Dr. Slaa Akamatwe, ahojiwe na ikiwezekana achukuliwe hatua

Heshima Mbele,

Mhe. Dr. Slaa anahitajika kukamatwa na Vyombo vya sheria hasa baada ya kuwa na Nyaraka ambazo ni siri za Serikali alizozipata kutoka wizara ya Mambo ya Ndani.Tunatambua ni kosa kisheria kwa Mtanzania yeyote kuwa na nyaraka za siri za serikali.

Nchi hii inaongozwa kisheria,na tumekuwa tukipigania hili siku zote .Kwa mtazamamo wangu Naona kuna haja ya Dr. Slaa kuhojiwa hata kukamtwa kwa kumiliki nyaraka za serikali!

Binafsi, sioni hii kama 'nyara ya serikali kwani' kwa vile inasaidia kuondoa utata fulani katika issue ambayo ina walakini. Our concern siyo 'how he got it' bali 'why he has it' na kwa vile inasaidia kuleta 'solution' kwenye swala lenye walakini, kwangu mimi sioni kama Dr Slaa ana hatia yoyote kwa mantiki hii.
 
1. Hii ni side effect ya mama kunywa gongo na kula mbuluga mahindi ambayo tayari yamewekewa dawa kuangamiza akili za watoto,

2. matatizo yake mtoto anazaliwa akili zake ziko upande upande.

3. kwa nini asikamatwe masha kwa kutaka kupindisha sheria

- Mkuu Kokolo, ulikuwa na haki zote za kudai Masha akamatwe na bado unayo, lakini hoja ijibiwe kwa hoja lugha za namna hii haziwezi kutusaidia hapa JF au wananchi tunaojaribu kuwaamsha.

Hakuna ubaya ukimuomba radhi Mkulu Gembe,na Mods tafadhalini hizi lugha zisiruhusiwe humu!

Wazee wa sauti ya umeme - FMES!
 
Dr Slaa ni sehemu ya serikali ya Tanzania. Mbunge ana haki ya kuwa na nyaraka zinazoitwa za "siri" ili aweze kutekeleza majukumu yake wa ufanisi, kuongea maneno yenye ushahidi na sio kupiga blaa blaa bungeni kama wabunge wengine wanavofanya.
By the way, sheria inamkataza mtanzania gani kuwa na siri zake, kama serikali ni ya kwake kwanini awe treated kama mgeni?
Au ndio tunataka turudi kulekule kwenye ujinga wa kila siri ya nchi anayo Nyerere na wenzake wawili, na wanazitumia kwa manufaa yao. Kama tumefikia hatua ya kuanza kutafuta namna ya kuwalinda mafisadi, kwa kisingizio cha kufuata sheria na kuacha maadili na common sense, basi akili zetu zitakuwa na matatizo.
Kama kongozi alipindisha sheria inabidi iangaliwekwa makini, alifanya hivyo kwa nia gani. Kama aifanya hivyo kwa manufaa ya umma na taifa, kuna ubaya gani kufumbia macho? kama alifanya hivyo kwa manufaa yake kuna kila sababu ya kumkamata na kumfikisha mbele ya sheria.
 
Kwa mwendo huu, siku nikiwa mkulu wa nchi au mkuu wa ka-wizara nitafanya mkataba wa kuwanajisi watoto wenu na mama zenu. Kwa kuwa mimi ni mkulu, nitaweka nembo ya siri! Hapo ndugu zangu mtakuwa mmeumia. Hata barua za nyumba yangu ndogo na ma-wife nitatumia nembo ya siri! Ole wake mtu akutwe na hizo nyaraka. Sitakuwa na utani na mtu wa namna hiyo, ni kifungo cha maisha au kitanzi, nukta!!
 
Heshima Mbele,

Mhe. Dr. Slaa anahitajika kukamatwa na Vyombo vya sheria hasa baada ya kuwa na Nyaraka ambazo ni siri za Serikali alizozipata kutoka wizara ya Mambo ya Ndani.Tunatambua ni kosa kisheria kwa Mtanzania yeyote kuwa na nyaraka za siri za serikali.

Nchi hii inaongozwa kisheria,na tumekuwa tukipigania hili siku zote .Kwa mtazamamo wangu Naona kuna haja ya Dr. Slaa kuhojiwa hata kukamtwa kwa kumiliki nyaraka za serikali!

Gembe, kwani vile vidubwasha vilivyobambwa kwenye chumba chake kule Dodoma unadhani vina lengo gani? Ni kutafuta watuhumiwa ambao wakibambwa basi Dk Slaa ataunganishwa nao. Tulia mkuu, hiyo ndiyo akili ya Dola kwa sasa.

Hata hivyo hii inanikumbusha kilio cha Wabunge kuwa Mikataba ya Serikali ipelekwe Bungeni badala ya kufanywa siri kama sasa. Hizo siri ndizo zimetufanya tuendelee kuliwa na kuumizwa hadi hii leo. Hizo siri ndiyo zinasababisha mikataba tata ya kuumizwa. Hizo siri ndo zinatutesa WaTz
 
Mhe. Dr. Slaa anahitajika kukamatwa na Vyombo vya sheria hasa baada ya kuwa na Nyaraka ambazo ni siri za Serikali alizozipata kutoka wizara ya Mambo ya Ndani.Tunatambua ni kosa kisheria kwa Mtanzania yeyote kuwa na nyaraka za siri za serikali.

- Mkulu Gembe, heshima mbele sana, tatizo ni kwamba utafukua mengi sana kwa mfano hii barua ya Masha kwa waziri mkuu, ninajua kuwa imelikishwa kwa makusudi na hao hao tuliowakabidhi dhamana ya kulinda sheria zetu,

- Again huwezi kuwa na maelezo ya kutosha kuhusu ni wapi magazeti ya Mengi yanapata habari nyeti nyingi za uporaji mali wa Mkapa na zingine mbali mbali, sasa tumefikia mpaka mawaziri kurekodiwa kwenye vikao muhimu vya serikali, sasa uta-draw wapi the fine line ya kamata kamata na siri za serikali?

Serikali yetu ya sasa sio siri ina matatizo makubwa sana na utunzaji wa nyaraka za serikali, infact sio vibaya kuiita ni Banana Republic, maana mimi sijawahi kuona mambo ya ajabu kama ya hii serikali, I mean haina siri tena kuna wanazozivujisha wenyewe na ambazo hawana control nazo kabisa,

Sasa ukimkamata Dr. Slaaa then utaishia kuikamata serikali nzima, ndio maaan hawawezi hilo, na besides DR. Slaaa analisaidia taifa zima na hizi nyaraka, na hata sometimes serikali yenyewe, sasa unaona ni kwa nini hii ni Banana Republic?
 
Mbona wamechelewa? Mimi nakuunga mkono wa mkamate mapema iwezekanavyo na wamfikishe Kisutu! Siyo kwa hilo tu ulilopendekeza lakini kwa mengine:

a. Kwa kuwataja watu mbalimbali kuhusika na ufisadi na kuwachafulia majina yao katika ile orodha ya ufisadi.

b. Kwa kukubali kupewa nyaraka mbalimbali za "siri" na kuzitumia nyaraka hizo kuibua madai mazito ya ufisadi ambayo yamesababisha watu kadhaa wamtangulie Kisutu.

Hili ndiyo litakuwa funzo kwa Mtanzania yeyote kupokea nyaraka za siri. Siyo yeye tu bali pia itakuwa somo kwa mitandao kama JF kutumika kuweka nyaraka za namna hiyo na watu kuzipata kwa urahisi.

POLISI MKAMATENI DR. SLAA SASA KAMA MHE. GEMBE ANAVYOPENDEKEZA! NAUNGA MKONO HOJA!

kAMA KWELI VILE!!!!!!
 
