Dr. Mwakyembe na Powerpool: Kuna mgongano wa maslahi na Dowans/Richmond?

Status
Not open for further replies.
Wachunguzi wa mambo wanaamini kuwa ushujaa wa Dk. Mwakyembe kuishambulia kampuni ya Richmond, na baadaye Dowans, unatokana na mgongano wa kimaslahi.

Kwa maneno mepesi, wanasema Dk. Mwakyembe na wenzake wanapinga Dowans kununuliwa ili wapate mwanya wa kuuza umeme utakaozalishwa na kampuni yao ya Power Pool East Africa Limited, ingawa nao kwa vyovyote vile utakuwa haujatosheleza mahitaji ya umeme nchini.

Dk. Mwakyembe na wenzake walianzisha kampuni yao kabla ya ujio wa kampuni iliyozua utata mkubwa wa Richmond. Matarajio yao yalikuwa kwamba wazalishe umeme na kisha waiuzie Tanesco, lakini ujio wa Richmond ulionekana kutaka kuwakwaza. Richmond ilisababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ajiuzulu Februari mwaka jana.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza Richmond, hakuwahi kutangaza hata mara moja mgongano wa kimaslahi aliokuwa nao kwenye suala hilo.

Pamoja na Dk. Mwakyembe anayemiliki hisa 1,485 katika kampuni hiyo, wengine wenye hisa katika kampuni hiyo ni Emmanuel Kasyanju (99), Victor Mwambalaswa (99), Mwacha Kagoswe (4,455), Josephine Pina (99), Athumani Ngwilizi (99), Prosper Tesha (99), TBC (199 Limited inayomilikwa na Isaac Mwamango (297) na MECCO Limited, inayomilikwa na Maungo Kwabibi hisa moja.

Wakuu nadhani sote sisi ni Wabongo na wepesi sana wa kussoma alama inapofikia hali kama hii...
Ukisoma kwa makini maelezo ya gazeti hili utaelewa kabisa kwamba hii ni njama nzito sana yenye malengo mabaya kwa Mwakyembe na sio shirika husika..
Kwanza, Hilo shirika la Mwakyembe hata kama lipo linafua Umeme kwa njia ya Upepe jambo ambao halikuwepo ktk mpango wa dharura..
Pili maeneo yanayozungumziwa hayahusiani kabisa na sehemu ambazo Richmond au Doiwans walitakiwa kuwekeshaji..
Tatu, shirika hili halipo ktk list za mashirika yaliyoomba tender ya ushindani ktk mchakato wowote ule unaowashirikisha Richmond na Dowans..

Kwa hiyo ukisoma habari hii utagundua kwamba imepambwa sana kuonyesha ubaya wa Mtu badala ya mapungufu ya shirika husika ktk ufuaji umeme..Labda kwa taarifa yao hawa vibaraza wanatakiwa kufahamu kwamba wananchi wanagomba na Richmond/Dowans kama mashirika yenye mpango wa ufisadi sio swala la Ushindani.. Issue kwetu sisi wananchi ni UFISADI sio swala la Uwekezaji ktk nguvu za umeme na nani mmiliki wa shirika fulani..Kila kiongozi nchini ana shirika au amenunua hisa ktk mashirika ya uzalishaji iweje issue hii igeuzwe toka UFISADI hadi kuwa nani kawekeza sehemu fulani..
Na kibaya zaidi ktk Unafiki wa watu hawa, gazeti hili limeweza kutaja kwa asilimia hisa zote za wamiliki wa shirika hili lakini wameshindwa kutupa mhisa hata mmoja (Mtanzania) ktk wamiliki wa Richmond au Dowans zaidi ya kutufunga kamba..
Mohammed Gire alikuwa CEO wa Richmond kulingana na taratibu za uongozi, CEO ni mwajiriwa sio lazima awe mmiliki wa hata asilimia moja..tunafahamu jinsi walivyomtumia Gire kama kawaida yao wanapowatumia watu kama Manji na wahindi wengine wezi kama wao...
Sasa nachotaka gazeti hili wafanye ni watupe wamiliki wa Dowans kwa utaratibu uliotumika kumuumbua Mwakeyembe kama wanavyodai..
Kutokana na kifo cha azimio la Arusha, miiko ya viongozi yote imeondolewa na Mwakyembe hana tofauti kabisa na viongozi wengine ktk uwekezaji na hakika binafsi napongeza sana kiongozi kama Mwakyembe ambaye kawekesha ktk muundombinu muhimu sana kwa Taifa letu from scratch..
Dr. Mwakyembe, kwa habari kama hizi mkuu tunakupongeza sana na hakika Tanzania inataka viongozi kama huyu ambaye binafsi amejikita ktk mradi mkubwa kama huu kisheria pamoja na kwamba hana uwezo mkubwa kam hao majambazi kina Rostam/Lowassa....
 
