Dr.Slaa apewa kazi nzito

nickname

JF-Expert Member
Dec 20, 2009
544
147
Elvan Stambuli na Makongoro Oging'
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa (pichani) amepewa kazi mpya ya kuhakikisha kuwa mwaka 2015, Tanzania inaingia katika uchaguzi mkuu ikiwa na katiba mpya ya nchi.

Habari kutoka ndani ya Chadema zinasema mkakati huo ndiyo aliopangiwa Dk. Slaa ambaye alikuwa mgombea urais na kwamba, atatakiwa kuanza mara moja kwa kuhamasisha wananchi kudai katiba mpya kupitia mikutano ya hadhara, taasisi zisizo za kiserikali na hata katika vikundi vya dini.

"Ni mkakati ambao utamfanya Dk. Slaa kuwa ‘bize' pengine kuliko hata wakati wa kampeni za kuwania urais, atashirikiana na wabunge ile sehemu yenye wabunge katika mikutano na ni lazima katiba mpya ya nchi ije, mapambano haya yatakuwa nje na ndani ya bunge," alisema mpashaji wetu wa habari aliye ndani ya chama hicho aliyeomba jina lake kutotajwa kwa kuwa si msemaji.

Hata hivyo, msaidizi mkuu wa Dk. Slaa, ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amethibitisha kuwepo kwa mikakati hiyo ya kushughulikia uwepo wa katiba mpya ya nchi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

"Tunajenga ajenda moja kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu ujao (2015), unafanyika kwa mujibu wa katiba mpya na mfumo mpya wa uchaguzi… sijawahi kusimamia ajenda ikaishia njiani," alitamba Zitto.

Naye Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alithibitisha Jumamosi iliyopita kuwa, suala la kudai katiba mpya na mfumo mzuri wa uchaguzi ni moja ya ajenda yao kuu na watataka ikamilike kabla ya mwaka 2015.

"Watu wengi wanalalamikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi na hii imetokana na katiba ya nchi, tutatumia nguvu ya umma kuhakikisha katiba mpya inatengenezwa na kutumika mwaka 2015.

"Uzoefu umeonesha kuwa hata katika majimbo tuliyoshinda, nguvu za umma zilitumika, tutahamasisha watu, taasisi zisizo za kiserikali, dini mbalimbali na watu, kudai katiba mpya na mfumo mzuri wa uchaguzi," alisema Mbowe.

Alifafanua kuwa hata alipokuwa Dodoma kuapishwa aliwaambia wabunge wa Chama Cha Mapinduzi kuwa, wao (Wapinzani) wamefika hapo walipo kwa njia iliyojaa miba, milima, kokoto na mashimo, tofauti na wenzao ambao walitumia barabara ya lami.

Baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kisiasa nchini walisema iwapo Chadema watafanikiwa katika kampeni yao ya kuandikwa kwa katiba mpya ya nchi, itakiumiza Chama Cha Mapinduzi ambacho kama chama tawala kimepewa mamlaka tena kama vile Mwenyekiti wake ambaye pia ni rais kuchagua wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inayolalamikiwa na wapinzani.

Juzi Jumapili, Mkurugenzi wa Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu alidai kuwa Jeshi la Polisi lina mkakati wa kudhoofisha chama chake baada ya kuwakatalia wabunge wao kufanya mikutano ya hadhara sehemu mbalimbali nchini na kusisitiza kuwa watafanya mikutano hiyo hata kama jeshi hilo litakataa kuruhusu, jambo lililotafsiriwa na wachambuzi wa siasa kuwa ni jino kwa jino.

Alisema jeshi la polisi katika kuwazuia kukutana na wapiga kura wao limetumia visingizio vya ‘taarifa ya intelijensia' au kwamba kuna baadhi ya vyama vya siasa ‘havina nia njema', kama sababu ya kupiga marufuku mikutano yao ya hadhara.

Aliwataja baadhi ya wabunge aliodai wamenyimwa kufanya mikutano na majimbo yao katika mabano kuwa ni Mhe. Saidi Arfi (Mpanda mjini), Annamary Stella Mallack (Viti Maalum, Rukwa), Mch. Peter Msigwa( Iringa mjini), Mhe. Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini) na Mhe. Ezekiah Wenje (Nyamagana, Mwanza).

