Elections 2010 Dr Slaa, tafadhali toeni tamko kuhusu ufisadi wa kupindukia unaofanywa na NEC

Mwafrika

JF-Expert Member
Nov 20, 2006
5,490
226
Dr Slaa,

Kwanza kabisa, Asante sana kwa kazi nzuri uliyotufanyia watanzania mwaka huu. Mafanikio ya vyama vya upinzani katika ngazi za udiwani na ubunge yamechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na ushiriki wako kwenye kampeni za uraisi.

Hata hivyo, hii speed ya kutangaza majimbo 14 kwa siku inayofanywa na tume ya uchaguzi, na hili la kuchagua tu baadhi ya majimbo ambayo "wamefanya vizuri" kwa mtizamo wao, ni jambo ambalo linahitaji tamko kubwa sana toka kwako na viongozi wa chadema.

Jana wakati tukifuatilia matangazo ya uchaguzi toka kwenye TV mbali mbali Tanzania, watangazaji wote walikuwa wanakwepa kutaja matokeo ya ngazi ya uraisi. Ilifikia hatua Masako wa ITV anamkataza mmoja wa watangazaji kutangaza matokeo ya uraisi kutoka katika vituo mbalimbali.

CCM waligundua kitu kimoja, watanzania walikuwa wanajumlisha matokeo ya kura yaliyokuwa yanatangazwa toka katika kila kituo. Na kama ukifuatilia uchaguzi wa kenya wa mwaka 2007, hii ndiyo ilisababisha ugumu sana kwa tume ya uchaguzi kubadilisha matokeo maana wananchi walikuwa wanajua tayari hesabu yao (kutokana na kura za kituo kimoja kimoja).

CCM wamecheza mchezo wa kuficha kura za uraisi toka kituo kimoja kimoja na wanazitoa kwa mafungu. Huu ni wakati wa nyie kutoa tamko ili kuwahakikishia wafuasi wenu (nikiwemo mimi) kuwa matokeo yanayotolewa sasa hivi na tume ya uchaguzi yanalingana na yale ambayo wasimamizi wenu wa kila kituo cha uchaguzi wameyathibitisha.

Again, asante sana kwa kazi nzuri unayolifanyia taifa la watanzania.

No matter what jeshi la wananchi watanzania litaamua kufanya, You are my president Dr Slaaa.

Asante
 
Angalizo na swali muhimu, ni nani mwenye mamlaka ya kupinga kinachoendelea sasa hivi? Kama nijuavyo mimi, matokeo yakishatangazwa ndio imetoka hivyo... je strategy ni ipi?
 
Hivi kwanini wananchi tusigome tukawasusia nchi hao CCM tuone watamtawala nani?
 
Hivi kwanini wananchi tusigome tukawasusia nchi hao CCM tuone watamtawala nani?

ccm wana msemo kuwa mkisusa wao wala (watakula tu). CUF waliwahi kususia enzi za komandoo na haikusaidia
 
Tena muda si mrefu mwenyekiti wa tume katoka kusema eti inaweza kufika hadi ijumaa.
chanzo by bbc
 
Hii inasikitisha sana. Ambako upinzani wameshinda, --recount--, ambako CCM wameshinda --straight anouncement--. Hii peke yake si sawa. Kwenye kambi za CCM, matokeo harakaharaka. Kwenye Kambi za Upinzani hasa CHADEMA, matokeo mpaka wananchi watishie kulala barabarani. Hii ni sawa jamani? Unapominya haki unachangia umwagaji damu, maana amani ni huzaliwa na haki.
Hivi hatutakubali kabisa, hata mabomu watupige, ni heri kufa unapigania uhuru wa nchi yako, uliyopewa na Mungu kuliko huu udhalimu.
Lakini hata hivyo, kuna raha gani kutawala pasipo kushinda, huu ni ufisadi wa kisiasa. Dr. wa ukweli toa tamko tafadhali.
 
kwa kweli hili linabidi kuangaliwa hawa ccm wanatuandaa kisaikologia kwa kutangaza majimbo ambayo wameshinda ili hata hapo watakapochakachua na kuja na takwimu zao wenyewe tusishtuke wanatafuta ushindi wa lazima kwanini jamani wasikubali kushindwa jamani wahusika wanaoweza kulizungumzia hioli hebu chukueni hatua tunaibiwa.
 
Hii inasikitisha sana. Ambako upinzani wameshinda, --recount--, ambako CCM wameshinda --straight anouncement--. Hii peke yake si sawa. Kwenye kambi za CCM, matokeo harakaharaka. Kwenye Kambi za Upinzani hasa CHADEMA, matokeo mpaka wananchi watishie kulala barabarani. Hii ni sawa jamani? Unapominya haki unachangia umwagaji damu, maana amani ni huzaliwa na haki.
Hivi hatutakubali kabisa, hata mabomu watupige, ni heri kufa unapigania uhuru wa nchi yako, uliyopewa na Mungu kuliko huu udhalimu.
Lakini hata hivyo, kuna raha gani kutawala pasipo kushinda, huu ni ufisadi wa kisiasa. Dr. wa ukweli toa tamko tafadhali.

na jamaa kila wanakofanya recount, wanashinda....

chadema acheni kucheza nice na ccm, mnapoteza kura hivi hivi.
 
