Elections 2010 Dr. Slaa alikuwa anaongoza Kwa 61.6% - Marando

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Source: Mwanahalisi: Jumatano, Novemba 3-9, 2010

NEC inatuhumiwa kuhujumu matokeo ya Uchaguzi kwa lengo la kukinyima ushindi CHADEMA.

Madai hayo yamo katika barua ambayo CHADEMA kiliwakilisha jana NEC kulalamikia utaratibu mzima wa kutangaza matokeo.


Katika barua hiyo, Mwanasheria wa CHADEMA, Mabere Marando anasema NEC inatumiwa na CCM kuhujumu matokeo hayo ili CCM kionekane kinashinda. "Wamepanga kupora ushindi wetu, ndiyo maana kila ambapo CHADEMA imeshinda, CCM wamekataa kusaini karatasi za kura" alisema Marando.


"Hata pale ambapo kura za madiwani na wabunge zimetangazwa, matokeo ya kura za urais hayatangazwi". Marando alisema NEC inafanya hivi kwa makusudi kwani maeneo ambayo CHADEMA haikuwa imeweka mkazo, matokeo ya madiwani, wabunge na ya urais yanatangazwa haraka . . . .


. . . . . Lakini hata katika maeneo ambayo CCM imeshinda, Marando alisema matokeo yanayotangazwa na NEC hayaendani na yale yaliyotangazwa vituoni. "Huu ni Uchakachuaji". . . .


. . . . . Marando alisema hadi juzi Jumatatu matokeo ambayo tayari walikuwa wamekusanya kutoka katika maeneo mbalimbali ya Nchi, yanaonyesha Mgombea Urais wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa anaongoza kwa wastani wa asilimia 61.6%..


Aidha taarifa hizo zinasema Dk. Slaa amepanga kuwakilisha ushahidi MZITO unaoonyesha uchakachuaji mkubwa wa kura za Urais ulivyofanyika. Ushahidi huo ni pamoja na matokeo halisi ya vituoni ambayo yanapishana na yale ya NEC.


Hatua zilizochukuliwa ni:


1. Kwenda NEC - kupeleka barua

2. Tunakwenda kueleza Nchi wahisani ambazo zimefadhili shughuli za Uchaguzi
3. Tunakwenda kuwaeleza wananchi kilichotokea kwa kuwaonyesha ushahidi kamili.

Malalamiko haya yanakuja siku chache baada ya lori lililoingia nchini likitokea zambia kukamatwa mjini Tunduma likiwa limesheheni karatasi za kupigia kura zilizowekewa alama ya vema kwa Kikwete. NEC ilikanusha.


Lakini katika kituo kimoja cha kupigia kura wilayani Musoma, lilikamatwa Lori lililokuwa na karatasi za kupigia kura na tayari zilikuwa na zimewekewa alama ya vema upande wa Kikwete. NEC haikutoa maelezo kuhusu tukio hilo.


My take:

Kama hizi taarifa ni za uhakika, basi hakuna maana ya zoezi zima la uchaguzi na ni dharau kubwa sana kwa Watanzania. Bahati mbaya mshindi wa Urais akishatangazwa, huwezi kuupinga ushindi huo mahakamani.

Ni vema sasa jumuiya zote za kiraia zinazotetea haki za kidemokrasia na za binadamu, wanachama na wapenzi wote wa haki na wana CCM wanaokerwa na hili kupaza sauti zao na kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu. Arusha, Mbeya, Mwanza, Kawe, Ubungo na Iringa wameonyesha njia.

Inawezekana, mambo mazuri yana gharama na si lazima gharama hiyo iwe ni kumwaga damu bali kupaza sauti na kukataa kutawaliwa na watu ambao watanzania hawajawachagua kwa haki.
 
Pasco (member wa JF), Umesoma alichosema Marando?

Chadema wamefuata process kama ilivyotakiwa........... good
 
Wanaofaidika na haki ni wengi lakini wanaoitafuta hukutana na mengi. VIVA SLAA
 
Swali moja rahisi ambalo NEC wangelitolea maelezo ni hivi...kwanini matokeo ya URAIS yalikuwa hayatangazwi sambamba na yale ya Udiwani na uBunge ilihali uchaguzi ulifanyika pamoja? Ninajua hata mtoto ''bright'' wa darasa la tatu anaweza kukupatia jawabu sahihi - CCM walijua kilichowapata na kwa bahati mbaya sana hawapo tayari kukubaliana na maamuzi ya wananchi walio wengi.

Nadhani kuna haja ya kuongea na wafadhili haraka ili haya matokeo fake yasimamishwe mara moja na uchaguzi wa Rais ufanyike upya.

Bila shaka Kiravu na Makame wameshatishwa na bila shaka wanafanya yale wanayoyafanya kwa amri kutoka juu
 
Wabunge majimbo 30 kati ya 200 plus na urais eti asilimia 61, give me a break! Kama huko si kuchakachua kwa mezani sijui utaita nini?
 
tuko pamoja wanamageuzi... viongozi wanamageuzi mtuambiwe siku ya kuandamana na kuikomboa nchi yetu...
 
