Dr Slaa na wabunge wawili wakamatwa

Nyie Chadema kuweni wakweli Banaaa.

Si msema wanahojiwa kutokana na kauli zao walizozitoa katika mikutano yao zenye kuashiria uvunjifu wa amani na uchochezi.

na ikibainika Nguvu za Doula lazima ziwaangukie kwa kishindo kikubwa sana mpaka wajute kuzaliwa nchi hii.

zimeshindwa kuwaangukiya mafisadi wanao liangamiza taifaletu haolitawaweza tujiulize jee? Kinachosemwana cdm nikweliau uzushi umatiwawatu unaoitikia maandamano hawanaakili?auhawanakazi? Vitisho kejeli sisuluhu kama madaiyao niyamsingi itashangaza kumwonamama anamfinya mwanaeanapolianjaa hatakikumnyonyesha wara kumpauji unategemea nini? Kamasimauwaji kupanda hgarama zamaisha umeme wanafunzikufeli okosefumadawahosipitalini umeme ufisadi nk kwambahayakunakuitaji kunawauso iliuyaone atakipofu anayaona kiziwi anayasikia tuachekibuli penyeukweli uongohujitenga wanasiasa wenyemajibumepesi kwenyemaswali magumu mudaumeisha
 
Wana JF mko biased sana. Nilipotoa hii taarifa mwanzo kama tetesi mkanikomalia kwa maneno MAKALI oh CCM. Sasa watu wamekuja na update ya the samething mnajifanya mnakimbilia mada. Acheni hizo. Nchi hii haiendi kwa JAZBA. Amani lazima ilindwe kwa gharama zozote.

Kweli mwanangu hasa kwa kumng'ooooa jk!
 
Hao polisi walikua wamefuata nini kama slaa alikua hajaruhusiwa kufanya mkutano? Wasitake kuvuruga watu waache waendelee kuandamana kwa amani.
 
mikutano yao zenye kuashiria uvunjifu wa amani na uchochezi.


Watanzania wa sasa sio wakudanganya. Wanaelewa kuwa kutochukua hatua za dhati za kuzibithi mfumko wa bei ndo uchochezi na uvunjifu wa amani. Lakini pia wanaelewa mahakama kutokutenda haki ktk na kuchelewesha kesi Mafisadi ndio uchochezi tena mbaya sana!. Zaidi wanajua Rais kutokumkamata mmilki wa DOWANs ambaye hakumfahamu mwanzo na sasa mejulikana ndo uchochezi hatari wa amani yetu.

Wito wangu kwa wana CCM (maana ndo wanajifanya hawaoni haya yanayoendelea nchini) ikiwamo na wabunge wao kuwa amani ya Tanzania inalindwa na italindwa tu pale HAKI INAPOTENDEKA. Ililindwa wakati wa Nyerere kwa sababu hakujilibilikizia mali yeye mwenyewe pamoja na watoto wake. AMANI haiwezi kuwepo kama ushaidi upo wa kutosha wa viongozi wetu kufanya kinyume na KATIBA ya Tanzania (japo nayo inampungufu yake).
 
Kumkamata Dr Slaa ni kosa kubwa sana! Serikali haijatumia Busara hata kidogo, matokeo yake yatakuwa Mabaya kweli,serikali Tatizo sio Dr Slaa Tatizo maisha yamekuwa magumu jamani! mfumuko wa bei usio wa kawaida ,hakuna ajira,tofauti ya masikini na matajiri imekuwa kubwa ktk historia ya Nchi Tangu dunia kuumbwa,Unyonyaji wa wazi kabisa,Mikataba ya udanganyifu,Tabaka la wakubwa limeongezeka, Ugandamizaji kama huu wa kumkamata Dr Slaa,Elimu kiwango Duni kabisa na haijawahi kushuhudiwa ktk historia ya Nchi tangu kuumbwa.

Jamani Serikali Mnawasha Moto,wazee wetu Babu zangu akina Butiku,Warioba,Kitine na wengine akina Msuya Mkowapi? mbona Mmekaa kimya na Nchi inaharibika! Saisieni Nchi hii itajengwa na watu wazalendo jamani! watoseni wanao haribu Nchi yetu.
 
misri libya na kwingineko walikamatwa wapinzani mara nyingi na wengine kunyongwa TV za mataifa zikionyesha live lakini mwisho tumeuona ngguvu ya umma ni sauti ya Mungu.
 
wanahojiwa na polisi kwa kuendesha mkutano jana. Cha ajabu jeshi la polisi lilikuwepo wakati wa mkutano kutoa ulinzi. Radio one

UPDATE: baada ya kuhojiwa kwa muda na polisi Kahama, Dr Slaa na wabunge wawili wa CHADEMA waachiwa hadi upelelezi utakapo kamilika. Wanaelekea kagera. RADIO1 STEREO.

ndiyo kishindo alichoacha 'mtalii' hiki?

