mafikiri11
Member
- Nov 9, 2010
- 7
- 0
Kunanini ikulu hat mwl.baba wa taifa alisema
Kunanini ikulu hat mwl.baba wa taifa alisema[/QUOTE] Haujaeleweka?? Taifa lahitaji watu safi kama Dr Slaa pale Ikulu.....
Bado upepo wa kisiasa Tanzania haijatulia....hata JK na CCM yake naamini bado hawajajua next move ya Dr. Slaa!! Jk anaweza kuwa surprised, tusubiri tuone!!
nadhani ni wakati wa watanzania kuacha tofauti zetu na kufanya kazi kwa bidii. marekani ni taifa kama mataifa mengine kwahiyo sidhani kwamba wao ndio wanaotupa maelekezo ya kufanya dhidi juu ya nchi yetu.sisi tuko huru na tunajua ya kuwa chaguzi wetu haukuwa huru na haki laikini kwa faida ya taifa letu tuvunje makundi , mbona wao BUSH alipomdhulumu all gore sisi hatukushirikishwa kwenye mahamuzi yao. tusiwe na fikara za kikoloni . tufute tofauti zetu tujenge nchi yetu ni wakati wa kujenga mahusiano mema kwa vyama vyote vya kisiasa
... Unajua, nafarijika sana na UKOMAVU alonao Dr Slaa. Hakurupuki! Wale walobobea kwa disinformation wamekuwa wanaasa kuhusu ..eti ukabila, mara udini na uvunjaji amani wakati hayo yote WAO ndio zao! Kama ilivyosemwa, HATUDANGANYIKI tena all the time. Wachakachuaji mjue kwamba Watanzania wenzenu wanajua mlichofanya. Kwa uhakika wanawajua washindi wao ktk uchaguzi 2010. Haya mambo mnayofanya yaliwashinda SECUROCRACIES nyingine. Mfano mzuri sana ni yule wa Romania, Ceausescu na SECURITATE yake. Siku ile ya mwisho hawa jamaa wa SECURITATE waliingia mitini na Ceausescu akachinjwa. hadi dakika ya mwisho alikuwa haamini kilichotokea.... NGUVU YA UMMA.
Nirejee kwenye mada niseme kwamba the next move has to be extremely well calculated. Hawa jamaa, WEZI (hijackers) wa DEMOCRACY hawataachia kirahisi. As for tactics, that is another chpater. Lets wait and see
maneno yako ni mazuri, lakini kwa vile serikali yetu inaishi kwa kutegemea misaada, na marekani ndio wanaotoa Oksijeni ya $$ zinazompa Kikwete kiburi cha kuiba kura zetu, tuna haja ya kuwahusisha. Kikwete katika moja ya kampeini zake alisema kuwa akaienda nje huwa anaenda kuhemea. Sasa atakosa kwa kwenda kuhemea iwapo marekani itakata mpira wa okisjeni hiyo. Serikali yake itakolapsi na haki yetu itaturudia tena. Obama alishasema siku nyingi kuwa hatavumilia utawala wa kimabavu katika bara hili la Afrika. Kikwete alikuwa anaaminika kuwa alichaguliwa na watu kwa furaha na kujizolea kura halali 80%, leo akishajulikana ni mwizi wa kura basi ndiyo mwisho wake. Kumbuka kuwa Marekani ikisema neno, basi ulaya ya magaharibi yote, Japan na India zitafuata; tutabakiwa na China na Urusi tu.
....na hivi karibuni wataanza kuchimba....:smile-big:Wadau kuna jamaa kanihabarisha kuwa leo asubuhi Mh. Dr. Slaa alionekana akipokewa na RSO wa ubalozi wa Marekani pale ubalozini. Bado hajafahamu nini kilizungumzwa katika mkutano huo.
Mwenye habari zaidi atujuze.
