Dr. Slaa - Maaskofu wahubiri haki kwanza, amani zao la haki

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Wakati huohuo Joseph Senga kutoka Chunya anaripoti kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa, amewataka maaskofu kutohubiri amani na badala yake wahubiri kwanza kupatikana kwa haki.

Akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kanga, wilayani Chunya, jana, Dk. Slaa alieleza kushangazwa kwake na viongozi hao wa dini ambao wanahubiri sana suala la amani ambalo ni tunda la haki. "Nawaomba hawa maaskofu wanisamehe tu, kuhubiri amani wakati hakuna haki haitoshi," alisema Dk. Slaa.

Alisema kuwa maaskofu wanashutumu vyama vya siasa vinaharibu amani wakati amani ni zao la haki. Amesema baadhi ya maaskofu na masheikh wamekuwa wakiunga mkono yanayotolewa na viongozi mbalimbali ambao wao wana maslahi katika hilo.

"Yesu alihubiri haki kwanza, na hawa wanatakiwa kuzingatia hilo kwani amani haiwezi kuwepo bila haki," alisema.


Tanzania daima
 
Nakubaliana naye kwani mahubiri ya msingi yawe kudai haki ipatikane ili amani idumu. Kamwe amani haitapatikana kama haki inakiukwa.

Mfano wamarekani wanavyohangaika kutifua kundi la magaidi ni kutokana na haki kutozingatiwa katika masuala ya haki za binadamu duniani wamarekani wakiwa ndio vinara. Mbona matajiri duniani kama Canada, Japan nk hayakumbwi na wimbi la kufuatwa na magaidi?
 
Kukiwa na haki na amani ya kweli inakuwepo sio hii ya sasa ya kiujanja ujanja. Kwa hili nakubaliana na Dr. Slaa
 
Dr Slaa nakuunga mkono viongozi wa dini waunge mkono kupatikana kwa haki kwanza badala kuwa wanafiki kuhubiri amani wakati haki hakuna.
 
Nakubaliana naye kwani mahubiri ya msingi yawe kudai haki ipatikane ili amani idumu. Kamwe amani haitapatikana kama haki inakiukwa.

Mfano wamarekani wanavyohangaika kutifua kundi la magaidi ni kutokana na haki kutozingatiwa katika masuala ya haki za binadamu duniani wamarekani wakiwa ndio vinara. Mbona matajiri duniani kama Canada, Japan nk hayakumbwi na wimbi la kufuatwa na magaidi?
Sasa mkuu wangu Wamarekani wanaingia vipi hapa.. Sijui kama unaelewa kwamba Marekani wanaitafuta haki pale tu penye interest zao na wako tayari kuvunja Amani.
Toka nimerudi majuu ni mwezi mzima leo, lakini sijaona kabisa ktk CNN wala BBC mauaji yanayofanyika Bahrain au Yemen (wana interest) lakini kila siku habari ni Libya na Syria wakati kinachofanyika huko kote ni kile kile..

Mimi nachoweza kusema ni kwamba Maaskofu wasijihusishe kabisa na siasa wafundishe dini kwani hiyo Haki na Amani vinapatikana kwanza ktk imani (kiroho) na sii kimwili..Nikiwa na maana kwamba unapofundisha gospel pasipo nukuu za aya za Biblia Ukafuata vitendo vinavyotokea hapa na pale kuwa ndio somo, hapo unaanza kufundisha gospel ya binadamu yaani mafundisho yako yanatokana na matendo ya wanadamu (Siasa)..
 
Sasa mkuu wangu Wamarekani wanaingia vipi hapa.. Sijui kama unaelewa kwamba Marekani wanaitafuta haki pale tu penye interest zao na wako tayari kuvunja Amani.
Toka nimerudi majuu ni mwezi mzima leo, lakini sijaona kabisa ktk CNN wala BBC mauaji yanayofanyika Bahrain au Yemen (wana interest) lakini kila siku habari ni Libya na Syria wakati kinachofanyika huko kote ni kile kile..

Mimi nachoweza kusema ni kwamba Maaskofu wasijihusishe kabisa na siasa wafundishe dini kwani hiyo Haki na Amani vinapatikana kwanza ktk imani (kiroho) na sii kimwili..Nikiwa na maana kwamba unapofundisha gospel pasipo nukuu za aya za Biblia Ukafuata vitendo vinavyotokea hapa na pale kuwa ndio somo, hapo unaanza kufundisha gospel ya binadamu yaani mafundisho yako yanatokana na matendo ya wanadamu (Siasa)..

