Dr Slaa atakuwa mgeni rasmi katika mahafali ya darasa la saba Queens' schools (Nursery and Primary) iliyopo Ukonga Dar es Salaam. Shule hiyo ipo karibia na kituo cha Polisi Sitakishari njia panda ya Segerea kama unatokea maeneo ya Uwanja wa Ndege. Kama unatokea Tabata ukifika Mbuyuni elekea njia ya Airport na ukivuka tu daraja utaona kibao cha Queens, kama unatokea upande mwingine ni kabla hujavuka daraja.
Wananchi wote mnakaribishwa na hasa wale wenye watoto wanaotarajia kujiunga mwaka 2013. Shule hii ilipewa cheti cha pongezi mwaka jana kufaulisha wanafunzi wote na inafanya vizuri sana katika taaluma. Karibu umsikilize Dr wa ukweli, njoo ujionee shule iliyopania kukijenga kizazi kipya chenye fikra mpya.
Mahafali yataanza saa 4 asubuhi kesho jumapili tarehe 28/10 na kutakuwa na burudani lukuki.
Source: Tangazo lililotolewa na uongozi wa shule hiyo makini
Wananchi wote mnakaribishwa na hasa wale wenye watoto wanaotarajia kujiunga mwaka 2013. Shule hii ilipewa cheti cha pongezi mwaka jana kufaulisha wanafunzi wote na inafanya vizuri sana katika taaluma. Karibu umsikilize Dr wa ukweli, njoo ujionee shule iliyopania kukijenga kizazi kipya chenye fikra mpya.
Mahafali yataanza saa 4 asubuhi kesho jumapili tarehe 28/10 na kutakuwa na burudani lukuki.
Source: Tangazo lililotolewa na uongozi wa shule hiyo makini