Dr Shein: Anabaguliwa?

Leo kuna habari inaeleza kuwa Ris Jakaya amekuwa anamtenga Shein na kumpendelea Pinda kwa nia ya kumwandaa kuwa Rais wa 2015. Nini maoni yenu kuhusu hili? Mimi naona hii habari kama yakichochezi hivi na ina nia ya kuchonganisha Wazanzibari na Wabara.
Washikaji nawaomba mjue kupambanua kati ya pumba na mchele! Watu wasimzulie JK majambo kwa sababu zao finyu za kisiasa. Anambaguaje Shein? Tunaomjua Shein tunasema, Shein si mtu wa jukwaa, si msemaji. Kama ni kutoonekana kwake, basi ni kutokana na tabia yake mwenyewe ya kukaa nyumanyuma. Msimsingizie JK wala Pinda kwa hili. Kama ni urais wa 2015, nani aliwaambia Shein anafaa? Lazaros
 
Washikaji nawaomba mjue kupambanua kati ya pumba na mchele! Watu wasimzulie JK majambo kwa sababu zao finyu za kisiasa. Anambaguaje Shein? Tunaomjua Shein tunasema, Shein si mtu wa jukwaa, si msemaji. Kama ni kutoonekana kwake, basi ni kutokana na tabia yake mwenyewe ya kukaa nyumanyuma. Msimsingizie JK wala Pinda kwa hili. Kama ni urais wa 2015, nani aliwaambia Shein anafaa? Lazaros

Bwana Lazarosmtindi ina maana mtu anafikia nafasi ya Umakamu wa Rais akiwa hana wazo la Urais? Mimi nadhani urais anautaka. I know the man is extremely intelligent hasa katika eneo lake la specialisation. Unajua hii ya kusema Wapemba hawafai ni potofu na ndo maana wakamzushia Salim kuwa Hizibu. Salim angekuwa Rais baada ya nyerere lakini hiyo xenophobea ya Upemba ikamwangusha. But, trust me, I think there are very brilliant chaps in Pemba than in Unguja!
 
Mama,
Na wewe unajuaga kuzibua majambo!


Siku nyingi sijamsikia, mara ya mwisho alihudhuria kuapishwa kwa rais mpya wa Zambia. Kabla ya hapo ilikuwa ziiiiiiiiiiii, na baada ya hapo ni kama vile ziiiiiiiiiiiiii. Mafile mengi sana mezani kwake nini?
 
sijamsikia siku nyingi vice president shein.


wakati huu ndio tulimtegemea azibe vacuum of power...hasa ukizingatia ana uzowefu tangu awamu ya tatu......yaani alikuwa hata anasikika kuliko sasa....

..nadhani kuna mambo hayaendi sawa ....na msishangae..mwaka 2010...hatakubali kugombea tena na muungwana...ataamua kwenda kulima nazi na karafuu kule wete........reserve this!!!
 
wakati huu ndio tulimtegemea azibe vacuum of power...hasa ukizingatia ana uzowefu tangu awamu ya tatu......yaani alikuwa hata anasikika kuliko sasa....

..nadhani kuna mambo hayaendi sawa ....na msishangae..mwaka 2010...hatakubali kugombea tena na muungwana...ataamua kwenda kulima nazi na karafuu kule wete........reserve this!!!



Lakini kikatiba 2010 ataruhusiwa kugombea, ameshakuwa kwa vipindi viwili tayari. Au kwa mavice pres inakuwa tofauti na muda wanaotakiwa waserve marais kikatiba?
 
So far Pinda ameprove kuwa Urais hauwezi, kama ukishindwa kuwa PM mzuri ni obvious kuwa urais hauwezi. Na sijui kama kweli JK ana uwezo wa kumuandaa mu kuwa rais, inawezekana hii ni porojo tu.
 
..ma vp hawapo binded....akitaka anaweza kugombea na jk 2010 na akipenda tena 2015 akagombea urais...hiyo ndio faida ya kuwa vp........lakini huyu inaonekana picha na jk hawaendani.....aliwekwa tu pale kwa kuwa ccm walikuwa hawataki kumuamini jk moja kwa moja.....jk wanted somebody else.......msishangae huyu 2010 akaamua kukaa kando.....
 
..ma vp hawapo binded....akitaka anaweza kugombea na jk 2010 na akipenda tena 2015 akagombea urais...hiyo ndio faida ya kuwa vp........lakini huyu inaonekana picha na jk hawaendani.....aliwekwa tu pale kwa kuwa ccm walikuwa hawataki kumuamini jk moja kwa moja.....jk wanted somebody else.......msishangae huyu 2010 akaamua kukaa kando.....


mmh vipi akiamua kugombea urais kabisa. Kimya kingi kina mshindo mkuu.
 
Leo kuna habari inaeleza kuwa Ris Jakaya amekuwa anamtenga Shein na kumpendelea Pinda kwa nia ya kumwandaa kuwa Rais wa 2015. Nini maoni yenu kuhusu hili? Mimi naona hii habari kama yakichochezi hivi na ina nia ya kuchonganisha Wazanzibari na Wabara.

Inategemea Makamu wa Rais anakuwa na shughuli gani pindi zinapotokea events kama hizo. Kuna mambo muhimu ambayo Mh. Shein anatakiwa kufanya kuliko kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa baraza la mawaziri nchi jirani. Ni mikutano mingapi ya Kimataifa ambayo Shein ameudhuria ambayo inaendana na ngazi yake!! Acheni mambo ya udaku. Si kila habari inayoandikwa kwenye gazeti Bongo JF inatakiwa kuisadiki. Kama itakuwa hivyo basi hata habari za magazeti ya mafisadi Rai, Tazama, Mtanzania na mengineyo kila leo yangekuwa yanajadiliwa hapa. Mie nafikiri hilo gazeti lililoandika hiyo habari linaweza likawa na MOJA YAKE KICHWANI.
 
mmh vipi akiamua kugombea urais kabisa. Kimya kingi kina mshindo mkuu.


...........mama ili kushinda political post tanzania kuna la zaidi ..kuliko uwezo,unatakiwa uwe unajuwa FITNA za kisiasa......na uwe ma migongo ya kupandia ....hadi tutakapoondokana na fitna kwenye siasa na kusimama kwenye kampeni za ukweli..wa kisiasa..na sera,hatutakuja kupata viongozi wazuri.....

ukweli wa kwamba shein haziwezi wala hazitaki FITNA za siasa ..ni dhahiri hataweza kugombea...alikuwa na nafasi kubwa mwaka 2005..lakini alikataa kwa sababu kama hizo...yeye ni msomi zaidi ya mwanasiasa...maisha yake ni NYUMBANI-OFISINI[ZIARA]-MSIKITINI.....,[au angekuwa mkristo ningeweka KANISANI]........Wakati wanasiasa wengine wanongezea hapo..jioni wanakuwa kwenye vikao vya pombe,karata,story....ets...ndio kwenye fitna huko.....

..shein hana tofauti na salim..kwani naye siasa za fitna haziwezi...ndio maana hajawahi kugombea elective post....pamoja na kuwa angekuwa rais mzuri ..wekness hiyo ndiyo ilimgharimu against kikwete ambaye....anajuwa fitna.....na ilikuwa ni kawaida tangu akiwa waziri baada ya kazi ..kupita huko na huko kwenye "vikao" na kujichanganya na watu wa kawaida .......ilifanya watu wamuone among of them[us]...ndio KIKWETE NI JACOB ZUMA WA TANZANIA ..au alikuwa!!!
 
Leo kuna habari inaeleza kuwa Ris Jakaya amekuwa anamtenga Shein na kumpendelea Pinda kwa nia ya kumwandaa kuwa Rais wa 2015. Nini maoni yenu kuhusu hili? Mimi naona hii habari kama yakichochezi hivi na ina nia ya kuchonganisha Wazanzibari na Wabara.

Nani kakwambia Shein anataka urais na umesikia wapi, tupatie hiyo source yako, MOD peleka kwenye Udaku hii thread
 
Leo kuna habari inaeleza kuwa Ris Jakaya amekuwa anamtenga Shein na kumpendelea Pinda kwa nia ya kumwandaa kuwa Rais wa 2015. Nini maoni yenu kuhusu hili? Mimi naona hii habari kama yakichochezi hivi na ina nia ya kuchonganisha Wazanzibari na Wabara.

Hivi uchochezi ni kitu gani? Pengine huyo mtu kapata tetesi. Kwa nini karibu kila kitu 'kigeni' kinachosemwa siku hizi kinasemekana kuwa uchochezi au uzushi au ni namna ya ku'suppress' maoni ya watu au hata 'interpretation' au tafsiri yao ya yale yanayotokea?

Mimi nadhani kuna haja ya kuwa wavumilivu zaidi na kujaribu kusoma alama za nykati. Baadhi ya mambo yamekuwa yakisemwa ni uchochozi au uzushi lakini baadaye yamekuja kuonekana kuwa kweli. Hivyo, tujipe nafasi ya kuona kama ni uchochezi au la.
 
Sheni hauwezi Uraisi na yeye mwenyewe anajua ila hapo alipo anaweza kubakia hata miaka mia hana makuu , mwenyewe na mikasi yake yaani mambo ya ndani tu si mtu wa misafara halafu jamaa ana wivu kibao si mnamwona ?Anaweza akakuchoma mkasi.

ila mzee mi namwaminia kwa kushusha nondo ndie mtu katika serikali nikisikia anaongea namsikiliza kama mkuu wa nchi wengine tabu tupu lazima waweke u CCM mwingiiiiii wanajisahau kama wanawaongoza watanzania na wala sio CCM mi wananiudhi wanapokwenda kwenye ziara zao za kiserikali halafu wanavaa mikijani belive it mtu kama sio CCM hatachukulia maanani yale unayozungumza na hao CCM wanzanzisha upinzani kwa kupiga vigelegele hata pale pasipotakiwa yani utumbo mtupu ndo maana tutaihusisha EPA na CCM maana wahusika walikuwa wanavaa kijani wakitoa misaada kijani na mkienda kupokea misaada kijani rais akienda kukutana nao anavaa kijani tabu tupo

tutawze kuiendeleza CCM km tutajitahidi kuitenganisha na serikali la sivyo km mjuavyo 60% ya wana CCM ni mafisadi mtajitenga vipi??
 
...........mama ili kushinda political post tanzania kuna la zaidi ..kuliko uwezo,unatakiwa uwe unajuwa FITNA za kisiasa......na uwe ma migongo ya kupandia ....hadi tutakapoondokana na fitna kwenye siasa na kusimama kwenye kampeni za ukweli..wa kisiasa..na sera,hatutakuja kupata viongozi wazuri.....

Hivi uchochezi ni kitu gani? Pengine huyo mtu kapata tetesi. Kwa nini karibu kila kitu 'kigeni' kinachosemwa siku hizi kinasemekana kuwa uchochezi au uzushi au ni namna ya ku'suppress' maoni ya watu au hata 'interpretation' au tafsiri yao ya yale yanayotokea?

Mimi nadhani kuna haja ya kuwa wavumilivu zaidi na kujaribu kusoma alama za nykati. Baadhi ya mambo yamekuwa yakisemwa ni uchochozi au uzushi lakini baadaye yamekuja kuonekana kuwa kweli. Hivyo, tujipe nafasi ya kuona kama ni uchochezi au la.

PM na Magobe T, mmesema kweli 100%. Taifa linaangamia kwa kukumbatia siasa za chuki, fitna na majungu. Vongozi waadilifu tunao lakini ndio hivyo tena.

Kuna waliokula yamini (mfano) Seif Sharif wala mpemba yeyote asiwe rais Zbar, ati kwakuwa waasisi wa Mapinduzi 'walishawakataa'. Tuliona Chimwaga hata SAS, alipopigwa chini pamoja na vijisababu vingine, eti 'uarabu' wake! ...JAMANI?

Hata Dr Shein huenda akaja wekewe zengwe hilo hilo la uarabu na upemba siku ya siku itapowadia, japo anajulikana kwa uadilifu na uweza wake. Ni matarajio yangu kuchaguliwa kwa OBAMA kutatufungua vichwa vyetu, kuangalia uwezo wa mgombea MTANZANIA, bila kujali eti babu/baba/bibi/mama yake walizaliwa wapi!

Tuacheni ujinga wa ubaguzi na kubaguana, na wala huu sio UDAKU.
 
Huu ni ukweli. Nimetafakari sana kuhusu hili na kugundua kitu muhimu sana. Nchi zinazofuata mfumo wa "Presidential" kama Marekani, Naibu Rais/Makamu ana nguvu sana. Tatizo letu ni kuwa tumechanganya Parliamentary system na presidential. Katika mfumo huu, Rais anakuwa mtendaji na ana nguvu sana lakini Makamu wake anakuwa ni symbolic na pengine yuko kama reserve ili kusiwe na power vacuum in case akisafiri, kuugua au vinginevyo. Waziri Mkuu anabaki kuwa mtu wa jikoni zaidi maana ni msimamizi wa kazi za kila siku za serikali na ni kama kiranja wa mawaziri wote. Kwa sababu hiyo naona siyo haki kusema kuwa JK anampendelea Mizengo at the expense of Shein. Ukweli ni kuwa ukimwondoa Sumaye ambaye alikuw ayes man zaidi, mawaziri Wakuu karibu wote waliopita walikuwa powerful. Ukianza na Sokoine, Salim, Waryoba, Malecela na hata Lowassa.

Nakubaliana na mchango wako kwa ujumla lakini sidhani kama mheshimiwa Warioba alikuwa powerful.Nilianza kuona cheche za Warioba baada ya kutoswa kwenye uwaziri mkuu.
 
Back
Top Bottom