CCM lazima kife tu!!!
 
Well done ! amani ya nchi lazima ilindwe kwa gharama zozote !

Ila wizi wa EPA,KAGODA,GREEN DEEP sijui nini hata vingine sasa inabidi tuwe na slide maana yamekuwa mengi sana,DOWANS,Richimond,TICS,IPTL AAA HAYO MAZURI TU YANASABABISHA AMANI,LAKINI MASIKINI WAKUBWA WANAOJIFANYA KUANDAMANA WATAIONA CHA MTEMA KUNI MAANA WANAVURUGA AMANI YA NCHI KWA KULALAMIKIA VIONGOZI WAO KUSHINDWA KUSIMAMIA WAJIBU WAO EEE! KAMA NI HIVYO BASI KAZI IPO NADHANI WAPELEKE VIFARU HAIWEZEKANI WALALAMIKE BWANA AMANI LAZIMA ILINDWE KWA GHARAMA YOYOTE DU
 
Viongozi wengi wa chadema ni madomokaya wasio na mkakati wowote wa kimaendeleo!...hawajui kutaifisha mali ni kinyume na katiba? kushuka kwa bei ya sukari kutaletwa na nguvu za soko huru(determined by demand and supply) na katiba yao inatetea soko huru,so wtf?
 
Ndugu yangu jazba za nini.

Kumbuka nchi hii inaendeshwa kwa kufuata utawala wa Sheria. Sasa sisemi umwondoe basi wewe au hao Chadema wajaribu tu kutaka kumwondoa waone nguvu za Doula zitaafanya nini.

Ile ya Arusha ilikuwa cha mtoto, Mnajazwa upepo tu ngojeni siku ukitolewa .

Kama JK aliwekwa madarakani na wananchi (na sio dola), ni wananchi hao hao ndio watakaomtoa madarakani, hakuna dola yoyote duniani iliyowahi kuzuia matakwa ya wananchi na ikafanikiwa! Kumbuka makaburu wa RSA na nyuklia/mizinga yao walisalimu amri mbele ya matakwa ya umma!
 
Habari za uhakika kutoka kwa diwani hapa kahama ni kwamba alipokuwa anapita kahama kuelekea Bukoba walimkamata kwa makosa haya:

1. Kufanya mkutano Malampaka bila kibali
2. Kwamba ametoa maneno ya uchochezi kwenye mkutano wa Maswa
3. Kwamba kuna nyaraka za siri wanazitafuta, wanahisi yeye anazo- hapo alikataa kukaguliwa

Magari mengi ya CHADEMA yalionekana kituoni na wananchi wakanusa kwamba Dr. amekamatwa wakaanza kusogea kituo cha polisi,

Wamemwachia na ameendelea na safari yake kwenda Bukoba muda mrefu.

Polisi wanasema ilikuwa ni mahojiano tu!!

Ooooph.....nafuu umenishusha pumzi. Nilishaanza kupanga mengine sa hizi.
 
Ina maana kila mkoa watakuwa wana kesi mbona kazi? Serikali ifike mahali ipambane na mataizo ya watanzania na siyo kuwazuia CHADEMA kufanya shughuli zao. Mbona wao wakiwa kwenye shughuli zao hakuna mtu anayewazuia au ni kwa sababu wana mamlaka na vyombo vya dola?
 
Moja ya vitu vinavyozungumzwa sana na vichwa vyenye PhD za ukweli kwenye hii mikutano na maandamano ni mfumuko wa bei unaoathiri bei za bidhaa ikiwemo sukari. Our most hopeless government ever imecopy hilo na kuanza kulifanyia kazi blindly kwenye sukari peke yake na kusahau bidhaa zingine. Anyway angalau watu watakunywa chai though bila vitafunwa.So hata ukiwa mtupu kiasi gani unao uwezo wa kutueleza kama maandamano yanabadilisha mambo au hapana. Tafakari usikukurupuke!
Vitafunwa tutapewa na mama jk,au yeye jk anaweza tushauri tuwe tunakunywa uji badala ya chai huku tukiimba maisha bora kwa kila Mtz
 
Nyie Chadema kuweni wakweli Banaaa.

Si msema wanahojiwa kutokana na kauli zao walizozitoa katika mikutano yao zenye kuashiria uvunjifu wa amani na uchochezi.

na ikibainika Nguvu za Doula lazima ziwaangukie kwa kishindo kikubwa sana mpaka wajute kuzaliwa nchi hii.

Mkuu., kusoma hujui hata picha huoni!
 
Back
Top Bottom