Mbona wamechelewa? Mimi nakuunga mkono wa mkamate mapema iwezekanavyo na wamfikishe Kisutu! Siyo kwa hilo tu ulilopendekeza lakini kwa mengine:

a. Kwa kuwataja watu mbalimbali kuhusika na ufisadi na kuwachafulia majina yao katika ile orodha ya ufisadi.

b. Kwa kukubali kupewa nyaraka mbalimbali za "siri" na kuzitumia nyaraka hizo kuibua madai mazito ya ufisadi ambayo yamesababisha watu kadhaa wamtangulie Kisutu.

Hili ndiyo litakuwa funzo kwa Mtanzania yeyote kupokea nyaraka za siri. Siyo yeye tu bali pia itakuwa somo kwa mitandao kama JF kutumika kuweka nyaraka za namna hiyo na watu kuzipata kwa urahisi.

POLISI MKAMATENI DR. SLAA SASA KAMA MHE. GEMBE ANAVYOPENDEKEZA! NAUNGA MKONO HOJA!
Tupo pamoja mkuu. Hivi mh acha tu
 
FMES na wakuu wengine,

Nini maana ya nyaraka za serikali? Hivi hata vile dawa za kuongeza nguvu za wale waathirika nazo ni NYARAKA ZA SIRI ZA FAMILIA?
 
Tatizo siyo kupokea Nyaraka za Siri kama unavyopendekeza Hapo,Ni yeye kumiliki Nyaraka za Siri za serikali.Sheria Zipo na lazima zifuatwe!

Tunataka Utawala wa Kisheria,Kwanini hatuoni hili linahitaji kupewa kipaumbele?



Gembe, kwako kipaumbele ni kipi? kufichua ufisadi au kuwa na nyaraka za siri za serikali? kwanza nyaraka za siri kwa nani? serikali ni kwa ajili ya nani. Kwa nini uibaptize kuwa siri ya serikali na siyo siri ya Masha? na kama Masha ametumia vibaya ofisi yake na stationeries za serikali bado utaiita siri ya serikali? inanipa tabu kuulewa uelewa wako, anagalau ungesoma alama za nyakati!
 
Dr Slaa apewe nishani ya utumishi bora na tupendekeze Mo Ibrahim amtunze.

Huwa najiuliza, kwa nini serikali yetu (toa jeshi/polisi/usalama) iwe na siri? Wanaficha nini?
 
Gembe, kwako kipaumbele ni kipi? kufichua ufisadi au kuwa na nyaraka za siri za serikali? kwanza nyaraka za siri kwa nani? serikali ni kwa ajili ya nani. Kwa nini uibaptize kuwa siri ya serikali na siyo siri ya Masha? na kama Masha ametumia vibaya ofisi yake na stationeries za serikali bado utaiita siri ya serikali? inanipa tabu kuulewa uelewa wako, anagalau ungesoma alama za nyakati!
Watu hapa tumekimbilia kumzungumzia Masha wakati hoja haimhusu Masha. Hoja ipo wazi ni kuhsu Dr. Slaa kumiliki Nyaraka Za serikali, Je tatizo liko wapi na madhara ya kuliki kwa siri za serikali ni yapi?

There is apoint ambayo tunamiss hapa, tunatawaliwa na mawazo ya kumzungumzia mtu na siyo kuzungumzia yale ambayo watu wanayataka.

Jiulize kama Barua hiyo ingekuwa inahusu mambo ya kijeshi na nia ya serikali ingekuwaje? Kuna tatizo sehemu na hapa ndipo pahala pa kupata suluhisho lenyewe. Mie nimeanza kuogopa kwa kweli, kama watu wanaweza kupata Barua kutoka kwa Waziri kwenda kwa waziri Mkuu? kuna tatizo hapa

Basi kama Dr. Salaa akihojiwa itavuruga mambo ya serikali eti kwasababu kuna viongozi wataguswa, ni kheri tuwe na serikali ambayo itaendeshwa kwa usiri na yenye kulinda mambo muhimu ya taifa letu!

