Dr. Slaa timiza ahadi yako uliyoitoa wakati wa uchaguzi

Mkondakaiye

JF-Expert Member
Dec 5, 2011
838
174
Napenda kuchukua nafasi hii kumkumbusha Rais wetu Dr. Slaa kutimiza ahadi yako uliyoitoa wakati wa kampeni za uchanguzi ukiwa mjini njombe kuwa kama hutachaguliwa kuwa rais basi utakuwa na muda wa kupita kijiji hadi kijiji kuimarisha chama kwani utakuwa na muda mwingi wa kuimarisha chama.


Toka uchaguzi uishe kazi ya kuimarisha chama kama ulivyo ahidi bado haijafanyika. Kumbuka kuwa huku mawilayani viongozi wa wilaya wengi wao bado hawakubaliki na jamii inayowazunguka. Wale wanao kubalika wanaogopa nguvu ya ccm kuwahujumu kikazi (kama ni waajiliwa wa serikali) au kibiashara (kama ni wafanyabiashara)


Katika nchi hii kuna baadhi ya mikoa ambayo imesha amu na kujua upinzani ninini. Mikoa kama Arusha, Kilimanjaro, Mbeya (baadhi ya wilaya), Mwanza, Dar na kigoma. Lakini kuna mikoa bado nguvu ya ziada inahitajika ili kuteka kundi kubwa la watu ambao bado mawazo yao yapo kwa magamba. Mikoa kama Mtwara, Lindi, Tabora, Dodoma, Morogoro, Singida, Ruvuma na Iringa.


Kumbuka kuwa jimbo la iringa mjini wananchi walipiga kura kuwaadhibu magamba kwa kuondolewa chaguo lao. Ndo hapo CDM ikapata hicho kiti. Kwahiyo ,Tafadhali Dr slaa timiza ahadi yako ya kupita mawilayani ili kuimalisha chama. Kumbuka kuwa CDM haiwezi kuchukua nchi mwaka 2015 kwa kutegemea mikoa ya Arusha, Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na Dar pekeyake.

Nimefurahi kusikia kuwa kamanda lema atatembea mikoa mbalimbali kuitangaza CHADEMA. Nadhani huu utakuwa mwanzo mzuri katika kuitimiza ahadi ya Dr slaa. Nashauri kazi hiyo ianzie vijijini.
 
Mawazo haya ni jmazuri sana na ninayaunga mkono. Nilishasema kuwa kampeni hii ikianza wananchi tutachanga wenyewe kuwezesha movement za Chadema vijijini..na si ajabu wanakijiji wakachanga wenyewe ili Dr Slaa na wenzake wafike. Nilishauri kuwa Kama inawezekana CDM itusambazie wadau Strategic Plan yake tujue wapi tunaweza kuchangia lakini sehemu kubwa ya plan iwe ni kwenda vijijini. Fundraising wa chame aisambaze kwa wadau fedha zitachangwa tu. Naungana na wewe 100%. CCM wanastahili kichapo pande zote kama hapo chini.........hamna kupumzika

01AweCZs7YcLIAKT0OAADnMuRMsCY:.mp3
 
Wazo zuri!
Pia ukumbuke kuwa huyu mtu halali toka siku hizo za uchaguzi...kumbuka mgogoro wa Arusha, Igunga, Arumeru, na sasa kwa mara ya pili mgogoro wa Arusha tena!
Naamini mambo haya yakipita atakuwa available na atatimiza ahadi, kama yeye personally ndio anayetakiwa!
 
Wazo zuri!
Pia ukumbuke kuwa huyu mtu halali toka siku hizo za uchaguzi...kumbuka mgogoro wa Arusha, Igunga, Arumeru, na sasa kwa mara ya pili mgogoro wa Arusha tena!
Naamini mambo haya yakipita atakuwa available na atatimiza ahadi, kama yeye personally ndio anayetakiwa!

Ingawa nimemtaja Dr. slaa, lakini naamini kazi hii siyo yake pekee yake. Uongozi wa taifa unatakiwa kuratibu kazi hii kwa kuwatumia makamanda wake ilionao, kama zito, lema (hata kama amevuliwa ubunge), Mdee, Mnyika, Sugu, na wengine wengi. Tukimwachia Dr. pekee hatutafanikiwa
 
Ingawa nimemtaja Dr. slaa, lakini naamini kazi hii siyo yake pekee yake. Uongozi wa taifa unatakiwa kuratibu kazi hii kwa kuwatumia makamanda wake ilionao, kama zito, lema (hata kama amevuliwa ubunge), Mdee, Mnyika, Sugu, na wengine wengi. Tukimwachia Dr. pekee hatutafanikiwa

Hivi Arumeru Mashariki ni jiji? au unazungumzia Vijiji gani?
 
CCM inatumia mbinu chafu ya kutuhangaisha mahakamani ili watuchukulie muda wa kuhangaikia shida za wananchi na rasilimali za nchi mimi ningependelea ss vijana popote tulipo tukawafumbue macho wenzetu popote pale walipo mimi nimeanza kwetu huku mtwara na nitafanya juhudi zote ili watu waamke naomba tuungane mkono. Najua ninachokifanya na naamini tutashinda 2015. kwetu huku inahitajika elimu tu basi kwani wengi wapo gizani.
 
