Dr.W.Slaa asipopitishwa na (CHADEMA) KURA YANGU WAMEIKOSA

Kwani chama ni nini? Chama siyo physical object bali sura ya chama hutambulika kwa mwonekano wa viongozi wake yaani misimamo yao na kile wanachoamini, malengo yao, miongozi na zaidi jinsi wanavyoishi kile wanchokitamka.

Wapiga kura wengi walio makini humchagua mtu na wala siyo chama, hiyo ni kwa mataifa yote. Hata chaguzi za mataifa yaliyoendelea kama Marekani, leo hii wanavyoendesha tafiti zao, wanalinganisha wagombea wanavyoungwa mkono, wala siyo vyama vyao jinsi vinavyoungwa mkono.

Si kitu cha ajabu kusikia na kutokea kuwa watu ambao watawachagua wagombea wa CHADEMA, wengi wao watafanya hivyo kwa kuangalia ni nani aliyesimamishwa. Hata mimi nitafanya hivyo maana sera za chama au manifesto havina maana yeyote kama huna imani na msimamizi mkuu, ambaye ni Rais. Kama CHADEMA wasipomsimamisha ambaye dhamira yangu inaamini ana uwezo wa kusimamia mabadiliko, sitamchagua mgombea wa CHADEMA lakini pia sitamchagua mgombea wa CCM.
JApo amutegemeae mwanadamu amelaaniwa but Tuko kuangalia nani zaidi anaposema anamaanisha. KAma Dr.Slaa asipoteuliwa kugombea kwa mizengwe ya kinafiki watu wengi hawatapiga kura kabisa. Mwaka 2010 Dr.Slaa alifanya kazi kubwa na hata CDM ikapata wabunge wengi tu kwa mgongo wake.
 
Kifo cha cdm pale ZZK akisimama ktk nafasi ya urais.
the guy is not stable. Bado sana. Kelele zake si ni kibali cha kupambana ktk post kubwa hivyo.
abaki kuleta solidarity among vijana.
cdm itapoteza muelekeo kumpitisha huyu binadam.
Kura yangu hatopata. bora nipeleke TLP
 
Itaamuliwa muda utakapofika nani aipeperushe bendera ya CDM kwenye uchaguzi mkuu maana wananchi wameshakiweka chama mioyoni mwao. Yeyote atakayechaguliwa itabidi tumspoti ili awe rais. Naimani kua yeyote atakayechaguliwa na akashinda, hao wengine watajumuishwa katika serikali. But personally namkubali sana dk. Slaa for the position.
 
Huwa napata shida sana pale tunapodhani taasisi haiwezi kuishi bila mtu mmoja.

Ingawa naamini Daktari ni kiongozi mahiri, ni lazima CDM iwe mahiri hata bila Daktari vinginevyo mnataka kutupigia nyimbo (zidumu fikra) ile ile isipokuwa mdundo ndo tofauti!

Realman uko sahihi, nakumbuka wakati Mwl Jk alipong'atuka watu wakasema nchi haitawaliki, ndio sawa na wale wanaosema Dr sla asipokuwa Rais CDM kwisney.
 
Zzk ni yuko poa ,lakini kama mambo yenyewe ndio haya ya kuwa na task force za kumtetea wakitumia karata za kibaguzi za ujana basi siwezi kumchagua.nadhani hakuna zaidi ya dr slaa kwa sasa ingawa kwa hekima hajatangaza nia ya kugombea.
 
Kweli Dr. anafaa sana kwa sasa hata anayepigwa vita na kushambuliwa na ccm ni dr. maana hata wao wanajua uwezo anao tena wa kutosha na anaweza kuwashughulikia ipasavyo he is not a neutral man is very straight person
 
Kweli Dr. anafaa sana kwa sasa hata anayepigwa vita na kushambuliwa na ccm sana ni dr. maana hata wao wanajua uwezo anao tena wa kutosha na anaweza kuwashughulikia ipasavyo he is not a neutral man is very straight person
 
wewe sasa ndio undandia treni kwa mbele maana hapa tulikuwa tunajadili swala la chadema na uteuzi wa mgombea wapo wanaosema bila slaa watapigia chama kingine kura ndio maana nikasema chama kwanza mtu baadae ila yanapokuja maswala ya kitaifa huwa inatakiwa utaifa kwanza chama baadae so kabla ya kurukia kuchangia ujue mtu anachangia hoja kutoka kwenye context ipi??
Jitafakari jinsi unavyofikiri hauelewi na haueleweki.
 
Kuna makundi ndani ya Chadema kuna "Chadema Zitto Kabwe", kuna "Chadema Dr Slaa", kuna "Chadema Mbowe." kuna "Chadema Shibuda."
 
Kuna makundi ndani ya Chadema kuna "Chadema Zitto Kabwe", kuna "Chadema Dr Slaa", kuna "Chadema Mbowe." kuna "Chadema Shibuda."

Hamna kitu kama hicho, mnachofanya nyie ni kutugawa na hamta fanikiwa, 2015 mgombea ni Slaa full stop!!
 
Hayo ni baadhi ya maneno na kauli za wananchi wa maeneo mbalimbali nchini. Ikiwemo Dar,Mwanza,Tabora.Kigoma,shinyanga,singida,manyara,Arusha,Kilimanjaro,Tanga.mbeya,Iringa,Dodoma,Sumbawanga,Morogoro,Mtwara,nk. Katika mikoa hiyo watu saba kati ya kumi wanadai katibu mkuu wa chadema taifa asipopitishwa na chama chake 2015 katika uchaguzi mkuu.basi kura zao watatoa kwa chama kingine. Kwa kile wanachokiita uadilifu wa kiongozi huyo na msimamo(standpoint) wa kiongozi huyo wa chama cha demokrasia na maendeleo ambaye amekuwa akifanya kazi ya ziada katika maeneo mengi nchini. Kwa elimu ya uraia pamoja na serikali kwa ujumla kitu ambacho ni nadra sana kwa kiongozi mwingine ndani ya cdm. Wakizungumza na wawakilishi wa shirika la utafiti wa wa save the childrens tanzania bwana haroun mafuru mkoani lindi wiki ,alisema Ni vizuri kwa wananchi na jamii kwa ujumla kuamua ni nani wanataka kumtuma akawatetee katika taifa lao. Na vile vile si dhambi kuonyesha ni nani wanayempendeza awe rais wao ifikapo 2015!

:israel: :israel::israel: naunga mkono hoja.!
 
Kama kweli misimamo ya wanachama ndo kama hiyo basi ccm bado wana muda mrefu wa kututawala, kwa sababu slaa ni binadamu tu anaweza kuugua, kuhama chama, kustaafu siasa, kufanya makosa ya kisiasa yanayoweza kumpunguzia hadhi yake ya kuaminika na nk, ina maana huo ndo mwisho wa cdm!? Ndo mwisho wa harakati zote! Nadhani chama kina kazi kubwa ya kufanya maana ni dhahiri wanachadema ni wachache kuliko nilivyodhani, inasikitisha..

we endelea kusikitika tu ila bila Dr. Slaa bora turudi CCM . Eti Zitto ??? who the hell is this, akafie mbele huko. Tuko CDM kwa sbb ya Dr. Slaa na sasa Mnyika,Lissu,Lema,Heche na Msigwa na si kibaraka wenu huyo Mkabwela.
 
hapa raisi ni dk slaa tumuombe uzima kwa mwwnyezi Mungu, huku tukimuanda mnyika aje kushika nchi tena

Ndugu zanguni wacha niwaambieni toka moyoni,Dr Slaa mwachieni awe Rais na mbowe awe waziri mkuu,kama nadanganya wekeni kura ya maoni kati ya slaa na mbowe nani atazoa kura,mbowe anafiti kuwa mtendaji mkuu wa serikali jamani,tumekaribia kuikomboa nchi mikononi mwa wakoloni weusi ndugu zanguni,slaa apeperushe tena bendera utaona matunda yake,uambieni mkisha kosea lowasa na richmond yake anachukua nchi,please please slaa ajaribu tena,mbowe bado kijana,anafaa kuwa pinda wa 2015:embarassed2:
 
Nakuunga mkono 100% Bila ya Dr SLAA kuwa mgombea Wa CDM 2015 mimi, familia yangu na ukoo wangu HATUTA PIGA KURA KABISA!
 
Back
Top Bottom