Elections 2010 Dr. Slaa agombee urais 2015, watanzania tumuunge mkono

Mkombozi

JF-Expert Member
Feb 19, 2008
806
426
Wakuu wote,mi naona ni vyema tukaanza kujiandaa kumpa urais Dr Slaa 2015.

Serikali hii bado imeshindwa kutatua matatizo yetu ya msingi. Wananchi wameanza kuonja madhara ya kuvaa kofia,T-shirt, kanga za kijani.

Makali ya mgao wa umeme hayaishi tangia uhuru, DOWANS, bidhaa bei juu, maji tatizo, mifereji ya maji taka issue, matibabu issue, kiwango cha elimu kinashuka kila kukicha na mengine mengi. Bado mwananchi huyu huyu atasahau yote 2015. Cha kufanya ni kumwandaa Dr Slaa angalau aingie ikulu 2015.

Hatuna budi kubadilisha mfumo ili tuone utendaji wa wengine pia. CHADEMA inatakiwa ianzishe operation dondora part 2 ili kupata wanancha wa kutosha na pia kufungua matawi mengi nchi nzima. Jamani maisha kwangu ni magumu mno!

Kila kukicha afadhali ya Jana
 
Atagombea na tutampa KURA, Unajuwa safari yoyote ya ukombozi huwa ndefu na yenye vikwazo vingi, sisi tusikate Tamaa, zaidi tuendelee kuelimishana na hatmae saa ya Ukombozi wa mTANZANIA itafika.
 
dk agombee kwani watanzania wengi walimuunga mkono 2010 wengine walimpigia tu kura kwa kuwa hawaipendi tu ccm lakini wale waliompigia kura hawatakuwa na kazi kubwa sana ya kuwashawishi wengine wamuunge mkono dk kwa kuwa hali ya sasa ni ngumu. maisha ni magumu mno na mkombozi wa kweli ni dk. kwa kuwa ameonyesha nia na hacheki na mafisadi wanaofilisi nchi
 
Hivi hamna mwingine ? Aafu anaonekana kachoka ,uzee unamvamia kwa nguvu ni bora apumzike tu !
 
Mkuu, nafikiri itakuwa vizuri sana Dr Slaa akigombea tena kwa mwaka 2015 kwa sababu haujapita muda mrefu tokea tutoke kwenye uchaguzi mkuu lakini gharama za maisha zinazidi kupanda, mgao wa umeme unazidi kuwa mkali, kwa hiyo tunahitaji uongozi mpya wenye fikra mbadala na tunahitaji kubadilisha utawala mzima wa uongozi mwaka 2015, mwaka 2015 tunahitaji mabadiliko katika uongozi na utawala kiujumla.
 
Mwaka 2015 ni mwaka ambao Mbowe atakuwa anamalizia kipindi chake cha pili cha uenyekiti. Nafahamu kuwa hakuna kipengele kinachomzuia Mbowe kuomba kipindi cha tatu, lakini kwa kuwa utashi wa mafisadi ni kuona CDM inaongozwa na mtu wao, napendekeza Dr sambamba na kugombea urais, achukue pia fomu za uenyekiti wa chama taifa. Huyu anao uwezo wa kumsambaratisha kibaraka yeyote atakayekuwa ameandaliwa na wabaya wa chama.
 
PIPOOOOOOOOOOZZZZZZZZZZZZ P*W*R...Makali yake bado yapo na yanazidi kuongezeka,anayebisha afuatilie anapotoka na hoja zake kwa waandishi wa habari,zinakuwa ni hoja zenye nguvu.Namtakia afya njema kwani Ikulu inamuhitaji.
 
Wagombea hata mara 100 hawezi kuwa rais wa Tanzania...hawezi kuongoza watu makini wa nchi hii

Ajitoe kwanza na hiyo "hidden agenda" yake
 
Sijui kwanini naona kama si Dr Slaa sina wa kumpa kura yangu huko CHADEMA,yaani waliobaki sioni kama wana uwezo wa kuongoza nchi......labda aje mtu mpya lakini hizi type za ZT,Mbowe,Tundu,sijui Mdee sijui Mnyika sijui Selasini,Wenje,Lema,bado kabisaaa,hakuna mwenye hekima na busara ya Dr Slaa,wajipange labda atakuwepo come 2015!!!!
 
Wagombea hata mara 100 hawezi kuwa rais wa Tanzania...hawezi kuongoza watu makini wa nchi hii

Ajitoe kwanza na hiyo "hidden agenda" yake

Typical reflection of Illiterate Tanzanians. Some of you are born Haters,complainers. you do, they complain, you dont, they complain. what solution have you put beside your criticisms? NONE. really i dont get it.

What do you people really want? you want to battle over the true meaning of the word 'politician' or do you really want change. do you want CCM to continue to flow unopposed or do you want a party that can challenge it 'man to man'.

How many times you dont pay your way thru?

My point is: Dr Slaa is not a saint and he does not claim to be one. if he steps into government he will still not be one. he will still have some of his shortcomings,but if he works for the masses, runs an open government, settles some of our aching needs, what more will we want?

The bottom line is WE ARE TIRED, WE ARE FED UP, WE ARE SICK TO OUR STOMACHS with this political recycling, with unopposed corrupt leadership, with tea drinking and glass clinking and conference-holding politicians. All they are known for is TALK.

Corruption will not be cleansed overnight, but people will be held accountable for their actions, they will be made to face the consequences of their actions. Ofcourse Dr.Slaa is capable,he can lead us there and that is the beginning.

Ofcourse will prefer him from now on to engineer and organise corvertly to bringing on board people that have worked and made an impact in their political endeavours into the party so that they can build an extremely strong opposition and i am not talking about those political pro, stitutes who change parties like they change their .......Oops!was almost runnin out of control!.

Dr.Slaa is the best,huyu ndiye Rais wa watanzania,yupo mioyoni mwao.Nimefanya Research ambayo si official most of those who didnt vote they were for Slaa,but had no comfidence with our electorate machinery.Honestl,and probably the bad news for you and other blind followers of CCM is that In free and fair Contest,Slaa is the man to beat in 2015

I stand to be corrected!
 
Hivi hamna mwingine ? Aafu anaonekana kachoka ,uzee unamvamia kwa nguvu ni bora apumzike tu !

mwenzako topical keshapigwa ban shauri ya kuharibu hali ya hewa hovyo... hivi kwa nini msianzishe thread zenu mkachangia ulimbukeni wenu
 
Mwaka 2015 ni mwaka ambao Mbowe atakuwa anamalizia kipindi chake cha pili cha uenyekiti. Nafahamu kuwa hakuna kipengele kinachomzuia Mbowe kuomba kipindi cha tatu, lakini kwa kuwa utashi wa mafisadi ni kuona CDM inaongozwa na mtu wao, napendekeza Dr sambamba na kugombea urais, achukue pia fomu za uenyekiti wa chama taifa. Huyu anao uwezo wa kumsambaratisha kibaraka yeyote atakayekuwa ameandaliwa na wabaya wa chama.

Dr Slaa ni mtendaji nafasi ya ukatibu inamfaa zaidi kuliko uenyekiti.Nafassi hiyo inaweza kugombewa na wengine jambo moja Ukatibu mkuu bado ni nafasi inayomfaa dr Slaa.
 
In terms of Assets we can compare Dr. Slaa with the value of land,it always appreciate and never depreciate like others.Other politician especially from CCM are depreciating while others have no value at all.Dr. atakuwa juu sana by 2015 na hakuna wa kumzuia kuukwaa Urais, we know he can change things around, but for CCM can not be.Lets pray for him buddies.
 
eti sisiemu nao wanamuweka " Eng. Pombe Magufuli" kuwapambanisha na daktari wetu - wameshakwisha hao JK na Makamba washaivuruga sisiemu.
 
Sijui kwanini naona kama si Dr Slaa sina wa kumpa kura yangu huko CHADEMA,yaani waliobaki sioni kama wana uwezo wa kuongoza nchi......labda aje mtu mpya lakini hizi type za ZT,Mbowe,Tundu,sijui Mdee sijui Mnyika sijui Selasini,Wenje,Lema,bado kabisaaa,hakuna mwenye hekima na busara ya Dr Slaa,wajipange labda atakuwepo come 2015!!!!

We shida yako ni majina makubwa au utendaji? nyie ndiyo watanzania mnaotuangusha. Hayo majina yako yamefanya nini so far kama siyo kuuza nchi kwa bei chee?
 
Back
Top Bottom