Ili dondoo ieleweke zaidi hutumika mifano inayoweza kutoa picha ya jambo linazoongelewa. Mfano wa Wamarekani kuchukiwa na baadhi ya mataifa au kufuatwa na magaidi ni kutokana na ukiukwaji wa haki za msingi kwa mataifa hayo. Mapato yake amani inakosekana duniani na kufikia hatua ya kuyumbisha uchumi wa dunia. Wanaoathirika ni dunia nzima wakiwemo wamarekani, lakini hawakati mzizi wa fitina ila matawi yake.
 
Wakristo tunahubiri habari njema za Yesu Kristo - imani, upendo kwa Mungu na watu wote, na matumaini ya wokovu. Justice has been done at the cross! The price has been paid by the blood of Jesus christ! We are free.

Wanasiasa ndio wahubiri wajibu na haki. wakishindwa waachie ngazi
 
Ili dondoo ieleweke zaidi hutumika mifano inayoweza kutoa picha ya jambo linazoongelewa. Mfano wa Wamarekani kuchukiwa na baadhi ya mataifa au kufuatwa na magaidi ni kutokana na ukiukwaji wa haki za msingi kwa mataifa hayo. Mapato yake amani inakosekana duniani na kufikia hatua ya kuyumbisha uchumi wa dunia. Wanaoathirika ni dunia nzima wakiwemo wamarekani, lakini hawakati mzizi wa fitina ila matawi yake.
Mkuu wangu nchi zote nazozijua mimi huwa zina amani kabla Marekani hajaingia kati. Marekani akisha kuwa na interest zake mahala basi jua haki itaondoka na wataanzisha makundi kuipinga serikali iliyopo. Kwa Mfano, Afghanstan unaweza kunipa sababu ya wao kuwepo huko ikiwa Osama alikuwa Pakistan na wahusika wote wa 9/11 ni Wasaudia?...Leo hii Afghan ndio hakujna haki kabisaaaa..

Haya Gadhaffi miaka yote zaidi ya ishirini alikuwa salama pamoja na kufungiwa kiuchumi, wananchi wake walipata elimu hadi chuo kikuu bure, walipewa nyumba bure kwani Libya swala la kutafuta nyumba sii la mwananchi ila ni jukumu la serikali kukupatia nyumba..
Kosa la Ghaddaff ni kuwaelemisha wananchi wake, nchi imefungiwa kiuchumi hakuna ajira za kutosha ingawa walikuwa wanapata zaka, kisha akaamua kuwaingiza Waingereza na na deal la Shell miaka miwili iliyopita. Hapo ndipo alipokiona cha moto Waingereza na MI6 pamoja na CIA wakaingia na kuanzisha propaganda zao dhidi ya Ghadaff na leo hii ndio tunayaona...

Kifupi hakuna nchi isiyokuwa na haki kama Marekani kwani hadi leo hii zipo sehemu wewe Mmatumbi (mtu mweusi) huwezi kuishi na utabaguliwa. Tuseme nchi zote za Ulaya Ubaguzi ni utamaduni wao lakini wao wepesi sana kusema nchi nyingine. Sijui kama uliwahi kuona yaliyofanyika Philly wakati wa mkutano wa G8 miaka michache iliyopita...Amani huwezi kuitafuta kwa vita na mabomu bali ni ubabe kama CCM walivyofanya Pemba mwaka 2000..
 
Dr. Slaa nakupongeza kwa kulisema hilo wazi wazi. Baadhi ya Maaskofu wanaelekezwa vitu vya kuhubiri. Inanishangaza sana tunapowaona Watanzania wamekuwa wanyonge pale wanapoishi maisha ya shida huku viongozi wao wakiendelea kuwagandamiza kwa kodi na michango mingi, wakati huo huo raslimali za wananchi zinaondoka na huku kodi kidogo zinatumiwa kwa anasa na viongozi.

Wananchi wanapoeleweshwa kudai haki zao na kuzidai wanaambiwa wasivuruge amani. Je, wananchi wakibaki kulinda amani huku raslimali zao zinaondoka nani wa kulaumiwa. Kuhubiri kuwa wananchi wakae kimya ni sawa na kuwaambia kuwa mnapoibiwa msihangaike kuokoa mali zenu
 
Back
Top Bottom