Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,884
- 6,885
Mahusiano Dr. Slaa na Rose Kamili
Pingamizi la Rose Kamili dhidi ya Ndoa tarajiwa ya Dr. Slaa ni majeruhi anayetafuta mganga wa kienyeji amponye. Kuna dondoo kadhaa za kujiuliza katika tukio hili:
- Dr. Slaa hajawahi kuonekana hadharani na Rose Kamili kwamba ni wachumba, wanandoa au mahusiano ya kindoa katika muda wote ninaomfahamu Dr. Slaa.
- Dr. Slaa hawajawahi hata mara moja kutamka juu ya mahusiano yake na Rose Kamili.
- Rose Kamili hajaonyesha uthibitisho wa hati ya ndoa ila anatoa maelekezo kwamba ndugu na jamaa wanafahamu ndoa ya kienyeji ilifanyika kitu ambacho hakitambuliwi kisheria.
Kinyume chake:
- Dr. Slaa ametangaza mara ya kwanza kuwa na mchumba katika kampeni za uchaguzi Mkuu uliopita na kumtambulisha mchumba wake hadharani na mchumba wake huyo kumhudumia Dr. Slaa muda wote hadi sasa.
- Tangu Dr. Slaa atangaze hivyo Rose kamili hajawahi kuchukua hatua zo zote au kutoa kauli ye yote hadi pale alipoambiwa Dr. Slaa anajiandaa kufunga ndoa na kuamua kuweka pingamizi.
- Rose kamili hajawahi kuonekana hadharani au kuonyesha dalili ya wazi kwa umma kwamba Dr. slaa ni mchumba au mume wake.
- Dr. Slaa hajawahi kusema chochote kibaya juu ya Rose Kamili hali kadhalika Rose kamili hajafanya hivyo juu ya Dr. Slaa.
Mgongano wa kisiasa.
Muda wote Dr. Slaa alipokuwa Mbunge wa Karatu kupitia Chadema, Rose Kamili alikuwa diwani huko Babati kupitia CCM.
Dr. Slaa akiwa Candidate wa kiti cha urais kupitia Chadema, Rose Kamili alikuwa anagombea ubunge kupitia CCM na akatolewa nje ya uringo kwa kura za maoni.
Rose Kamili baada ya kutupwa nje ya uringo ndipo alipoamua kugeukia upande wa Chadema kupata ridhaa ya kuendelea na azima yake ya kugombe kiti cha Ubunge.
Rose Kamili baada ya kushindwa kwa kura dhidi ya mpinzani wa CCM, kwa huruma Chadema wakamzawadia ubunge wa viti maalum na akapokea kwa unyonge mkubwa.
Dr. Slaa alijihadhari dhidi ya Rose kamili
Dr. Slaa angeshinda kiti cha Urais kwa tiketi ya Chadema na anayesema kwamba alikuwa mke wake na angeshinda kuwa mbunge kwa tiketi ya CCM, maana yake Rais kutoka Chadema angekuwa na mke ambaye ni wa kutoka CCM wakiishi pamoja wenye itikadi tofauti.
Hapa kuna picha kamili ya yaliyojilia, kwani muda mrefu tu Rose kamili hakuwa upande wa Chadema aliko Slaa kiitikadi, wakati huo Dr. Slaa amekuwa na wadhifa mkubwa chamani akiwa Katibu Mkuu na pia Mbunge. Kama katibu mkuu wa chama kuna mambo mengi ndani ya nyumba ambayo ni siri za chama mke anaweza kuzijua na kuzivujisha kwa CCM kwa vile ndiko aliko na mapenzi nako.
Jambo hili kwa mtazamo wangu isingewezekana Dr. Slaa aamua kufunga ndoa na mwanamke ambaye anaonekana kisiasa yuko kinyume kabisa na msimamo wake wakati ana wadhifa mkubwa kitaifa. Kwa vyo vyote uamuzi wa busara ulihitajika na ndivyo alivyofanya Dr. Slaa. Rose Kamili alikosa ustahimilivu na unyenyekevu na kuwa na jicho la kuona mbali, mwenzake Mshambuzi aliwahi kuona.
Mshambuzi ameonyesha ukomavu wa hali ya juu, uvumilivu wa hali ya juu na kujituma kwa hali ya juu dhidi ya mchumba wake Dr. Slaa. Hadi damu imemtoka dhidi ya mchumba wake ni dalili tosha aliamua kwa moyo wake liwalo na liwe Josephine Mshumbuzi once for all Dr Slaa projected her all in all for life. Rose Kamili ana nini binafsi alichoonyesha katika maisha yake kwa Dr. Slaa kama ana upendo wa kweli tukilinganisha na Josephine Mshumbuzi?
Nguvu ya Pingamizi la Ndoa
Katika kesi nyingi unahitajika ushahidi wa hati za ndoa ambazo ni kithibitisho kwamba kuna ndoa ambayo imefungwa kisheria iwe ni serikalini au kanisa katoliki ambalo huongozwa na Canon Law. Ndoa za kimila hazina hati na hivyo hazitambuliwi kama ndoa. Sina hakika kama utoaji mahari ni uthibitisho wa kufunga ndoa kimila, lakini kisheria halikubaliki.