Ila mpaka sasa wazo langu ni hilo: Naomba Dr. Slaa Akamatwe na ahojiwe na aeleze alitoa wapi vielelezo hivyo, ikiwezekana awataje waliompa ili nao wachukuliwe sheria.

Tuache uongozi wa kuogopana, haya ndiyo yanaleta mambo ya kuwa nchi itashindwa kutawalika kama jambo flani likitokea. We need to take action

 
jamani nalia.jamani nalia,jamani nalia,tanzania yetu inateketea,jamani kama nchi ina watu ma imbecile kama huyu itakuwaje,kweli sasa hata udongo wa rufiji tutakula,siyo majani tu.au we umetumwa na hawo watu useme slaa akamatweeeeee????duh,jamani i am f....g.. tired.........................i need some break...
 
Namsomaga Gembe kama mwanachama wa CCM na alikuwa anasomea Msc kule SA. Sijui kama nikwa pesa yake, mwajiri au nani. Naombeni hili mlijue wakati mnachangia.
 
There is no need to get personal. Gembe mkuu umeleta an unpopular but very important argument, and I welcome very much the debate.

Lakini kabla hatujakimbilia kusisitiza kuhusu sheria inayohusu kuweka hadharani kitu cha siri, naomba niulize sheria inasemaje kuhusu nyaraka a siri ni nini. Unajua kesi kama hii haitakuwa mara ya kwanza kufanyika duniani, na si tu huko USSR kama wanavyotukumbusha wachangiaji wengine, bali hata marekani pia, wale waliosoma Communications na Journalism watakumbuka kesi ya Pentagon Papers iliyoikabili New York Times miaka ile ya Vietnam War. Ni kweli hata vyombo vya habari vinabanwa kisheria kuchapisha nyaraka za siri, lakini baada ya back - and forth juu ya ishu hii, kuna ishu nyingine muhimu iliibuka, ni ile excuse ya watendaji kuweka information ambayo ni public information katika makaratasi yaliyoandikwa Top Secret. In the end, ikaja kuwa wazi kwamba si ile top Secret bali "theratens the security of the nation".

So Gembe mkuu, unachosema ni sawa but in the context na kwa kutumia kigezo cha ku-threaten national security - je barua ya Masha iliconstitute that? Je nyaraka za siri za Richmond ziliconstitute a threat to national security? Kama siyo, hakuna haja ya kumshtaki Dr Slaa, maana ni njia ya kuzuia information pertaining to the nation kuwekwa siri kisivyostahili.

Based on my assessment, dr Slaa hakusambaza waraka huu kwa waandishi, kwa hiyo yeye alipewa nyaraka hizo. Alipopewa alizipeleka bungeni na kukabidhi kamati husika. So hii ya kuw ain possession of as it is pia haijakaa sawa kwani anaweza kudai kuwa alipewa aipeleke bungeni na alifuata utaratibu. So pia katika hilo, hawataweza kumpata na hatia.

Inakera na inaudhi wahusika kama akina Masha, kwamba dr Slaa anapata hizi nyaraka, lakini wajue fika ya kuwa hawawezi kutumia wadhifa wao kujiandikia madudu na kutoa amri zisizo za maana na kudai eti top secret. Sasa ile barua yake kwa Waziri mkuu ili kuwa na haja gani kuandikwa Top Secret kama si kuficha makosa yake?
 
Nyaraka za siri ni zipi na ambazo za si za siri ni zipi hasa? Nakumbuka kule Zanzibar wakati wa utawala wa Dr Salmin alimfungulia mashtaka Seif Shariff Hamad kwa kukutwa na nyaraka za siri lakini walishindwa kuendesha kesi na hatimaye aliachiwa huru na haijawahi kuelezwa kinaganaga nyaraka gani za siri alizokutwa nazo Seif Shariff sasa sijui kwa Dr. Slaa kama kweli anazo hizo nyaraka za siri au la.
 
