Dr Shein Huyooo!

Engineer Mohamed

JF-Expert Member
Jul 27, 2007
451
9
Shein aenda Denmark, Uingereza

2008-04-15 10:33:26
Na Mwandishi Wetu

Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein, jana aliondoka nchini kwenda Copenhagen, Denmark na London, Uingereza kwa ziara ya kikazi ya siku tano.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na ofisi ya Makamu wa Rais ilieleza, akiwa nchini Denmark, Dk. Shein atamwakilisha Rais Jakaya Kikwete kwenye mkutano wa kwanza wa Kamisheni ya Afrika unaotarajiwa kufanyika kesho.

Kamisheni hiyo ya Afrika ambayo imebuniwa na serikali ya Denmark, inalenga kuyapa msukumo na kipaumbele masuala ya ukuaji wa uchumi na ajira barani Afrika katika ngazi ya kimataifa.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mbali na kuhudhuria kikao hicho, Makamu wa Rais pia atakutana na baadhi ya viongozi wa Denmark akiwemo Waziri Mkuu Bw. Anders Fogh Rasmussen na Waziri wa Mambo ya Nje, Dk. Per Sting Moller
Nchini Uingereza ambako atawasili keshokutwa asubuhi, Dk. Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa uwekezaji ambao utafanyika baadae mchana na jioni atahudhuria chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima yake na waandaaji wa mkutano huo.

Siku inayofuata Makamu wa Rais atazindua `forum` ya watanzania waishio nje ambapo anatarajiwa kuelezea dhamira ya serikali ya kushirikiana na kusaidia namna Watanzania waishio nje wanavyoweza kutoa mchango wao katika maendeleo humu nchini.

Makamu wa Rais anatarajiwa kurejea nchini Jumamosi ijayo.
 
Hii imekata kebe yote!!! kama nijuavyo hii safari ni ya kitaifa... haijalishi ameenda JMK au AMS!

Wale watu wa kuhesabu safari za Rais kazi kwenu!!!
 
Kwani Kikwete amepatwa na udhuru gani? I mean yuko wapi kwa sasa maana haya mambo yanatuchanganya.
Na mkutano wa dharura Zambia alikwenda pia?
 
Kwani Kikwete amepatwa na udhuru gani? I mean yuko wapi kwa sasa maana haya mambo yanatuchanganya.
Na mkutano wa dharura Zambia alikwenda pia?

Amejialika USA kuzungumzia swala la Zim wakati waafrika wenzake wako Zambia. Ameogopa kupita Denmark na U.K. kwa ajili ya issue ya Chenge kwa sababu wabunge wa huko wamepamba moto wanadai misaada inayokuja bongo inaishia kwa viongozi.Kinachoshangaza zaidi magazeti yetu ya bongo yaliaandika suala la Chenge lakini wakasema tunamjua lakini jina tunalihifadhi lakini magazeti ya hawa wenzetu wajibikaji wametaja jina lake ndipo magazetti yetu bongo yakatoa jina nina wasiwasi hata magazeti yetu yana wahifadhi hawa mafisadi.
 
Ni Bora Mzee Wa watu akapumzike kwanza,

Je ingekuwa vipi kama Lowassa angekuwapo mpaka leo,wakati Mkuu wa nchi hayupo na makamu wa Rais hayupo.Je angemteua M.M Mwanakijiji kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya miundo Mbinu??

Mzee wa kasungura Bwana
 
Du ina maana Pinda sasa yeye ndiye?aminiaa jamaa anatisha sana kwa sasa......balaa sana ...sasa hao kina Chenge watadhibitiwa kwa tamko la Pinda?
 
Hivi rais wetu vipaumbele vyake vimekaajekaaje? Yaani anakimbilia US kuongelea maswala ya Zimbabwe wakati ya Zanzibar tu hapo nyumbani kwake anayapiga chenga? Ndio maana alishawahi kusema "ukiitwa na wakubwa(akimaanisha Bush, Blair et. al) utakataa?" kumbe ndio keshajipachika ukibaraka...

