Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Martin Luther King, Jr., Desmond Tutu, Frederick Chiluba
Chadema imekua na kukomaa zaidi tangu Dr. Slaa agombee urais awamu iliyopita, na alitikisa nchi hadi CCM kubabaika. Alimwaga ukweli bila waga. Hayuko tayari kurubuniwa wala kutetereka kwa vile azima ni kutetea watu si masilahi binafsi.
Katika historia tumeshuhudia mchungaji wa makanisa ya Baptisti nchini Marekani Martin Luther King, Jr kwa mgongo wa kanisa na msukumo wa moyo wa kujitolea kwa ajili ya wengine alifanikiwa kuigeuza mioyo migumu ya wazungu na kuridhia kuondoa sheria ngumu za kibaguzi nchini humo.
Askofu Desmond Tutu wa Afrika Kusini ni kiongozi pekee mpigania haki za Waafrika kupinga ubaguzi wa rangi kutetea hadharani kwa nguvu zote na kilichomsaidia kutoshikwa kuunganishwa na akina Mandela ni wadhifa wake wa Kanisa. Kamwe hatasahaulika katika historia ya ukombozi wa kupinga ubaguzi nchini humo.
Hayati Rais wa Zambia aliyemwondoa Kaunda madarakani back ground alitokana katika mgongo wa makanisa ya kipendekoste.
Je, historia kujirudia kwa Tanzania CCM kuondolewa kwa njia hiyo?