Amakando
Senior Member
- May 9, 2011
- 158
- 27
Wana jamvi nimetafakari swala la kutokuhudhuria kwa Dr Slaa katika kikao cha wajumbe wa CDM na Rais Kikwete sambamba na mambo yaliojiri nikapata majibu kuwa huenda Marehemu Sheikh Yahya alikuwa mtabiri wa Ukweli kwa sababu zifuatazo.
a) Alitabiri kuwa Dr Slaa na Kikwete watakaa pamoja na kukumbatiana kabla mwaka haujamalizika.
b) Mwitikio wa haraka wa Mheshimiwa Rais wa kukubali kukutana na wana CDM hasa ukizingatia kuwa Dr Slaa alikuwa miongoni mwa majina tajwa katika kamati iliyoteuliwa na CDM kumuona Rais japo hakutokea, je inawezekana Rais nae alikuwa ana kumbukumbu za utabiri huu.
c) Kwa kuwa hakuna sababu maalumu mpaka sasa ya kutokuwepo kwa Dr Slaa katika kikao kile nafikiri Dr aliona asitekeleze kwa makusudi ili kuepuka utabiri kutimia kikamilifu.
d) Katika utabiri alisema kuwa hawa wanasiasa wakionana hali itakuwa shwari na hii inanielekeza kuamini hivyo kutokana na kauli ya Mh Freeman Mbowe kuwa baada ya makubaliano kwa sasa hakutakuwa na maandamo tena.
Wanajamvi nawasilisha.
a) Alitabiri kuwa Dr Slaa na Kikwete watakaa pamoja na kukumbatiana kabla mwaka haujamalizika.
b) Mwitikio wa haraka wa Mheshimiwa Rais wa kukubali kukutana na wana CDM hasa ukizingatia kuwa Dr Slaa alikuwa miongoni mwa majina tajwa katika kamati iliyoteuliwa na CDM kumuona Rais japo hakutokea, je inawezekana Rais nae alikuwa ana kumbukumbu za utabiri huu.
c) Kwa kuwa hakuna sababu maalumu mpaka sasa ya kutokuwepo kwa Dr Slaa katika kikao kile nafikiri Dr aliona asitekeleze kwa makusudi ili kuepuka utabiri kutimia kikamilifu.
d) Katika utabiri alisema kuwa hawa wanasiasa wakionana hali itakuwa shwari na hii inanielekeza kuamini hivyo kutokana na kauli ya Mh Freeman Mbowe kuwa baada ya makubaliano kwa sasa hakutakuwa na maandamo tena.
Wanajamvi nawasilisha.