, wanalielewa hilo na sidhani kama wanapinga hiyo adhabu kama inavyopingwa humu JF!

Well, tupo third world, dunia ya mwisho huku, hatuna concept ya utawala wa sheria, tunatawaliwa na matamko ya Selemani Kova na whims za Mizengo Pinda, si ajabu kuona watu wanapinga application of law kama hii, hatujazoea.
 
Back
Top Bottom