By the way, Serikali ya marekani imeshampongeza JK kwa ushindi?
kwa vyovote vile kama marekani akisitisha misaada basi viongozi wetu sio wataoteseka bali ni yule mwananchi wa kijijini. leo mimi na wewe tunaweza kuishi ata kama nchi yetu ikisitishiwa misaada lakini kizazi cha masikini katika taifa letu kitateseka .kwa maslahi ya taifa letu nadhani ni vema tufanye chaguzi huu umepita na tugange yajayo. dr slaa bado ananafasi ya kujijenga kwani yeye ni katibu mkuu wa chama kitachokuwa na wabunge kama 50(+viti vya wakike ,maalum). mimi ni mshabiki wa haki daima lakini sitokuwa tayari kuunga mkono kauli na shinikizo la marekani ata kama kwa lengo zuri. daima naipenda tz na naheshimu tawala zilizopo pia nazikosoa lakini sitokubali kupokea amri ya kuishinikiza serikali yangu toka kwa wakoloni. ni bora nitawaliwe na kiongozi nisiyempenda kuliko kusalimu amri kwa marekani.
daima chaguzi za kibabe zina mwisho lakini uwezi kukwepa mabadiliko. pia tambua kuanguka kwa ccm ghafla kungeweza kuleta magonjwa ya moyo kwa makada wake na ata machafuko. nadhani tupeni kipindi cha kuwaandaa wana CCM kwa miaka 5 ,hapo itakuwa ni wakati ambao ata wao wanajua watashindwa na hakutakuwa na madhara makubwa. CHADEMA tambueni miaka 5 si mingi. msivuruge nchi mtayokuja kuitawala
unaambiwa adui muombee njaa ili anyooshe mikono juu....mimi nawaombea maisha magumu, ya tabu, ya kuhangaika na kusaga meno wananchi wa tabora, pwani, dodoma, singida kwa kuchagua ccm
MOVE ON ! ELECTIONS ARE OVER ! ITS TIME TO BUILD THE NATION !. TOWENI MAWAZO MGANDO, WAMAREKANI WAMAREKANI...American govt serve the interests of Americans not yours ( get over it!)
Hana lolote slaa amebaki ombaomba hata udiwani hana, arudi kanisani akahubiriinjili apate sadaka za wauminiaendeshee maisha yake
Hana lolote slaa amebaki ombaomba hata udiwani hana, arudi kanisani akahubiriinjili apate sadaka za waumini aendeshee maisha yake
Marekani wangekuwa wapenda demokrasia ya wasingekuwa rafiki wa Hosni Mubarak wa Egypt. Kuwashirikisha katika mambo yetu ya ndani ni kuwapa mwaya wa kupenyeza interests zao.
[/color]
taifa la wamerekani halisubiri kushirikishwa au kutoshirikishwa - wao wakiwa na interests zao kwa taifa lolote duniani wanaingia -
mambo ya ndani ya nchi yetu - yako wapi ya siri??? Kwanza jk alivyokuwa anapiga trip kwenda marekani si ndio alikuwa anawashirikisha??? Wacha dr. Slaa naye aongee na wamerekani - nani asiyejua wamarekani ni wababe tena polisi wa mataifa yote duniani??? hata kama nao wana matatizo yao - lakini ni waingiliaji wakubwa wa utawala wa nchi nyingine na zamu hii ni ya jk..... Atajuta kuchakachua kura zetu.......................
taifa letu.... Taifa letu.... Lipi - hili la tanzania?????? Limeingiliwa na viongozi wabinafsi, wafuja rasilimali zetu, wakatili, wasio na huruma; wapenda kushikilia madaraka na kupeana kifamilia................ Siwezi kusema najuta kuzaliwa kwenye taifa hili la tanzania - ila naomba mungu alete mabadiliko na atuondolee wote wasio faa - kwani mungu ana uwezo - yeye ndio ameshikilia pumzi wanazopumua - na kama oxygen ingekuwa mali ya hawa mafisadi.............du!!!! Watanzania wengi tungekuwa tumekufa ......lakini ashukuriwe mungu they are just human beings ........... Ufisadi wao hautawasaidia pumzi ikinyang'anywa na muumba wao