Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,427
- 911,172
Ni nani atasahau hizi picha.....................
Ni nani atasahau hoja hizi za Dr. Slaa.......................
Dk. Slaa apinga matokeo
*Asema Usalama wa Taifa wamechakachua kura
*Aeleza tofauti ya zinazotangazwa na za vituoni
*Sasa aiomba jumuiya ya kimataifa iingilie kati
*Ridhiwan asema ameshaona dalili za kushindwa
Na Maregesi Paul
MGOMBEA urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa, ametoa tuhuma nzito za wizi wa kura akiihusisha Idara ya Usalama wa Taifa.
Amesema kuwa kitendo cha Idara hiyo kujiingiza katika siasa na kushiriki kubadili matokeo ya kura katika maeneo mbalimbali nchini ni cha hatari kwa kuwa viongozi wanaopatikana sio chaguo la wananchi.
Amesema kwamba kubadili matokeo kunaweza kuzua vurugu kwa kuwa wapigakura wanajua ukweli juu ya kinachofanywa.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, jana.
Mmoja wa watuhumiwa wa "uchakachuaji kura", Ridhiwan Kikwete, amejitokeza haraka kujibu tuhuma hizo, akisema Dk. Slaa ametoa madai hewa baada ya kuona kuna dalili zote za yeye kuukosa urais.
Ridhiwan alisema Dk. Slaa anachofanya ni kutapatapa kutokana na imani yake kwamba watu wengi waliokuwa wakifika kwenye mikutano yake wangempa kura.
"Asidanganywe na umati aliokuwa akiupata, awaulize kina Augustine Mrema au Freeman Mbowe, asichukulie kuwa wote aliowaona walikuwa wapigakura wake, wengine walifika kumshangaa mambo aliyokuwa akizungumza," alisema Rishiwan.
Maudhui ya mkutano wa Dk. Slaa yalikuwa kueleza jinsi Chadema isivyoridhishwa na mwenendo wa utoaji matokeo ya kura zilizopigwa Oktoba 31.
"Tumewaiteni hapa ili kuzungumzia mwenendo wa kura za urais kwani kwa mujibu wa Katiba yetu, Rais akishaapishwa hakuna chombo chochote kinachoruhusiwa kuhoji ushindi wake.
"Kwa kuwa NEC inaendelea kutangaza matokeo yanayoonekana kuwa na dosari, naomba nisema yafuatayo kwa kuwa ni ya msingi kwa mustakabali wa nchi hii.
"Kama wote tunaitakia mema nchi hii, naiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifute matokeo yote ya urais na kura zirudiwe upya kwa kuwa hayo yanayotangazwa sio matokeo ya wananchi.
"Hatuwezi kukubali matokeo ya dola, hizo si kura za wananchi, ni kura za Usalama wa Taifa ambao wameshiriki kuchakachua matokeo haya.
"Vile vile matokeo ya ubunge yaliyochakachuliwa katika majimbo yote, NEC iyafute na uchaguzi urejewe upya ili haki iweze kutendeka.
"Lakini, kama tabia hii ya kuchakachua matokeo haitakoma, siku uzalendo utakapotushinda na tukawaamuru wananchi waingie mitaani, tusilaumiwe.
"Hivi wananchi wakiingia mitaani nani atabaki, siyo CCM wala Chadema, CCM wasitake kutupeleka huko tusikotaka.
"Katika haya, jumuiya ya kimataifa lazima itoe hadharani ripoti yake, TEMCO nao wasiogope kuitoa, waitoe ili wananchi wajue kilichofanywa na CCM," alisema Dk. Slaa.
Alimtaka Mkuu wa Usalama wa Taifa ajiuzulu wadhifa huo kwa maelezo kwamba ana hakika maofisa wa Idara yake wameshiriki kubadili matokeo ya kura zinazoelekea kumpa ushindi mgombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.
Katika mkutano huo, mgombea huyo wa urais alitumia muda mrefu kueleza jinsi matokeo yalivyobadilishwa.
Alisema kuwa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC kutoka katika majimbo nchini yanatofautiana na matokeo yaliyoko katika vituo vya kupigia kura.
Katika hatua nyingine, alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, aongoze Jeshi hilo kwa mujibu wa Kitabu cha Haki na Wajibu kwa Mpiga Kura kilichotungwa na Jeshi la Polisi.
Ama kweli kimya cha Dr. Slaa kina mshindo mkuu......................
Ni nani atasahau hoja hizi za Dr. Slaa.......................
Dk. Slaa apinga matokeo
*Asema Usalama wa Taifa wamechakachua kura
*Aeleza tofauti ya zinazotangazwa na za vituoni
*Sasa aiomba jumuiya ya kimataifa iingilie kati
*Ridhiwan asema ameshaona dalili za kushindwa
Na Maregesi Paul
MGOMBEA urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa, ametoa tuhuma nzito za wizi wa kura akiihusisha Idara ya Usalama wa Taifa.
Amesema kuwa kitendo cha Idara hiyo kujiingiza katika siasa na kushiriki kubadili matokeo ya kura katika maeneo mbalimbali nchini ni cha hatari kwa kuwa viongozi wanaopatikana sio chaguo la wananchi.
Amesema kwamba kubadili matokeo kunaweza kuzua vurugu kwa kuwa wapigakura wanajua ukweli juu ya kinachofanywa.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, jana.
Mmoja wa watuhumiwa wa "uchakachuaji kura", Ridhiwan Kikwete, amejitokeza haraka kujibu tuhuma hizo, akisema Dk. Slaa ametoa madai hewa baada ya kuona kuna dalili zote za yeye kuukosa urais.
Ridhiwan alisema Dk. Slaa anachofanya ni kutapatapa kutokana na imani yake kwamba watu wengi waliokuwa wakifika kwenye mikutano yake wangempa kura.
"Asidanganywe na umati aliokuwa akiupata, awaulize kina Augustine Mrema au Freeman Mbowe, asichukulie kuwa wote aliowaona walikuwa wapigakura wake, wengine walifika kumshangaa mambo aliyokuwa akizungumza," alisema Rishiwan.
Maudhui ya mkutano wa Dk. Slaa yalikuwa kueleza jinsi Chadema isivyoridhishwa na mwenendo wa utoaji matokeo ya kura zilizopigwa Oktoba 31.
"Tumewaiteni hapa ili kuzungumzia mwenendo wa kura za urais kwani kwa mujibu wa Katiba yetu, Rais akishaapishwa hakuna chombo chochote kinachoruhusiwa kuhoji ushindi wake.
"Kwa kuwa NEC inaendelea kutangaza matokeo yanayoonekana kuwa na dosari, naomba nisema yafuatayo kwa kuwa ni ya msingi kwa mustakabali wa nchi hii.
"Kama wote tunaitakia mema nchi hii, naiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifute matokeo yote ya urais na kura zirudiwe upya kwa kuwa hayo yanayotangazwa sio matokeo ya wananchi.
"Hatuwezi kukubali matokeo ya dola, hizo si kura za wananchi, ni kura za Usalama wa Taifa ambao wameshiriki kuchakachua matokeo haya.
"Vile vile matokeo ya ubunge yaliyochakachuliwa katika majimbo yote, NEC iyafute na uchaguzi urejewe upya ili haki iweze kutendeka.
"Lakini, kama tabia hii ya kuchakachua matokeo haitakoma, siku uzalendo utakapotushinda na tukawaamuru wananchi waingie mitaani, tusilaumiwe.
"Hivi wananchi wakiingia mitaani nani atabaki, siyo CCM wala Chadema, CCM wasitake kutupeleka huko tusikotaka.
"Katika haya, jumuiya ya kimataifa lazima itoe hadharani ripoti yake, TEMCO nao wasiogope kuitoa, waitoe ili wananchi wajue kilichofanywa na CCM," alisema Dk. Slaa.
Alimtaka Mkuu wa Usalama wa Taifa ajiuzulu wadhifa huo kwa maelezo kwamba ana hakika maofisa wa Idara yake wameshiriki kubadili matokeo ya kura zinazoelekea kumpa ushindi mgombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.
Katika mkutano huo, mgombea huyo wa urais alitumia muda mrefu kueleza jinsi matokeo yalivyobadilishwa.
Alisema kuwa matokeo ya urais yanayotangazwa na NEC kutoka katika majimbo nchini yanatofautiana na matokeo yaliyoko katika vituo vya kupigia kura.
Katika hatua nyingine, alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, aongoze Jeshi hilo kwa mujibu wa Kitabu cha Haki na Wajibu kwa Mpiga Kura kilichotungwa na Jeshi la Polisi.
Ama kweli kimya cha Dr. Slaa kina mshindo mkuu......................