Angalizo na swali muhimu, ni nani mwenye mamlaka ya kupinga kinachoendelea sasa hivi? Kama nijuavyo mimi, matokeo yakishatangazwa ndio imetoka hivyo... je strategy ni ipi?

Mwafrika, kilichobaki ni wananchi kuchukua madaraka tu. Sheria inayotumika ni mbovu, na hii ndo huwakatisha tamaa watanzania kupiga kura, sababu ni usanii mtupu. Only people's power can work.
 
Mwafrika, kilichobaki ni wananchi kuchukua madaraka tu. Sheria inayotumika ni mbovu, na hii ndo huwakatisha tamaa watanzania kupiga kura, sababu ni usanii mtupu. Only people's power can work.

itakuwa kazi kwa wananchi kuchukua madaraka mkuu, ni vigumu sana. Cha muhimu ni kwa chadema kuhakikisha wanatoa tamko sasa hivi ili kuweka mwelekeo wa nini kifanyike kwa muda huu
 
Dr Slaa,

Kwanza kabisa, Asante sana kwa kazi nzuri uliyotufanyia watanzania mwaka huu. Mafanikio ya vyama vya upinzani katika ngazi za udiwani na ubunge yamechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na ushiriki wako kwenye kampeni za uraisi.

Hata hivyo, hii speed ya kutangaza majimbo 14 kwa siku inayofanywa na tume ya uchaguzi, na hili la kuchagua tu baadhi ya majimbo ambayo "wamefanya vizuri" kwa mtizamo wao, ni jambo ambalo linahitaji tamko kubwa sana toka kwako na viongozi wa chadema.

Jana wakati tukifuatilia matangazo ya uchaguzi toka kwenye TV mbali mbali Tanzania, watangazaji wote walikuwa wanakwepa kutaja matokeo ya ngazi ya uraisi. Ilifikia hatua Masako wa ITV anamkataza mmoja wa watangazaji kutangaza matokeo ya uraisi kutoka katika vituo mbalimbali.

CCM waligundua kitu kimoja, watanzania walikuwa wanajumlisha matokeo ya kura yaliyokuwa yanatangazwa toka katika kila kituo. Na kama ukifuatilia uchaguzi wa kenya wa mwaka 2007, hii ndiyo ilisababisha ugumu sana kwa tume ya uchaguzi kubadilisha matokeo maana wananchi walikuwa wanajua tayari hesabu yao (kutokana na kura za kituo kimoja kimoja).

CCM wamecheza mchezo wa kuficha kura za uraisi toka kituo kimoja kimoja na wanazitoa kwa mafungu. Huu ni wakati wa nyie kutoa tamko ili kuwahakikishia wafuasi wenu (nikiwemo mimi) kuwa matokeo yanayotolewa sasa hivi na tume ya uchaguzi yanalingana na yale ambayo wasimamizi wenu wa kila kituo cha uchaguzi wameyathibitisha.

Again, asante sana kwa kazi nzuri unayolifanyia taifa la watanzania.

No matter what jeshi la wananchi watanzania litaamua kufanya, You are my president Dr Slaaa.

Asante
mamii usijali chadema wanafanya mkutano kesho Arusha......nadhani watatumia nafasi hiyo kulizungumzia hili..hope umenisoma
 
Hii inasikitisha sana. Ambako upinzani wameshinda, --recount--, ambako CCM wameshinda --straight anouncement--. Hii peke yake si sawa. Kwenye kambi za CCM, matokeo harakaharaka. Kwenye Kambi za Upinzani hasa CHADEMA, matokeo mpaka wananchi watishie kulala barabarani. Hii ni sawa jamani? Unapominya haki unachangia umwagaji damu, maana amani ni huzaliwa na haki.
Hivi hatutakubali kabisa, hata mabomu watupige, ni heri kufa unapigania uhuru wa nchi yako, uliyopewa na Mungu kuliko huu udhalimu.
Lakini hata hivyo, kuna raha gani kutawala pasipo kushinda, huu ni ufisadi wa kisiasa. Dr. wa ukweli toa tamko tafadhali.
CHADEMA tambueni hili
Wakati wa kura kuhesabiwa na mawakala vituoni idadi inaandikwa na kwenye fomu wanasaini. Ila mchezo hutokea inbetween kituo to wilayani. hapo kati kama gari halisindikizwi na wakala basi masanduku mapya yanapakizwa kwenye gari ili wakifika mwisho wa safari msimamizi analazimisha recount.
Lazima mtoe tamko ili dunia ielewe kinachoendelea.
TUMEZILINDA KURA, SASA NI KAZI YENU KUYALINDA MATOKEO
 
Hiki ni kitu ambacho ingebidi wakifanye over and over hadi makamba na yule pirate Kinana waogope
 
Back
Top Bottom