Ndugu yangu Sangarara, hakuna aliyetaja arumeru mashariki hapa, kama bado una maumivu ya arumeru chuku panado unywe tukutane tena arusha.
 
Wazo ni zuri sana, nawashauri CDM mimi mwenyewe ni mwanachama tuorganize fundraisng kila mkoa kama ile iliyofanyika Arusha, inayopatikana kila mkoa tunaitumia kuhamasisha mkoa huo. Hii iwe kwa miaka yote mpaka uchaguzi wa 2015 nina uhakika tutashinda URAISI na VITI VINGI VYA WABUNGE
 
Wazo ni zuri sana, nawashauri CDM mimi mwenyewe ni mwanachama tuorganize fundraisng kila mkoa kama ile iliyofanyika Arusha, inayopatikana kila mkoa tunaitumia kuhamasisha mkoa huo. Hii iwe kwa miaka yote mpaka uchaguzi wa 2015 nina uhakika tutashinda URAISI na VITI VINGI VYA WABUNGE

Yeah kamanda wazo zuri hilo. One time nakumbuka wakati wa maandamano ya mikoa sita ya Kusini, Daktari Slaa alikutana na vijana wa vyuo vikuu ambao walisema wanandaa proposal ya namna ambavyo wanaweza kusaidiana na chama, ili wao waende vijijini kueneza elimu ya uraia/siasa (ukombozi). Yakiwepo mawazo ya namna hiyo kw ania ya dhati, hata kazi ya Daktari kupita vijijini ku-cement nguvu ya chama itakwenda vyema sana mkuu.
 
CCM inatumia mbinu chafu ya kutuhangaisha mahakamani ili watuchukulie muda wa kuhangaikia shida za wananchi na rasilimali za nchi mimi ningependelea ss vijana popote tulipo tukawafumbue macho wenzetu popote pale walipo mimi nimeanza kwetu huku mtwara na nitafanya juhudi zote ili watu waamke naomba tuungane mkono. Najua ninachokifanya na naamini tutashinda 2015. kwetu huku inahitajika elimu tu basi kwani wengi wapo gizani.

Mbinu zao tutazishinda kwa kutwanga kotekote, yaani kwenye chaguzi ndogo na kuhamasisha na kueneza elimu ya uraia vijijini
 
Wazo ni zuri sana, nawashauri CDM mimi mwenyewe ni mwanachama tuorganize fundraisng kila mkoa kama ile iliyofanyika Arusha, inayopatikana kila mkoa tunaitumia kuhamasisha mkoa huo. Hii iwe kwa miaka yote mpaka uchaguzi wa 2015 nina uhakika tutashinda URAISI na VITI VINGI VYA WABUNGE

Yeah kamanda wazo zuri hilo. One time nakumbuka wakati wa maandamano ya mikoa sita ya Kusini, Daktari Slaa alikutana na vijana wa vyuo vikuu ambao walisema wanandaa proposal ya namna ambavyo wanaweza kusaidiana na chama, ili wao waende vijijini kueneza elimu ya uraia/siasa (ukombozi). Yakiwepo mawazo ya namna hiyo kw ania ya dhati, hata kazi ya Daktari kupita vijijini ku-cement nguvu ya chama itakwenda vyema sana mkuu.
 
Yeah kamanda wazo zuri hilo. One time nakumbuka wakati wa maandamano ya mikoa sita ya Kusini, Daktari Slaa alikutana na vijana wa vyuo vikuu ambao walisema wanandaa proposal ya namna ambavyo wanaweza kusaidiana na chama, ili wao waende vijijini kueneza elimu ya uraia/siasa (ukombozi). Yakiwepo mawazo ya namna hiyo kw ania ya dhati, hata kazi ya Daktari kupita vijijini ku-cement nguvu ya chama itakwenda vyema sana mkuu.

Kwahiyo ina maana huo mpango wa kuwatumia vijana wa vyuo vikuu na wengine watakaojitolea ndo ulifia hapo kwenye kikao cha dr slaa na hao vijana? Nadhani CDM ina bidi tufanye kazi ya ziada ya kutoa elimu ya uraia.
 
Angaika na kikwete ambaye ametoa ahlukuki ma hakuna hata mojailiyotekelezwa
 
Wazo zuri!
Pia ukumbuke kuwa huyu mtu halali toka siku hizo za uchaguzi...kumbuka mgogoro wa Arusha, Igunga, Arumeru, na sasa kwa mara ya pili mgogoro wa Arusha tena!
Naamini mambo haya yakipita atakuwa available na atatimiza ahadi, kama yeye personally ndio anayetakiwa!

Hayataisha mkuu, unawafahamu CCM or unawasikia. Watafanya kila njia ili viongozi wa CDM wasitulie na kufuatilia mambo yanayoweza waharibia. Hizi zote ni mbinu za magamba.
 
Back
Top Bottom