It's about time someone drilled some commonsense into the head of this sorry excuse of a president!
 
Baadhi ya sponsors wa Diaspora forum wamejitoa baada ya kusikia JK haji. Walikuwa wanategemea publicity na kupiga picha na JK.

Inasemekana pia kuna Wahindi wengi waliomba ubalozi ili wakutane na JK, baada ya kuona ni Shein, wakaomba majina yao yaondolewe.

Shein kaambiwa, lakini yeye kasema kwanza huwa hataki kukutana na watu wa namna hiyo maana wanatanguliza interests zao mbele.

Hao ndio aina ya watu ambao Watanzania tuna deals nao. Shein ni makamu wa rais, lakini wao wanaona biashara ni kuonana na JK tu.

Inaelekea hata ubalozi umechukizwa na vitendo hivyo. Huenda huko mbele ni wale wavumilivu, waliokubali kuendelea kushiriki kwenye forum hata baada ya kusikia JK haji ndio watapewa nafasi huko mbeleni ya kuonana na JK

Habari zingine zinasema, Shein kawaambia mawaziri na wasaidizi wengine ambao alikuwa nao Denmark warudi TZ maana hawana kazi za kufanya London. Hataki waendelee kuunguza pesa za walala hoi.

Huyu Shein kakaa na fisadi Mkapa lakini hakuna hata tope moja lililo mrukia, inaeleke jamaa ni msafi mno. Ndio maana matapeli wa London wanaona
hakuna deal.

Mwana JF, Yebo Yebo, kesho ana nafasi kubwa kwenye forum, wana JF jiandaeni mkao wa kula.

Ndio hayo tu wakuu kwa leo.
 
Kikwete amepoteza urafiki na wazungu ,wamemshitukia kuwa hana ukweli juu ya feza iliyotafunwa ,ndio sasa anajielekezesha kwa wachina ,wandugu huo ndio ukweli na mtaona siku hizi kuwa safari zote za ulaya zitakufa yaani sasa wanamwona ni kibaka tu.
 
Kwa nini MKAPA (Che-nkapa) alipoacha madaraka aliwasihi wana CCM wenzake wamwache Shein aendelee kuwa makamu wa rais? Je, walikuwa na deal gani pamoja?

Kama shein ni msafi inakuwaje yote haya yanatokea na yeye amekaa tu anangoja nini kulinusuru taifa na hawa Mafisadi.
 
...jamani mimi nashauri hii miaka miwili iliyobaki wamalizie ,,,,dr shein ..kama kaimu rais..na pinda...at least tunaweza kuwaelewa...
 
Baadhi ya sponsors wa Diaspora forum wamejitoa baada ya kusikia JK haji. Walikuwa wanategemea publicity na kupiga picha na JK.

Inasemekana pia kuna Wahindi wengi waliomba ubalozi ili wakutane na JK, baada ya kuona ni Shein, wakaomba majina yao yaondolewe.

Shein kaambiwa, lakini yeye kasema kwanza huwa hataki kukutana na watu wa namna hiyo maana wanatanguliza interests zao mbele.

Hao ndio aina ya watu ambao Watanzania tuna deals nao. Shein ni makamu wa rais, lakini wao wanaona biashara ni kuonana na JK tu.

Inaelekea hata ubalozi umechukizwa na vitendo hivyo. Huenda huko mbele ni wale wavumilivu, waliokubali kuendelea kushiriki kwenye forum hata baada ya kusikia JK haji ndio watapewa nafasi huko mbeleni ya kuonana na JK

Habari zingine zinasema, Shein kawaambia mawaziri na wasaidizi wengine ambao alikuwa nao Denmark warudi TZ maana hawana kazi za kufanya London. Hataki waendelee kuunguza pesa za walala hoi.

Huyu Shein kakaa na fisadi Mkapa lakini hakuna hata tope moja lililo mrukia, inaeleke jamaa ni msafi mno. Ndio maana matapeli wa London wanaona
hakuna deal.

Mwana JF, Yebo Yebo, kesho ana nafasi kubwa kwenye forum, wana JF jiandaeni mkao wa kula.

