Dr. Slaa anakosea:Enyi wana CDM, wanavyuo, na wanaharakati sikieni

slaa wanamwangalia kama kiongozi wa dini zaidi kuliko wa siasa,hivyo kusema kakosea never,hata akinya barabarani watashangilia na kuwataka wengine waige uzalendo wa slaa

As low as it get. Why mpaka descriptions za namna hii? Inaonekana kweli you have nosecence mpaka mdomoni...wananchi wasio na solutions au hawajui jinsi ya kudialog this is what they have left.

"Don't take politics personal utaumia wewe mwenyewe"
 
Hapo umenena. Unajua wengi wanafikiri MATOKEO ya madai ya katiba mpya ni SLAA kuingia madarakani, na tuwaulize shwali hili dogo endapo katiba mpya itaandikwa na SLAA asiingie ikulu watadai nyingine? watu tuwe n amawazo ya kufikri badala ya mawazo kugundisha kwa super glue. Kama huoni udhaifu hata mmoja wa SLAA wewe hufai, kwani wao kwa wao SLAA, MBOYE, ZITTO, LISU,MNYIKA, MDEE na wengine wengi kila mmoja anajua udhaifu wa mwingine
Kwani katiba ni kamanufaa ya Dr Slaa na CDM tu, kama huoni umhimu wa katiba na matatizo yaliyosababishwa na katiba basi wewe ni zuzu...
 
sijapewaga thanks tokea nijiunge JF kwa sababu yakuhoji mambo muhimu.ukitaka sredi yako iwe na wachangiaji wengi wengi andika HAJAWAI KUTOKEA DUNIANI MTU MAKINI KAMA SLAA hapo utaona nanma JF ilivyopoteza mwelekeo.
Pole sana hata MS alikuwa anapewa thanks, imekuwaje wana jf hawaoni mchango wako au huwa ni upupu halafu unategemea thanks sahau kupewa thanks kwenye ujinga na kusapoti mafisadi....
 
"We all must die" lakini kwa nini tusubiri kufa kizembe?.....Kama nchi inapelekwa pabaya na mafisadi.... and Dr. Slaa wa ukweli (PhD). watanzania tunamuamini, tunamheshimu.......longolongo likiendelea sie tunapachimba tu. Tutakufa lakini watoto na wajukuu wetu watafurahia matunda ya damu yetu. Kitu gani bwana....kama umetumwa hapa sio mahala pake.
 
Mkuu nadhan hata wewe unashaliona hili kuwa kandia wote ila sio Dr Slaa, nakiri tunamatatizo pale LUMUMBA, mbona JF hawaruhusu kabisa mabaya ya Slaa kuanikwa?

Mtu anayezeeka sio wa kumkumbatia sana, CDM cHAMA CHA VIJANA kwa hiyo hata Slaa ni kijana???watakwambia ndio!!!aibu hawana
Umeona namna walivyohalalisha ishu ya kumpora mtu mkee? hawa ndio CDM Wanavyuo Wanaharakati na magreat thinkers


vyuoni hapakaliki kisa Slaa,yaan always maneno ya slaa ni dhahabu kwao na hukaririwa.
Mkuuu sema mwenyewe lakini kwa miaka hii kuna mzee mwenye hekima nchi hii zaidi ya Slaa! tuache ushabiki mkuu!
Hata kwa hao wakina makamba wabakaji na mkwere wake wengi, ni bora ya Slaa mkuu. kunakipindi vijana walikuwa wanasubili kauli ya Dr but yeye alivyomstaarabu na Hekima ametuliza! Hebu niambie huyo makamba ananini!? Siyo kuwa namfagilia sana Dr but wachache sana wenye hekima kama yeye wacha vijana wamfuate than hao MAFISADI!
 
Kama unajua wana jf wanafikiri Dr hakosei kwa nini basi unawauliza? Waulize wananchi ili wakwambie kwanini wanafikiri hakosei. Ila kumbuka kwamba ni yeye aliyesema wizi wa madeni ya nje na kukalia kidedea, wananchi walifikiri kakosea lakini baada ya uchunguzi ilionekana kweli. Alisema kuhusu mikataba mibovu baada ya ufuatiliaji ilionekana kweli, alisema kuhusu Radar ilipofuatiliwa ilionekana kweli, alisema kuhusu ndege ya raisi ilipofuatiliwa ilionekana kweli. Sasa amekosea wapi?
Tunajua kwamba anaweza kukosea lakini hatujaona kakosea hivyo mpaka sasa tunasema hakosei na hakurupuki. Hii nakuhakikishia Dr wa kweli hakosei na hakurupuki, si mwoga na ni mwadilifu.
 
kaka kiiza!!! Hapa swala si kwamba ccm tunawabaya wangapi? ni ile hali ya nyie kutaman kuisikia sauti ya dr. Slaa hata kama anakohoa.
wahariri na waandishi nao wamepotoka kwa huyu jamaa kuna siku magazeti yatatoka na headline dr. Slaa atakula wali samaki leo na ninyi siku hiyo lazima mule wali samaki hata kama kuna walio na allergy ya samaki.

crap
 
Ni mpuuzi sana..
Mpuuzi ni huyu aliatuahidi vitu ambavya kamwe hawezi kuvitekeleza:

1.Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora
2.Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini
3.Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga
4.Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga
5.Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma
6.Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini
7.Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma
8.Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera
9.Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera
10.Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini
11.Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
12.Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera
13.Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera
14.Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera
15.Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya
16.Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera
17.Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
18.Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza
19.Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum
20.chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza
21.Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita
22.Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba
23.Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro
24.Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini
25.Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
26.Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
27.Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya
28.Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga
29.Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa
30.Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na
31.kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro
32.Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini
33.Kuboresha barabara za Igunga - Tabora
34.Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu
35.Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini
36.Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara
37.Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa -Musoma
38.Kulinda haki za walemavu - Makete
39.Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini
40.Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha
41.Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
42.Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora
43.Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini
44.Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma
45.Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido
46.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
47.Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini
48.Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma
49.Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido
50.Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
51.Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara
52.Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini
53.Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini
54.Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa
55.Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa
56.Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa
57.Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi - Ifunda
58.Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara
59.Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa
60.Kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii – Kibandamaiti Mjini Zanzibar
61.Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa – Kibandamaiti mjini Zanzibar
62.Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti
63.Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma
64.Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma
65.Kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma
66.Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma
67.Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
68.Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara
69.Ahadi ujenzi wa kiwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha
 
Mpuuzi ni huyu aliatuahidi vitu ambavya kamwe hawezi kuvitekeleza:

1.Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora
2.Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini
3.Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga
4.Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga
5.Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma
6.Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini
7.Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma
8.Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera
9.Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera
10.Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini
11.Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
12.Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera
13.Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera
14.Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera
15.Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya
16.Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera
17.Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
18.Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza
19.Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum
20.chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza
21.Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita
22.Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba
23.Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro
24.Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini
25.Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
26.Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
27.Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya
28.Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga
29.Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa
30.Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na
31.kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro
32.Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini
33.Kuboresha barabara za Igunga - Tabora
34.Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu
35.Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini
36.Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara
37.Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa -Musoma
38.Kulinda haki za walemavu - Makete
39.Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini
40.Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha
41.Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
42.Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora
43.Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini
44.Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma
45.Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido
46.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
47.Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini
48.Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma
49.Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido
50.Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
51.Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara
52.Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini
53.Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini
54.Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa
55.Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa
56.Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa
57.Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi - Ifunda
58.Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara
59.Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa
60.Kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii – Kibandamaiti Mjini Zanzibar
61.Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa – Kibandamaiti mjini Zanzibar
62.Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti
63.Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma
64.Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma
65.Kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma
66.Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma
67.Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
68.Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara
69.Ahadi ujenzi wa kiwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha
Toa bwana hajawahi ahidi yoote haya! YATOE TUUU TUYAFUTE KWENYE VICHWA VYETU MKUU!
 
sijapewaga thanks tokea nijiunge JF kwa sababu yakuhoji mambo muhimu.ukitaka sredi yako iwe na wachangiaji wengi wengi andika HAJAWAI KUTOKEA DUNIANI MTU MAKINI KAMA SLAA hapo utaona nanma JF ilivyopoteza mwelekeo.

Nafikiri assumptions zako siyo sahihi.
Kwanza kwenye hii post yako hujasema jambo muhimu lolote. Umejaribu kusema kuwa Dr Slaa anakosea bila kutoa sababu na mifano anakosea vipi.
Pili usiishutumi JF kwamba imepoteza muelekeo kwa sababu zifuatazo;
a. Wanamvi wa JF sio lazima wawe wanachama wa chama ama mrengo fulani wa siasa
b. Wengi wao nikiwemo (mimi mwenyewe) wanaangalia nani ana nia ya dhati ya kutuondoa kwenye dimbwi la umasikini na kutuletea maandeleo.
Kama utakumbuka JK alikuwa kwenye hali kama ya Dr Slaa mwaka 2005 ambapo alipata wafuasi wengi hasa vijana na zaidi alipata kundi kubwa la wafuasi toka vyuo vikuu mbalimbali (na mimi nikiwa mmoja wapo kwani nilikuwa mwanachuo kwa kipindi hicho).
Sasa kwa kuwa JK muda wake umepita, na nafasi ya kuaminiwa na watanzania wengi walalahoi ameichezea na imepita, hivyo usione gere kumwona Dr Slaa akipendwa na watu wengi na kuaminiwa.
Ukumbuke kuwa Dr Slaa sio tu ana kauli za kisiasa za kuvutia watu, pia ana uwezo wa kujenga na kutetea hoja, kuwa na misimamo thabiti za zaidi ya hapo ana uthubutu na ametuonyesha hivyo kwa vitendo. (na ndio maana wafuasi wake ni watu wa aina zote, kuanzia walalahoi vibabu vijana na hata wenye ma-Phd)
Kama binadamu Dr Slaa hawezi kuwa "perfect" ila kwa matendo yake na jinsi anavyochukia ufisadi na ukandamizaji na kuionea huruma TZ huyu mheshimiwa ana-rank way above his peers na itawagharimu sana wana CCM kupambana na huyu bwana.
Kwa kuwasaidia CCM na serikali yake ni kuhakikisha kuwa inaboresha maisha ya watanzania walio wengi na hapo ndio mtakuwa mnapambana na Dr Slaa kwa vitendo. Na sio vishutuma vya Makamba na Tambwe vya mara Dr kaiba mke mara Padre nk. havisaiidi
 
Enyi wana CDM na wanaharakati wote

Baada ya kusoma maoni ya wengi nimegundua kuwa wanaJF hawataki aguswe Dr. Slaa kwa baya lolote. Namheshim Dr. Slaa ni msomi mwanaharaki mwenye ubongo uliohai ILA KWA NINI wanainchi wanamchukulia kuwa HAKOSEI?

(imefikia pahala TUMAINI University wanataka Dr. Slaa apewe saa nne za kulecture pale chuoni kila mwezi ili kufufua uzalendo kama vile hii nchi haina mzalendo mwingine)

KOSA NI KWA WENGINE ila makosa ya Dr. Slaa huitwa critical analysed ideas hence FACTS+media coverage mara gafla HUGEUKA MSIMAMO WA WANAINCHI.

Labda tuambie mwingine nani ambaye atamkaribia Dr Slaa, ni mara ngapi watu wanaona maovu na kuyanyamazia? Je unataka na hao tuwaite wazalendo?

Matukio ya Dr Slaa, yanayomfanya kila moja wetu amuone ni Mzalendo wa Kweli:

1. Aliweza kutaja orodha ya Mafida pale Mwembeyanga ambayo hadi leo karibu nusu yake wako mahakamani.
2. Ndiye aliyeondoa marupurupu ya viongozi wa CCM kwa kufuta Kodi ya kichwa maana hiyo ilikuwa ni kichaka cha makada wengi wa CCM kujipatia utajiri 2000-2004 akiwa mbunge.
3. Aliyeibua ufisadi wa EPA na kuusimamia hadi sasa.
4. Na ni hivi mwaka jana tu aliamua kuwatangazia umma kuwa hawezi kwenda Ikulu huku damu ya mtanzania ikimwagika baada ya UWT na NEC kuchakachua kura zake.
5. Ni mtetezi wa wanyonge.
........................................

Sasa hayo ni machache tu labda tukuulize, wewe unafikiri ni nani ana uzalendo kama Dr. Slaa? Labda Said Kubenea.
 
Nakubali CCM imeiumiza nchi kwa namna gharama za maisha zinavyopaa,ila mbona mko tayari kumkandia yeyote kasoro Dr. Slaa?Kumbuken uzee unaanza kumjia Slaa ataanza kauMAKAMBA kidogokidogo lakin bado mtamkubali.

Ahaa mh oyaa
OLD IS GOLD
CDM NEVER DIE DOGO
TAKE CARE!
 
Toa bwana hajawahi ahidi yoote haya! YATOE TUUU TUYAFUTE KWENYE VICHWA VYETU MKUU!

Aliahidi,
Tena mkuu ameyakumbuka machache tu, alitoa ahadi zaidi ya 200 za matrilioni ya shilingi kuzidi bajeti ya serikali ya miaka mi5, na aliahidi zote kuzitekeleza ndani ya miaka mi5.
 
Toa bwana hajawahi ahidi yoote haya! YATOE TUUU TUYAFUTE KWENYE VICHWA VYETU MKUU!

Kitu ambacho mheshimiwa hakukiahidi ila kinatekelezwa kikamilifu ni kwenda kijijini Ms(z)oga kila wiki na msusuru wa ma-nissan! Damn
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Isitoshe Roma haikujengwa kwa siku moja!
 
Labda hujaelewa vizuri siyo kwamba Dr wa ukweli hasei ila ndiye mtu pekee mwenye mapenzi mema ya nchi! hebu fikiria sukari kg 50 inauzwa 80,000/= yaani kwa bei ya jumla ya kilo moja ya sukari ni Tshs 1600 hapo bado hujaisafirisha mpaka unapouzia. Wakuu wa nchi wanaona ni sawa! Sembe kg 50 ni Tshs 30,000/= mafuta ya kupikia ndoo kubwa 50,500/=. Je nchi inakwenda wapi? Inamaanisha mwenye kipato cha chini hataweza kunywa hata chai.................
Mkuu,
Soma hiyo red ulijisahau.
Hapa ushabiki umepitiliza kiwango!!! Kuwa makini,, Dr, siye mtu pekee, ila ni katika wachache wenye uchungu na mapenzi ya nchi.
Sikulaumu kwa ushabiki wako....nakuzindua tu, mkuu
 
Aliahidi,
Tena mkuu ameyakumbuka machache tu, alitoa ahadi zaidi ya 200 za matrilioni ya shilingi kuzidi bajeti ya serikali ya miaka mi5, na aliahidi zote kuzitekeleza ndani ya miaka mi5.
Mengine yaliongezwa tuu na wahuni flani! kauli zake zinahamasisha fujo sasa ahadi zoote hizo si anataka watu wafanye fujo kweli!
 
Back
Top Bottom