Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Joyce Mmasi | Friday, 15 October 2010
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Wilbroad Slaa alisema akichaguliwa kuwa rais, serikali yake itaondoa matumizi yote ya anasa na kifahari serikalini, akisema kuwa yuko tayari kula mihogo Ikulu kuliko mayai na mapochopocho huku wananchi wakifa kwa kukosa dawa hospitalini.
Dk Slaa, ambaye amekuwa akipinga kitendo cha serikali kutenga fedha nyingi kwa ajili ya kukirimu wageni, amesema atafyeka kabisa bajeti hiyo aliyoiita ya chai na vitafunwa ambayo alisema kiwango chake cha fedha huzidi vya baadhi ya wizara muhimu.
Dk Slaa alisema hayo jana katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika Bunazi, nje kidogo ya mji wa Bukoba ambako alisema ni aibu na fedheha kwa bajeti moja ya chai na vitafunwa ya serikali kutengewa Sh30 bilioni wakati bajeti ya wizara muhimu kama ya Maji na Umwagiliaji ikitengewa Sh29 bilioni.
"Huu ni ufisadi mkubwa; ni jambo la aibu na fedheha kubwa kwa wizara muhimu kama ya Maji na Umwagiliaji kutengewa bejeti ndogo ukilinganisha na ile chai na vitafunwa ambayo inaizidi kwa bilioni moja zaidi... angalieni wenyewe aibu hii. Nikiingia Ikulu, jambo la kwanza nitalimaliza tatizo hilo," alisema.
Alisema ataondoa magari ya anasa kwa kuhakikisha watendaji, wakiwemo mawaziri, wanatumia magari aina ya Toyota Land Cruiser-Hardtop maarufu kama mkonge, ambayo alisema bei yake ni Sh60 milioni tu badala ya magari aina ya Toyota Land Cruiser VX ambayo alisema moja hugharimu Sh200 milioni.
"Nipo tayari kwenye kula mihogo ikulu, badala ya mayai na mapochopocho mengine huku wananchi wangu wanakufa kwa kukosa dawa hospitalini. Serikali ya Chadema itasamehe starehe na anasa zote ili iwatumikie wananchi," alisema.
Akizungumzia suala la afya, Dk. Slaa alisema Bunge la kwanza la bajeti la serikali yake litatenga fedha za kutosha kwenye sekta ya afya ilio huduma zitolewe bure kwa kila Mtanzania tofauti na hali ilivyo sasa ambayo wenye uwezo wa kiuchumi tu ndio wenye uhakika wa matibabu bora.
"Mfano ni mimi mwenyewe. Nilivunjika mkono wangu huu (alinyoosha mkono wa kushoto juu), lakini ndani ya kipindi cha mwezi mmoja nimepona na kuweza kuendelea na maisha. Mimi nimeweza kwa sababu nina uwezo wa kulipa zaidi ya Sh4 milioni MOI (Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Muhimbili) Muhimbili. Je ni Watanzania wangapi wenye uwezo kama wa Dk Slaa," alihoji.
Alisema kutokana na bajeti ndogo ya wizara ya afya, Watanzania wengi wanahukumiwa hukumu ya kifo kwa kuendelea kusumbuliwa na hata kufa kutokana na magonjwa ambayo yanatibika na yalishafutika duniani kote.
Alitoa mfano ugonjwa hatari wa Malaria ambao unaoongoza kwa vifo vingi nchini licha ya kuwa ni ugonjwa unaotibika na kwamba hata katika maeneo mengine duniani ikiwemo, kisiwani Zanzibar umetokomezwa kabisa.
"Ni ajabu sana, na ni uthibitisho wa kukosa vipaumbele vya taifa kwa serikali ya CCM kujisifu kuwa inagawa vyandarua. Sasa hivi wanatangaza wanatoa viwili kwa kila familia. Sasa najiuliza, kwa familia yenye watu zaidi ya saba watafanya nini? Hii inamaanisha kuwa wale wengine waendelee kuumwa na mbu na kufa kwa malaria," alisema.
Wakati huo huo, helkota iliyokuwa ikitumiwa na mgombea huyo wa Chadema katika kampeni zake imetengemaa baada ya kupata hitilafu ya kiufundi na kusababisha mgombea huyo kufanya kampeni zake kwa kutumia magari katika mkoa wa Kigoma. Sasa itaanza kuchanja mbuga wakati Dk Slaa akielekea Mwanza kuendelea na kampeni zake.