Swali moja rahisi ambalo NEC wangelitolea maelezo ni hivi...kwanini matokeo ya URAIS yalikuwa hayatangazwi sambamba na yale ya Udiwani na uBunge ilihali uchaguzi ulifanyika pamoja? Ninajua hata mtoto ''bright'' wa darasa la tatu anaweza kukupatia jawabu sahihi - CCM walijua kilichowapata na kwa bahati mbaya sana hawapo tayari kukubaliana na maamuzi ya wananchi walio wengi.

Nadhani kuna haja ya kuongea na wafadhili haraka ili haya matokeo fake yasimamishwe mara moja na uchaguzi wa Rais ufanyike upya.

Bila shaka Kiravu na Makame wameshatishwa na bila shaka wanafanya yale wanayoyafanya kwa amri kutoka juu
Ukisoma sheria za uchaguzi zinasemaje utapata jibu.

Matokeo yote yanabandikwa vituoni kuanzia udiwani, ubunge mpaka urais. Kata inatangaza matokeo ya diwani, wilaya matokeo ya mbunge na NEC makao makuu matokeo ya rais.
 
[Hatua zilizochukuliwa ni:[/COLOR][/SIZE][/FONT]

1. Kwenda NEC - kupeleka barua

2. Tunakwenda kueleza Nchi wahisani ambazo zimefadhili shughuli za Uchaguzi
3. Tunakwenda kuwaeleza wananchi kilichotokea kwa kuwaonyesha ushahidi kamili.


Hatua number 3 (kuonyesha ushahidi kamili wa kile kilichotokea) ingeunganishwa na zile mbili za juu. Lazima NEC wajue kwamba watu wameshtuka na wanajua kwa uhakika kila kinachofanyika. Wale wafadhili wetu ambao Mkwere anashinda huko na bakuli lazima nao wajue ukweli
 
Ukisoma sheria za uchaguzi zinasemaje utapata jibu.

Matokeo YOTE yanabandikwa vituoni kuanzia udiwani, ubunge mpaka URAIS. Kata inatangaza matokeo ya diwani, wilaya matokeo ya mbunge na NEC makao makuu matokeo ya rais.

Kwa nini hayatangazwi kituoni wakati wanayabandika kituoni
 
But the National Electoral Commission chairman rejected the idea.
"There could be irregularities in terms of arithmetic in the vote tallying, but not enough to change the final results," Lewis Makame is quoted by the Reuters news agency as saying" Source BBC

Hayo ni maneno ya Jaji Lewis Makame kuthibitisha kuwa matokeo wanayotangaza siyo yaliyotangazwa vituoni. Ni ajabu kwa Jaji kufanya vitukama hivyo halafu utegemee kupata haki mahakamani.
Inauma sana, Mungu saidia Tanzania.
 
Source: Mwanahalisi: Jumatano, Novemba 3-9, 2010

NEC inatuhumiwa kuhujumu matokeo ya Uchaguzi kwa lengo la kukinyima ushindi CHADEMA.

Madai hayo yamo katika barua ambayo CHADEMA kiliwakilisha jana NEC kulalamikia utaratibu mzima wa kutangaza matokeo.

Katika barua hiyo, Mwanasheria wa CHADEMA, Mabere Marando anasema NEC inatumiwa na CCM kuhujumu matokeo hayo ili CCM kionekane kinashinda. "Wamepanga kupora ushindi wetu, ndiyo maana kila ambapo CHADEMA imeshinda, CCM wamekataa kusaini karatasi za kura" alisema Marando.

"Hata pale ambapo kura za madiwani na wabunge zimetangazwa, matokeo ya kura za urais hayatangazwi". Marando alisema NEC inafanya hivi kwa makusudi kwani maeneo ambayo CHADEMA haikuwa imeweka mkazo, matokeo ya madiwani, wabunge na ya urais yanatangazwa haraka . . . .

. . . . . Lakini hata katika maeneo ambayo CCM imeshinda, Marando alisema matokeo yanayotangazwa na NEC hayaendani na yale yaliyotangazwa vituoni. "Huu ni Uchakachuaji". . . .

. . . . . Marando alisema hadi juzi Jumatatu matokeo ambayo tayari walikuwa wamekusanya kutoka katika maeneo mbalimbali ya Nchi, yanaonyesha Mgombea Urais wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa anaongoza kwa wastani wa asilimia 61.6%..

Aidha taarifa hizo zinasema Dk. Slaa amepanga kuwakilisha ushahidi MZITO unaoonyesha uchakachuaji mkubwa wa kura za Urais ulivyofanyika. Ushahidi huo ni pamoja na matokeo halisi ya vituoni ambayo yanapishana na yale ya NEC.

Hatua zilizochukuliwa ni:

1. Kwenda NEC - kupeleka barua
2. Tunakwenda kueleza Nchi wahisani ambazo zimefadhili shughuli za Uchaguzi
3. Tunakwenda kuwaeleza wananchi kilichotokea kwa kuwaonyesha ushahidi kamili.