Ufisadi wa kampuni ya Mwakyembe ni upi huo? Upepo?

Mkuu jmushi1, umelonga sawasawa! Hivi Mwakyembe kuwa na kampuni ni ufisadi, ni breaking news, ni suala la kushangaza! Hii ni mentality ya kitumwa ya zamani ya kwamba ni wahindi au washihili tu sampuli ya Rostam Aziz, Shubash Patel, Somaiya na Yusuf Manji ndiyo wenye haki ya kumiliki makampuni Tanzania! Sisi waswahili au wazawa, kazi yetu kujipanga na mabakuli ya kuombea msaada kwa hao mafisadi. Kwa mentality hiyo, hatufiki!

Afterall, taarifa za Mwakyembe kumiliki kampuni hiyo zimetolewa na gazeti linalomilikiwa na fisadi nambari moja Tanzania, Rostam Aziz ambaye Watanzania wote tunajua anamchukia na kumwinda Mwakyembe ammalize kisiasa! Sitashangaa kusikia kuwa hata taarifa hizi siyo sahihi. Ni Rostam huyu huyu na magazeti yake ya kifisadi aliyedai wiki nzima kuwa Mwakyembe ni mwizi wa maji ya DAWASA! Sikushangaa baadaye Serikali ikimwomba radhi Dk. Mwakyembe Bungeni! Safari hii Mwakyembe usikubali, mkabe koo Rostam kisawasawa, tuko nyuma yako!
 
NI vyema tukaanza mapema kutofautisha terminilogy vinginevy tunarudi Dark Ages:
Mwekezaji, mjasiriamali (entrprenuer) SI SAWA na fisadi
Hili neno FISADi tunalitumia hovyo tu, bila kufikiri. Mwakyembe ni mwekezaji na SIYO fisadi! Fisadi ni wale wanaoiba pesa za walipakodi wa Tanzania wakitumia kampuni zao (halali au la). Mtu akiwekeza pesa zako na kwa ngvu yake akajinyanyua ni mtu wa kumpongeza na kumtakia kila la kheri!
Tuwe makini na matumizi ya maneno na tusikubali kupotoshwa na watu wenye mawazo finyu.
 
tatizo la nishat ya umeme hapa tz ni la muda mrefu. sehem kubwa ya tz mpaka leo hii haipat umeme. tanesco na serikali hazionyeshi dalili ya kuleta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili katka miaka ya hivi karibuni.

katka mazingira hayo akitokea mtu akaamua kuwekeza kwenye uzalishaji umeme ni dhambi? there is a problem and they come with a solution. hii ni sawa na ndivyo dunia inavyokwenda. umeme wenyewe wa nguvu za asili ya upepo! likely cheap! atakuwa amekosea kama atakuwa anazalisha na kuuza umeme kwa bei kubwa zaidi kwasababu hili litasababisha sisi watumiaji tukamuliwe zaid (na hii itakuwa hasara kwake kwani tanesco watasusia umeme wake)

najaribu kuimagine dowans/richmond kuwa mshindani mkubwa wa ppea ya dr. na dr. anapewa nafas aichunguze richmond/dowans.

alichofanya mwakyembe na wenzake ni kuweka waz kila kitu kilivyokwenda wakat wa mchakato wa kuipitisha richmond. hii ni pamoja na kuweka wazi uwezo wa kampuni yenyewe. ukweli uliidondosha richmond. kuna watu hapa walitaka ile kamat ya dr. ipeleke ripot ya uongo bungeni? iseme uongo kuhusu mchakato ulivyokuwa? isielezee uwezo halisi wa kampuni?