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Wilbroad Slaa alisema akichaguliwa kuwa rais, serikali yake itaondoa matumizi yote ya anasa na kifahari serikalini, akisema kuwa yuko tayari kula mihogo Ikulu kuliko mayai na mapochopocho huku wananchi wakifa kwa kukosa dawa hospitalini.
Dk Slaa, ambaye amekuwa akipinga kitendo cha serikali kutenga fedha nyingi kwa ajili ya kukirimu wageni, amesema atafyeka kabisa bajeti hiyo aliyoiita ya chai na vitafunwa ambayo alisema kiwango chake cha fedha huzidi vya baadhi ya wizara muhimu.
Dk Slaa alisema hayo jana katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika Bunazi, nje kidogo ya mji wa Bukoba ambako alisema ni aibu na fedheha kwa bajeti moja ya chai na vitafunwa ya serikali kutengewa Sh30 bilioni wakati bajeti ya wizara muhimu kama ya Maji na Umwagiliaji ikitengewa Sh29 bilioni.
"Huu ni ufisadi mkubwa; ni jambo la aibu na fedheha kubwa kwa wizara muhimu kama ya Maji na Umwagiliaji kutengewa bejeti ndogo ukilinganisha na ile chai na vitafunwa ambayo inaizidi kwa bilioni moja zaidi... angalieni wenyewe aibu hii. Nikiingia Ikulu, jambo la kwanza nitalimaliza tatizo hilo," alisema.
Alisema ataondoa magari ya anasa kwa kuhakikisha watendaji, wakiwemo mawaziri, wanatumia magari aina ya Toyota Land Cruiser-Hardtop maarufu kama mkonge, ambayo alisema bei yake ni Sh60 milioni tu badala ya magari aina ya Toyota Land Cruiser VX ambayo alisema moja hugharimu Sh200 milioni.
"Nipo tayari kwenye kula mihogo ikulu, badala ya mayai na mapochopocho mengine huku wananchi wangu wanakufa kwa kukosa dawa hospitalini. Serikali ya Chadema itasamehe starehe na anasa zote ili iwatumikie wananchi," alisema.
Akizungumzia suala la afya, Dk. Slaa alisema Bunge la kwanza la bajeti la serikali yake litatenga fedha za kutosha kwenye sekta ya afya ilio huduma zitolewe bure kwa kila Mtanzania tofauti na hali ilivyo sasa ambayo wenye uwezo wa kiuchumi tu ndio wenye uhakika wa matibabu bora.
"Mfano ni mimi mwenyewe. Nilivunjika mkono wangu huu (alinyoosha mkono wa kushoto juu), lakini ndani ya kipindi cha mwezi mmoja nimepona na kuweza kuendelea na maisha. Mimi nimeweza kwa sababu nina uwezo wa kulipa zaidi ya Sh4 milioni MOI (Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Muhimbili) Muhimbili. Je ni Watanzania wangapi wenye uwezo kama wa Dk Slaa," alihoji.
Alisema kutokana na bajeti ndogo ya wizara ya afya, Watanzania wengi wanahukumiwa hukumu ya kifo kwa kuendelea kusumbuliwa na hata kufa kutokana na magonjwa ambayo yanatibika na yalishafutika duniani kote.
Alitoa mfano ugonjwa hatari wa Malaria ambao unaoongoza kwa vifo vingi nchini licha ya kuwa ni ugonjwa unaotibika na kwamba hata katika maeneo mengine duniani ikiwemo, kisiwani Zanzibar umetokomezwa kabisa.
"Ni ajabu sana, na ni uthibitisho wa kukosa vipaumbele vya taifa kwa serikali ya CCM kujisifu kuwa inagawa vyandarua. Sasa hivi wanatangaza wanatoa viwili kwa kila familia. Sasa najiuliza, kwa familia yenye watu zaidi ya saba watafanya nini? Hii inamaanisha kuwa wale wengine waendelee kuumwa na mbu na kufa kwa malaria," alisema.
Wakati huo huo, helkota iliyokuwa ikitumiwa na mgombea huyo wa Chadema katika kampeni zake imetengemaa baada ya kupata hitilafu ya kiufundi na kusababisha mgombea huyo kufanya kampeni zake kwa kutumia magari katika mkoa wa Kigoma. Sasa itaanza kuchanja mbuga wakati Dk Slaa akielekea Mwanza kuendelea na kampeni zake.