Malalamiko haya yanakuja siku chache baada ya lori lililoingia nchini likitokea zambia kukamatwa mjini Tunduma likiwa limesheheni karatasi za kupigia kura zilizowekewa alama ya vema kwa Kikwete. NEC ilikanusha.

Lakini katika kituo kimoja cha kupigia kura wilayani Musoma, lilikamatwa Lori lililokuwa na karatasi za kupigia kura na tayari zilikuwa na zimewekewa alama ya vema upande wa Kikwete. NEC haikutoa maelezo kuhusu tukio hilo.

My take:

Kama hizi taarifa ni za uhakika, basi hakuna maana ya zoezi zima la uchaguzi na ni dharau kubwa sana kwa Watanzania. Bahati mbaya mshindi wa Urais akishatangazwa, huwezi kuupinga ushindi huo mahakamani.

Ni vema sasa jumuiya zote za kiraia zinazotetea haki za kidemokrasia na za binadamu, wanachama na wapenzi wote wa haki na wana CCM wanaokerwa na hili kupaza sauti zao na kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu. Arusha, Mbeya, Mwanza, Kawe, Ubungo na Iringa wameonyesha njia.

Inawezekana, mambo mazuri yana gharama na si lazima gharama hiyo iwe ni kumwaga damu bali kupaza sauti na kukataa kutawaliwa na watu ambao watanzania hawajawachagua kwa haki.
Shule Jamaa wamekwenda. si mbumbumbu kama kiwete. hiyo ndo njia.
there is not freedom without cost. let us free ourselves from ccm oppression.
Change never by siting and singing we will overcome. change costs. dare not how much will cost us. w
we need respect: ccm must respect the decision of millions of Tanzanians who decide to go for change.
Katika historia ya dunia nzima hakuna mageuzi yaliyokuja bure bure tu!! kuwa namageuzi ya kweli lazima tukubali cost yoyote itakayo tupata. nawapa mfano mzuri mdogo.. wazanzibar iliwacost 2000 leo hii wanaheshimiana. wakenya 2007 ilwakost leo hii kuna utulivu. Kwa hiyo ndugu zangu tusife moyo. tusiogope vitisho. haki utafutwa, haki hupiganiwa. hata damu ikimwagika, lakini wajue kuwa ni hao hao Kikwete na wenzake ambao watakuwa chanzo. lete the world see. let the world witness and know that Kikwete is the DICTATOR:
huko anakojivunia kuwa watamsaidia wakuuwa watanzania, nako kumesha gawanyika. tutapata support kubwa mno. Kila mtanzania aliye na macho ya kuona na masikio ya kusikia ameyaona na amesikia jinsi gani kikwete na wenzake ambao wanajiita wasomi lakini bado wanatumika kukandamiza haki za watu. hii ni Karne ya 21. lazima ujue hivyo baba. soma maandiko, ujue alama za nyakati. Watanzania tujue kuwa hata French revolution haikutokea tu. they paid for it.
Watanzaia tuamke.
 
Rasta! Na Botswana, Namibia iliwacost nini? Huko kwenye utulivu bila kumwaga damu. Tusiige mifano isiyofaa. Na mbona mifano yako imelala hapa hapa tu? Japan, Australia na Uswisi imewacost nini kujenga amani. Fikiri kama mtu mzima.......AMANI KWANZA
 
Rasta! Na Botswana, Namibia iliwacost nini? Huko kwenye utulivu bila kumwaga damu. Tusiige mifano isiyofaa. Na mbona mifano yako imelala hapa hapa tu? Japan, Australia na Uswisi imewacost nini kujenga amani. Fikiri kama mtu mzima.......AMANI KWANZA

riziwani umekujahuku ?karibu sana
 
Mabere haya yasiishie Tume tu. Wao ndo wahalifu twategemea wajikosoe? Ifunguliwe kesi mahakamani na mahakama iombwe kutoa amri ya kusitisha zoezi ovu linaloendelea mpaka haya yapatiwe majibu. Tukichelewa wakatangaza imekula kwetu. Tupo pamoja??
 
Ukitaka serikali ya kiafrika/kifisadi ishike adabu, dawa ni moja tu vikwazo vya uchumi. Na hasa kunyimwa misaada, mikopo na kufungiwa kwenda ughaibuni kwa viongozi wake wakuu. Chupi zitawabana tu.
 
The whole thing was a farce and its too bad chadema has in essence no meaningful legal recourse
 
Wabunge majimbo 30 kati ya 200 plus na urais eti asilimia 61, give me a break! Kama huko si kuchakachua kwa mezani sijui utaita nini?

Mkulima acha upupu. Huko Kyela na Kigoma Slaa alikataliwa wagombea wake wa ubunge. Lakini akaahidiwa kura za uraisi. Pia kuna jimbo moja Chadema wamelichukua, lakini wamepata diwani mmoja tu, wakati CCM wamechukua kata zilizobaki kama nane hivi au zaidi.
 
popcorn.gif

Very good CHADEMA, very good.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom