Dr. Mwakyembe on KLH News

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Kesho nina interview kubwa mbili, lakini kutokana na ukata nalazimika kuchagua moja. Kuna ya Prof. Njozi kuhusu ujio wa Rais Bush, na kuna Dr. Harrison Mwakyembe kuhusu Kamati yake na yale yaliyojiri Bungeni. Naomba mnichagulie ipi tuifanye ili nimuombe mmoja wao kuahirisha.
 
Mkuu Mwenzangu MMJ,

Heshima mbele, hilo sidhani kama lina ubishi Mwakyembe kwanza, mlete the man, na shujaaa wa taifa Mwakyembe ili tukate naye mzizi wa fitina,

Mkuu itakuwa saa ngapi tujiweke sawa mkuu?
 
Kesho nina interview kubwa mbili, lakini kutokana na ukata nalazimika kuchagua moja. Kuna ya Prof. Njozi kuhusu ujio wa Rais Bush, na kuna Dr. Harrison Mwakyembe kuhusu Kamati yake na yale yaliyojiri Bungeni. Naomba mnichagulie ipi tuifanye ili nimuombe mmoja wao kuahirisha.

Uwamuzi hapana shaka unao wewe mwenyewe.. Au kama unatangaza biashara then unaweza kuuliza maoni ya wasikilizaji.
 
MKJJ

....mtake radhi Prof Njozi...............tuletee Dr Mwakyembe mwanawane!!
 
Prof Mwakyembe hands down.Njozi anaweza kuombwa radhi.

Mkazanie swali letu tuliosisitiza a "fair hearing" on the part of Lowassa na muulize "if justice must not only prevail, but it must also appear to prevail" haoni kwamba uamuzi wao wa kutomhoji Lowassa unaleta walakini, kama siyo kumpa cha kusema Lowassa?

Muulize pia kuhusu the way forward na prosecution, kwamba the people, particularly the "you tube generation" tuna mashaka kuwa kila kitu kitakuwa swept under the carpet na kujiuzulu kwa Lowassa kuwe mwisho wa habari.What will happen na kama asipofungwa si tutakuwa na bad precedent?

Pia muulize kuhusu maelezo yaliyotolewa nje ya kiapo, na kama kiapo kiliapisha kutoa "the truth and the whole truth" na kama ni hivyo kwa nini waliotoa habari potofu wasishtakiwe kwa perjury? Au kuna deal lilitembea? Tume ilirekodi maongezi yao au ina ushahidi gani kwamba yalitokea?

Ahsante
 
mkjj

ww mtu wa maaajabu kwa kweli hilo tatizo la kutoweza kuwahoji wote wawili hukulijua kabla ya kuekeana ahadi?


kama ulikuwa ukijua mapema kwa nn ukajitia kwenye mashaka hayo.


au ulikuwa unakumbuka ujana unadoea wanawake kama kumi kwa kutegemea wengine watakataa sasa wamekubali wote kichwa kinaanza kuuma.


umelikoroga huna jinsi ni juu yako kulinywa
 
mkjj

ww mtu wa maaajabu kwa kweli hilo tatizo la kutoweza kuwahoji wote wawili hukulijua kabla ya kuekeana ahadi?


kama ulikuwa ukijua mapema kwa nn ukajitia kwenye mashaka hayo.


au ulikuwa unakumbuka ujana unadoea wanawake kama kumi kwa kutegemea wengine watakataa sasa wamekubali wote kichwa kinaanza kuuma.


umelikoroga huna jinsi ni juu yako kulinywa

mbona siyo gumu nimeshaamua... soma tena uamuzi wangu.
 
Hey, achana na mambo ya Njozi, si wakati wa kuota ndoto huu. Lete shujaa Mwakyembe akate issues za kitaifa sio blah blah za kinjozi. JF is not Njozi type. Periopd!
 
Kesho nina interview kubwa mbili, lakini kutokana na ukata nalazimika kuchagua moja. Kuna ya Prof. Njozi kuhusu ujio wa Rais Bush, na kuna Dr. Harrison Mwakyembe kuhusu Kamati yake na yale yaliyojiri Bungeni. Naomba mnichagulie ipi tuifanye ili nimuombe mmoja wao kuahirisha.

Huyu shujaa wetu hayuko katika mapokezi na kumtembeza mgeni wetu?
 
Mimi naomba umuulize

1. Chombo kilicho chunguza Richmond kabla ya Kamati ya Bunge chini yake, Kilikuwa ni PCB au PCCB?

2. Je kama chombo kilichochunguza Richmond kilikuwa PCB, haoni kwamba ripoti yao haikuwa na tatizo? zaidi ya tatizo la paragraph ile inayosema nchi haikupata hasara yoyote?
 
Pole sana mwanakijiji naona kuna wahuni na majibu ya kihuni wakati umekuwa sincere kwetu na unajitolea.

Naomba Mlete Mwakyembe ila muulize juu ya hatua dhidi ya Yona na Rostam kwa kudharau Kamati za Bunge .Kama hawatachukuliwa hatua je kesho wanaweza kuwaoa adhabu wapinzani wakigomea jambo kama wao wnavyo onekana kugomea na Spika haonyeshi hata ishara kwamba Bunge limedharauliwa ?
 
Back
Top Bottom