Elections 2010 Dr. Slaa: CCM imebanwa Igunga; yajipanga kuchakachua kura

palalisote

JF-Expert Member
Aug 4, 2010
8,335
1,455
ZIKIWA zimesalia siku nne kabla ya wananchi wa Igunga kuamua nani atakuwa mbunge wao, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbroad Slaa amenasa siri nzito ya jinsi vigogo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), walivyojipanga kuiba kura.

Dk. Slaa alisema kwa takriban wiki moja sasa, CCM imekuwa ikifanya mbinu mbalimbali na juzi na jana walikuwa na vikao vizito kupanga jinsi ya kuiba kura baada ya kubaini kuwa chama hicho hakiwezi kushinda. “Safari hii, CCM wamekabwa kwelikweli na ukiona mtu mzima (CCM), analalamika, ujue ameshikwa mabaya. Sasa kwa kujua hilo, wamepanga mikakati ya kuiba kura. Jana walikuwa na kikao cha siri kilichofanyika Peac Hotel na leo walikuwa na kikao kingine, mipango na kila walichojadili nimepata,” alisema Dk. Slaa.

Dk. Slaa ambaye amepata kuwa mgombea urais wa CHADEMA katika uchaguzi uliopita na kutoa ushindani mkubwa kwa mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, alitaja mbinu nyingine ya CCM kuhakikisha inapata ushindi kuwa ni pamoja na kutengeneza kura hewa, kuchoma karatasi za kula kama walivyofanya Msalala, kununua shahada na kuwapiga wafuasi wa CHADEMA.

“Kama mlivyosikia, tayari wameanza kuwapiga watu wetu, wameanza kuwapa vitisho, vijana wanakamatwa na kuwekwa ndani hovyo ili kuwatisha,“ alisema Dk. Slaa.

Kiongozi huyo wa CHADEMA, pia alisema mbinu nyingine inayotumiwa na CCM ni kumwaga pesa na kutolea mfano wa kijiji cha Karenga ambacho kimepewa sh milioni 10 kwa kisingizio cha kutumika kwenye miradi ya maendeleo, jambo ambalo alisema sio kweli.
“Katika baadhi ya vijiji jana nilishuhudia mwenyewe watu wa CCM wakigawa mahindi. Vijiji hivyo ni Mwamwapuli, Mwamwagogo na vingine ambavyo sivikumbuki kwa sasa, kote huko waligawa mahindi ili kuwarubuni wawapigie kura,” alisema Dk. Slaa.

Hata hivyo pamoja na mbinu zote hizo za kuiba kura, Dk. Slaa alisema chama chake kimejipanga vizuri na kuwahakikisha wanachama wake kuwa hakuna kura itakayoibwa.

“Nakuhakikishia, mbinu zote tunazijua, tumejipanga vizuri sana kuhakikisha hakuna hata kura moja itakayoibwa au kuchomwa moto. Tutapambana hadi tone la mwisho na tuko tayari kufia kwenye vituo vya kupigia kura,” alitamba Dk. Slaa.

Alilitahadharisha jeshi la polisi pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa makini siku hiyo, vinginevyo taifa linaweza kuingia katika matatizo mazito sababu ya kuibeba CCM ambayo alisema kwa sasa haibebeki.

Malalamiko ya Dk. Slaa, yaliungwa mkono na Chama cha Wananchi (CUF) ambacho kimedai kuwa CCM ina mpango wa kuiba kura na inacheza rafu kwa kuleta malori saba ya sukari, kugawa mahindi na kuingiza Janjawid ili kuwatisha wananchi wa Igunga siku ya kupiga kura.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF bara, Julius Mtatiro, aliliambia gazeti hili kuwa malori hayo yako njiani kutoka Mara kuelekea Igunga kwa lengo la kugawa kwa wapigakura.

“Kwa sababu vyombo vya dola ukiripoti havitachukua hatua kwa vile wanailinda CCM, tumejipanga vya kutosha kuyadhibiti malori hayo, tunazo taarifa za kutosha tunajua yamelala wapi juu wameweka nini, chini wameweka nini.

“Tumewapanga vijana wetu na tutayakamata kwa nguvu zetu kisha tutawaonyesha waandishi wa habari na taifa lione, tunatoa tahadhari kwamba mbinu zao zimegundulika, makontena ya sukari yanaletwa Igunga ili kuigawa siku mbili kabla ya kupiga kura.

“Hatutakubali haki za Watanzania kuchagua kiongozi bora ziondolewe kwa sababu ya kilo za sukari…tunalishughulikia hili,” alisisitiza kiongozi huyo wa timu ya kampeni za CUF Igunga.

Aidha, ameionya CCM kuacha mpango wa kutaka kugawa mahindi Septemba 30 na Oktoba mosi kwa wakazi wa jimbo hili kwa kuwa hiyo ni rushwa wanayoitoa kwa mgongo wa njaa.

CHANZO. GAZETI LA TANZANIA DAIMA
 
mmeanza kuleta visingizio sasa.chadema inatoa vitisho kuwa itapambana mpaka tone la mwisho, kwani tuko vitani?,tuko tayari kufia kwenye vituo vya kupigia kura,jamani hivi sinivitisho?.visingizio vya nini kama unauhakika wa kushinda?.nyie kila siku mnaibiwa na njia za wizi mnazifaham kwanini msizitumie kama mnazifaham sasa?.
 
Sambamba na mipango hiyo, habari iliyonifikia kutoka kwenye chanzo kinachofanya kazi ili kufanikisha mpango huo ni kwamba CCM wameamua kupeleka mamluki toka mikoa mingine hasa Dar. Chanzo hicho kinadokeza kuwa kuna vijana waliopelekwa Igunga kutokea Dar es salaam ili wakasaidie CCM.

Miongoni mwa kazi wanazofanya ni

(i) Kuhakikisha wanashangilia sana kwenye kampeni za CCM ili kuoesha kuwa chama hicho kinakubaliwa

(ii) Kufanya fujo, kutisha na kupiga wananchi kwa kujifanya wao ni supporters wa vyama vya Upinzani.

(iii) Kwa kutumia kadi na majina feki watatumiwa kupiga kura ili kukipatia ushindi CCM

Wengi wa vijana hao ni wale wanao patikana kwenye vijiwe, na wengi wao ni madereva Bajaji, Madereva Pikipiki na wale wasio kuwa na kazi maana huko wanalipwa.

Source ni muhusika anayehusika kufanya kazi hiyo huku akiamlishwa na walio juu yake. Anafanya hayo kulinda kitumbua chake ila hafurahishwi na mipango hiyo.

Mpango wa CDM wa kulaza helkopita yao Nzega tena kwenye kituo cha polisi nao umeonesha kuharibu mipango ya CCM walio kuwa wameshapanga. Kitendo hicho kimeonesha kuwazidi kete maana walishapananga kuichoma moto, ila issue inabaki itachomwaje ikiwa polisi.

My take CDM kuweni makini sana kwa kila hatua na mipango mnayo ipanga. Mnayo support toka kwa hao waliotumwa wengine, ingawa hawajioneshi ila mnatakiwa kuwa makini kwa kila movement mnayofanya.

Imarisheni ulinzi wa kura. Hakikisheni vizuri majina ya wapiga kura na je anayepiga ndiye aliyeandikishwa! Hakuna kulala.
 
Nadhani kama wamegundua mbinu hizo kama alivoziainisha basi ni kudhibiti,kuanzia hayo malori ya sukari,mahindi na inshu ya kuchoma kura au kupandikiza zingine. mawakala wawekwe kuhakikisha hilo halitendeki. Otherwise itakuwa ni kuweweseka tu so far so good naombea upinzani CDM ama CUF washinde jimbo hilo kutoka kwa manyang'au ccm
 
mmeanza kuleta visingizio sasa.chadema inatoa vitisho kuwa itapambana mpaka tone la mwisho, kwani tuko vitani?,tuko tayari kufia kwenye vituo vya kupigia kura,jamani hivi sinivitisho?.visingizio vya nini kama unauhakika wa kushinda?.nyie kila siku mnaibiwa na njia za wizi mnazifaham kwanini msizitumie kama mnazifaham sasa?.
Kuna hoja katika hayo yaliyosemwa na Dr. Slaa na siyo kuishia kusema tu kuwa kila siku nyie. Ni jambo lililo wazi kuwa kuna upendeleo wa hali juu kuanzia uripotiji wa habari hadi vyombo vya dola. Cha msingi narejea kauli fulani iliyowahi kutolewa na mwanasiasa mmoja kuwa "KUWA IKITAKA KUISHINDA CCM BASI ISHINDE KWA KURA NYINGI ILI HATA WAKITAKA KUIBA BASI WASHINDWE" Kauli hiyo inabidi kufanyiwa kazi kwa vitendo na watu kujitoa mhanga ili kuhakikisha haki yao haipotei.
 
Kuna hoja katika hayo yaliyosemwa na Dr. Slaa na siyo kuishia kusema tu kuwa kila siku nyie. Ni jambo lililo wazi kuwa kuna upendeleo wa hali juu kuanzia uripotiji wa habari hadi vyombo vya dola. Cha msingi narejea kauli fulani iliyowahi kutolewa na mwanasiasa mmoja kuwa "KUWA IKITAKA KUISHINDA CCM BASI ISHINDE KWA KURA NYINGI ILI HATA WAKITAKA KUIBA BASI WASHINDWE" Kauli hiyo inabidi kufanyiwa kazi kwa vitendo na watu kujitoa mhanga ili kuhakikisha haki yao haipotei.
Mkuu! Kwa mtazamo wangu bila shaka pale Igunga hawa magamba wakitaka pachimbike wajaribu wanachotaka kufanya. Wao wana pesa,CDM wana MUNGU.
 
Sambamba na mipango hiyo, habari iliyonifikia kutoka kwenye chanzo kinachofanya kazi ili kufanikisha mpango huo ni kwamba CCM wameamua kupeleka mamluki toka mikoa mingine hasa Dar. Chanzo hicho kinadokeza kuwa kuna vijana waliopelekwa Igunga kutokea Dar es salaam ili wakasaidie CCM. Miongoni mwa kazi wanazofanya ni

(i) Kuhakikisha wanashangilia sana kwenye kampeni za CCM ili kuoesha kuwa chama hicho kinakubaliwa

(ii) Kufanya fujo, kutisha na kupiga wananchi kwa kujifanya wao ni supporters wa vyama vya Upinzani.

(iii) Kwa kutumia kadi na majina feki watatumiwa kupiga kura ili kukipatia ushindi CCM
Wengi wa vijana hao ni wale wanao patikana kwenye vijiwe, na wengi wao ni madereva Bajaji, Madereva Pikipiki na wale wasio kuwa na kazi maana huko wanalipwa.

Source ni muhusika anayehusika kufanya kazi hiyo huku akiamlishwa na walio juu yake. Anafanya hayo kulinda kitumbua chake ila hafurahishwi na mipango hiyo.

Mpango wa CDM wa kulaza helkopita yao Nzega tena kwenye kituo cha polisi nao umeonesha kuharibu mipango ya CCM walio kuwa wameshapanga. Kitendo hicho kimeonesha kuwazidi kete maana walishapananga kuichoma moto, ila issue inabaki itachomwaje ikiwa polisi.

My take CDM kuweni makini sana kwa kila hatua na mipango mnayo ipanga. Mnayo support toka kwa hao waliotumwa wengine, ingawa hawajioneshi ila mnatakiwa kuwa makini kwa kila movement mnayofanya. Imarisheni ulinzi wa kura. Hakikisheni vizuri majina ya wapiga kura na je anayepiga ndiye aliyeandikishwa! Hakuna kulala.

CCM wana roho mbaya kama mashetani. Wanaoijua tabia ya shetani huwa hawapendi maendeleo mazuri ila wanaushawishi wa kuangamiza. Yaani waichome helkopta kwa ajili ya kumpeleka Kafumu bungeni, Kafumu mwenywe muongo kama nyoka alivyojichubua na kusema amejitoa gamba. Kumbafu kabisa.
 
mmeanza kuleta visingizio sasa.chadema inatoa vitisho kuwa itapambana mpaka tone la mwisho, kwani tuko vitani?,tuko tayari kufia kwenye vituo vya kupigia kura,jamani hivi sinivitisho?.visingizio vya nini kama unauhakika wa kushinda?.nyie kila siku mnaibiwa na njia za wizi mnazifaham kwanini msizitumie kama mnazifaham sasa?.

wewe tahira wa wapi..hujui hata vita ni nini?
 
mmeanza kuleta visingizio sasa.chadema inatoa vitisho kuwa itapambana mpaka tone la mwisho, kwani tuko vitani?,tuko tayari kufia kwenye vituo vya kupigia kura,jamani hivi sinivitisho?.visingizio vya nini kama unauhakika wa kushinda?.nyie kila siku mnaibiwa na njia za wizi mnazifaham kwanini msizitumie kama mnazifaham sasa?.

Mkuu kwa madaraka uliyo nayo huko kwenye chanma chenu cha magamba hustahili kabisa kuzungumza manenno kama haya!!!!!!!!! bwahaha ahahah ahahaha ahahaha ahahahah!!!!
 
Only I can push is for cdm to get tactical and protecting all the votes. Starting today, cdm should have plans to check all voting boxes before the votes and to protect all polling stations and vote counting. cdm must have a plan for responding to all voting criminality, even to remove this gov.

cdm must make this clear, ccm are not supported by the people and full of arm gangs!

ccm can only fool the foolishness!

 
Mods isitoshe tu kuiondoa Post ya Omr isipokua mngempa Ban ya ukweli kwa sababu hawezi mtukana Dr Slaa ndio maana nilijaribu kureply nikaambiwa sina access hyo,kipi cha ajabu ambacho Dr Slaa kakosea juu ya hizo wakati inajulikana wazi kua CCM ni wezi wakubwa wa kura na wanajulikana na mbinu zao chafu za kuiba kura? Madai ya Dr Slaa yana ukweli kabisa sio kupuuza kama baadhi ya wana Magamba wanavyotaka kutuaminisha hapa.
 
Ukiona mtu mzima tena ana PHD ya ucha mungu kutoka vatikan anadanganya ujue anazeeka vibaya na ndio matatizo ya kuanza mapenzi uzeeni haya.Kulalama kwa chadema na cuf ni alama tosha kuwa CCM imeisha shinda.
 
Kuna hoja katika hayo yaliyosemwa na Dr. Slaa na siyo kuishia kusema tu kuwa kila siku nyie. Ni jambo lililo wazi kuwa kuna upendeleo wa hali juu kuanzia uripotiji wa habari hadi vyombo vya dola. Cha msingi narejea kauli fulani iliyowahi kutolewa na mwanasiasa mmoja kuwa "KUWA IKITAKA KUISHINDA CCM BASI ISHINDE KWA KURA NYINGI ILI HATA WAKITAKA KUIBA BASI WASHINDWE" Kauli hiyo inabidi kufanyiwa kazi kwa vitendo na watu kujitoa mhanga ili kuhakikisha haki yao haipotei.

Niliisha wahi kuuliza swali humu ndani ya JF na hakuna hata mmoja aliyejibu. Na nauliza tena ' KURA ZINAIBIWAJE?'
 
Mods isitoshe tu kuiondoa Post ya Omr isipokua mngempa Ban ya ukweli kwa sababu hawezi mtukana Dr Slaa ndio maana nilijaribu kureply nikaambiwa sina access hyo,kipi cha ajabu ambacho Dr Slaa kakosea juu ya hizo wakati inajulikana wazi kua CCM ni wezi wakubwa wa kura na wanajulikana na mbinu zao chafu za kuiba kura? Madai ya Dr Slaa yana ukweli kabisa sio kupuuza kama baadhi ya wana Magamba wanavyotaka kutuaminisha hapa.

CDM bana mkipingwa kidogo kwa hoja zenu dhaifu mnazoleta ndani, mnaanza kuwatishia watu kuwa ban, sasa hapo watu wataacha kuamini vp kuwa JF ni jukwaa la CDM? ni ngumu kulibishia hili labda uwe zuzu
 
Niliisha wahi kuuliza swali humu ndani ya JF na hakuna hata mmoja aliyejibu. Na nauliza tena ' KURA ZINAIBIWAJE?'

Hata hapo juu kabisa imeelezwa.
Kuchoma moto/kuharibu kwa makusudi kura za mpinzani wako, kurubuni mawakala wa mpinzani wako ili muhujumu, kushiriki katika kuelekeza wapiga kura kumpigia kura (ndani ya kituo cha kura) mgombea wako, kuchukua shahada za wapiga kura hasa wale ambao unaamini watampigia mpinzani wako, kutoa vitisho kwa wapiga kura ambao unaamini ni wa mpinzani wako, kuingiza kura hewa ndani ya ballot box........njia zipo nyingi sana zinazotumiika na magamba.
 
Sina hakika kama tangu mfumo wa vyama vingi TZ uanze, kuna hata mara moja CCM waliwahi kushinda kihali!
 
mmeanza kuleta visingizio sasa.chadema inatoa vitisho kuwa itapambana mpaka tone la mwisho, kwani tuko vitani?,tuko tayari kufia kwenye vituo vya kupigia kura,jamani hivi sinivitisho?.visingizio vya nini kama unauhakika wa kushinda?.nyie kila siku mnaibiwa na njia za wizi mnazifaham kwanini msizitumie kama mnazifaham sasa?.

Twahil kwanini unafanya watu wote watoto? Unajua fika kinachoendelea na unajua wazi kuwa watu wote wanajua kuwa dola na ccm ni moja. Kesi ya ngedere kuamuliwa na nyani haki itapatikana? Tutaendeleza kesi zetu kwenye majukwaa kama haya ili tuweke wazi uozo wenu! Ipo siku kamba itakata jiwe!
 
Hata hapo juu kabisa imeelezwa.
Kuchoma moto/kuharibu kwa makusudi kura za mpinzani wako, kurubuni mawakala wa mpinzani wako ili muhujumu, kushiriki katika kuelekeza wapiga kura kumpigia kura (ndani ya kituo cha kura) mgombea wako, kuchukua shahada za wapiga kura hasa wale ambao unaamini watampigia mpinzani wako, kutoa vitisho kwa wapiga kura ambao unaamini ni wa mpinzani wako, kuingiza kura hewa ndani ya ballot box........njia zipo nyingi sana zinazotumiika na magamba.

Kama ndivyo basi huwa mnashindwa kihalali . Mbinu mnazijua na mnasema mnazidhibiti halafu mnashindwa, hapo hakuna kuibiwa kura huwa mnashindwa kihalali.
 
Back
Top Bottom