Dr.Riwa anastahili pongezi sana katika hili jukwaa

Dr Riwa pamoja na pongezi toka kwa ndg yetu kauk najumuika naye kukupongeza kwa kutokuwa mchoyo wa tiba. Vile vile nina shida kubwa ya fungus kwenye vidole vya miguu, nimejitahidi kutumia dawa nyingi na lotion pia lakini sipati nafuu ya kudumu. Hivi sasa naumwa miguu siwezi hata kuvaa viatu vidole vimevimba na vinatoa maji kwenye joints, naomba msaada wako Dr!!!!!!!!!! Naishi Arusha.

Japo thread hii haihusu Fungus lakini labda nikujibu tuu....

Fungus ni moja ya vimelea vigumu sana kutibu kwani upata usugu wa dawa haraka sana, hasa Fungus wa kati kati ya vidole vya miguuni (Athlete's foot). Fungus hawa hufaidika sana na hali ya maji maji/unyevu miguuni.

Vitu vinavyopelekea kuwa tabu kuwatibu:
1. Unyevu unyevu miguuni, hasa kama unavaa viatu vya kufunika...kijasho kitatoka kidogo miguuni na hivyo kufanya hali ya unyevu. Hata kama unatumia dawa hawatapona
- cha kufanya ni kuhakikisha miguu inakaushwa vizuri baada ya kunawa au kuoga, vaa viatu vya wazi..sandals au kandambili kwa muda mrefu, uvae viatu inapohitajika tuu. Ofcn ukifika basi toa viatu ushinde na ndala.

2. Dawa zenye steroid...dawa nyingi za Fungus huwa zinakuwa na steroids ndani yake, steroids husaidia kupunguza inflammation (kama reaction ya mwili kwa ile infection). Lakini ubaya wa steroid zikitumiwa kwa muda mrefu zinapunguza local immunity ya eneo hilo husika, na hiyo immunity inapopungua hapo Fungus ndio wanachanua zaidi
- cha kufanya ni kuacha kutumia Antifungal zenye steroids (zipo nyingi, ukienda pharmacy mwambie akupe antifungal lakini isiyo na steroids, wanaelewa). Na kama ukitumia yenye steroids basi tumia kwa muda mfupi tu

3. Hygienic measures...fungus huwa wanapenda mazingira machafu (miguu, soksi, viatu), lakini tricky part is, huwezi kuosha miguu yako mara kwa mara kwani hutaifanya iwe na unyevu.
- cha kufanya kuosha miguu kwa maji yenye antiseptic (dettol), usiloweke, osha tu...kisha ikaushe kwa taulo safi ikauke kabisa, kisha paka dawa. Fanya hivi mara mbili kwa siku. Hili taulo unalofutia miguu usilirudie bila kuliosha na maji yenye dettol na kuanika likakauka. Na vivyo hivyo kwa soksi, zifue kwa dettol, na usizirudie bila kufua. Usivae viatu vya kufunika bila soksi, na ukifanya hivyo usivirudie mpaka uvifue preferably kwa dettol na uvianike vikauke.

Pia unaweza tumia Antifungal za vidonge mara moja kwa wiki kwa wiki si chini ya sita kama bado watakuwa wanasumbua. Pole
 
Dokta RIWA hongera sana!kuna mambo nimeyaweka sawa kupitia ushauri wako muhimu kwa sisi wana JF Tusio na taaluma ya utabibu.Amini kwa Uwezo wake MWENYEZI Huwezi shuka hata kidogo.Pia nakuomba sana usije ukakasirika na kulisusa jukwaa hili kwa maneno ya kejeri kutoka kwa watu wasiojua lolote kuhusu matatizo ya wenzao.Nakumbuka kuna mtu walimkejeli kule kwenye jukwaa la Tekenolojia na akaamua kususa binafsi niliumia sana sababu michango yake ilikuwa muhimu sana.Kumbuka watanzania wengi ni masikini wa kipato.Ni rahisi kwangu kununua vocha ya 200 na kuingia JF kumwaga matatizo yangu kuliko kwenda hospitali na kutoa sh 10000.
Dokta Riwa si mchoyo,Kwa hilo nakusifia.
Usifwate mapoyoyo,Elimu kuibania.
Kwani wao ni wachoyo,Pesa wanahusudia.
Mungu akupe uhai,Uzidi tusaidia.
ASANTEN.
 
Dokta RIWA hongera sana!kuna mambo nimeyaweka sawa kupitia ushauri wako muhimu kwa sisi wana JF Tusio na taaluma ya utabibu.Amini kwa Uwezo wake MWENYEZI Huwezi shuka hata kidogo.Pia nakuomba sana usije ukakasirika na kulisusa jukwaa hili kwa maneno ya kejeri kutoka kwa watu wasiojua lolote kuhusu matatizo ya wenzao.Nakumbuka kuna mtu walimkejeli kule kwenye jukwaa la Tekenolojia na akaamua kususa binafsi niliumia sana sababu michango yake ilikuwa muhimu sana.Kumbuka watanzania wengi ni masikini wa kipato.Ni rahisi kwangu kununua vocha ya 200 na kuingia JF kumwaga matatizo yangu kuliko kwenda hospitali na kutoa sh 10000.
Dokta Riwa si mchoyo,Kwa hilo nakusifia.
Usifwate mapoyoyo,Elimu kuibania.
Kwani wao ni wachoyo,Pesa wanahusudia.
Mungu akupe uhai,Uzidi tusaidia.
ASANTEN..
 
Naunga mkono hoja! nakumbuka enzi zile kabla ujio wa Dr Riwa kulikuwa na madaktari wafuatao :- figganigga, aspirin, Uporoto, husninyo, wiselady, Lizzy ,Dena Amsi, n.k Dah! ilikuwa balaa! ilikuwa ukisema umefanya kijipu cha ufizi tu wanakuambia ukapime ukimwi, Halaf nakumbuka siku moja jamaa alikuja kusema anawashwa sana na mgongo madaktari wetu wakamuambia ana tubakulosis. Khaaa!

ubarikiwe Dr Riwa.
 
si afadhali walikuwa hawa-prescribe klorokwini manake ungewakomesha wagonjwa,lol
Naunga mkono hoja! nakumbuka enzi zile kabla ujio wa Dr Riwa kulikuwa na madaktari wafuatao :- figganigga, aspirin, Uporoto, husninyo, wiselady, Lizzy ,Dena Amsi, n.k Dah! ilikuwa balaa! ilikuwa ukisema umefanya kijipu cha ufizi tu wanakuambia ukapime ukimwi, Halaf nakumbuka siku moja jamaa alikuja kusema anawashwa sana na mgongo madaktari wetu wakamuambia ana tubakulosis. Khaaa! <br />
<br />
ubarikiwe Dr Riwa.
<br />
<br />
 
dr riwa,nami nichukue nafwasi hii kukupongeza na kukushukuru pia. mi naandaa hoja binafsi ya matatizo yangu,nikija nayo haa naomba unifanyie overhaul! hongera sana,kama ulisoma kwa mkopo wa loan board, tutaandika usikatwe kwenye mshahara for this charity work. let us know..kila la kheri dakta
 
si afadhali walikuwa hawa-prescribe klorokwini manake ungewakomesha wagonjwa,lol
<br />
<br />

heheh Dah! mimi ni daktari wa rufaa! hata huyu Dr Riwa akichemka basi nitakujulisheni, lakini mpaka sasa kijana anafanya vizuri sana! hongera Dr Riwa, halaf mimi nikimwaga CV langu hapa nazani kesho wagonjwa wote watatoroka muhimbili wajiunge JF. PAW na Cookie watasibitisha hii
 
mtumishi wetu, pamoja na majibu mazuri ya dr riwa, ambayo yatatusaidia wengi wenye tatizo hilo la fungus, naomba kutilia mkazo kwenye hygiene...
1- usirudie kuvaa viatu pia mfululizo. hakikisha una minimum ya pair 2 ili zipate muda walau wa siku moja kupumzika,kupumua na kukauka. ukipata viatu vya ngozi tupu ni vizuri zaidi kwani vinanyonya unyevu. unapovua viatu hakikisha hutumbukizi soksi ndani. weka soksi pembeni ikiwezekana zitundike.
2- kuna powder imeandikwa mycoderm C clotrimazole dusting powder w/w. ni nzuri kwa kunyunyizia kwenye viatu na miguu pia. dr riwa atanisaidia kama inaleta usugu manake mie naiweka kwenye viatu kuzuia any odor na kuweka miguu mikavu.
3- my mom's concotion: loweka miguu kwenye maji ya uvuguvugu yenye chumvi kabla ya kunawa na hiyo dettol. mostly usiku. chumvi ni anti-septic pia na inapunguza muwasho. manake fungus zikichachamaa unaweza ukaajir mtu wa kuzikuna,lol
pole sana, ukipambana na usafi na dawa pia hizo fungus zitaisha. ikishindikana peleka sadaka kwa rev masanilo kwa ajili ya maombi..
 
hehehe! ww ushashindwa kazi banaa. siku hizi mambo yote miseto! kwanza ulikuwa mchungu kama unakomeshea aisee! wagonjwa wengine tunaugua vichaa hapa, shaurilo!
heheh Dah! mimi ni daktari wa rufaa! hata huyu Dr Riwa akichemka basi nitakujulisheni, lakini mpaka sasa kijana anafanya vizuri sana! hongera Dr Riwa, halaf mimi nikimwaga CV langu hapa nazani kesho wagonjwa wote watatoroka muhimbili wajiunge JF. PAW na Cookie watasibitisha hii
<br />
<br />
 
hehehe! ww ushashindwa kazi banaa. siku hizi mambo yote miseto! kwanza ulikuwa mchungu kama unakomeshea aisee! wagonjwa wengine tunaugua vichaa hapa, shaurilo!
<br />
<br />

huku ninakoishi kichaa si marazi kichaa ni moja katika hobbies mashuhuri.
 
sikujua unaishi mirembe. ntakuja hukohuko tumalizane, tusichakachue uzi wa dr,lol
dr riwa, nasubiri order yako tuanzishe petisheni against makato yako ya mkopo eh..
huku ninakoishi kichaa si marazi kichaa ni moja katika hobbies mashuhuri.
<br />
<br />
 
Ahsante dada'angu King'asti,

Bahati nzuri sikuingia mkataba na HELSB (sijui bado wanaitwa hivyo!), wakati ule bado Medicine tulikuwa hatukopeshwi..hivyo sina deni na tume! Klorokwini...salut!
 
nakupongeza sana DR RIWA kwa msaada wa ushauri unaoutoa hapa JF ,MUNGU AKUZIDISHIE UZIMA NA AFYA NJEMA, KILA JAMBO JEMA LIWE SEHEMU YA PUMZI YAKO.
 
Dr. Riwa pamoja na pongezi zote hapo juu kutoka kwa mabrodaaaaaaaaz and sistaaaaaaaaaz napenda kuongezea kwa kukushukuru kwa mchango wako mkuu doctor..pia si vibaya kama itawezekana kukupa ka verse kidogo hii ndio zawadi yangu kwako dr...

iyoo ayoo ooh yoyo iyoo ayooo x2 Dr. Riwa iyoo ayooo oyoyo iyoo ayooo x2 Dr. Riwa. this is my dedication to you usikilize huu wimbo ukiwa na moja baridiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii sana...

thanks have a nice day...dr.
 
Dr. Riwa pamoja na pongezi zote hapo juu kutoka kwa mabrodaaaaaaaaz and sistaaaaaaaaaz napenda kuongezea kwa kukushukuru kwa mchango wako mkuu doctor..pia si vibaya kama itawezekana kukupa ka verse kidogo hii ndio zawadi yangu kwako dr...

iyoo ayoo ooh yoyo iyoo ayooo x2 Dr. Riwa iyoo ayooo oyoyo iyoo ayooo x2 Dr. Riwa. this is my dedication to you usikilize huu wimbo ukiwa na moja baridiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii sana...

thanks have a nice day...dr.

tusiwe wepesi wa kusahau....moja baridi ni sumu mwilini. karibu migonjwa mikubwa mikubwa yote inasababishwa na pombe na sigara. dr. kula mbege na si bia bwasheee
 
Wandugu,

Nashukuru sana...tena sana kwa kuona na kuthamini mchango wangu hapa JF sana katika jukwaa hili la JF Doctor. Ahsanteni pia kwa dua, Husninyo ahsante 'free style'! Najitahidi kila pale ninapoweza kuchangia na/au kushea nanyi elimu hii ya utabibu na afya nikiamini kuwa kuna matatizo mengi ambayo hata wengine hawawezi kuongea na daktari wake, lakini anayamwaga hapa na tunajadili. Najua jukwaa hili lina madaktari wengine, manesi na wadau wengine mbali mbali wa afya ambao wana michango mizuuri tu, nami mara kwa mara najifunza kwao na kwa wachangiaji wengine pia! kwa kifupi ni jukwaa nilipendalo...

Nilifanya kazi kama daktari kwa miaka kadhaa Muhimbili, nikapata matatizo na mwajiri wangu (Wizara ya Afya), nikawa frustrated sana na kupractice clinical medicine, nikahamia kwenye utafiti wa masuala mbali mbali ya afya. Nimejikita zaidi kwenye 'afya ya jamii' kwa sasa, sitibu tena...hivyo sina hospitali ninayofanya kazi kwa sasa.

Lakini mara zote unapohitajika ushauri/ufafanuzi ambao upo ndani ya uwezo wangu, au issue ambayo naweza soma zaidi ili kuweza kushea nanyi nijuacho, basi karibuni kwa kuanzisha thread hapa jukwaani...au hata kwa PM...ni furaha yangu pale ninapoweza kusaidia.


nathamini sana mchango wako... madactri wengine wamekimbia hili jukwaa na umebaki peke yako, MZIZIMKAVU, NJIWA na wengine ... rudini humu wana JF bado wanawahitaji.

kuna tiba flani nilipata toka katika thread ya mzizimkavu ilinisaidia sana aisee..

long live JF doctor
 
Back
Top Bottom