Dr. Pombe Magufuli kuvunja Ukuta Wa Mwinyi, Waziri wa Zamani Kenja na Benki ICS

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Ukisikia kufuata sheria imefikia pazuri, ambapo wale wote waliojenga bila vibali au kuingilia hifadhi za barabara wote watuvunjiwa. Sheria hii imempitia Rais wetu mstaafu Mzee "Ruksa" pale kwake msasani, tayari vipimo vinavyoonyesha mita 33 na mstari mwekundu vimewekwa kwenye ukuta wake, sikuweza kupiga picha kwa sababu za usalama wangu na ka mkebe kangu.

Vunja vunja na Bomoa bomoa zimekumba sehemu kubwa ya Old Bagamoyo, hadi nakuja mitamboni, nimeona nyumba nyingi zenye kuta zilizotiwa nakshi nakshi zikiwekwa alama ya hatari.

Hata hivyo sijajua wanapanua barabara au wanatekeleza amri ya kuhifadhi barabara, vivyo hivyo bara bara ya Ali Hassani Mwinyi AKA New Bagamoyo Road, huko ndiko utamkuta Kenja pale Victoria katulia akisubiri kijiko kifanye vituko, hipo pia shule ya aliyekuwa meya wa jiji mzee wa Green Acre , naye kukumbwa zoezi hili, ingawaje yeye bado ana kagorofa kake pale kalikowekewa alama zikafutwa ingawaje jirani yake anayepakana na UWT, kashavunjiwa na kurudi kinyume nyume.

Source ya Habari Nimeona Mwenyewe na Nishawahi kuona miaka ya nyuma na nafahamu vipimo vya barabara . msije kuniuliza sana.
 
Kwa Keenja pale victoria ni nyumba ya NHC.
Labda kama kauziwa! Nothing is impossible in this country.
 
Tatizo letu lingine ni 'ulemavu' wetu kama heading ya uzi inavyosema. Tafadhali ungelekebisha hapo, anayebomoa sio Magufuli bali ni sheria/serikali.

Hili kosa pia limefanyika hata kwenye 'samaki wa Magufuli', watu miaka yote wanaiba rasilimali za nchi na kuvunja sheria na viongozi wabovu wako tu wamekaa. Akija mtu anayeweza kutekeleza majukumu yake mnadhani anafanya kwa ajili yake kumbe ni kwa ajili yangu mimi na wewe. Kwa nini usiseme "
"Dr. JK kuvunja Ukuta Wa Mwinyi, Waziri wa Zamani Kenja na Benki ICS"???


Tukitaka kuwa kama Zambia/Senegal nk hatuna budi kubadilisha akili zetu kwanza kabla ya kuwalalamikia viongozi
 
Avunje aanzie wapi? We subiri tu waliopaka rangi wameweka geresha tu,ila mwinyi pale ana kama heka mbili hv daaa si mchezo!!
 
Tatizo letu lingine ni 'ulemavu' wetu kama heading ya uzi inavyosema. Tafadhali ungelekebisha hapo, anayebomoa sio Magufuli bali ni sheria/serikali.

Hili kosa pia limefanyika hata kwenye 'samaki wa Magufuli', watu miaka yote wanaiba rasilimali za nchi na kuvunja sheria na viongozi wabovu wako tu wamekaa. Akija mtu anayeweza kutekeleza majukumu yake mnadhani anafanya kwa ajili yake kumbe ni kwa ajili yangu mimi na wewe. Kwa nini usiseme "
"Dr. JK kuvunja Ukuta Wa Mwinyi, Waziri wa Zamani Kenja na Benki ICS"???


Tukitaka kuwa kama Zambia/Senegal nk hatuna budi kubadilisha akili zetu kwanza kabla ya kuwalalamikia viongozi


Ahsante sana kwa kunifundisha kuandika kichwa cha Habari, lakini kumbuka wakati wa utekelezaji wa jambo fulani, mhusika hutajwa hili kuwepo msisitizo, au wa kumuongezea nguvu zaidi au kumpongeza kwa juhudi zake, hivyo yeye kuonekana kuwa anafuata sana sheria, bila kujari ukuu wa mtu yeyote au cheo chochote. Hivyo mimi nimemsifu sana, hila nina hofu ya utekelezaji maana hospitali ya TMJ nayo inaonekana kuwa ndani ya hifadhi lakini zoezi hili bado, wakati majirani zake tayari kuna alama. Yasije yakawa kama yaleeee ya kiwanja cha ROSE GARDEN na TTCL Kijitonyama vilivyomletea msuko suko hadi kung'olewa na kupelekwa kwenye Ardhi
 
Nadhan Hapo kwa Mheshimiwa Mzee Mwinyi ndio wa kwanza aliyeharibu plan za hii old Bagamoyo road!! Na alichukua eneo la Hifadhi ya barabara wazi wazi!! Ila Namshauri Mzee mwinyi ili kuruhusu Utawala wa sheria uchukue Mkondo wake yeye mwenyewe avunje ukuta!! Ila najua utajengwa mwingine Haraka na wengine nao waweze Kuiga Mfano Huo!!! Kwani adha ya foleni barabara hii Inatisha!!
 
Nadhan Hapo kwa Mheshimiwa Mzee Mwinyi ndio wa kwanza aliyeharibu plan za hii old Bagamoyo road!! Na alichukua eneo la Hifadhi ya barabara wazi wazi!! Ila Namshauri Mzee mwinyi ili kuruhusu Utawala wa sheria uchukue Mkondo wake yeye mwenyewe avunje ukuta!! Ila najua utajengwa mwingine Haraka na wengine nao waweze Kuiga Mfano Huo!!! Kwani adha ya foleni barabara hii Inatisha!!
ni kweli mkuu, nakumbuka magazeti ya nyakati hizo moja liliwahi kuchapisha kimemo kikiwaelekeza waliokuwa wanajenga hiyo barabara kuisogeza mbali na makao yake.

Na matokeo ya uvunjaji huu wa sheria ulichochea watu wengi kuvamia maeneo mengi ya barabara na viwanja vya wazi. Ni bora haya mambo yaibuke sasa ili baadhi ya watu walioanzisha 'mchakato wa uvunjaji seria' walau tuwajue!

 
Yale yale ya CHENJI YA RADA! Waliojenga kwenye HIFADHI ya barabara kuvunjiwa FINE.

JE wale waliotoa vibari vya kujenga kwenye hifadhi ya barabara wamechuliwa hatua gani?

Usinieleze upambavu kwamba Mzee Mwinyi, Green Acre etc zilijengwa bila vibari vya mamlaka husika.
Hii ndiyo double standard ya sheria zetu, SIO MSUMENO haukati huku na kule!
 
mavi yake ajaribu aone kama atujamlewesha kama alivyookolewa na ma polisi mjinga huyo
nilijua unamjua vizuri na porojo zake mpwa kumbe wale wale
 
Back
Top Bottom