Dr. Sheni azindua Sherehe za Miaka 52 ya Mapinduzi kwa kufanya usafi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Dr.Sheni azindua sherehe za miaka 52 ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kufanya usafi.

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dr Ali Mohamed Shein amezindua sherehe za miaka 52 ya mapinduzi huku akisisitiza kuwa mapinduzi ya mwaka 1964 yalikuwa lazima yafanyike kwa vile ndiyo yalikuwa njia pekee ya kuwakomboa wazanzibari.

Uzinduzi huo wa sherehe hizo ilifanyika kwa zoezi la usafi wa mazingira nchi nzima ambapo Dr Shein aliwaongoza mamaia ya wananchi wakiwemo viongozi na askari wa vikoisi vya ulinziui kwa kushiriki zoezi hilo katika soko la mbogamboga Mombasa wilaya ya Magharibi ambapo Dr Shein aliweza kufagia katika badhi ya sehemu na kushirki kuweka usafi katika soko hilo huku akitamka kuwa wazanzibari wana kila haki ya kujivumnia mapinduzi hayo ambayo yameleta mabadilko makubwa kwa jamii.

Akizumgmzia suala la umuhimu wa usafi kwa nchi nzima Dr Shein ameendelea kuwalaumu wahusika wa kuweka mji na nchi katika mazingira mazuri ya usafi ambapo amesema sheria zipo lakini wahusika wamekuwa wazito kuzitekeleza na kuzifanyika kazi hali inayosababisha zoezi hilo kundelea kuwa gumu.

Sherehe hizo za miaka 52 ya mapinduiz ya Zanaziabr ambapo viongzoi wa sekta mbalimbali Unguja na Pemba wameshiriki katika usafi wa mazingira na kusafisha maeneo mbali mbali katika nchi ikiwa ni miongoni mwa sherehe hizo ambapo miradi 16 na mawe nane ya msingi yanatarajiwa kuwekwa.
092fdc4aab28c94d250c5124d12d9956.jpg

Chanzo: ITV
 
Aache mazingaombwe,atafanyaje usafi akiwa pekeyake?igizo wamelikosea ilitakiwa na wenzie wangekuwa na matololi ya uchafu
 
Hivi huyo jamaa Urais wake si ulifikia kikomo tarehe 2/11/2015 kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984?
Nafasi pekee inayomstahili huyo jamaa kwa sasa ni ya kuitwa Rais mstaafu kama anavyoitwa mwenzie JK.
 
hawa wanawafanya wazanzibari na watanzania kama ni wapumbavu sana,kwa wao ni maigizo na maonesho tu,sawa picha tumeiona na apige na push ups basi,
mpaka picha inaeleza kuwa haya ni maigizo tu watu wote wesimama na kumungalia tu mpaka meya wa mji wa zanzibar pembeni yake hapo wote wanamsindikiza tu akifanya maigizo,sura zao hata vibaya hazioni kwa walivyoizoea dhulma kwao ni jambo la kawaida tu sasa
 
Last edited:
Back
Top Bottom