Katika hali ya kushangaza ambayo haikutarajiwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi Emmanuel Nchimbi amemuumbua mkuu wa jeshi la polisi nchini-IGP Said Mwema.
Waziri Nchimbi amesema usiku wa kuamkia Jumapili IGP Mwema alimpigia simu kumtaarifu kwamba Katibu Mkuu wa CDM Dr Wilbroad Slaa ameapa ni lazima chama chake kifanye mikutano ya hadhara na maandamano na kamwe hawatambui zuio la polisi.Kama vile haitoshi IGP Said Mwema akafoward SMS aliyotumiwa na Dr Slaa kwa waziri Nchimbi kuthibitisha maneno yake.Lengo la IGP ni kuomba msaada wa waziri Emmanuel Nchimbi.
Kauli hiyo imethibitisha lawama za muda mrefu za CDM kwamba jeshi la polisi halifuati sheria katika kazi zake badala yake linafuata maelekezo ya wanasiasa.Ikumbukwe Waziri Nchimbi ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM.
Source:Chanel 10
Kusoma alama za nyakati kwa watawala ni somo gumu sana. Daima wengi hawawezi kulifaulu.