cha muhimu kwetu zaman, sasa na baadae ni kuwapa watu majukumu amabao watayatekeleza kwa moyo wa ujasiri, uaminifu, kujituma na mapenz na maslahi kwa nchi yetu. ile timu ya dr. ingeweza kuundwa na watu ambao hawana kampuni za umeme lakin nawahakikishieni hiyo isingemaanisha kuwa lazima wangeibua na kuweka waz ukweli wote kuhusu kampun ile - kitu cha muhimu zaid kwetu. na huenda ilikuwa bahat yetu mwenye ideas na uwekezaj katka umeme alikuwa ndo ana head ile kamat.

kwamba dr. ana kampun kwangu mi sawa.
kwamba dr. alipewa aichunguze kampun shindan kwangu mi sawa so long aliibua ukweli kuhusu mchakato ulivyokuwa ovyo na uwezo ulivyokuwa mdogo wa kampuni husika etc. ukweli amabao haujakanushwa na wahusika

mwenye ya ovyo kuihusu ppea ya dr. (na assume ipo) weka vituz hapa…..

kuwekeza au kuwa tajiri si ufisad wala dhambi. china ni miongoni mwa nchi zinazochukia sana ufisad. majuz juz walihukumu watu waliotia kemikali kwenye maziwa wanyongwe etc. lakin huko huko china kuna matajir na wawekezaj kibao
 
...La msingi hapa ni kuwa kwa kanuni za kawaida, ingebidi Dk. afanye declaration alipochaguliwa ku head Kamati Teule ya Bunge kuwa nayeye pia anayo kampuni ya kufua umeme ambayo nia yake ni kuiuzia

...Na hata ujumbe wake pia katika Kamati Teule ingebidi ujadiliwe. Uhalali wake wa ku serve kwenye kamati hiyo ungetokana na yeye ku declare ineterest zake kwenye hiyo kampuni ambayo ina nia ya kufanya shughuli hizo hizo zinazichunguzwa.

Kwa misingi hiyo bado nasisitiza kuwa hii ni breaking news...

Mimi niko neutral kabisa na wala nisieleweke vibaya.

Sasa uko neutral kivipi, TK, kama unaamini hapa panaweza kuwa na conflict of interest?

Kamata mustendi mzee, usijiumeume, usihofie "kueleweka vibaya" kwa vile tu utitiri mwingi wa jamvi hauelewi concept ya conflict of interest!
 
NI vyema tukaanza mapema kutofautisha terminilogy vinginevy tunarudi Dark Ages:
Mwekezaji, mjasiriamali (entrprenuer) SI SAWA na fisadi
Hili neno FISADi tunalitumia hovyo tu, bila kufikiri. Mwakyembe ni mwekezaji na SIYO fisadi! Fisadi ni wale wanaoiba pesa za walipakodi wa Tanzania wakitumia kampuni zao (halali au la). Mtu akiwekeza pesa zako na kwa ngvu yake akajinyanyua ni mtu wa kumpongeza na kumtakia kila la kheri!
Tuwe makini na matumizi ya maneno na tusikubali kupotoshwa na watu wenye mawazo finyu.

Susuviri nadhani mjadala hapa ni conflict of interest rather than just ufisadi...Hapo sijui kama kuna tofauti...Kwasababu conflict of interest hupelekea ufisadi.Hata hivyo bado hakuna ushahidi kwamba kuna conflict of interest coz kampuni hiyo (ya Mwakyembe) Haikuwepo kwenye bidding kama tulivyoelewa...Madai ya meleta mada yame base kwenye "Tunadhani" nk.
Pia wamedai kuwa yeye ni mmiliki wa kampuni hiyo ya kufua umeme. Hivyo all in all hakuna uwezekano wa ku mbrand Mwakyembe "Fisadi" as long as habari hii remain as it is...Kama alivyosema Nono hapo nyuma...Maji taka flani.
 
"Zak hii nadharia yako tete inaongeza utata. Kuna uhusiano gani kati ya Rostam vs Zitto na Mtanzania/Rai vs Tanzania Daima? Kwa nini tunalinda mashujaa wetu hata kama ukweli unaonesha kuwa samaki mmoja akioza wote wameoza ndio maana kuna kulindana sana kule Bungeni na huko vyamani?

Hivi unaamini Shujaa wetu alisema...."

COMPANERO: Sikuleta nadharia yoyote, Mkubwa. Nilichotaka kusema ni kwamba habari zinazotoka magazeti ya Rostam ziangaliwe kwa chumvi yake. Ni lazima zitakuwa zinapigia debe masilahi yake -- kwa mfano Dowans na hata kagoda. Aidha niliongezea kwamba magazeti ya Mbowe hayaaminiki, kwani baadhi ya wahariri wake wamenunuliwa na Rostam... na hili linajulikana wazi miongoni mwa watu wa media.
 
...whistling...

MKJJ Huna haja ya ku whistle sana....Upande wa Dowans na Mwakyembe unachagua upi?
Ni simple tu....Tusubiri na mawazo ya Mwenyekiti wa mahesabu.
Ila unaonaje kuhusu hili la upepo? Isn't it bora than mashine chakavu? Ama unadhani giza la mwezi wa nne litaleta mushkeli?
 
Hivi DOWANS kwanini wasiuze Umeme maeneo ambayo Umeme Hakuna....Au sheria inawabana?..au wanataka lazima waiuzie Tanesco?...

Otherwise Ipo haja ya kurekebisha sheria zetu ili Kuwekeza ktk Umeme kuwa SOKO HURIA lkn lipo controlled.Lets maeneo Mapya ambayo huwekwa Mitambo mipya ya Umeme...kwani hadi uje uunganishiwe na Tanesco tayari ushaweka Generator au invetor
 
COMPANERO: Sikuleta nadharia yoyote, Mkubwa. Nilichotaka kusema ni kwamba habari zinazotoka magazeti ya Rostam ziangaliwe kwa chumvi yake. Ni lazima zitakuwa zinapigia debe masilahi yake -- kwa mfano Dowans na hata kagoda. Aidha niliongezea kwamba magazeti ya Mbowe hayaaminiki, kwani baadhi ya wahariri wake wamenunuliwa na Rostam... na hili linajulikana wazi miongoni mwa watu wa media.

Na ndio maana Companero akakwambia kwamba hiki sio kitu cha kujiuliza whether gazeti linaongopa au haliongopi au agenda ya Rostam na kadhalika. Umiliki wa kampuni halali is a matter of official records. Kwishne!

Kama ni kweli Mwakyembe ni mmiliki basi mjadala wa nani kaandika hii habari au nani ana miliki gazeti la aliyeandika unakufa papo hapo. Mjadala unakuwa ni whether or not kuna conflict of interest, na kama ipo kwa nini hakutangaza toka mwanzo. It doesn't matter nani atakuwa kaanika ukweli huo - again, kama ni kweli.

Soma tena:
Kwa nini tunaandikia mate ilhali wino upo. Taarifa za makampuni zinahifadhiwa wapi? Maadam wote tunajua zilipo si twende tukaangalie hizo data kuhusu shujaa wetu.
 
Mimi nashangaa sana Shujaa Zitto kachemka watu kibao tumemvalia njuga. Sasa kuna kila dalili kuwa Shujaa Mwakyembe naye kachemka ila watu kibao tunanyanyua bango kumtetea bila hata kuziona taarifa kamili. Nasema hivi: Tuzisome taarifa kamili kutoka Brela n.k. tuone kama ni kampuni ya upepo au la na pia tuone kama alipaswa kulieleza Bunge kuwa kuna mgongano wa kimaslahi au la wakati wanamteua kuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule. Hayo yote yatatusaidia kujua kwa nini Bunge linashindwa kuisimamia Sirikali ili iliue jinamizi la Richmond ikiwa ni mwaka zaidi ya mmoja toka Kamati Teule itoe maazimio/maagizo yake kwa Serikali kuhusu kutatua suala hili tete. Hali kadhalika itatusaidia kuujua ukweli wote kuhusu Richmond na Dowans ambao Kamati Teule iliuficha eti kwa maslahi ya 'umma/taifa'!

Mkuki kwa nguruwe mtamu...
 
wandugu,

..hii taarifa inakuwa ngumu kuielewa kwasababu wengi wetu tume-invest emotionally ktk "wapinga" ufisadi.

..zinapokuja taarifa kwamba hata hao wapinga ufisadi nao wana mushkeli kidogo basi tunapata matatizo ktk ku-analyze taarifa tulizoletewa.

