Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Ukiona mtu anaanza kuota kuibiwa ujue hayo ni maandalizi ya kufanya fujo watakaposhindwa waseme si tulisema wataiba kura?. Haiingii akilini umegundua njama, unajua njia zinazotumika kuoba, umeweka mawakala kila kona, kura zinahesabiwa vituoni mbele ya mawakala wa vyama vyote na tena umetangaza kuwa mmejipanga vizuri kuhakikisha kura haziibiwi halafu siku ya siku umeshindwa udai umeibiwa!...Uchaguzi kuna kushinda na kushindwa tuache uroho wa madaraka kwa gharama za damu na roho za watu..TUKUBALI MATOKEO
Ni kweli kwamba magamba wamezoea kuiba kura. Pamoja na njama hizo kubainika bado chadema wamefanya jambo la msingi kuwafahamisha wananchi wakati huo nao wakijiandaa kukabiliana na wizi huo.
Na kwakuwa magamba wanatumia vyombo vya dola kulazimisha ushindi ni vizuri waambiwe mapema ili wafahamu kwamba njama zao zimegundulika.