Again huwezi kuwa na maelezo ya kutosha kuhusu ni wapi magazeti ya Mengi yanapata habari nyeti nyingi za uporaji mali wa Mkapa na zingine mbali mbali, sasa tumefikia mpaka mawaziri kurekodiwa kwenye vikao muhimu vya serikali, sasa uta-draw wapi the fine line ya kamata kamata na siri za serikali?

Mkulu tupo pamoja.
Mkuu Gembe ungekuja na agenda ya safisha safisha serikalini kama Paul Kagame tungekuwa ukurasa mmoja siri zinavujishwa humo humo serikalini na si kwamba Dr.Slaa ana password za government kwenda kuchungulia kila nyaraka za siri.
 
Namsomaga Gembe kama mwanachama wa CCM na alikuwa anasomea Msc kule SA. Sijui kama nikwa pesa yake, mwajiri au nani. Naombeni hili mlijue wakati mnachangia.

Analejesha fadhira si unajua tena mtu akikusaidia huwezi mtupa hivi hivi lazima umpiganie.Uzuri kama ndo anakuweka mjini ule ulale na ushibe aaah utakufa na maadui wanao mkwaza muwezeshaji wako.
 
Mimi nadhani tatizo sio kuvujishwa kwa siri na wala sio kukamatwa kwa Dr Slaa.

Tatizo ni kuwa zinazodaiwa kuwa ni siri sio kwa ajili ya ustawi wa taifa bali ni kwa ajili ya watu wachache. Huwezi kuueleza umma kuwa mipango ya kuibia nchi ambayo wamekaa viongozi wachache walafi kuwa ni siri za serikali. Unapoona nyaraka hizi zikivuja ni kwa kuwa hao wanaohusika na utunzaji wa nyaraka wamejiridhisha kuwa huo ni ubadhirifu na ufedhuli mkubwa kwa nchi na wala sio siri za serikali.

Ili sheria iweze kuchukua mkondo wake, tunatakiwa kuanzia huko juu ambapo wizi na ubadhirifu wa mali ya umma unafanywa ndio siri za serikali, tukifanikiwa hapo, basi wenye kutunza nyaraka za serikali hawatakuwa na sababu ya kuzivujisha kwasababu ya maana halisi ya maslahi ya taifa.

Siamini kuwa nyaraka zinazoonyesha wizi wa BOT, mikataba mibovu n.k ni siri za serikali hata kidogo!

Tukianzia huko safari itakuwepo, vingenevyo ni jitahada tu za kuendelea kuficha maovu kwa kisingizio cha siri za serikali. Tunajua wachache kati ya watanzania milioni 40 mmefaidi matunda ya ubadhirifu wa mali ya umma kwa kisingizio cha siri za serikali na huo uhondo ndio msiotaka kuona ukitoweka!
 
Heshima Mbele,

Mhe. Dr. Slaa anahitajika kukamatwa na Vyombo vya sheria hasa baada ya kuwa na Nyaraka ambazo ni siri za Serikali alizozipata kutoka wizara ya Mambo ya Ndani.Tunatambua ni kosa kisheria kwa Mtanzania yeyote kuwa na nyaraka za siri za serikali.

Nchi hii inaongozwa kisheria,na tumekuwa tukipigania hili siku zote .Kwa mtazamamo wangu Naona kuna haja ya Dr. Slaa kuhojiwa hata kukamtwa kwa kumiliki nyaraka za serikali!

Kwa nini siri? Serikali ni ya nani na anafichwa nani? Wangekamatwa hao siri kali kwa kupeleka mambo yetu kwa mataifa ya nje lakini huyu anayewajulisha watu mambo yao akamatiwe nini?
 
Back
Top Bottom