Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Source: Mwanahalisi: Jumatano, Novemba 3-9, 2010
NEC inatuhumiwa kuhujumu matokeo ya Uchaguzi kwa lengo la kukinyima ushindi CHADEMA.
Madai hayo yamo katika barua ambayo CHADEMA kiliwakilisha jana NEC kulalamikia utaratibu mzima wa kutangaza matokeo.
Katika barua hiyo, Mwanasheria wa CHADEMA, Mabere Marando anasema NEC inatumiwa na CCM kuhujumu matokeo hayo ili CCM kionekane kinashinda. "Wamepanga kupora ushindi wetu, ndiyo maana kila ambapo CHADEMA imeshinda, CCM wamekataa kusaini karatasi za kura" alisema Marando.
"Hata pale ambapo kura za madiwani na wabunge zimetangazwa, matokeo ya kura za urais hayatangazwi". Marando alisema NEC inafanya hivi kwa makusudi kwani maeneo ambayo CHADEMA haikuwa imeweka mkazo, matokeo ya madiwani, wabunge na ya urais yanatangazwa haraka . . . .
. . . . . Lakini hata katika maeneo ambayo CCM imeshinda, Marando alisema matokeo yanayotangazwa na NEC hayaendani na yale yaliyotangazwa vituoni. "Huu ni Uchakachuaji". . . .
. . . . . Marando alisema hadi juzi Jumatatu matokeo ambayo tayari walikuwa wamekusanya kutoka katika maeneo mbalimbali ya Nchi, yanaonyesha Mgombea Urais wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa anaongoza kwa wastani wa asilimia 61.6%..
Aidha taarifa hizo zinasema Dk. Slaa amepanga kuwakilisha ushahidi MZITO unaoonyesha uchakachuaji mkubwa wa kura za Urais ulivyofanyika. Ushahidi huo ni pamoja na matokeo halisi ya vituoni ambayo yanapishana na yale ya NEC.
Hatua zilizochukuliwa ni:
1. Kwenda NEC - kupeleka barua
2. Tunakwenda kueleza Nchi wahisani ambazo zimefadhili shughuli za Uchaguzi
3. Tunakwenda kuwaeleza wananchi kilichotokea kwa kuwaonyesha ushahidi kamili.
Malalamiko haya yanakuja siku chache baada ya lori lililoingia nchini likitokea zambia kukamatwa mjini Tunduma likiwa limesheheni karatasi za kupigia kura zilizowekewa alama ya vema kwa Kikwete. NEC ilikanusha.
Lakini katika kituo kimoja cha kupigia kura wilayani Musoma, lilikamatwa Lori lililokuwa na karatasi za kupigia kura na tayari zilikuwa na zimewekewa alama ya vema upande wa Kikwete. NEC haikutoa maelezo kuhusu tukio hilo.
My take:
Kama hizi taarifa ni za uhakika, basi hakuna maana ya zoezi zima la uchaguzi na ni dharau kubwa sana kwa Watanzania. Bahati mbaya mshindi wa Urais akishatangazwa, huwezi kuupinga ushindi huo mahakamani.
Ni vema sasa jumuiya zote za kiraia zinazotetea haki za kidemokrasia na za binadamu, wanachama na wapenzi wote wa haki na wana CCM wanaokerwa na hili kupaza sauti zao na kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu. Arusha, Mbeya, Mwanza, Kawe, Ubungo na Iringa wameonyesha njia.
Inawezekana, mambo mazuri yana gharama na si lazima gharama hiyo iwe ni kumwaga damu bali kupaza sauti na kukataa kutawaliwa na watu ambao watanzania hawajawachagua kwa haki.
NEC inatuhumiwa kuhujumu matokeo ya Uchaguzi kwa lengo la kukinyima ushindi CHADEMA.
Madai hayo yamo katika barua ambayo CHADEMA kiliwakilisha jana NEC kulalamikia utaratibu mzima wa kutangaza matokeo.
Katika barua hiyo, Mwanasheria wa CHADEMA, Mabere Marando anasema NEC inatumiwa na CCM kuhujumu matokeo hayo ili CCM kionekane kinashinda. "Wamepanga kupora ushindi wetu, ndiyo maana kila ambapo CHADEMA imeshinda, CCM wamekataa kusaini karatasi za kura" alisema Marando.
"Hata pale ambapo kura za madiwani na wabunge zimetangazwa, matokeo ya kura za urais hayatangazwi". Marando alisema NEC inafanya hivi kwa makusudi kwani maeneo ambayo CHADEMA haikuwa imeweka mkazo, matokeo ya madiwani, wabunge na ya urais yanatangazwa haraka . . . .
. . . . . Lakini hata katika maeneo ambayo CCM imeshinda, Marando alisema matokeo yanayotangazwa na NEC hayaendani na yale yaliyotangazwa vituoni. "Huu ni Uchakachuaji". . . .
. . . . . Marando alisema hadi juzi Jumatatu matokeo ambayo tayari walikuwa wamekusanya kutoka katika maeneo mbalimbali ya Nchi, yanaonyesha Mgombea Urais wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa anaongoza kwa wastani wa asilimia 61.6%..
Aidha taarifa hizo zinasema Dk. Slaa amepanga kuwakilisha ushahidi MZITO unaoonyesha uchakachuaji mkubwa wa kura za Urais ulivyofanyika. Ushahidi huo ni pamoja na matokeo halisi ya vituoni ambayo yanapishana na yale ya NEC.
Hatua zilizochukuliwa ni:
1. Kwenda NEC - kupeleka barua
2. Tunakwenda kueleza Nchi wahisani ambazo zimefadhili shughuli za Uchaguzi
3. Tunakwenda kuwaeleza wananchi kilichotokea kwa kuwaonyesha ushahidi kamili.
Malalamiko haya yanakuja siku chache baada ya lori lililoingia nchini likitokea zambia kukamatwa mjini Tunduma likiwa limesheheni karatasi za kupigia kura zilizowekewa alama ya vema kwa Kikwete. NEC ilikanusha.
Lakini katika kituo kimoja cha kupigia kura wilayani Musoma, lilikamatwa Lori lililokuwa na karatasi za kupigia kura na tayari zilikuwa na zimewekewa alama ya vema upande wa Kikwete. NEC haikutoa maelezo kuhusu tukio hilo.
My take:
Kama hizi taarifa ni za uhakika, basi hakuna maana ya zoezi zima la uchaguzi na ni dharau kubwa sana kwa Watanzania. Bahati mbaya mshindi wa Urais akishatangazwa, huwezi kuupinga ushindi huo mahakamani.
Ni vema sasa jumuiya zote za kiraia zinazotetea haki za kidemokrasia na za binadamu, wanachama na wapenzi wote wa haki na wana CCM wanaokerwa na hili kupaza sauti zao na kupinga kwa nguvu zote uzandiki huu. Arusha, Mbeya, Mwanza, Kawe, Ubungo na Iringa wameonyesha njia.
Inawezekana, mambo mazuri yana gharama na si lazima gharama hiyo iwe ni kumwaga damu bali kupaza sauti na kukataa kutawaliwa na watu ambao watanzania hawajawachagua kwa haki.