johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,591
- 141,393
Kwa wale Wahenga mnaokumbuka vizuri ni sababu gani za msingi zilimfanya Daktari huyu wa Falsafa kuamua kujishusha cheo?
Maendeleo hayana vyama!
cc: Pohamba
====
Ana rekodi ya miaka 10 ya kufundisha na miaka 25 ya kutumikia serikali. Katika miaka hii 25, amekuwa mkuu wa mkoa, balozi, na waziri. Aidha, amekuwa mbunge wa jimbo la Maswa, mkoani Shinyanga tangu 1980 hadi 2005 alipoamua kuacha uwakilishi.
Dk. Ng'wandu anaharakisha kukueleza mambo mawili makubwa katika maisha yake yote ya utumishi. Kwanza, utumishi wa umma ni uadilifu na utii. Pili, mtumishi wa umma lazima aamue kuachia ofisi akingali na nguvu na wakati anaowatumikia bado wanampenda.
Mwalimu huyu anaamini kwamba siasa siyo njia pekee ya mtu kuishi. Kutumikia watu kupo kwa namna nyingi; si siasa peke yake.
Dk. Ng'wandu alipata shahada ya kwanza ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki (Dar es Salaam).
Alipata Shahada ya Uzamili katika Sosholojia mwaka 1973 kutoka Chuo Kikuu cha Alberta, Canada na baadaye Shahada ya Uzamivu (Ph.D) katika Elimu kwenye Chuo Kikuu cha Stanford, Marekani.
Akiwa mbunge, Dk. Ng'wandu aliamua kusomea sheria na kufaulu kujinyakulia shahada ya Uzamili ya Sheria (LLM) kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT).
Dk. Ng'wandu, alizaliwa 15 Julai 1943 katika kijiji cha Budekwa wilayani Maswa. Alisoma Shule ya Msingi ya Bura wilayani humo na baadaye Seminari ya Nyegezi, nje ya jiji la Mwanza kabla ya kujiunga na Chuo cha Ualimu, Morogoro ambako alirudi kufundisha.
Pamoja na shule nyingine, alifundisha sekondari ya Tosamaganga, Chuo cha Ualimu Kleruu, Iringa; Mwalimu Mkuu Sekondari ya Mpwapwa, Dodoma, Mkuu wa Chuo cha Ualimu Butimba, Mwanza na kiongozi wa elimu wizarani kwa miaka kadhaa hadi kufikia kuwa Mkurugenzi wa Elimu ya Juu.
Maendeleo hayana vyama!
cc: Pohamba
====
Ana rekodi ya miaka 10 ya kufundisha na miaka 25 ya kutumikia serikali. Katika miaka hii 25, amekuwa mkuu wa mkoa, balozi, na waziri. Aidha, amekuwa mbunge wa jimbo la Maswa, mkoani Shinyanga tangu 1980 hadi 2005 alipoamua kuacha uwakilishi.
Dk. Ng'wandu anaharakisha kukueleza mambo mawili makubwa katika maisha yake yote ya utumishi. Kwanza, utumishi wa umma ni uadilifu na utii. Pili, mtumishi wa umma lazima aamue kuachia ofisi akingali na nguvu na wakati anaowatumikia bado wanampenda.
Mwalimu huyu anaamini kwamba siasa siyo njia pekee ya mtu kuishi. Kutumikia watu kupo kwa namna nyingi; si siasa peke yake.
Dk. Ng'wandu alipata shahada ya kwanza ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki (Dar es Salaam).
Alipata Shahada ya Uzamili katika Sosholojia mwaka 1973 kutoka Chuo Kikuu cha Alberta, Canada na baadaye Shahada ya Uzamivu (Ph.D) katika Elimu kwenye Chuo Kikuu cha Stanford, Marekani.
Akiwa mbunge, Dk. Ng'wandu aliamua kusomea sheria na kufaulu kujinyakulia shahada ya Uzamili ya Sheria (LLM) kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT).
Dk. Ng'wandu, alizaliwa 15 Julai 1943 katika kijiji cha Budekwa wilayani Maswa. Alisoma Shule ya Msingi ya Bura wilayani humo na baadaye Seminari ya Nyegezi, nje ya jiji la Mwanza kabla ya kujiunga na Chuo cha Ualimu, Morogoro ambako alirudi kufundisha.
Pamoja na shule nyingine, alifundisha sekondari ya Tosamaganga, Chuo cha Ualimu Kleruu, Iringa; Mwalimu Mkuu Sekondari ya Mpwapwa, Dodoma, Mkuu wa Chuo cha Ualimu Butimba, Mwanza na kiongozi wa elimu wizarani kwa miaka kadhaa hadi kufikia kuwa Mkurugenzi wa Elimu ya Juu.