Dr. Slaa, Lipumba, Sendeka na Anna Mghwira

sirluta

JF-Expert Member
Nov 28, 2012
6,325
2,486
Nawaona kama watu muhimu katika serikali ya Dr Magufuli endapo watapata nafasi kwani wamekuwa wakionyesha uwezo wao katika nyanja mbali mbali za kisiasa. Ni mawazo yangu lakini.

Dr. Slaa katika mambo ya kimataifa anafaa sana.

Sendeka pale bungeni anafaa sana katika kujenga hoja

Lipumba katika mambo ya uchumi pia anafaa.

Mghwira katika mambo ya maendeleo ya jamii akishirikiana na Mama Magreth Sitta watasaidiana kutatua changamoto nyingi za jamii.

Nawasilisha.
 
KWA serikali ipi ya ccm ?? wataisoma namba.
nafasi zishajaaa washalipana fadhila .

tatizo nchi yetu hatuongozi kwa manufaa ya nchi Bali kwa manufaa ya kulipana fadhila
 
Slaa na Mambo ya kimataifa!!!!! Daah!
After all wameshamalizana,
"They dont know him, He dont know them"
 
mkuu kwani hao uliowataja hapo si washirika wa ccm,dr.slaa alikuwa anafany kazi ya kuuchafua upinzan so lazima ccm ilipe fadhila
 
Nawaona kama watu muhimu katika serikali ya Dr Magufuli endapo watapata nafasi kwani wamekuwa wakionyesha uwezo wao katika nyanja mbali mbali za kisiasa. Ni mawazo yangu lakini.

Dr. Slaa katika mambo ya kimataifa anafaa sana.
Sendeka pale bungeni anafaa sana katika kujenga hoja
Lipumba katika mambo ya uchumi pia anafaa.
Mghwira katika mambo ya maendeleo ya jamii akishirikiana na Mama Magreth Sitta watasaidiana kutatua changamoto nyingi za jamii.
Nawasilisha.
Huyo Slaa na Lipumba tayari walishakabidhiwa chao kwa ajili ya 'special mission' ya kuiangamiza Ukawa, sasa unataka CCM baada ya tayari kupata kile walichokuwa wanakitaka wataona tena umuhimu wa hao watu?
Hao watu hivi sasa wanaonekana kama 'rubbish' ambapo hawahitajiki tena kwenye hicho chama ambacho kina wenyewe.
 
Ccm imekamilika haikodi viongozi wamejaa tele. Mambo ya kukodi ni kwa wachaga kule
 
Ana mughwira,amwamwimbie wamuombee kwa ccm amewe ubunge wa viti malumu kupitia viti kumi vya Rais
 
Kwa nini tunapenda sana ku-recycle viongozi? Hawa wote uliowataja walishapata nafasi wakafanya walichofanya. Kwa nini tusiwape nafasi watu wengine wenye uwezo zaidi? Kwa nini baraza la mawaziri lisiundwe na technocrats? Kama walivyofanya Kenya? Mama Sitta, Ole Sendeka watatusaidia nini karne hii ya 21 zaidi ya kutupotezea muda? Tufikirie nje ya box. Tusifikiri kwamba nafasi za uongozi serikalini ni kulipana fadhila au zawadi kwa washirika wetu. Hivi kweli bado unaamini tunahitaji hawa watu kama tunataka kujenga uchumi wa kisasa, unaoendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia?
 
Ana mughwira,amwamwimbie wamuombee kwa ccm amewe ubunge wa viti malumu kupitia viti kumi vya Rais

Hebu nisaidie kidogo historia ya huyu mama? Naona siku za karibuni amepata sifa nyingi ila sijaweza kujua sifa hizo zinatokana na nini? Na CCM wanampenda sana, pengine kwa kuwa hakuonesha kuikosoa serikali ya CCM? Ukiona wewe ni kiongozi wa chama cha upinzani na CCM wanakusifia, basi ujue hufanyi kazi yako sawasawa.
 
Kwa nini tunapenda sana ku-recycle viongozi? Hawa wote uliowataja walishapata nafasi wakafanya walichofanya. Kwa nini tusiwape nafasi watu wengine wenye uwezo zaidi? Kwa nini baraza la mawaziri lisiundwe na technocrats? Kama walivyofanya Kenya? Mama Sitta, Ole Sendeka watatusaidia nini karne hii ya 21 zaidi ya kutupotezea muda? Tufikirie nje ya box. Tusifikiri kwamba nafasi za uongozi serikalini ni kulipana fadhila au zawadi kwa washirika wetu. Hivi kweli bado unaamini tunahitaji hawa watu kama tunataka kujenga uchumi wa kisasa, unaoendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia?

Mkuu wapi kitufe cha like??? Yaani huwa nakereka sana na haya mawazo mgando ya viongozi wale wale, eti Olesendeka, mara Slaa, mara Sitta atafaa uspika, mara Shukuru kawambwa anafaa elimu etc. Hivi hapa Tanzania watu wengine wamesoma kwa ajili ya nini?
 
Tunaposema ELIMU, ELIMU, ELIMU ndio maanake. Tunataka tuone sura mpya tena vijana kwenye baraza la mawaziri.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom