Dr. Mwinyi "Zanzibar haiwezei kujiunga IOC"

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Mapema leo Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Raia anayeshughulikia masuala ya Muungano Dr. Hussein Mwinyi amesema kuwa Zanzibar haiwezi kujiunga na vyombo vya kimataifa ambavyo vinahitaji nchi yenye dola iwe mwanachama. Amesema kwa vile Zanzibar siyo dola (sovereign) basi haiwezi kujiunga na chombo kama IOC na zaidi ya yote alihofia mgongano wa Kikatiba. Kwa namna fulani inaonekana yeye na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje ambaye ndiye msemaji kwenye masuala ya kimataifa wanatakiwa kuwekwa kwenye chumba kimoja ili wawasiliane!!
 
Mapema leo Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Raia anayeshughulikia masuala ya Muungano Dr. Hussein Mwinyi amesema kuwa Zanzibar haiwezi kujiunga na vyombo vya kimataifa ambavyo vinahitaji nchi yenye dola iwe mwanachama. Amesema kwa vile Zanzibar siyo dola (sovereign) basi haiwezi kujiunga na chombo kama IOC na zaidi ya yote alihofia mgongano wa Kikatiba. Kwa namna fulani inaonekana yeye na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje ambaye ndiye msemaji kwenye masuala ya kimataifa wanatakiwa kuwekwa kwenye chumba kimoja ili wawasiliane!!

Kuwaweka pamoja itakuwa kazi kweli ukichukulia kuwa Vasco da gama sasa hivi yuko kwenye uvumbuzi wa dunia!

Hii sio serikali bali ni laana! laana tena kubwa tu na Tanzania na watanzania wake wameacha katikati wasijui wafuate lipi.
 
yaani huwa nashangaa hivi hakuna mawasiliano kati ya mawaziri, wizara, na maofisi? Rais anasema kapokea majina vigogo wa madawa; waziri Mkuu anasema mbona vigogo wa madawa hawatajwi? what on earth is going on?
 
yaani huwa nashangaa hivi hakuna mawasiliano kati ya mawaziri, wizara, na maofisi? Rais anasema kapokea majina vigogo wa madawa; waziri Mkuu anasema mbona vigogo wa madawa hawatajwi? what on earth is going on?

Mkuu Mwenzangu,

I must agree na wewe on this one, yaani mara Marmo anashugulikia ishu za Palestina, sasa Dr. Mwinyi anashughulikia ishu za Zanzibar na IOC, oooh no! Where does this nonesense stops?

Yaani kila kiongozi anajaribu kujiweka sawa ili aje agombee urais, jamani viongozi wetu huu ujiko wa kisiasa unawafikisheni mbali sasa, I mean who is in the contrl over hawa leaders wetu?

Damn!
 
Niliuliza hapa wakati fulani hivi kwenye vikao vya baraza la mawaziri huwa wanaongelea vitu gani? Maana yake kuna mambo huwa yanatokea hata huelewi inakuwaje.

Je, baraza la mawaziri huwa wanakutana mara ngapi kwa mwezi au mwaka?
 
Ukiona mawaziri kila mtu anakuja na tamko la kwake, basi elewa kwamba kuna mgongano wa kazi au watu hawajui mipaka ya kazi zao. Hii inatokana na kuwa na baraza kubwa sana la mawaziri kiasi kwamba kuna baadhi ya wizara zinaingiliana (overlap) katika utendaji wa kazi. Leo hii ukimuuliza Dr Mwinyi yeye kama waziri anayeshughulikia maswala ya Muungano atakuambia kwamba swala la OIC liko chini yake na Bwana Membe nae atasema liko chini yake. Sasa kama siyo wastage of resources ni nini? Mfano hauko kwenye hizo wizara tu bali kuna wizara nyingi tu ambazo mambo yake yanaingiliana sana. Mipaka ya wizara ya Usalama wa Raia na Mambo ya Ndani ni nini? Hii ni msg kwa JK kwamba muundo wake wa Baraza la Mawaziri na wizara zake zina mgogoro na ndiyo maana kuna baadhi ya mawaziri hawajui mipaka yao ya kazi au majukumu yanagongana na wizara nyingine.
 
Ukiona mawaziri kila mtu anakuja na tamko la kwake, basi elewa kwamba kuna mgongano wa kazi au watu hawajui mipaka ya kazi zao.

Amina maneno mazito haya mkuu!
 
Niliuliza hapa wakati fulani hivi kwenye vikao vya baraza la mawaziri huwa wanaongelea vitu gani? Maana yake kuna mambo huwa yanatokea hata huelewi inakuwaje.

Je, baraza la mawaziri huwa wanakutana mara ngapi kwa mwezi au mwaka?

Baraza la Mawaziri hukutana kila wiki, in the past it used to be Thursday (I think). Probably the meet every Tuesday.
 
Baraza la Mawaziri hukutana kila wiki, in the past it used to be Thursday (I think). Probably the meet every Tuesday.

Kama ni hivyo kwa nini hawamalizi mijadala yao huko na kuwapa wananchi kile walichoamua na kuacha pumba ambazo kila mara zinatoka. Rejea Magufuli alipomwambia rais kule Mtwara kuhusu kodi (msamaha)bali waende TIC; Swala la Zanzibar kujiunga IOC n.k.
 
Kama ni hivyo kwa nini hawamalizi mijadala yao huko na kuwapa wananchi kile walichoamua na kuacha pumba ambazo kila mara zinatoka. Rejea Magufuli alipomwambia rais kule Mtwara kuhusu kodi (msamaha)bali waende TIC; Swala la Zanzibar kujiunga IOC n.k.

Inawezekana huwa hawa-discuss hayo mambo kwenye vikao vya Baraza la Mawaziri. Kama wangekuwa wana-discuss lazima wote wangekuwa wanakuja na tamko linalofanana na siyo kila mtu anaibuka na tamko lake. Swali la msingi ni kwamba, kama huwa hawa-discuss haya mambo, je huwa wanaongelea maswala gani na kama hawajaongelea kwanini mtu ajifanye mwepesi wa kutoa tamko kabla ya kujadiliana kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri? OIC ni swala zito sana na linaweza kuyumbisha Muungano kwa hiyo nilitarajia kwamba watu wangeliongelea kwa umakini mkubwa sana na pia baada ya kupata baraka za kikao cha Baraza la Mawaziri.

Msg hapo ni kwamba may be huwa wanapiga porojo kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri na ndiyo maana tunaona hizi pumba. Au inawezekana kila mtu anajiona ni msemaji wa swala fulani hata bila ya baraka za Baraza la Mawaziri na matokeo tunapata version zaidi ya moja on same thing! Wapunguze ushikaji kwenye vikao na hata uteuzi wa baraza la mawaziri.
 
Kama ni hivyo kwa nini hawamalizi mijadala yao huko na kuwapa wananchi kile walichoamua na kuacha pumba ambazo kila mara zinatoka.

Ukweli ni kwamba kutokana na kauli zinazogongana, ina maana kuwa wanapokutana huwa hakuna protocol, kati ya hawa mawaziri kuna wanaojona kuwa wako karibu sana na rais, kuna wanajiona kuwa wamepewa uwaziri kutokana na uwezo wao mkubwa kikazi, na kuna wanaojiona kuwa ni haki yao kuwa mawaziri, na kuna wanyonge ambao ni mungu nisaidie, katika huu mchanganyano protocol huwa zinawekwa pembeni, ikiwa na maana kwamba nani ni makamu wa rais, nani waziri mkuu, nani waziri senior huwa hakuna mpangilio,

Ukiziangalai kwa makini hizi kauli zao zina maana moja tu, kwamba kabla ya kuzisema waliongea na mkubwa mmoja mzito sana, naye lazima awe ni rais tu, haiwezekani wazriri akatimka tu kauli nzito nzito tu za kuwakilisha taifa, hata kama sio kwenye sekta yake, kwenye hili wale wa upande wa pili wana point, serikali ianze kufuata protocol, na mipangilio ya kazi za mawaziri, unless ni wengi mno na responsibilities hazijulikani mipaka yake,

Sasa katibu wa mawaziri na waziri mkuu, pamoja na makamu wanafanya nini? Mbona ndani ya CCM ambako ukifanya kosa hata liwe dogo utakuja kuwajibika nalo huwa hawafanyi hayo makosa ya kuchanganyana wadhifa na shughuli?
 
Ukiona mawaziri kila mtu anakuja na tamko la kwake, basi elewa kwamba kuna mgongano wa kazi au watu hawajui mipaka ya kazi zao.

Naam maana juzi nimemuona mgonjwammoja wa akili pale Kilimo alipokuwa anaweweseka baada ya kutolewa kwa tathmini ya REDET "Wassira anadhani bado yuko enzi za chama kimoja,hajui hata namna ya kukabiliana kisiasa na reporters!! Ni aibu aibu sana kwa mzee Tyson kukurupuka na kuhoji uhalali wa kura ya maoni hiyo ya REDET na kuendelea kushutumu baadala ya ku face ukweli kwa hekima kama alivyojibu Capt Chiligati na wenziwe akina Kingunge jana akiongozwa na Mtaalam Salva.

Nirudi tu pale kuwa wenzetu hawa sasa wanatuthibitishia kuwa hawajui wanachokifanya aidha kwa makusudi au ni ulevi tu wa madaraka.

Dkt Mwinyi huenda akawa yumo ktk harakti takatifu za kisiasa lakini ni wazi na dhahiri kwa majibu hayo nahisi anaingia ktk mtego wa wajanja wanaojiweka sawa ktk kusaka mamlaka za kisiasa na dola huko mbeleni.
Alamsiki
Kila la heri
 
Naamini Zanzibar waliungana hiyo 1964 kwa nia njema kabsaa, na kuhakikisha kuwa Zanzibar inasimama kama nchi forever, mambo yamebadilishwa na wao wapohapohapo wanapiga makofi then wanamwaga wino, just wanajali matumbo yao, sasa kitanzi kinakaba wanalalama! Ebwanae kusudi haiambiwi pole.
 
Back
Top Bottom