..tulipaswa ku-invest zaidi katika kuupinga ufisadi, na siyo "wapinga" ufisadi.

..kuna matatizo hapa. Dr.Mwakyembe ni mmiliki wa kampuni ya umeme, halafu akapewa jukumu la kuongoza kamati ya Bunge kuchunguza kampuni nyingine ya umeme. hakuna ufisadi, lakini kuna mgongano wa kimaslahi.

..halafu tukianza kuichokonoa hii kampuni ya Mwakyembe, share holders wake, uwezo wake wa kifedha, uwezo wa kitaalamu, uzoefu na historia ya kazi zake, sina uhakika kama tutapata mambo mazuri ya kuvutia.

..kwa mfano: kuna waliohoji kama Richmond na Dowans wana track record yoyote ile ktk shughuli ya kuzalisha umeme. je, tuko tayari kumuuliza swali hilo Mh.Dr.Mwakyembe?

..au, Dr.Mwakyembe ametoa wapi fedha na mtaji wa kuanzisha kampuni ya kufanya shughuli kubwa kama kuzalisha umeme? je, ameandikisha taarifa hizo kwa msajili wa tume ya maadili ya viongozi?

..tusioneana haya au huruma. tuweke maslahi ya Taifa mbele.


NB:

..HISTORIA YA NCHI YETU IMENIFUNDISHA KUTOKUAMINI MWANASIASA YEYOTE YULE TANZANIA.

..WANASIASA HAWA WENGEKUWA WAADILIFU KWELIKWELI NCHI YETU ISINGEKUWA NA MATATIZO KIASI HIKI.
 
kama ni hivyo, ni bora kuliko tapeli wa dowans an richimondi. hivi tapeli na mtu anayefanya vitu bila utapeli bora nani. unaweza ukawalingalisha kweli? wanatapatapa. waache wapate hasara kwa kutonunuliwa mitambo yao. kikwete naye nusu aingie laini, sijui kapewa hela. ati anasema kuna umuhimu wa kureview sheria ya manunuzi? for wat? kwasababu ya downs ndo kikwete alisema tureview sheria ili tuirepeal kwasababu ya dowans? au kwasababu mmiliki wake ni mtu wa kujilipua wa oman anaogopa asijetuma watu waje hapa wajilipue...hahaha. yaani ukombozi wa akili za watz wengine na nchi bado sana. kama hatujapata uhuru vile.
 
bora mwakyembe mmoja kuliko kina Rostam milion moja. kama kungekuwa na kina RA milioni moja wamejipanga hapo, ni hasara kuliko makyembe mmoja. acheni kupiga vita wabongo wenzetu wanaojaribu kufanya kitu cha maana kwa maslahi yetu. kama ni hivyo ninyi mlitaka nini? mlitaka kina RA wanaoingia dili za kiwiziwizi na waarabu ndo wawekeze kwenye umeme? kosa la kina mwakyembe ninini? conflict of interest kwa vipi? hivi ni bora muajemi anayejifanya mbongo na mbunge wa kibongo kuliko mnyakyusa?
 
bora mwakyembe mmoja kuliko kina Rostam milion moja. kama kungekuwa na kina RA milioni moja wamejipanga hapo, ni hasara kuliko makyembe mmoja. acheni kupiga vita wabongo wenzetu wanaojaribu kufanya kitu cha maana kwa maslahi yetu. kama ni hivyo ninyi mlitaka nini? mlitaka kina RA wanaoingia dili za kiwiziwizi na waarabu ndo wawekeze kwenye umeme? kosa la kina mwakyembe ninini? conflict of interest kwa vipi? hivi ni bora muajemi anayejifanya mbongo na mbunge wa kibongo kuliko mnyakyusa?

Acha ubaguzi wa rangi, malizia basi kwa kusema bora mzawa Karamagi anayewekeza...mzawa Mkapa anayewekeza...
 
..HISTORIA YA NCHI YETU IMENIFUNDISHA KUTOKUAMINI MWANASIASA YEYOTE YULE TANZANIA.

..WANASIASA HAWA WENGEKUWA WAADILIFU KWELIKWELI NCHI YETU ISINGEKUWA NA MATATIZO KIASI HIKI.

Most often times I'm forced to believe that intergrity and politics are mutually exclusive....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom