Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,304
- 12,965
Mh. Dr. Mwakyembe amekanusha kuhusika kumchafua Lowassa katika mbio za kugombea urais. Katika maelezo yake amesema kazi ya kuchunguza kashfa ya Richmond walitenda haki na kwa uadilifu mkubwa.
Lakini wakati alipowasilisha ripoti bungeni na wakati mjadala umepamba moto wakidaiwa kutokutenda haki katika kazi yao ya kuchunguza, alisimama akasema kama watu hawaridhiki waombe kanuni zitenguliwe ili awasilishe upya ripoti yao ili aseme na siri waliyoificha ili kuiokoa serikali isiporomoke yote.
Sasa wakati akisisitiza kuwa walitenda haki wakati alisema kuwa kuna siri waliificha inakuwa vigumu kumuelewa huo uadilifu anaousema. Mimi namshauri Dr. Mwakyembe sasa aitoe hadharani ile siri waliyoificha kuepusha serikali kuporomoka yote na hivyo kupelekea serikali kuporomoka nusu kwa kujiuzulu kwa Mh. Lowassa.
Kwa sasa hakuna cha kupoteza Dr. kwasababu serikali iliyopo inaenda kuporomoka yenyewe kwa mujibu wa katiba hapo ifikapo mwezi Octoba. Hivyo wewe huna cha kupoteza na wala serikali iliyopo itakuwa haina cha kupoteza kwasababu uhai wake unaishia ukingoni. Bila kuisema hiyo siri uliyosema mliificha, suala la Richmond litabaki kuwa tata hadi ukamilifu wa dahari.
Tuliwagharimia kwa mamilioni mzunguke duniani kwenda kuutafuata ukweli. Nanyi mkafanya kazi yenu vizuri na kuupata ukweli wote. Mliporudi badala ya kutupa ukweli tuliowatuma, mkatupa ukweli nusu. Ukweli usiposemwa wote huo huwa hauwi ukweli kamili, na kwakuwa unakuwa haujasemwa wote, ndani ya huo ukweli nusu unaosemwa huwa kunakuwa kumechanganyika na uongo na uongo ukichukua nafasi kubwa maana nzima ya ukweli hupotea.
Hivyo ndivyo mlivyoipoteza maana nzima ya ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya Richmond kwani ukweli mkuu haukusemwa. Hiyo ilikuwa ni sawa na kumpa mgonjwa nusu dozi matokeo yake maradhi huwa sugu. Maradhi sugu tuliyoyapata ni kuzaliwa kwa ESCROW ambayo nayo haina tofauti sana na EPA na RADA. Ukiangalia maradhi yote hayo ni kutokana na kutotoa ukweli kamili.
Hivyo kama nawe ni mmoja wa watangaza nia, msalaba wako mkubwa itakuwa ni kuusema ukweli kwani ukweli humuweka mtu huru naye huwa huru kweli kweli. kwakuwa mpaka sasa unajaribu kujitetea bila kusema ukweli, itakuwa vigumu kwa watu wenye akili timamu kukuamini kwa lolote sana sana utaonekana ni mtu uliyetayari kuificha kweli kwa tamaa ya vyeo vipitavyo.
Ni dhahiri katika kuuficha huo UKWELI mtakuwa mliwaumiza watu wengine ambao hawakupaswa kuumia na kudharilika. Mlichokifanya kilikuwa sawa na kukivunja kichwa kwa kosa lililofanywa na ulimi - Ulimi uliponza kichwa, kichwa kikavunjwa bila sababu "NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO!"
Lakini wakati alipowasilisha ripoti bungeni na wakati mjadala umepamba moto wakidaiwa kutokutenda haki katika kazi yao ya kuchunguza, alisimama akasema kama watu hawaridhiki waombe kanuni zitenguliwe ili awasilishe upya ripoti yao ili aseme na siri waliyoificha ili kuiokoa serikali isiporomoke yote.
Sasa wakati akisisitiza kuwa walitenda haki wakati alisema kuwa kuna siri waliificha inakuwa vigumu kumuelewa huo uadilifu anaousema. Mimi namshauri Dr. Mwakyembe sasa aitoe hadharani ile siri waliyoificha kuepusha serikali kuporomoka yote na hivyo kupelekea serikali kuporomoka nusu kwa kujiuzulu kwa Mh. Lowassa.
Kwa sasa hakuna cha kupoteza Dr. kwasababu serikali iliyopo inaenda kuporomoka yenyewe kwa mujibu wa katiba hapo ifikapo mwezi Octoba. Hivyo wewe huna cha kupoteza na wala serikali iliyopo itakuwa haina cha kupoteza kwasababu uhai wake unaishia ukingoni. Bila kuisema hiyo siri uliyosema mliificha, suala la Richmond litabaki kuwa tata hadi ukamilifu wa dahari.
Tuliwagharimia kwa mamilioni mzunguke duniani kwenda kuutafuata ukweli. Nanyi mkafanya kazi yenu vizuri na kuupata ukweli wote. Mliporudi badala ya kutupa ukweli tuliowatuma, mkatupa ukweli nusu. Ukweli usiposemwa wote huo huwa hauwi ukweli kamili, na kwakuwa unakuwa haujasemwa wote, ndani ya huo ukweli nusu unaosemwa huwa kunakuwa kumechanganyika na uongo na uongo ukichukua nafasi kubwa maana nzima ya ukweli hupotea.
Hivyo ndivyo mlivyoipoteza maana nzima ya ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya Richmond kwani ukweli mkuu haukusemwa. Hiyo ilikuwa ni sawa na kumpa mgonjwa nusu dozi matokeo yake maradhi huwa sugu. Maradhi sugu tuliyoyapata ni kuzaliwa kwa ESCROW ambayo nayo haina tofauti sana na EPA na RADA. Ukiangalia maradhi yote hayo ni kutokana na kutotoa ukweli kamili.
Hivyo kama nawe ni mmoja wa watangaza nia, msalaba wako mkubwa itakuwa ni kuusema ukweli kwani ukweli humuweka mtu huru naye huwa huru kweli kweli. kwakuwa mpaka sasa unajaribu kujitetea bila kusema ukweli, itakuwa vigumu kwa watu wenye akili timamu kukuamini kwa lolote sana sana utaonekana ni mtu uliyetayari kuificha kweli kwa tamaa ya vyeo vipitavyo.
Ni dhahiri katika kuuficha huo UKWELI mtakuwa mliwaumiza watu wengine ambao hawakupaswa kuumia na kudharilika. Mlichokifanya kilikuwa sawa na kukivunja kichwa kwa kosa lililofanywa na ulimi - Ulimi uliponza kichwa, kichwa kikavunjwa bila sababu "NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO!"