Source : Global Publishers(GPL)
 
Mchakato huu ni mzuri lakini sithani kama taarifa hizi ni rasmi.......nadhani hizi ni tetesi! mungu ibariki CDM na watu wake
 
embu tungoje taarifa rasmi ili tumpe kampani kamanda wetu wa mabadiliko:whoo:
 
aaah Dr.bana hivi tamko lako utatoa lini mi niko standbye muda wote nasubiria tu utoe tamko ....maana kuna jizi limeiba kura na inafahamika hivyo
 
Ni kweli tusubiri taarifa rasimi ya Chadema, maana kuanza kujadili hoja ambayo bado haiko rasimi sio vizuri sana. Lakini katiba mpya tunaihitaji sana watanzania japo serikali haiko tayari kuruhu hili litokee
 
Hili ni jambo zuri sana!Mungu ibariki CHADEMA iendelee kuwepo,ikiwa na nguvu kubwa kuliko ilivyo kwa sasa,iepushe na migogoro kama iliyoikumba NCCR MAGEUZI,iepushe na mapandikizi ili ifikapo 2015 iwe CHADEMA yenye nguvu!
 
kila la heri sie tunataka kazi acha wenyewe wagombanie u kuu wa mikoa chadema nyie chapeni kazi italipa tu.
 
Elvan Stambuli na Makongoro Oging'
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa (pichani) amepewa kazi mpya ya kuhakikisha kuwa mwaka 2015, Tanzania inaingia katika uchaguzi mkuu ikiwa na katiba mpya ya nchi.

Habari kutoka ndani ya Chadema zinasema mkakati huo ndiyo aliopangiwa Dk. Slaa ambaye alikuwa mgombea urais na kwamba, atatakiwa kuanza mara moja kwa kuhamasisha wananchi kudai katiba mpya kupitia mikutano ya hadhara, taasisi zisizo za kiserikali na hata katika vikundi vya dini.

"Ni mkakati ambao utamfanya Dk. Slaa kuwa ‘bize' pengine kuliko hata wakati wa kampeni za kuwania urais, atashirikiana na wabunge ile sehemu yenye wabunge katika mikutano na ni lazima katiba mpya ya nchi ije, mapambano haya yatakuwa nje na ndani ya bunge," alisema mpashaji wetu wa habari aliye ndani ya chama hicho aliyeomba jina lake kutotajwa kwa kuwa si msemaji.

Hata hivyo, msaidizi mkuu wa Dk. Slaa, ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amethibitisha kuwepo kwa mikakati hiyo ya kushughulikia uwepo wa katiba mpya ya nchi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

"Tunajenga ajenda moja kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu ujao (2015), unafanyika kwa mujibu wa katiba mpya na mfumo mpya wa uchaguzi… sijawahi kusimamia ajenda ikaishia njiani," alitamba Zitto.

Naye Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alithibitisha Jumamosi iliyopita kuwa, suala la kudai katiba mpya na mfumo mzuri wa uchaguzi ni moja ya ajenda yao kuu na watataka ikamilike kabla ya mwaka 2015.

"Watu wengi wanalalamikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi na hii imetokana na katiba ya nchi, tutatumia nguvu ya umma kuhakikisha katiba mpya inatengenezwa na kutumika mwaka 2015.

"Uzoefu umeonesha kuwa hata katika majimbo tuliyoshinda, nguvu za umma zilitumika, tutahamasisha watu, taasisi zisizo za kiserikali, dini mbalimbali na watu, kudai katiba mpya na mfumo mzuri wa uchaguzi," alisema Mbowe.

Alifafanua kuwa hata alipokuwa Dodoma kuapishwa aliwaambia wabunge wa Chama Cha Mapinduzi kuwa, wao (Wapinzani) wamefika hapo walipo kwa njia iliyojaa miba, milima, kokoto na mashimo, tofauti na wenzao ambao walitumia barabara ya lami.

Baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kisiasa nchini walisema iwapo Chadema watafanikiwa katika kampeni yao ya kuandikwa kwa katiba mpya ya nchi, itakiumiza Chama Cha Mapinduzi ambacho kama chama tawala kimepewa mamlaka tena kama vile Mwenyekiti wake ambaye pia ni rais kuchagua wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inayolalamikiwa na wapinzani.

Juzi Jumapili, Mkurugenzi wa Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu alidai kuwa Jeshi la Polisi lina mkakati wa kudhoofisha chama chake baada ya kuwakatalia wabunge wao kufanya mikutano ya hadhara sehemu mbalimbali nchini na kusisitiza kuwa watafanya mikutano hiyo hata kama jeshi hilo litakataa kuruhusu, jambo lililotafsiriwa na wachambuzi wa siasa kuwa ni jino kwa jino.

Alisema jeshi la polisi katika kuwazuia kukutana na wapiga kura wao limetumia visingizio vya ‘taarifa ya intelijensia' au kwamba kuna baadhi ya vyama vya siasa ‘havina nia njema', kama sababu ya kupiga marufuku mikutano yao ya hadhara.

Aliwataja baadhi ya wabunge aliodai wamenyimwa kufanya mikutano na majimbo yao katika mabano kuwa ni Mhe. Saidi Arfi (Mpanda mjini), Annamary Stella Mallack (Viti Maalum, Rukwa), Mch. Peter Msigwa( Iringa mjini), Mhe. Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini) na Mhe. Ezekiah Wenje (Nyamagana, Mwanza).

Source : Global Publishers(GPL)

Kweli Chama hakina hata watu wanao fikiria. Suala la katiba mpya ni mchakato na haiwezekani 2015 tukawa na katiba mpya hata malaika washuke. Hakuna nchi duniani iliyo anza mchakato wa kutengeneza katiba mpya na ndani ya miaka 5 ikawa tayari. Mtamzeesha bure mzee watu na ana machungu ya kushindwa Urais
 
Hili ni jambo zuri sana!Mungu ibariki CHADEMA iendelee kuwepo,ikiwa na nguvu kubwa kuliko ilivyo kwa sasa,iepushe na migogoro kama iliyoikumba NCCR MAGEUZI,iepushe na mapandikizi ili ifikapo 2015 iwe CHADEMA yenye nguvu!

Waepushe viongozi wake waache Uzinifu, waache ukabila na waache udini ambao wako nao hivi sasa
 
Kweli Chama hakina hata watu wanao fikiria. Suala la katiba mpya ni mchakato na haiwezekani 2015 tukawa na katiba mpya hata malaika washuke. Hakuna nchi duniani iliyo anza mchakato wa kutengeneza katiba mpya na ndani ya miaka 5 ikawa tayari. Mtamzeesha bure mzee watu na ana machungu ya kushindwa Urais

kwa ubongo huo hata ufikiri mara saba hata mara sabini hutafanikiwa. lakini kwa watu makini wanao ona mbele katiba ni swala miaka hata miwili. Zanzibar wamechukua muda gani? Umeona FFU na mabomu yao wanalinda masanduku ya kura zanzibar? . Shida ni hao wanaojua hawakubaliki lkn wanataka washinde kwa kishindo kwa kutumia TUME YAO, ASKARI WAO, MABOmu YA MACHOZI, WAKURUGENZI walio wateua wao kusimamia uchaguzi.
 
Kweli Chama hakina hata watu wanao fikiria. Suala la katiba mpya ni mchakato na haiwezekani 2015 tukawa na katiba mpya hata malaika washuke. Hakuna nchi duniani iliyo anza mchakato wa kutengeneza katiba mpya na ndani ya miaka 5 ikawa tayari. Mtamzeesha bure mzee watu na ana machungu ya kushindwa Urais

Think Twice kama lilivyo jina lako unaishi dunia gani? Huo muda unatosha tena saana. Usikatishe watu tamaa, kama tumedhamilia inawezekana.
Tutoe taadhari kuwa hatukwenda kwenye uchaguzi mpya 2015, bila katiba mpya, huo uwe mkakati wa Watanzania wote!!!!!!!!!!!!!
Wewe unajiweka wapi unaonekana kama haikuhusu vile?
 
Yes sasa Chadema wanamuvuzisha mambo ...... step by step....nashukuru
 
mimi nasema tu ni KATIBA KATIBA ndiyo siri ya mafanikio kwa watanzania wote


jamani watanzania tuamke kutetea maslahi ya wote walio na uelewa jaribu kuwaelimisha wale ambao hawajapata uelewa wa uhalisia wa uongozi wa serikali yetu


moz-screenshot.png
 
@nickname

tunataka katiba mpya na hamna anayelazimisha mchakato uishe mapema swala ni kuanza kwa mchakato wa KATIBA mpya na kuundwa tume huru ya uchaguzi ambayo haitachaguliwa na rais aliye madarakani

kuanza kwa mchakato wa kuunda katiba ndiyo mwanzo wa mafanikio na matarajio ya watanzania na kuchelewa kwa mchakato wa katiba ni kuchelewa kwa maendeleo ya watanzania jaribu kutafakari kwa makini na kuangalia baada ya miaka kumi tutakuwa wapi?
 
Back
Top Bottom