Behaviourist
JF-Expert Member
- Apr 8, 2016
- 39,901
- 95,404
Huyu jamaa nimefuatilia taarifa zake wanadai ana fedha na ana vitalu vya uwindaji, kuwa na fedha kumembeba kufika hapa alipo.
Wanaomfahamu wanadai kati ya 2010 kwenda 2015 aligawa sana fedha za Rushwa kuupata ubunge , aliwanunulia vijana magari ya kushawishi watu wamchague. Ni rafiki yake nyarandu na walicheza Sana na fursa nyarandu akiwa maliasili.
Pamoja na kuwa fedha nyingi wapiga kura wake wanadai hana alichowahi kufanya tofauti na kujenga kituo kimoja Cha polisi. Sasa ni wakati wa yeye kutoa pesa kwenye miradi ya wananchi la sivyo akienda kwenye sanduku la kura ataanguka maana hadi anapata ubunge hakupigiwa kura
Hamna uchaguz uliofanyika mkuu, 2015 nassar alimshinda kwa 85%Hii ni Tanzania huyo kapigiwa kura nyingi tuu
Tuna Kundi kubwa la Wasomi wa Nadharia na sio wa Vitendo Mkuu.Ni tatizo la watu kupewa madaraka au nafasi kwa kuzingatia umri au kiasi chake Cha fedha. Msomi wa PHD kushindwa kutofautisha kutoa hotuba na kuuliza swali ni jambo la kushangaza. Nimesikiliza clip, inaonekana hata issue ya kutumza muda,kutumia mic hajui. Lakini mwishoni anasikika akimtaka waziri/Naibu waziri waongozane kwenda jimboni mwake
Kauli ya tuongozane ni ya kukariri, Ni kauli pendwa ya wabunge wengi lakini mnaongozana kufanya nini wakati hata swali tu umeshindwa kumuuliza Waziri?
CCM washinikizeni wabunge wenu kusoma na kujielimisha, wamerelax Sana kwa sababu angekuwa mpinzani lazima angekesha kusoma kanuni na taratibu zote bila kujali ngazi ya elimu yake
Huyu DR. Hawezi kusoma files yawezekana amezoea kuelekeza watu wafanye kama anataasisi anayoingoza au alikuwa mtumishi wa umma
Mh rais ? HahahahahahaMimi nadhani mnamuonea huyo mbunge, wakati alichokifanya ndio uwezo wake! Ebu wote tujiulize mbunge hakupiga kampeni na kukutana na wapiga kura na kujua kero zao, mlitaka aulize swali gani? achilia mbali kuzijua kanuni siyo issue sana ila angeuliza maswali gani wakati katokea nyumbani kwake moja kwa moja kwenda bungeni? Inawezekanaje mbunge kabisa yupo ndani ya ukumbi wa bunge na anamuona spika mbele yake anamuita mh rais? soo sad.