Uchaguzi 2020 Dr. Shein miaka 10 iliyopita, nitaifanya Zanzibar iwe kama Dubai. Mwaka huu Magufuli nae kaahidi kuifanya Tanzania kuwa kama Ulaya

Jile79

JF-Expert Member
May 28, 2009
17,668
13,237
Dr Shein alitoa hii ahadi miaka 10 iliyopita..
Sasa mimi nawauliza wa Zanzibar, Je hali ikoje hapo Zanzibar?🤣🤣

Baada ya kumsaidia Shein kubadilisha Zanzibar, Magufuli nae kaahidi kuifanya Tanzania kuwa kama Ulaya....

Jamani🤔🤔
118580777_699683057285165_881653632863396829_n.jpg
 
Sasa hivi TBC baada ya Aridhio kuna kituko wanarusha wanaita "bongo kama Ulaya " wanaonyesha treni za Ulaya ,magari ya mwendo kasi na flyovers eti wapo kama Ulaya.

Wanatia aibu wangeonyesha maisha ya Tandale pia tuone kama ipo kama Ulaya.
 
Dr Shein alitoa hii ahadi miaka 10 iliyopita..
Sasa mimi nawauliza wa Zanzibar, Je hali ikoje hapo Zanzibar?🤣🤣

Baada ya kumsaidia Shein kubadilisha Zanzibar, Magufuli nae kaahidi kuifanya Tanzania kuwa kama Ulaya....

Jamani🤔🤔

Mnapashwa kuwa mnauliza ufafanuzi wa namna gani ahadi hizo zinatekelezwa. Dubai inamambo mengi na kwa mantiki nyingine ni dhahiri ahadi imetekelezwa.

Zanzibar sasa ni kama Dubai.

Dubai iko katika falme za kiarabu na inaongozwa kifalme? Nini tena unataka?
 
Sasa hivi TBC baada ya Aridhio kuna kituko wanarusha wanaita "bongo kama Ulaya " wanaonyesha treni za Ulaya ,magari ya mwendo kasi na flyovers eti wapo kama Ulaya.

Wanatia aibu wangeonyesha maisha ya Tandale pia tuone kama ipo kama Ulaya.
Hahahaaa....... Viongozi wengi hata Nairobi tu hawajafika lkn wanazungumzia Ulaya😄😄
 
Dr Shein alitoa hii ahadi miaka 10 iliyopita..
Sasa mimi nawauliza wa Zanzibar, Je hali ikoje hapo Zanzibar?🤣🤣

Baada ya kumsaidia Shein kubadilisha Zanzibar, Magufuli nae kaahidi kuifanya Tanzania kuwa kama Ulaya....

Jamani🤔🤔View attachment 1565787
Mimi so mshabiki wa Shein wala sio mfuasi wa CCM. Ila chini ya Utawala wa Dk Shein mambo mengi yamefanyika kama haha
1. Ujenzi wa mitaro ya maji ya mvua hivyo karibuni mafuriko Znz yatakua historia.
2. Ujenzi wa miundombinu ya maji safi katika mji wa Zanzibar pamoja na ujenzi wa matank makubwa ya kuhifadhia maji.
3. Ujenzi wa majengo ya kisasa ya makaazi pamoja na kuanzishwa miji mipya.
4. Ujenzi wa shopping malls na ukarabati wa majengo ya zamani.
5. Ujenzi wa ofisi za kisasa
6. Ujenzi wa shule za kisasa
7. Ujenzi wa Barbara
8. Uwekaji taa za barabarani mjini Kate.
9. Uboreshwaji huduma za Afya.
10. Kuheshimu haki za binaadamu.

Mwisho namuomba do.Shein awaachie huru masheikh wa Uamsho warudi katika familia zao.
 
Hivi nyinyi mnafikiri Magufuri ni mtu ona tu chama chake kushindwa kukiongoza anasaidiwa na maafisa vipenyo tu , Chama chake chenyewe hawamtski Ila hawawezi kuonyesha hadharani pamoja na kuwa wanasimamia na kupiga kampeni wanaogopa tu asiwakolimbe .
 
Hujamsikia Balozi Seif Ali Idi ivi karibuni alipokwenda kutembelea ile michenzani mall na kisonge maskan? kwa majengo yale mawili tayari Zanzibar imekuwa Dubai kwa mujibu wake na amesisitiza kuwa wafanyabiashara badala ya kwenda Dubai sasa watakuwa wanaenda michenzani kununua mizigo! Hio ndio Zanzibar chini ya Ma CCM bana, ata kuweka taa barabarani basi ni jambo la sherehe. :D
 
Hujamsikia Balozi Seif Ali Idi ivi karibuni alipokwenda kutembelea ile michenzani mall na kisonge maskan? kwa majengo yale mawili tayari Zanzibar imekuwa Dubai kwa mujibu wake na amesisitiza kuwa wafanyabiashara badala ya kwenda Dubai sasa watakuwa wanaenda michenzani kununua mizigo! Hio ndio Zanzibar chini ya Ma CCM bana, ata kuweka taa barabarani basi ni jambo la sherehe. :D
Wawa wekee taa aisee usiku muwe mnashinda mnapiga ma-drift na 0-60 kwa sana tu,hahah.
 
Mimi so mshabiki wa Shein wala sio mfuasi wa CCM. Ila chini ya Utawala wa Dk Shein mambo mengi yamefanyika kama haha
1. Ujenzi wa mitaro ya maji ya mvua hivyo karibuni mafuriko Znz yatakua historia.
2. Ujenzi wa miundombinu ya maji safi katika mji wa Zanzibar pamoja na ujenzi wa matank makubwa ya kuhifadhia maji.
3. Ujenzi wa majengo ya kisasa ya makaazi pamoja na kuanzishwa miji mipya.
4. Ujenzi wa shopping malls na ukarabati wa majengo ya zamani.
5. Ujenzi wa ofisi za kisasa
6. Ujenzi wa shule za kisasa
7. Ujenzi wa Barbara
8. Uwekaji taa za barabarani mjini Kate.
9. Uboreshwaji huduma za Afya.
10. Kuheshimu haki za binaadamu.

Mwisho namuomba do.Shein awaachie huru masheikh wa Uamsho warudi katika familia zao.


Yaani, ivo ulivovilist hapo ni vichekesho kabisa, average yake ni kuwa kila mwaka kimefanyika kimoja tu mfano.
kwaio unataka kutwambia kuwa ni wa kupongezwa kufanya vitu ambavyo ndani ya miaka miwili vingekuwa vishamalizwa vyote?

Halafu unampongeza rais kwa majengo yanayojengwa kwa pesa za ZSSF? Yaani ni sawa na mimi nijenge nyumba halafu uje umsifie rais kama vile yeye ndio alienijengea au amechangia kwenye ujenzi!

Yaani watu kama wewe, ndio wanaochelewesha maendeleo. tusubiri miaka 50 ijayo waje kusifiwa kuwa wameweza kubandika alama za barabarani :D
 
Hahaha huwezi amini kuna vichwa huko CCM vinaamini kila kitu wasemacho hao watawala.

Kuna mtu wa CCM tulikuwa tukiongea akasema daraja la mfugale ndiyo ulaya wanaziita highway.
walichowaweza ccm watanzania ni kuwanyima elimu ili wawatawale vizuri
 
Back
Top Bottom