Ndio hayo tu wakuu kwa leo.

Huyu Mzee stand to be clean sijui kama kuna mtu ana issue za madeal yake, as far as i know this man is clean pampja na kukaa na mlafi wa mali za umma Che nkapa
 
Kwa nini MKAPA (Che-nkapa) alipoacha madaraka aliwasihi wana CCM wenzake wamwache Shein aendelee kuwa makamu wa rais? Je, walikuwa na deal gani pamoja?

..mkapa alijua kuwa shein yupo serious na kazi na haingiliki....huku akijua udhaifu wa kikwete alijua kuwa dr shein angemsaidia kuuziba....

..lakini tukubali watu wote jk aliokuwa anashauriwa na mkapa na idara iliyopita ...ni hawa dr shein na pinda ..na ndio at least wamebakiwa wasafi kwenye serikali yake...hawa alioingia nao kina..rostam,meghji,lowassa,chenge ...membe..anaowabeba naona kweli wazee walikuwa right hawafai!!
 
Baadhi ya sponsors wa Diaspora forum wamejitoa baada ya kusikia JK haji. Walikuwa wanategemea publicity na kupiga picha na JK.

Inasemekana pia kuna Wahindi wengi waliomba ubalozi ili wakutane na JK, baada ya kuona ni Shein, wakaomba majina yao yaondolewe.

Shein kaambiwa, lakini yeye kasema kwanza huwa hataki kukutana na watu wa namna hiyo maana wanatanguliza interests zao mbele.

Hao ndio aina ya watu ambao Watanzania tuna deals nao. Shein ni makamu wa rais, lakini wao wanaona biashara ni kuonana na JK tu.

Inaelekea hata ubalozi umechukizwa na vitendo hivyo. Huenda huko mbele ni wale wavumilivu, waliokubali kuendelea kushiriki kwenye forum hata baada ya kusikia JK haji ndio watapewa nafasi huko mbeleni ya kuonana na JK

Habari zingine zinasema, Shein kawaambia mawaziri na wasaidizi wengine ambao alikuwa nao Denmark warudi TZ maana hawana kazi za kufanya London. Hataki waendelee kuunguza pesa za walala hoi.

Huyu Shein kakaa na fisadi Mkapa lakini hakuna hata tope moja lililo mrukia, inaeleke jamaa ni msafi mno. Ndio maana matapeli wa London wanaona
hakuna deal.

Mwana JF, Yebo Yebo, kesho ana nafasi kubwa kwenye forum, wana JF jiandaeni mkao wa kula.

Ndio hayo tu wakuu kwa leo.

Shein ninamwamini kabisa. Ni system tu ya chama chao ndio haimruhusu am-challenge Kikwete uchaguzi ujao. Hata ile 'modesty' yake nadhani haiwezi kumruhusu kufanya hivyo. What a pity!

Hao wahindi waliojitoa ndio mafisadi hao. Ubalozi ututajie majina yao, na wasiruhusiwe kamwe kuja kutuibia mali zetu kwa kisingizio cha kuwekeza.
 
Huyu Mzee stand to be clean sijui kama kuna mtu ana issue za madeal yake, as far as i know this man is clean pampja na kukaa na mlafi wa mali za umma Che nkapa

1. Muungwana, kule Chamwino mbele ya wakulu wa ccm, aliambiwa achague pm, akmachagua lowassa, wakulu wakamjia juu sana kuwa haiwezekani, akasema kuwa hilo halina mjadala, wakaishia kukubali,

2. Alipoambiwa makamu, akasema either awe meghji, khatibu, au shamuhuna, wakulu wote waliokuwepo wakagoma, ikakubaliwa kuamuliwa kesho yake kwenye kikao cha cc, walipofika kule mkapa akawaomba salmin na mwinyi, watoke chemba ili wao wawili waamue nani awe!

Waliporudi, waliamua huyu mkulu aendelee, sababu muhimu ni kwamba hana makuu wala ambitions za urais, kwa sababu aliombwa na mapema na baadhi wakulu achukue fomu ya urais akakataa kata kata, tena kwa very strong arguments, moja wapo ikiwa ni yeye atawafanya nini mafisadi, hasa wa kutoka bara ambao wamekuwa wakijifanyia wanachotaka in all their political career, akawauliza yeye ni nani wakuja kuwasafisha, ndipo kwa mara ya kwanza alipojiwekea heshima nzito sana na wakulu, ndio maana mpaka leo bado anasimama akiwa clean na with more moral authority, ingawa huwa hasemi kabisa kwenye vikao muhimu.

Lakini ni a clean leader na anafaaa kwa sababu ana mawazo ya mapinduzi, ingawa pamoja na kwamba haisemwi sana au kabisa, ukweli ni kwamba wa-Tanzania, tungekuwa better off na rais kama Marehemu Omari Juma angekuwepo, maana that was a leader, uliza wakulu wote huko cc vitu vyake akiwa hai, nakumbuka siku moja nilimwambia mlizni wake mmoja twende shopping akanijibu kuwa sio wakati anamlinda Omari juma, labda viongozi wengine, akaniambia usicheze na huyu mpemba, Mungu amlaze mahali pema, na inaeleweka wazi wala sio siri kuwa ndiye aliyetakiwa kupewa ukulu Anyways,


Mungu Aibariki Tanzania!
 
Mkuu FMES
Sisi Wengine ni wadogo sana. Lakini huwa tunakaa hapa ni kwa sababu ya maneno ya busara kama haya.
 
Wote tunajua ..viongozi toka Pemba sikuzote huwa ni SAFI

hivi mnamkumbuka mzee IDRISSA ABUL WAKIL aka BABU?

hivi familia yake inatunzwa au ndio wameachwa tuuu

 
Waliporudi, waliamua huyu mkulu aendelee, sababu muhimu ni kwamba hana makuu wala ambitions za urais, kwa sababu aliombwa na mapema na baadhi wakulu achukue fomu ya urais akakataa kata kata, tena kwa very strong arguments, moja wapo ikiwa ni yeye atawafanya nini mafisadi, hasa wa kutoka bara ambao wamekuwa wakijifanyia wanachotaka in all their political career, akawauliza yeye ni nani wakuja kuwasafisha, ndipo kwa mara ya kwanza alipojiwekea heshima nzito sana na wakulu, ndio maana mpaka leo bado anasimama akiwa clean na with more moral authority, ingawa huwa hasemi kabisa kwenye vikao muhimu.
mkuu field Marshal hii argument ya mzee Shein naikataa kabisa. yeye hapo alipo yupo katika line ya kuwa prizidaa wetu. at any time T yeye anaweza kulikwaa rungu kwa mujibu wa katiba, kama alikataa uraisi kwa hoja ya kwamba atawafanya nini mafisadi sasa kwa nini akubali umakamu wa Raisi?.
kama kweli alitoa hiyo argument basi mimi ninadhani hiyo argument siyo nzito sana.kwa hiyo ina maana pindi anapokaimu uraisi suala la kuwashughulikia mafisadi huwa halimo katika agenda yake au?.

Ila frankly speaking tulipompoteza marehemu dk Omar Ali Juma lile lilikuwa ni pengo kubwa sana kwa Taifa. unajua yule mzee alikuwa hata akiongea mtu unafeel kabisa kwamba huyu ni mtu mwenye kujali watu, unahisi kabisa sauti ile inatoka ndani ya roho.

Rest in peace dk Omar, may the Almighty God rest your soul in peace.
 
Kuwa na watu aina hii ni hatari ,je huyu jamaa amewahi kuukemea ufisadi si ajabu ikawa hata hajui lililopo ,maana kila wakati ni kama mtu yupo usingizini tu ,hivi anaelekea akiwepo ofisini na hana la kufanya basi inawezekana kabisa seketari wake akawa anasikia mkoromo wa mbali.
Kiongozi huyu hafai kwa nchi inayotafuta maendeleo kwa nchi ambayo imo katika misukosuko,kwa nchi ambayo imejaa viongozi wezi ,sasa hivi aulizwe anawajibika vipi ,anamsaidia vipi Raisi na Wananchi wake juu ya suala kama hili lililoikumba nchi la kumegwamegwa uchumi wake na watu wasioheshimu umasikini wao au watu wasioridhika na umasikini wao ambao wamegeuza Serikali sehemu ya kufanya mambo yao binafsi.
Shein inabidi ajiuzulu kwani inaonekana kabisa hawezi kuilinda nafasi aliyopo wala kuitetea,ameshindwa kikazi au sehemu aliyopo hailingani na utendaji wa ngazi hiyo,hivi huyu jamaa kama makamo wa raisi anao ubavu wa kumwajibisha mtu ,je anaweza kuutumia ni lini alilihutubia Taifa ?
Halafu mnasema anafaa kuwa Raisi hao machachari inaonekana kushindwa ,huyu si ndio itakuwa watu wanafika na gari na kuisafisha benki kuu mpaka fanicha watakongoa.
Huyu anakula feza ya Umma bure ,yaani naweza kusema ni katika wale wanaosema wacha wafanye wanavyotaka ikifika mwisho wa mwezi yeye anachoosha mkono tu kupokea kitita chake.Hii ni aina ya viongozi ambao pia wamo katika Serikali ya Kikwete ni ufisadi pia kwani hawana mchango wa aina yeyote ,mambo ambayo yanatakiwa yawe yanafanywa na meya ankwenda kufanya yeye ,umeona wapi mambo haya Makamo wa Raisi anakwenda kufungua soko ,anakwenda kufungua jengo haya si mambo ya kufanywa na makamo wa Raisi ,mambo ya kuweka majiwe ya msingi haya ni mambo ya wakuu wa wilaya na mikoa au hao mimeya.
Huyu anatakiwa kazi yake iwe anaweza kuwaita mawaziri na kuwaweka kiti moto,kuwaita wakuu wa mikoa kuwaweka kiti moto kuwaita wakuu wa polisi kuwaweka kiti moto , kuzunguluka nchi nzima kuwaweka viti moto wakuu wa mashirika ya umma na yanayomilikiwa na serikali ,isingelifika hali hii tuliyonayo ya kuzuka baadhi ya makampuni eti yanamilikiwa na serikali wakati serikali yenyewe haiyajui ,wanabaki kurushiana mpira ,tatizo ni hili la kuwa na viongozi wasio wajibika na kuhusika katika mambo muhimu ,viongozi ambao hawawezi kumkea mtu , hawawezi kutenganisha uswahiba na kazi waliyokabidhiwa ,wanashindwa kutenganisha urafiki uliopo kazini na katika vilabu vya pombe unategemea nani atamuwajibisha nani.
Kiongozi ni yule ambae anabadilika na kutenganisha kazi na urafiki,unapokuwa katika Uongozi unahakikisha unakuwa na sura nyengine na unapokuwa kwenye uswahiba unakuwa na sura nyengine..wanasema unapokuwa katika uongozi unatakiwa uwe unalinda tonge yako na usikaribishe kitu ambacho kitahatarisha tonge yako kuharibika na kutofika mdomoni.
Unapokuwa katika uongozi ni lazima uheshimike na kutoingiliwa katika maamuzi ya kiungozi katika utekelezaji na hapo ndipo unapojenga nguvu ya Uongozi kiongozi ni lazima aogopwe anapokuwa kazini ni lazima awe na amri juu ya maamuzi yake na sio kuwa kiongozi legelege ,ionekane anachokiamrisha kinatekelezwa kwa wakati.
 
Wote tunajua ..viongozi toka Pemba sikuzote huwa ni SAFI

hivi mnamkumbuka mzee IDRISSA ABUL WAKIL aka BABU?

hivi familia yake inatunzwa au ndio wameachwa tuuu



al-marhumu BABU alikuwa mtu wa MAKUNDUCHI.

mungu amlaze mahali pema peponi.

tuwekee pic ya mzee wa mikasi akiwa ktk salah ya IJUMAA huko LONDON.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom