Dr. Slaa Atoa Sharti!

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566
na Irene Mark na Janet Josiah


amka2.gif
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeipa serikali sharti la kufanya mazungumzo ya kumaliza utata uliotokana na kinachodaiwa kuwa uchakachuaji wa matokeo ya uchaguzi.

Kimesema kiko tayari kukutana na serikali ilimradi ikubali kuunda tume huru ya kuchunguza uhalali wa matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kuunda upya Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kuandika Katiba mpya.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, katika Ofisi za chama hicho, Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alisema utayari wa CHADEMA kukutana utatokana na utayari wa serikali kukubali mapendekezo hayo, ili kujiridhisha na kuwapa haki Watanzania wanaolalamikia mfumo wa uchaguzi na katiba mbovu.


Alisema azma ya CHADEMA ni kushinikiza mabadiliko ya Katiba kabla ya 2015 ili kuepusha shari inayoweza kutokea siku za usoni kutokana na dhuluma inayolindwa na mfumo wa Katiba na sheria.


Alisema haikubaliki kimantiki kwamba matokeo ya ubunge yanaweza kuhojiwa lakini ya rais hayawezi kuhojiwa, hata kama kuna kasoro za wazi.


Alisema pia kuwa si sahihi kuacha Tume itangaze mshindi wa urais hata kama ameshinda kwa kura moja tu, kama ilivyo sasa. Anapendekeza mfumo uruhusu mshindi apatikane kwa zaidi ya asilimia 50 ya kura zote.


Alisema pia ni vema Watanzania wapatiwe majibu kwa nini Tume ilitangaza kuwa waliojiandikisha kupiga kura ni milioni 20, lakini waliojitokeza ni milioni nane (8); jambo ambalo linatia shaka kwamba huenda kulikuwa na hila katika mfumo mzima wa uchaguzi.
“Ninaamini kwamba kama umeshindwa kupigiwa kura na Watanzania wapatao asilimia 70, ujue wananchi hawakupendi, na nchi haiwezi kutawalika,” alisema Dk. Slaa.


Hata hivyo, alisema kutokana na kasoro hizo pamoja na nyingine zilizomo katika Katiba, kuna ulazima wa kuwapo kwa Katiba mpya ili chaguzi zitakazofuata zifanyike kwa uhuru na haki.


Hivi karibuni CHADEMA ilitoa tamko la kutoyatambua matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa na NEC kwa madai kuwa taratibu nyingi zilivurugwa na Tume hiyo kwa lengo la kumbeba mgombea wa chama tawala, Rais Kikwete.


Alisema ingawa katika kipindi hicho cha kutangaza matokeo ya rais, CHADEMA iliipelekea NEC malalamiko ya kutoridhika na kuitaka isitishe na wao kuendelea kwa kukubali kasoro za jimbo moja la Geita ni udhaifu.
Msimamo wa tamko hilo ulionyeshwa kwa vitendo mwishoni mwa wiki iliyopita na wabunge wa chama hicho walipotoka kwenye ukumbi wa Bunge mara baada ya Rais Kikwete kuanza kuhutubia.
 
Dr Slaa ajue hayupo kwenye nafasi ya kuipa serikali masharti na pia serikali haitaona haja ya kukubali bila ya kuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa wananchi na wafadhili wa nje.Pia kufikisha malalamiko SADC/UN/EU kutasaidia kila viongozi wetu wakisafiri wanaulizwa kuhusu tatizo hilo.CUFwaliwanyima raha Kikwete/Membe kila wakienda nje wanaulizwa mumefikia wapi tatizo la Zenj.Kukaa kimya baada ya uchaguzi pia kumeipotezea Chadema momentum sio rahisi tena kupata muamko uliokuwepo wakati ule.
 
Dr Slaa ajue hayupo kwenye nafasi ya kuipa serikali masharti na pia serikali haitaona haja ya kukubali bila ya kuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa wananchi na wafadhili wa nje.Pia kufikisha malalamiko SADC/UN/EU kutasaidia kila viongozi wetu wakisafiri wanaulizwa kuhusu tatizo hilo.CUFwaliwanyima raha Kikwete/Membe kila wakienda nje wanaulizwa mumefikia wapi tatizo la Zenj.Kukaa kimya baada ya uchaguzi pia kumeipotezea Chadema momentum sio rahisi tena kupata muamko uliokuwepo wakati ule.



Moto wa CHADEMA utakuwa mkubwa kuliko hata wakati wa uchaguzi, we subiri operation sangara ianze baada ya serikali kuapishwa!
 
Moto wa CHADEMA utakuwa mkubwa kuliko hata wakati wa uchaguzi, we subiri operation sangara ianze baada ya serikali kuapishwa!

Mungi nakubaliana na wewe sana. Wengi wamedhani kukaa kimya kwa Chadema ni makosa lakini kishindo cha ukimya huo wakitafakari njia za amani na za kueleweka kuendeleza haya mapambano ni kikubwa sana. Watu wanatafakari nia nzuri waliyo nayo. Kuna ambao walikuwa na haja sana ya kuwaona wananzisha maandamano ili watume wahuni wao humo wakasababishe vurugu halafu waseme "si unaona ndiyo haya tulikuwa tunawaambia!" Chadema siyo wajinga kihivyo! Wahafahamu kuwa walishaandaliwa wahuni wengi tuu tena walishalipwa huenda! Sassa isijekuwa ndiyo yale ya Mkoa mmoja, wajanja hukubali kupokea lakini wanafanya wanachojua ni kizuri kwa Taifa. Wananchi wanazidi kuelimika. Tena kwa kasi kubwa mno. Asiyefahamu ni chama tawala tu na tena siyo wote!.
 
Hoja za Dk. Slaa ni za msingi sana na ni ambazo kila mwananchi mwenye kulitakia mema taifa hili na vizazi vijavyo anatakiwa ajiulize, aulize na atafute majibu. Ila ni je iwapo serikali itakataa hili "sharti", Dk. Slaa na Chadema watafanya nini?
 
Hoja za Dk. Slaa ni za msingi sana na ni ambazo kila mwananchi mwenye kulitakia mema taifa hili na vizazi vijavyo anatakiwa ajiulize, aulize na atafute majibu. Ila ni je iwapo serikali itakataa hili "sharti", Dk. Slaa na Chadema watafanya nini?

Ila aki MS hawaoni hilo!!
 
Back
Top Bottom